Monday, July 22, 2013

MESSI AMPIGIA UPATU KOCHA MPYA MARTINO KUCHUKUA MIKOBA YA VILANOVA

Mshambuliaji nyota wa klabu ya Barcelona na timu ya taifa ya argetina Lionel Messi amempigia upatu kocha Gerardo Martino kuchukua mikoba ya kuinoa klabu hiyo. Baada ya nafasi ilikuwa wazi kutokana na aliyekuwa kocha wa timu hiyo Tito Vilanova kulazimika kuachia ngazi kutokana na maradhi ya saratani yanayomsumbua. 
Martino ambaye aliiongoza timu ya Old Boys kushinda taji la Ligi Kuu chini Argentina msimu uliopita ni mmoja wa makocha wanaoewa nafasi ya kuchukua nafasi ya Vilanova na Messi ana imani kuwa kocha huyo anastahili nafasi hiyo. Messi alidai kuwa Martino ni mmoja wa makocha wenye kiwango cha juu na kila mtu anamheshimu hivyo haoni tatizo kama akikabidhiwa mikoba ya kuinoa Barcelona.