Timu ya Taifa ya Wanawake (Twiga
Stars) inaendelea kujinoa kwa ajili ya mechi ya marudiano ya raundi ya kwanza
ya Kombe la Afrika kwa Wana
Twiga Stars chini ya Kocha Rogasian
Kaijage na Msaidizi wake Nasra Juma inaendelea vizuri, na kwa mujibu wa programu
ya benchi lao la ufundi kesho (Jumatatu), Jumanne na Jumatano itafanya mazoezi
saa 10 jioni.

Shepolopolo ambayo ilishinda mechi ya
kwanza mabao 2-1 wiki iliyopita inatarajiwa kuwasili nchini Alhamisi (Februari
27 mwaka huu) kwa ndege ya Fastjet, na siku hiyo hiyo itafanya mazoezi Azam
Complex.
Waamuzi wa mechi hiyo Ines Niyonsaba,
Jacqueline Ndimurukundo, Axelle Shikana na Suavis Iratunga, wote kutoka Burundi
wanatarajiwa kuwasili nchini Jumatano