Monday, July 22, 2013

UONGOZI WA URA YA UGANDA YAJIA JUU SIMBA KUHUSU OWINO"

URA ya Uganda kupitia uongozi wake umeamua kujajuu na kusema unashangazwa na kuiona inamtaka beki Joseph Owino.
Meneja wa URA, Sam Okabo amesema Simba walimuona mchezaji huyo hana thamani wakati akiwa mgonjwa.
Simba ilimuacha Owino ikiwa ni siku chache baada ya kubadilishana na Uhuru Selemani ambaye alikwenda Azam FC.
Lakini ikaonekana alikuwa hajapona vizuri hivyo viongozi wa Simba wakaamua kuachana naye na kuanza kuhaha kusaka mabeki wengine.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Pope alimfuata Owino baada ya mechi ya kirafiki dhidi ya URA ambayo Msimbazi walilala.