MAKUNDI:
KUNDI A: Netherlands, Czech Republic, Turkey, Latvia, Iceland, Kazakhstan.
KUNDI B: Bosnia-Hercegovina, Belgium, Israel, Wales, Cyprus, Andorra.
KUNDI C: Spain, Ukraine, Slovakia, Belarus, FYR Macedonia, Luxembourg.
KUNDI D: Germany, Republic of Ireland, Poland, Scotland, Georgia, Gibraltar.
KUNDI E: England, Switzerland, Slovenia, Estonia, Lithuania, San Marino.
KUNDI F: Greece, Hungary, Romania, Finland, Northern Ireland, Faroe Islands.
KUNDI G: Russia, Sweden, Austria, Montenegro, Moldova, Liechtenstein.
KUNDI H: Italy, Croatia, Norway, Bulgaria, Azerbaijan, Malta.
KUNDI I: Portugal, Denmark, Serbia, Armenia, Albania.
Timu mbili za juu toka kila Kundi pamoja
na Timu moja Bora iliyoshika Nafasi ya 3 kwenye Makundi zitatinga
Fainali na Timu 8 zilizobaki ambazo zitamaliza Nafasi ya Tatu
zitapangiwa Mechi maalum za Mchujo ili kupata Timu 4 za mwisho kuingia
Fainali.
Mechi za Makundi zitaanza Septemba 2014 hadi Oktoba 2015 na Ratiba kamili itatolewa na UEFA baada ya Droo.
Fainali za UEFA EURO 2016 zitachezwa
Nchini Ufaransa kuanzia Juni 10, 2016 hadi Julai 10, 2016 na kwa mara ya
kwanza Fainali hizo zitakuwa na Nchi 24 badala ya zile 16 za kawaida.
Kwa mara ya kwanza, UEFA imebuni Mtindo wanaouita ‘Wiki ya Soka’ ambao utafanya Gemu zichezwe kuanzia Alhamisi hadi Jumanne.
Saa za Mechi kuanza ni 18.00CET na 20.45CET kwa Jumamosi na Jumapili na 20.45CET kwa Alhamisi, Ijumaa, Jumatatu na Jumanne.
CET ni Saa za Ulaya ya Kati ambazo ni Masaa mawili nyuma ya Saa za Bongo kwa Majira ya Sasa.
Pia, Mtindo huo wa ‘Wiki ya Soka’
utakuwa na Wiki maalum ambapo Mechi mbili zitachezwa mfululizo, yaani
Alhamisi/Jumapili, Ijumaa/Jumatatu au Jumamosi/Jumanne.
Droo kwa ajili ya Mechi za Fainali itafanyika Mjini Paris hapo Desemba 12, 2015.