KOCHA wa timu ya taifa ya
Brazil, Luis Felipe Scolari amekiri kuwa kikosi chake bado hakiwezi
kuanza kuweka matumaini ya kutwaa kombe lao la sita la Kombe la Dunia mwaka ujao
lakini wamebakisha mechi moja kunyakuwa taji lao la tatu la Kombe la
Shirikisho baada ya kuiengua Uruguay katika hatua ya nusu fainali. Scolari
amesema anafikiri kikosi hicho kimefikia mahali pazuri lakini bado kuna
vitu vingi vya kufanyia marekebisho mpaka kikamilike kwa ajili ya
michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Kocha
huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa wanahamishia nguvu zao katika mchezo
wa fainali na baada ya hapo wataangalia mapungufu yalijitokeza ili
kuhakikisha wanakuwa na kikosi imara kitakachoweza kulibakisha Kombe la
Dunia nyumbani. Brazil
kwasasa wanasubiri mshindi wa nusu fainali nyingine ya michuano hiyo
itakayopigwa baadae leo kati ya mabingwa wa Ulaya na Dunia Hispania
watakaochuana na Italia.
Thursday, June 27, 2013
ABEL NA KISPANG WAJITOA TIMU YA WANARIADHA WA KENYA
BINGWA mara mbili wa
dunia mashindano ya mbio ndefu Abel Kirui na mshindi wa medali ya shaba
katika michuano ya olimpiki Wilson Kipsang wamejitoa katika timu ya
wanariadha ya Kenya itakayoshiriki michuano ya riadha ya dunia
itakayofanyika jijini Moscow. Makamu
wa rais wa Chama cha Riadha cha nchi hiyo Paul Mutwii amedai kuwa Kurui
aliwafahamisha kwamba amejitoa kwasababu ya kusumbuliwa na majeraha
wakati Kipsang yeye amewaambia kuwa ana majukumu mengine. Kirui
ambaye alishinda taji la dunia la mbio ndefu mwaka 2009 na 2011 amekuwa
akisumbuliwa jeraha la kifundo cha mguu wake wa kulia na anatarajiwa
kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki sita. Kuziba
nafasi hizo Mutwii amesema wamewaita Mike Kipyego ambaye alishinda mbio
za marathon jijini Tokyo mwaka jana, Bernard Kipyego mshindi wa medali
ya fedha mbio za nusu marathon 2009 na bingwa wa mbio za marathoni za
Paris Peter Some. Kikosi cha mwisho kitakachokwenda Moscow kitatajwa mwezi ujao baada ya kufanyika mbioza mchujo.
JUVESTUS YATANGAZA RASMI KUMSAJILI TEVEZ
KLABU ya Juventus ya
Italia jana ilimtangaza rasmi kumsajili mshambuliaji nyota wa kimataifa
wa Argentina, Carlos Tevez kutoka timu ya Manchester City kwa mkataba wa
miaka mitatu. Taarifa
zinadai kuwa klabu yenye maskani yake katika jiji la Turin wamelipa
kiasi cha paundi milioni 10 kwa nyota huyo mwenye umri wamiaka 29. Lakini
Tevez atatakiwa kumaliza adhabu yake ya kutumikia jamii kwa saa 250 ili
kuondoka jijini London salama na kuepuka kuburuzwa tena mahakamani. Tevez
alikatisha likizo yake huko Amerika Kusini na kupanda ndege kuelekea
Italia jana lakini pia atatakiwa kumaliza adhabu yake aliyopewa na
mahakama ya Macclefield April mwaka huu kwa kuendesha huku akiwa
amefungiwa kufanya hivyo.
Tuesday, June 25, 2013
VALCKE-ASEMA BRAZIL NDIO MAHALA PA KOMBE LA DUNIA"
KATIBU Mkuu wa
Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Jerome Valcke amesema kuwa hawana
mpango wa kubadili mahali patakapochezwa michuano ya Kombe la Dunia
mwakani. Valcke
alibainisha kwamba michuano hiyo itafanyika nchini Brazil katika miji 12
kama ilivyopangwa na hakuna mpango mwingine wowote wa kuhamisha
mashindano hayo kwenda sehemu nyingine. Kauli
ya Valcke imekuja kufuatia maandamano ambayo yamekuwa yakiendelea
nchini humo wakati huu wa michuano ya Kombe la Shirikisho wakipinga
gharama kubwa za matayarisho ya Kombe la Dunia wakati wananchi wake wana
hali duni katika maisha yao ya kawaida. Valcke
pia alipinga kauli ya Waziri wa Michezo wa Brazil, Aldo Rebelo
aliyekuwa amekaa pembeni yake katika mkutano na waandishi wa habari
aliyedai kwamba kuna nchi zimeonyesha nia ya kuwa mwenyeji wa mashindano
hayo kama Brazil ikijitoa. Katibu
mkuu huyo amesema hajapokea ofa yoyote kutoka katika nchi yoyote
duniani kutaka kuandaa michuano hiyo ya 2014 na kumuondoa hofu Rebelo
ambaye alidai amesoma katika vyombo vya habari kwamba nchi za Marekani,
Uingereza, Ujerumani na Japan zinamendea nafasi hiyo.
EFF-LAMTIMUA KIBARUA KATIBU MKUU WAKE""
SHIRIKISHO la Soka la
Ethiopia-EFF limemtimua kibarua katibu mkuu wake baada ya kukiri
kumtumia mchezaji kimakosa katika mechi za kufuzu michuano ya Kombe la
Dunia 2014 hatua ambayo inaweza kuigharimu timu nchi hiyo kukatwa alama
tatu. Kamati ya
Utendaji ya EFF ilipiga kura za kumtimua katibu huyo aitwaye Ashenafi
Ejigu lakini walipinga barua ya kujiuzulu kwa makamu wa rais wa
shirikisho hilo Berhanu Kebede ambaye ndiye alikuwa akilaumiwa kutokana
na mkanganyiko huo. Baadhi
ya wajumbe na waandishi wa habari za michezo waliokuwepo katika mkutano
huo walikuwa wakitaka uongozi mzima wa shirikisho hilo ujiuzulu kwa
kile walichokiita uzembe. Rais
wa EFF, Sahilu Gebremariam alikiri kuwa suala hilo ni la kizembe na
wanapaswa wote kujiuzulu na kudai kuwa atafanya hivyo katika mkutano
mkuu utakaofanyika Septemba mwaka huu. Akihojiwa
kuhusiana na suala la kumchezasha mchezaji aliyepewa kadi mbili za
njano kocha wa Ethiopia Sewnet Bishaw alijitetea kuwa anapokuwa uwanjani
huwa hatumii karatasi na kalamu anachofanya yeye ni kuhakikisha timu
inapata matokeo mazuri.
YANGA WAJIPNGA NA MECHI ZA KIRAFIKI
Mabingwa wa soka Tanzania Bara , Afrika Mashariki
na Kati, Klabu ya Dar Young Africans watacheza mechi za kirafiki dhidi
ya Rayon Sport ya Rwanda Julai 6 na 7, mwaka huu katika sehemu ya ziara
yake ya kulitembeza Kombe lake la ubingwa wa Ligi Kuu mikoa ya kanda ya
Ziwa inadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake,
Kilimanjaro Premeum Lager.
Kwa
mujibu wa taarifa kutoka kwa kaimu katibu mkuu wa Yanga Lawrence
Mwalusako , Yanga maarufu kama Kwalalumpa Malysia itaondoka Dar es
Salaam Julai 5, siku mbili tu baada ya kuanza mazoezi Uwanja wa
sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam kuelekea Mwanza tayari kwa
mchezo wa kwanza dhidi ya mabingwa hao wa zamani wa Afrika Mashariki na
Kati, Uwanja wa CCM Kirumba, Julai 6.
Baada
ya kipute hicho, Julai 7, timu hizo ambazo zimewahi kufundishwa na
kocha kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Raoul Jean Pierre
Shungu kwa wakati tofauti na kwa mafanikio, zitarudiana kwenye Uwanja wa
Kambarage mjini Shinyanga.
“Yanga
tuna mipango mingi sana, bahati mbaya tumeshindwa kwenda Sudan kutetea
ubingwa wetu wa Kagame, lakini bado tuna michuano mikubwa barani Afrika,
ikiwa ni heshima kwa mashabiki wetu na wanachama wanaotuunga mkono, ni
nafasi yao kuliona taji letu la ligi msimu uliopita, tutapita mikoani na
kushangilia pamoja”. Alisema Mwalusako.
Baada ya hapo , Yanga SC
wataelekea mjini Tabora, kucheza mechi nyingine na wenyeji, Rhino FC
waliopanda Ligi Kuu msimu huu Julai 11, mwaka huu Uwanja wa Ally Hassan
Mwinyi.
Katika
ziara hizo, Yanga watatembeza Kombe lao la ubingwa wa Ligi Kuu,
walilolitwaa kwa mara ya 24 msimu huu kwenye mitaa mbalimbali
kushangilia na mashabiki wao.
Yanga
SC, imekuwa na mafanikio makubwa tangu ianze kudhaminiwa na TBL mnamo
2008, ikitwaa jumla ya mataji sita katika kipindi hicho, yakiwemo mawili
ya Kagame, 2011 na 2012 na manne ya Ligi Kuu Bara, 2008, 2009, 2011 na
2013.
Agosti 2, mwaka 2011, TBL ilisaini Mkataba wa udhamini na Yanga wa miaka minne sawa na kwa watani wao pia, Simba SC.
Katika
mkataba huo mpya, uliotiwa saini kwenye hoteli ya Double Tree, Masaki,
Dar es Salaam, TBL iliongeza dau la fedha za mishahara kwa wachezaji
kutoka Sh. Milioni 16 hadi Milioni 25 kwa mwezi, ikaongeza basi moja
kubwa, Yutong lenye uwezo wa kubeba abiria 54 na fedha kwa ajili ya
kugharamia mikutano ya wanachama ya kila mwaka Sh. Milioni 20 kugharamia
tamasha la mwaka la klabu na vifaa vya michezo vyenye thamani ya Sh.
Milioni 35 kila msimu.
Yanga pia inapewa bonasi ya Sh. Milioni 25 ikitwaa ubingwa wa Ligi Kuu
Bara au Milioni 15, ikishika nafasi ya pili katika Mkataba huo wenye
thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 5 tangu Agosti 8, mwaka huu hadi Julai
31, mwaka 2016.
TETESI ZA MASTAA NA KITUO CHA REDIO CHA NAPOLI MARTE-CAVANI
KITUO
cha Redio cha Napoli, Marte kimetangaza kuwa dau la Pauni Milioni
49.3 limetolewa na Chelsea kwa ajili ya mshambuliaji Edinson Cavani
ambaye muda wote anampasua kichwa mmiliki wa klabu ya Chelsea Bilionea
Roman Abramovich mwenye lengo la kuimarisha kikosi chake chini ya kocha
Jose Mourinho.
Katika
taarifa ya jana usiku, Radio Marte ilitangaza: “Tumepokea taarifa
kutoka ofisini kwa vyanzo vya kuaminika kwamba, Napoli imekubaliana dili
la kuiuzia Chelsea Cavani.
Kitu moto: Chelsea sasa ipo katika nafasi ya kumnasa Edinson Cavani
“Rafa
Benitez pia amebariki, lakini kabla ya kutangaza rasmi, Napoli inataka
kupata mshambuliaji atakayeziba pengo la Il Matador.
“Aurelio De Laurentiis”, klabu itasomba kiasi cha Euro Milioni 58, sawa na dili la Ezequiel Lavezzi kwenda PSG mwaka jana.
“Mchezaji huyo atajiingizia mshahara wa Euro Milioni 8.5 kwa msimu pamoja na haki za picha,”. Habari zimevuja kama kwamba Cavani
ametangaza anataka kukutana uso kwa uso na Rais, Aurelio de Laurentiis
na kuna taarifa kwamba Manchester United nayo imo kwenye mbio hizo.
Mshambuliaji
huyo wa Uruguayna baba yake awali walionyesha nia ya kutaka kwenda Real
Madrid. Klabu hiyo ya Hispani iliwasiliana na Napoli, lakini sasa
itabidi waipiku ofa iliyotolewa na Chelsea.
Subscribe to:
Posts (Atom)