Thursday, May 23, 2013

CITY YAKANUSHA KUWAWINDA FALCAO NA NEYMAR

NEYMAR_THE_BRAZILIAN
MKURUGENZI MKUU wa Manchester City chief Ferran Soriano amekanusha taarifa kuwa wanahaha kuwasaini Masupastaa Radamel Falcao na Neymar.
Hivi karibuni kumezagaa ripoti kuwa Man City ni miongoni mwa Klabu zinazokimbiza saini za Straika wa Atletico Madrid, Radamel Falcao, na yule wa Santos ya Brazil, Neymar.
Falcao anawindwa na msululu wa Klabu zikiwemo Chelsea, Monaco na Real Madrid baada ya kung’ara sana kwa kuifungia Atletico Mabao muhimu kwa Misimu kadhaa.
Nae Neymar, anaewindwa na Klabu kubwa Barani Ulaya, anatarajiwa kuihama Brazil baada ya Nchi hiyo kuwa Mwenyeji wa Kombe la Dunia Mwaka 2014.
Hata hivyo, Soriano amekanusha kwa kutamka: “Neymar na Falcao? Habari hizo ni uongo, hawajawahi kuwa kwenye ajenda yetu!”
Vile vile, Soriano aliponda habari kuwa wanataka kumuuza Straika wao mahiri Serio Aguero, mwenye Miaka 24, huku Real Madrid ikitajwa kuwa ndio atatua.
Soriano amesisitiza: “Hatujawahi kufikiria kumuuza Aguero. El Kun ana furaha kubaki kwetu Mwaka huu!”