Tuesday, December 16, 2014

MICHUANO YA COPA COCA-COLA YAENDELEA KUTIMUA VUMBI.

Michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 ngazi ya Taifa inaendelea leo jioni (Desemba 16 mwaka huu) kwa mechi mbili zitakazochezwa jijini Dar es Salaam na mkoani Pwani.


Uwanja wa Nyumbu uliopo mkoani Pwani utazikutanisha timu za Mjini Magharibi na Dodoma katika mechi ya kundi B, wakati kundi C kutakuwa na mechi kati ya Arusha na Mwanza itakayochezwa Uwanja wa Tanganyika Packers uliopo Kawe jijini Dar es Salaam.

Wakati kesho (Desemba 17 mwaka huu) ikiwa ni mapumziko, michuano hiyo itaingia hatua ya robo fainali keshokutwa (Desemba 18 mwaka huu) kwenye viwanja hivyo hivyo.

RAMBIRAMBI MSIBA WA KOCHA MADEGA

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Kocha Mshindo Madega kilichotokea leo (Desemba 16 mwaka huu) mjini Bukoba.

Mbali ya kuwahi kuwa mchezaji katika timu ya RTC Kagera, Kocha Madega aliwahi kufundisha timu za Kagera Stars, Mwadui na kombaini ya Copa Coca-Cola ya Mkoa wa Kagera.

Mchango wake katika mchezo wa mpira wa miguu tangu akiwa kocha na baadaye kocha utakumbukwa daima.

Tunatoa salama za rambirambi kwa familia ya marehemu, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera (KRFA), Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) Mkoa wa Kagera na klabu ya Bukoba Veterans na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo.


TFF itawakilishwa kwenye msiba huo na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera (KRFA).

15 KUTOKA NJE WAOMBEWA USAJILI DIRISHA DOGO

Usajili wa dirisho dogo msimu wa 2014/2015 umefungwa jana (Desemba 15 mwaka huu) huku wachezaji 15 kutoka nje wakiombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kutoka nchi mbalimbali.

Wachezaji walioombewa ITC kwa timu za Ligi Kuu ni Abdulhalim Humoud kutoka Sofapaka ya Kenya kwenda Coastal Union, Brian Majwega kutoka KCC (Uganda) kwenda Azam, Castory Mumbara kutoka Three Star Club (Nepal) kwenda Polisi Mara, Charles Misheto kutoka SP Selbitiz (Ujerumani) kwenda Stand United na Chinedu Michael Nwankwoeze kutoka Nigeria kwenda Stand United.

Dan Serunkuma kutoka Gor Mahia (Kenya) kwenda Simba, Emerson De Oliveira Neves Roque kutoka Emerson De Oliveira Neves Roque kutoka Bonsucesso FC (Brasil) kwenda Yanga, Halidi Suleiman kutoka Flambeau (Burundi) kwenda Stand United na Juuko Murushid kutoka SC Victoria University (Uganda) kwenda Simba.

Kpah Sean Sherman kutoka Aries FC (Liberia) kwenda Yanga, Meshack Abel kutoka KCB (Kenya) kwenda Polisi Morogoro, Moussa Omar kutoka Flambeau (Burundi) kwenda Stand United, Nduwimana Michel kutoka Flambeau (Burundi) kwenda Stand United, Serge Pascal Wawa kutoka El Merreikh (Sudan) kwenda Azam na Simon Serunkuma kutoka Express FC (Uganda) kwenda Simba.


Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF inatarajia kukutana hivi karibuni kwa ajili ya kupitia usajili wa wachezaji wote walioombewa katika dirisha dogo wakiwemo wale wa mkopo.

LIGI KUU VODACOM TZ BARA DIMBA DEC 26 TIMU KUUMANA DIMBANI

Timu zinazoshiriki ligi kuu vodacom tanzania bara kila moja tayari imekamilisha usajili ili kuimarisha vikiosi vyao kwa ajili ya Raundi ya nane ya ligi hiyo.
LIGI KUU VODACOM
RATIBA
Ijumaa Desemba 26
Simba v Kagera Sugar
Jumamosi Desemba 27
Mtibwa Sugar v Stand United               
Prisons v Coastal Union             
JKT Ruvu v Ruvu Shootings
Jumapili Desemba 28
Mbeya City v Ndanda FC            
Polisi Moro v Mgambo JKT          
Yanga v Azam FC   
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Mtibwa Sugar
7
4
3
0
10
3
7
15
2
Yanga
7
4
1
2
9
4
4
13
3
Azam FC
7
4
1
2
8
4
4
13
4
Coastal Union
7
3
2
2
8
6
2
11
5
Kagera Sugar
7
2
4
1
5
3
1
10
6
JKT Ruvu
7
3
1
3
7
7
0
10
7
Simba
7
1
6
0
7
6
1
9
8
Polisi Moro
7
3
2
2
6
7
-1
9
9
Mgambo JKT
7
3
0
4
4
7
-3
9
10
Stand United
7
2
3
2
5
9
-4
9
11
Ruvu Shooting
7
2
1
4
4
7
-3
7
12
Tanzania Prisons
7
1
3
3
5
6
-1
6
13
Ndanda FC
7
2
0
5
8
12
-4
6
14
Mbeya City
7
1
2
4
3
5
-2
5

SIMBA YAFUNGA USAJILI KWA KUMNASA BEKI WA MTIBWA HASSAN KESSY RAMADHANI

Wekundu wa Msimbazi Simba imetua nanga baada ya kufunga usajili wake wa dirisha dogo kwa kumsaini beki kijana wa kulia wa Mtibwa Sugar ya Morogoro, Hassan Ramadhani Kessy.
Kessy amesaini usiku huu Mkataba wa miezi 18 baada ya mvutano wa muda mrefu na klabu hiyo juu ya dau.
Zaidi ya mara tatu, Kessy alikwishakutana mezani na uongozi wa Simba SC bila kufikia maafikiano na baada ya mvutano huo uliodumu kwa takriban mwezi mzima, leo mambo yameisha.
Kaburu amesema kwamba baada ya kumpata Kessi wanadhani sasa kikosi chao kimekamilika na wanaelekeza nguvu zao katika maandalizi kwa ajili ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Kessy anakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Simba SC katika dirisha dogo, baada ya Waganda beki Juuko Murushid na washambuliaji Dan Sserunkuma na Simon Sserunkuma.
Murushid amesaini miaka mitatu, wakati akina Sserunkuma wamesaini miaka miwili kila moja.
Simba SC imewatema Warundi kiungo Pierre Kwizera na mshambuliaji Amisi Tambwe aliyehamia kwa mahasimu, Yanga SC baada ya kuwasajili Waganda hao.
Simba SC ililazimika kuwatema Warundi hao ili kukidhi matakwa ya kanuni ya Usajili ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ya wachezaji watano wa kigeni.
Murushid na akina Sserunkuma wanaungana na Waganda wenzao, beki Joseph Owino na mshambuliaji Emmanuel Okwi kukamilisha idadi ya wachezaji watano wa kigeni.