Wednesday, July 17, 2013

WAKALA WA SUAREZ ASEMA KAMA KUNA CLUB INAMTAKA MCHEZAJI HUYO IWEKE MEZANI KITITA CHA NGUVU

Wakala wa mshambulaij  nyota wa klabu ya Liverpool na timu ya taifa ya Uruguay" Luis Suarez’ amebainisha na kuweka wazi kama kuna klabu inahitaji kumsajili nyota huyo lazima iandae dau la nono la pauni miliaoni 40 ili kupata huduma yake.

Klabu ya Liverpool imesema itasikiliza ofa ya pauni milioni 40, lakini kuna uwezekano wa ofa hiyo kupanda mpaka kufikia pauni milioni 50 kumnunua nyota huyo mwenye matukio ya aina yake nchini England, likiwemo la kumng`ata beki wa Chelsea,  Ivanovic na kusimamishwa mechi kumi, pamoja na tuhuma za ubaguzi wa rangi kwa beki wa mabingwa wa soka nchini Englanda, Manchester United, Mfaransa Patrick Evra.

Wakala wa Suarez bwana Pere Guardiola, ambaye ni kaka yake kocha wa wekundu wa kusini mwa Ujerumani, The Bavarian, klabu ya Bayern Munich , Joseph Pep Guardiola , amasema atakaa mezani na klabu yoyote yenye uwezo wa kuweka mezani mzigo wa pauni milioni 40.

Ambapo sasa Baadhi ya Klabu kubwa barani Ulaya zinataka kuinasa saini ya Luis Suarez kutoka kwa majogoo wa jiji.

Arsenal ni klabu pekee yenye mpango wa nguvu zaidi kutaka kumsajili Suarez kwa pauni milioni 35, lakini ofa hiyo inaonkana haina maana kwa wekundu wa Anfield waliotangaza pauni milioni 40.

Awali Asernal walituma ofa ya pauni milioni 30, Liver wakatupilia mbali, wakaongeza tano, bado wakagomewa kabisa kwani wanataka 40 tu, huna mzigo huo basi amekosa huduma ya nyota huyo.

Saurez ambaye atajiunga na Liverpool waliopo  Melbourne jumatatu ijayo, ana mkataba na Liverpool mpaka mwaka 2016. Lakini Liver wameonekana kuwa na msimamo wa kumbakisha, huku klabu za Arsena, Real Madrid na Chelsea zakiimarisha rada zao kutaka kumsajili.