Wakala
wa mshambulaij nyota wa klabu ya Liverpool na timu ya taifa ya Uruguay" Luis Suarez’ amebainisha na kuweka wazi kama kuna klabu
inahitaji kumsajili nyota huyo lazima iandae dau la nono la pauni miliaoni
40 ili kupata huduma yake.
Klabu
ya Liverpool imesema itasikiliza ofa ya pauni milioni 40, lakini kuna
uwezekano wa ofa hiyo kupanda mpaka kufikia pauni milioni 50 kumnunua
nyota huyo mwenye matukio ya aina yake nchini England, likiwemo la
kumng`ata beki wa Chelsea, Ivanovic na kusimamishwa mechi kumi, pamoja
na tuhuma za ubaguzi wa rangi kwa beki wa mabingwa wa soka nchini
Englanda, Manchester United, Mfaransa Patrick Evra.
Wakala
wa Suarez bwana Pere Guardiola, ambaye ni kaka yake kocha wa wekundu wa
kusini mwa Ujerumani, The Bavarian, klabu ya Bayern Munich , Joseph
Pep Guardiola , amasema atakaa mezani na klabu yoyote yenye uwezo wa
kuweka mezani mzigo wa pauni milioni 40.
Ambapo sasa Baadhi ya Klabu kubwa barani Ulaya zinataka kuinasa saini ya Luis Suarez kutoka kwa majogoo wa jiji.
Arsenal
ni klabu pekee yenye mpango wa nguvu zaidi kutaka kumsajili Suarez kwa
pauni milioni 35, lakini ofa hiyo inaonkana haina maana kwa wekundu wa
Anfield waliotangaza pauni milioni 40.

Saurez
ambaye atajiunga na Liverpool waliopo Melbourne jumatatu ijayo, ana
mkataba na Liverpool mpaka mwaka 2016. Lakini Liver wameonekana kuwa na
msimamo wa kumbakisha, huku klabu za Arsena, Real Madrid na Chelsea
zakiimarisha rada zao kutaka kumsajili.