Wednesday, July 17, 2013

CAF YATANGAZA KUSOGEZA MBELE MCHEZO WA LIGI YA MABINGWA KATI YA WATANI WA JADI"

Shirikisho la kandanda Barani Afrika-CAF limesogeza mbele mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Afrika ambao unawakutanisha watani wa jadi nchini Misri timu za Zamalek na Al Ahly mpaka Jumatatu ijayo.  
Vigogo hao wa soka nchini humo walitarajiwa kucheza Jumapili katika mji wa El Gouna ambao uko kilometa 500 kutoka mji mkuu wa Cairo kutokana na sababu za kiusalama. Katika taarifa iliyotolewa katika mtandao wa Zamalek, wamethibitisha kuwa FIFA imekubali mchezo huo kuchezwa El Gouna pamoja na kwamba uwanja huo haukuwepo katika ratiba za michuano hiyo na kuamua kuchelewesha mchezo huo kwa siku moja kwasababu za kibiashara. Wizara ya mambo ya ndani ya nchi hiyo ilikataa mapema kuhakikisha usalama wa mechi hiyo kuchezwa jijini Cairo au Alexandria kabla ya Zamalek kuchagua El Gouna.