CLUB ya soka FC Barcelona imefikia Makubaliano na Klabu
ya Brazil, Santos, ya kumsaini Neymar ambapo leo Jumatatu Mei 27 atasaini
Mkataba ili kukamilisha Dili hiyo ya Uhamisho.
Klabu ya Barcelona imetoa Taarifa rasmi ya kuthibitisha kufikia makubaliano ya kumsaini Nyota huyo wa Brazil mwenye Miaka 21.
WASIFU:
Neymar da Silva Santos Junior
KUZALIWA: 5 Februari 1992, Nchini Brazil
Santos: Mechi 229 Magoli 138
Brazil: Mechi 32 Magoli 20
Na
Mwenyewe Neymar alitoa Ujumbe kwenye Mtandao wa Instagram uliosema kuwa jumatatu nasaini Mkataba na Barcelona. Nataka kuwashukuru Mashabiki wa
Santos kwa Miaka hii 9 ya ajabu.
Juzi Klabu ya Santos ilitoa Taarifa kuwa
imepokea Ofa mbili za kumnunua Neymar na ilisadikiwa zimetoka toka
mbili kati ya Klabu za Barcelona, Real Madrid au Chelsea.
Mkataba wake na Santos ulitarajiwa kumalizika mwishoni mwa Msimu ujao, Mwezi Juni 2014.

Neymar ndie ameiongoza Santos kupata
mafanikio makubwa tangu Nguli Pele aache kuichezea Klabu hiyo kwenye
Miaka ya 1970 kwa kuisaidia kutwaa Kombe la Brazil Mwaka 2010, Copa
Libertadores Mwaka 2011 na Ubingwa wa Jimbo la Sao Paolo kwa mara 3
mfululizo.
Nayo Klabu ya Santos imesema kuwa ilijaribu kila njia ili Neymar abaki kwao lakini Ofa za nje zimewafanya wasiweze kushindana.
Hata hivyo, Santos imekataa kutaja Dili hiyo ya Uhamisho imegharimu kiasi gani kwa vile kila upande umekubaliana kuwa iwe siri.
WASIFU WA NEYMAR | |||
Taarifa kuhusu yeye | |||
---|---|---|---|
Full name | Neymar da Silva Santos Júnior | ||
Date of birth | 5 February 1992 | ||
Place of birth | Mogi das Cruzes, Brazi | ||
Height | 1.74 m (5 ft 9 in) | ||
Playing position | Mshambuliaji | ||
Club ya sasa | |||
Current club | Santos | ||
Number | 11 | ||
Timu za ujana | |||
1999–2003 | Portuguesa Santista | ||
2003–2009 | Santos | ||
Timu ya ukubwa | |||
Years | Team | Mechi | Goli |
2009– | Santos | 103 | (54) |
Timu ya Taifa | |||
2009 | Brazil U17 | 3 | (1) |
2011 | Brazil U20 | 7 | (9) |
2012 | Brazil U23 | 7 | (4) |
2010– | Brazil | 32 | (20) |