Usain Bolt Mwanariadha nyota wa
mbio fupi kutoka Jamaica,ametuma salamu kwa wapinzani wake
baada ya kufanikiwa kuibuka na ushindi katika mbio za mita 200 za Diamond League
zilizofanyika jijini Paris kwa kutumia muda wa sekunde 19.73 ukiwa ni
muda wa haraka zaidi kwa mwaka huu. Bolt
ambaye anashikilia rekodi ya dunia katika mbio hizo alifabnikiwa mbio
kirahisi na kuuzidi muda wa haraka zaidi uliowekwa kwa mwaka huu na
Tyson Gay wa Marekani mwezi mmoja kabla ya mashindano ya riadha ya dunia
yatakayofanyika jijini Moscow, Urusi. Akihojiwa
mara baada yam bio hizo Bolt amesema anajisikia vyema kwa kushinda mbio
hizo lakini bado bado ana kazi ya kufanya kuhakikisha anakuwa katika
kiwango chake ifikapo michuano ya dunia. Nafasi
ya pili katika mbio hizo ilikwenda kwa Warren Weir wa Jamaica
aliyetumia muda wa sekunde 19.92 huku nafasi ya tatu ikienda kwa
Christophe Lemaitre wa Ufaransa aliyetumia muda wa sekunde 20.07.
Sunday, July 7, 2013
Thursday, July 4, 2013
ROONEY ATAKIWA KUWA SILISHA BARUA KWA MAN U
MSHAMBULIAJI Wayne Rooney atatakiwa
kuwasilisha barua ya maandishi ya kuomba kuondoka ikiwa anataka kuachana
na Manchester United.
Mpachika mabao huyo wa Old Trafford,
alirejea mazoezini jana huku mustakabali wake ukiwa bado haueleweki.
Imefahamika hakuwa na Mkutano mahsusi na kocha mpya David Moyes juu ya
suala lake.
Hilo linaweza kutokea katika kituo cha
mazoezi cha klabu, Carrington leo. Wawili hao walizungumza jana, lakini
si kwa muda mrefu na msimamo wa United kwake bado haujabadilika.
Hajielewi: Mustakabali wa Wayne Rooney bao haueleweki licha ya jana kurejea mazoezini
Wamesema mshambuliaji huyo wa England
hauzwi. Kuhusu tetesi za wapinzani wao katika Ligi Kuu, Arsenal kutaka
rasmi kumsajili tangu wiki iliyopita, United bado haijawasiliana na
yoyote anayemtaka Rooney.
Sakata hili linaweza kugeuka tu iwapo
mshambuliaji mwenyewe ataamua kulazimisha kuondoka. BIN ZUBEIRY
iliandika mwishoni mwa msimu uliopita kwamba, Rooney aliomba kuondoka
kwa kocha aliyestaafu, Sir Alex Ferguson.
Ombi la kuondoka litamaanisha Rooney
hatadai chochote katika Mkataba wake wa miaka miwili uliobakia ambao
alikuwa analipwa Pauni 250,000 kwa wiki.
Huku Moyes akitarajiwa kuzungumza na Waandishi wa Habari kwa mara ya kwanza kesho, ufafanuzi utakuja muda si mrefu.
Wakati huo huo, mchezaji mwenzake wa
zamani Rooney, Mreno Cristiano Ronaldo ameendelea kuweka wazi juu
mapenzi yake na United. Mshambuliaji huyo wa Real Madrid amesema jana
kwamba anataka kurudi Ligi Kuu, lakini hakusema lini.
"Nalikosa kweli soka la England. Kwangu
ilikuwa moja ya miaka bora katika maisha yangu ya soka wakati nipo huko
Manchester United. Ni klabu ambayo bado ipo moyoni mwangu. naikosa kweli
kweli. Lakini kwa sasa maisha yangu yapo Hispania. Nafurahia kucheza
huko pia. Mustakabali hatuwezi kuujua,"alisema Ronaldo.
ISCO ASEMA LENGO KUU NI KUISAIDIA MADRID KUTWAA UEFA

GIGGS NAYE AWA KOCHA MCHEZAJI SAFU YA BENCH LA UFUNDI.

RYAN GIGGS NA MAN U
-UMRI: 39
-MECHI: 941
-MAGOLI: 168
-MATAJI YA LIGI: 13
-FA CUP: 4
-LIGI CUP: 4
-UEFA CHAMPIONZ LIGI: 2
HISPAIN BADO NAMBARI MOJA DUNIANI VIWANGO VYA FIFA
Ivory Coast ndiyo Nchi ambayo iko juu kupita zote Afrika na inakamata Nafasi ya 13.
Brazil, ambao Jumapili iliyopita walitwaa Kombe la Mabara, wamerudi 10 Bora na sasa wapo Nafasi ya 9.
20 BORA:
1 Spain
2 Germany
3 Colombia (Imepanda Nafasi 4)
4 Argentina (Imeshuka 1)
5 Holland
6 Italy (Imepanda 2)
7 Portugal (Imeshuka 1)
8 Croatia (Imeshuka 4)
9 Brazil (Imepanda 13)
10 Belgium (Imepanda 2)
11 Greece (Imepanda 5)
12 Uruguay (Imepanda 7)
13 Ivory Coast
14Bosnia-Herzegovina (Imepanda 1)
15 England (Imeshuka 6)
16Switzerland (Imeshuka 2)
17 Russia (Imeshuka 6)
18 Ecuador(Imeshuka 8)
19 Peru (Imepanda 11)
20 Mexico (Imeshuka 3).
WACHINA WAKABIDHI UWANJA WA TAIFA KWA SERIKALI.

Makabidhiano hayo ya Uwanja huo
uliochukua Miaka 7 kujengwa yalifanyika Jana kwa kutia saini na
kubadilishana Vyeti kati ya Balozi wa China Nchini Tanzania, Li Youqing,
na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Sihaba Mkinga.
Akizungumza, Waziri wa Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo, Dr. Fenella Mukangara, aliishukuru China
kwa msaada wao mkubwa wa Fedha na Ujenzi.
Pia, Waziri Mukangara, alisifu Usimamizi
wa China wa Uwanja huo tangu ujenzi ulipokamilika na tangu Uwanja huo
ulipofunguliwa rasmi hapo Tarehe 25 Februari 2009 na Rais wa zamani wa
China, Hu Jintao, na Rais Jakaya Kikwete.
Uwanja wa Taifa, unaochukua Washabiki
60,000 wote wakiwa Vitini, umegharimu Shilingi Bilioni 56 na kati ya
hizo China ilitoa Bilioni 33.4 na Tanzania ilitoa Fedha zilizobaki.
Uwanja huu ni wa kisasa na upo katika Viwango vinavyokubalika na FIFA na Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki.
Serikali imedokeza kuwa hivi sasa wapo
kwenye mazungumzo ya kutafuta Fedha ili kugharamia Ujenzi wa Awamu ya
Pili na inatarajiwa Serikali ya China itahusishwa na pia Mkandarasi
aliejenga Awamu ya Kwanaza, Beijing Construction Engineering Company
Limited, ndio watashughulikia Awamu hii.
Baada ya kukamilika kwa Ujenzi wa Awamu
ya Pili, Tanzania itakuwa iko tayari kuwa Mwenyeji wa Mashindano makubwa
ya Michezo ya kila aina.
CHELSEA YAFIKIA MAKUBALIANO NA MARCO VAN GINKEL WA VITESSE FC YA UHOLANZI".
WAKALI wa Darajani Club ya soka ya Chelsea imefikia makubaliano ya kumsajili kiungo wa klabu ya Vitesse Arnhem ya Uholanzi, Marco van Ginkel. Kiungo
huyo mwenye miaka 20 ambaye ametokea katika shule ya watoto ya Vitesse
kabla ya kupata namba katika kikosi cha kwanza April mwaka 2010
atajiunga na Chelsea baada ya kukamilisha taratibu za vipimo vya afya. Van
Ginkel amekuwa akicheza katika kikosi cha timu ya taifa ya vijana chini
ya miaka 21 ya Uholanzi na mara moja ameshaitwa katika kikosi cha timu
ya wakubwa akiingia kama mchezaji wa akiba katika mchezo dhidi ya
Ujerumani Novemba mwaka jana. Kiungo
huyo anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na meneja mpya wa Chelsea Jose
Mourinho kufuatia kusajiliwa kwa mshambuliaji Andre Schuerrle ktoka
Leverrkusen mwezi uliopita.
Subscribe to:
Posts (Atom)