Wednesday, November 19, 2014

KUUUZA KIPRE NA KUMLETA TRAORE INAHITAJI MOYO JE ANAWEZA KUZIBA PENGO

Mabingwa wa ligi kuu Msimu uliopita Azam fc Azam FC imekubali kumuuza mshambulizi wake bora zaidi, Muivory Coast, Kipre Tchetche kwa timu ya Kelntan FC ya nchini Malasyia ambapo nafasi yake ikitarajiwa kuzibwa na mshambulizi wa mali, Mohammed Traore. 
Tunaweza kusema toa kifaa pata kifaa wakati mwingine huzaa majibu mabaya kutokana na uwezo wa mtu alieondoka hatari sana i nahitaji maamuzi kumtoa mtu kama kipre. 
Hivyo kitendo cha kumuuza, Kipre mwenye kasi na kumsaini mchezaji anayetegemea kutengenezewa mipira tu kinaweza kuifanya timu hiyo kupooza kabisa katika safu ya ushambulizi.
Didier Kavumbagu, John Bocco, Gaudensi Mwaikimba, Leonel Saint wote hawa ni washambuliaji ambao hawana kasi sana uwanjani tofauti na Kipre alikuwa na uwezo binafsi katika uchezaji wake, alikuwa akishambulia vizuri kutokea pembeni ya uwanja na alikuwa hatari kutokana na kasi yake. 
Benchi la ugfundi la timu hiyo linakabiliwa na changamoto kubwa, lakini watalazimika kukubali changamoto kuishi bila msaada wa mabao ya Kipre’ mchezaji ambaye alijiunga na Azam FC miaka minne iliyopita na kushinda tuzo ya ufungaji bora msimu wa 2012/14 huku akishinda tuzo ya mchezaji bora wa msimu uliopita.