Wednesday, August 27, 2014

SIMBA YAMUWEKA KUNDINI MUSOTI AMPIGA BAO BUTOYI OKWI JE.



Rais wa Simba, Evans Aveva amemaliza utata wa usajili wa wachezaji wa kigeni uliokuwa umeigubika klabu hiyo kwa kusema Mkenya Donald Mosoti ndiye anabaki na Mrundi Butoyi Hussein wamempiga chini huku Yanga nao wakimpiga chini Emmanuel Okwi raia wa Uganda.
Simba na Yanga zimelazimika kufanya uamuzi mgumu wa kupunguza idadi ya wachezaji wa kigeni ambao wamezidi katika klabu zao kwa sababu usajili wa wachezaji katika klabu za Ligi Kuu Bara unamalizika leo saa 6 usiku.
Mrundi huyo alimvutia Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe akiichezea Telecom ya Djibouti katika Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame mjini Kigali, Rwanda mwezi huu.
Maana yake wachezaji wa kigeni katika kikosi cha Simba SC watakuwa mabeki Mganda Joseph Owino, Mkenya Mosoti, Warundi kiungo Pierre Kwizera, mshambuliaji Amisi Tambwe na Mkenya Mkenya Paul Kiongera.
Kwa upande wa Yanga ambapo nayo ilikuwa na wachezaji sita wa kigeni ambapo awali Hamis Kiiza ambaye ni raia wa Uganda ndiye aliyekuwa anadaiwa kuachwa, lakini habari za ndani kutoka katika klabu ya Yanga zinasema panga limemwangukia Emmanueli Okwi ambaye hadi jana asubuhi alikuwa hajajiunga na timu.

SIMBA YAIFUMUA MAFUNZO 2-0 MECHI YA KIRAFIKI

Elias Maguri mshambuliaji  mpya wa simba ameanza kufunga bao lake la kwanza baada ya Simba SC kuifumua bao 2-0 dhidi ya wenyeji Mafunzo jioni hii Uwanja wa Amaan, Zanzibar katika mchezo wa kirafiki. Mchezaji huyo aliyesajiliwa kutoka Ruvu Shooting ya Pwani msimu huu, alifunga bao hilo la kwanza katika mchezo huo, dakika ya 60 baada ya kuingia kuchukua nafasi ya Mrundi Amisi Tambwe ambapo Winga Haroun Chanongo aliifungia Simba SC bao la pili dakika ya 71 
Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Ivo Mapunda/Hussein Sharrif ‘Cassilas’ dk80, Miraj Adam/William Lucian ‘Gallas’ dk80, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’/Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ dk80, Joram Mgeveke/Donald Mosoti dk80, Joseph Owino/Hussein Butoyi dk80, Pierre Kwizera/Said Ndemla dk42, Haroun Chanongo/Uhuru Suleiman dk80, Amri Kiemba/Abdallah Seseme dk65, Amisi Tambwe/Elias Maguri dk46, Shaaban Kisiga ‘Malone’/Ibrahim Hajibu dk80 na Ramadhani Singano ‘Messi’/Twaha Ibrahim.

AZAM FC KESHO YATARAJI KUANZA TIZI ZA VPL YA SEPT 20

Timu ya Azam fc Mabingwa wa Bara Kesho wanatarajiwa kuanza tena mazoezi Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam baada ya kurejea kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame mjini Kigali, Rwanda.

Akizungumza na mkali wa dimba tz.blogspot.com afisa habari wa timu hiyo jaffari iddi maganga amesema kuwa wachezaji wote wataanza mazoezi kesho, kasoro wale ambao wameitwa timu ya taifa.

Maganga amesema kwamba wachezaji wawili, Aishi Manula na Kevin Friday japokuwa hawapo kwenye kikosi cha Taifa Stars, wao wamepewa mapumziko zaidi- hivyo si lazima waanze kesho.
Aidha Maganga amesema kwamba Simba SC waliomba mchezo wa kirafiki na wao wikiendi hii, lakini imeshindikana kwa sababu kocha Joseph Marius Omog amesema hawezi kuwa na mechi baada ya mazoezi ya siku mbili.
Mwalimu amesema mchezo wanaotaka Simba SC labda wiki ijayo, kwa sababu hawezi kufanya mazoezi Alhamsi na Ijumaa halafu baada ya hapo awe na mechi ngumu.

Mcamreoon huyo ambaye aliipatia azam Ubingwa msimu uliopita hivi karibuni ameifikisha Azam FC Robo Fainali ya Kombe la Kagame mjini Kigali kabla ya kutolewa na El Merreikh ya Sudan, iliyoibuka bingwa wa michuano hiyo mwaka huu.




MOROCCO YAIPOTEZEA TAIFA STAR MECHI YA KIRAFIKI YA FIFA.

Picture 079Timu ya taifa ya Morocco imeipotezea taifa star kucheza mechi ya kirafiki ya katika kalenda ya FIFA na sasa Taifa Stars itacheza na Burundi Septemba 5, mwaka huu mjini Bujumbura.

Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa amesema Morocco imejitoa kwa sababu imesema haitaweza kuwapata wachezaji wake wa kimataifa.

Mwesigwa amesema sasa Taifa Stars itacheza na Burun
di mjini Bujumbura siku hiyo hiyo. Kocha Mholanzi, Mart Nooij, tayari ameita kikosi cha wachezaji 26 kwa ajili ya mchezo huo.

Hao ni makipa; Deogratias Munishi (Yanga) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni Said Morad (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Shomari Kapombe (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondani (Yanga SC), Aggrey Morris (Azam), Joram Mgeveke (Simba) na Charles Edward (Yanga).

Viungo; Erasto Nyoni (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Amri Kiemba (Simba), Himid Mao (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Ndemla (Simba), Said Juma (Yanga) na Haruna Chanongo (Simba).

Washambuliaji; John Bocco (Azam), Khamis Mcha (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Yanga), Mwegane Yeya (Mbeya City) na Juma Liuzio 9ZESCO, Zambia).

Kikosi hicho kinatarajiwa kuingia kambini Jumapili (Agosti 31 mwaka huu) mchana katika hoteli ya Accomondia mjini Dar es Salaam na kitakuwa kikifanya mazoezi Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

ETO'O RASMI NA EVARTON,ASAINI MKATABA WA MIAKA

Klabu ya Everton imekamilisha usajili wa mchezaji wa kimataifa wa Cameroon  Samuel Eto'o.
Mshambuliaji huyo mzoefu amesaini kandarasi ya miaka miwili katika hiyo ya Goodison Park, baada ya kuitumika msimu uliopita katika klabu ya  Chelsea.

Eto'o ana vikombe 118 na rekodi ya magoli 56 kwa Cameroon, Eto'o imekua akicheza katika klabu kadhaa na ambavyo amekuwa akivipatia ubingwa kama Barcelona na Inter Milan.

QPR na majirani zao Liverpool walikuwa pia na  mawazo ya kumsajili Eto'o, ambaye anaweza kupatikana katika mchezo wa Premier League siku ya Jumamosi kati yake ya Everton na timu yake ya zamani  Chelsea katika uwanja wa Goodison Park.

Tuesday, August 26, 2014

TFF YAWEKA ADHABU KALI KWA WATOA RUSHWA KATIKA SOKA.

KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imeamua kuanzia sasa adhabu kwa watu wanaotoa rushwa au kupanga matokeo katika mchezo huo itakuwa ni kufungiwa maisha kujishughulisha na mchezo huo.

Taarifa katika tovuti 
ya TFF imesema kwamba hayo yamefikiwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya shirikisho hilo juzi.

Kwa muda sasa, kumekuwa na tuhuma nyingi za wachezaji na marefa kuhongwa ili kupanga matokeo- lakini hakukuwa na sheria madhubuti ya kupambana na hali hiyo- lakini kwa hatua hii mpya ya TFF dhahiri itasaidia kupunguza mchezo huo mchafu. 

Aidha, baada ya Libya kujitoa kuwa mwenyeji wa Fainali za Afrika (AFCON) za 2017, Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limealika nchi wanachama kuomba uenyeji wa fainali hizo.
Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Agosti 24, mwaka huu imeamua Tanzania kuomba uenyeji wa fainali hizo.

“Tunatambua kuwa moja ya masharti ya kuandaa fainali hizo ni pamoja na nchi kuwa imeandaa moja ya mashindano ya vijana. Lakini kwa kuwa suala hili liko katika mazingira maalumu (exceptional circumstances) tunaamini CAF watafikiria ombi letu kwa msingi huo.

Awali Libya ilipewa uenyeji wa fainali hizo 2015, lakini zikahamishiwa Afrika Kusini kutokana na sababu za kiusalama. Hivyo, Libya ikapewa fainali za 2017 ambapo sasa imejitoa yenyewe kuandaa fainali hizo.

Wakati huo huo: Kamati ya Utendaji ya TFF imemteua Boniface Wambura kuwa Mkurugenzi mpya wa Mashindano kuanzia Septemba 1 mwaka huu.


Kabla ya uteuzi huo, Wambura alikuwa Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF kuanzia Januari 1, 2011. Nafasi hiyo sasa iko wazi na itajazwa baadaye na Kamati ya Utendaji.