PAWASA ,MATOLA,LUNYAMILA MWAMEJA KUWAKABIRI MADRID REAL
KIKOSI maalumu cha ‘Tanzania
All Stars’ kitakachoshuka dimbani kuvaana na magwiji wa Real Madrid,
‘Real Madrid Legends’ kitaingia kambini jijini Dar es salaam kujiandaa
na mechi hiyo itakayopigwa uwanja wa Taifa Agosti 23 mwaka huu.
baadhi ya wachezaji hawa hapa pawasa,matola,Lunyamila,mwameja,manyika waitwa kukipiga na real madrid
Makocha maarufu nchini, Charles Boniface Mkwasa ‘Master’,
Fredy Felix Minziro na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ wataongoza benchi la
ufundi la kikosi hicho , huku Daktari wa timu akiwa ni Mwanandi Mwankemwa.