![]() |
Bratter akiyatafakari mazungumzo |
Tuesday, July 9, 2013
FIFA-SEPP BRATTER ATARAJI KUZUNGUMZA NA MAOFISA WA ISRAEL
MESSI RASMI ATARAJIWA KUREJEA BARCA MAZOEZINI JULAI 15

ROLNADO NAYE KUWANIA TUZO YA UNYAYO WA DHAHABU:
Mshambuliaji nyota mahiri wa club ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametajwa katika orodha ya
wachezaji 10 watakaowania tuzo ya kiatu cha Dhahabu kwa mwaka 2013. Mshambuliaji
huyo wa kimataifa wa ureno atakuwa mchezaji wa kwanza wan chi hiyo
kushinda tuzo hiyo ambayo ilianza kutolewa mwaka 2003 mahsusi kwa
wachezaji waliozidi umri wa miaka 28. Mchezaji
mwenzake wa Madri Iker Casillas na kiungo mahiri wa Barcelona Andres
Iniesta ni miongoni wa nyota wengine walioteuliwa kugombea tuzo hiyo. Wachezaji
waliwahi kushinda tuzo hiyo ambayo hutolewa kwa kuangalia uwezo wake wa
kipindi chote alichocheza soka na kiwango chake cha sasa, ni pamoja na
Roberto Carlos, Ronaldinho, Francesco Totti na mshindi wa mwaka uliopita
Zlatan Ibrahimovic. Wachezaji
wanaweza kushinda tuzo hiyo mara moja pekee, ambapo sherehe zake
hufanyika jijini Monaco kila mwaka toka ilipoanzishwa. Mbali
na hao wengine waliokuwemo katika orodha ya mwaka huu ni pamoja na
Samuel Eto'o kutoka Anzhi Makhachkala, Andrea Pirlo anayekipiga
Juventus, Didier Drogba kutoka Galatasaray, Frank Lampard-Chelsea,
Miroslav Klose-Lazio, David Trezeguet-River Plate and David
Beckham-Paris Saint-Germain.
Sunday, July 7, 2013
STEWART HALL AMKUBALI KASEJA ASEMA BADO NI BONGE LA KIPA TZ"
![]() |
Stewart hall akitabasamu kwa pozi la aina yake |
Hall amesema kipa wake mwingine "Jackson Wandwi anafikiria kumpeleka kucheza kwa mkopo katika Club ya Ashanti United ya Ilala iliyopanda Ligi Kuu msimu huu, ili kupata uzoefu baadaye arejee kushindana na Mwadini na Aishi.
“Aidha Hall amesema nafahamu fika kuwa Kaseja ametupiwa virago MSimbazi na nasikia watu wanamzungumzia sana wakimhusisha na Azam fc. Mimi nakubali yule ni kipa mzuri na ana uzoefu. Ila mimi nina makipa wazuri wawili, Aishi na Mwadini. Nataka hawa washindane ili kumpata kipa nambari moja wa timu"
Hata hivyo Hall amesema kuwa bado Azam ina makipa wengine wazuri wa timu za vijana, ambao watakuwa wakipewa nafasi ya kujifua na kikosi cha kwanza msimu ujao.
“Hivyo nitakuwa na Aishi na Mwadini kama makipa wawili imara wa timu ya kwanza, maana yake Wandwi ataendelea kupoteza kiwango chake. hivyo nifikiria bora nimpeleke Ashanti ili akakuze kipaji chake na kupata uzoefu, baadaye arejee kwenye timu akiwa imara zaidi".
Mbali na hilo tulipomuuliza kuhusu maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara na michuano ya kombe la shirikisho barani afrika Hall amesema kwamba Azam
ambayo itaipeperusha bendera ya Tanzania kwa mara ya pili mfululizo kwenye Kombe la
Shirikisho Afrika mwakani, iko katika mazoezi.
“Tunaendelea na mazoezi ya msimu mpya. Kwa sasa tupo katika programu ya ufukweni na gym. Baada ya hapo tutaanza programu rasmi ya uwanjani. Lakini wiki mbili za mwanzo za Agosti tutakwenda Afrika Kusini kuweka kambi,”.
“Tunaendelea na mazoezi ya msimu mpya. Kwa sasa tupo katika programu ya ufukweni na gym. Baada ya hapo tutaanza programu rasmi ya uwanjani. Lakini wiki mbili za mwanzo za Agosti tutakwenda Afrika Kusini kuweka kambi,”.
MARION AFANIKIWA KUTWAA TAJI LA KWANZA LA MICHUANO YA GRAND SLAM.
Marion Bartoli mwanadada nyota katika
tenisi, amefanikiwa kushinda taji lake la kwanza la
michuano ya Grand Slam baada ya kumchalaza Sabine Lisicki wa Ujerumani
kwa seti 6-1 6-4 kwenye mchezo wa fainali ya michuano ya Wimbledon. Bartoli
ambaye anashika namba 15 katika orodha za ubora kwa upande wanawake
alitumia dakika 30 pekee kushinda seti ya kwanza wakati mpinzani wake
Lisicki akionekana kushindwa kumudu vishindo katika fainali yake ya
kwanza ya Grand Slam. Akihojiwa
mara baada ya mchezo huo Bartoli amesema haamini kama amenyakuwa taji
hilo na alikuwa akijisikia kucheza kwa kiwango chake cha juu huku kila
kitu alichofanya kikimuendea sawa. Michuano
hiyo inaendelea tena baadae kwa mchezo wa fainali kwa upande wa wanaume
ambapo Andy Murray wa Uingereza anayeshika namba mbili katika orodha za
ubora atachuana na Novak Djokovic wa Serbia anayeshika namba moja
katika orodha za ubora.
HISPAIN YATOLEWA NJE MASHINDANO YA VIJANA FIFA U-20" LEO GHANA VS CHILE


>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
MATOKEO MENGINE"
ROBO FAINALI
France 4 Uzbekistan 0
Magoli:
*Yaya Sanogo (dk31')
*Paul PogbaP (dk35' Penati)
*Florian Thauvin (dk43' Penati)
*Kurt Zouma (dk64')
Uruguay 1 Spain 0
Goli:
*Felipe Avenatti (dk103’)
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>Hivyo sasa kwa ushindi huo Uruguay katika hatua ya Nusu Fainali watashuka dimbani kupepetana na Mshindi wa Mechi ya Iraq vs South Korea.
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
RATIBA ROBO FAINALI LE; JULAI 7
[Saa 12 Jioni]
Kayseri
Iraq v South Korea
[Saa 3 Usiku]
Istanbul
Ghana v Chile
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
Katika Robo Fainali nyingine iliyochezwa jana Timu ya Taifa ya France
ilifanikiwa kutinga hatua ya Nusu Fainali baada ya kuilaza Uzbekistan kwa Bao 4-0 hivyo sasa kwa matokeo hayo France itacheza na Mshindi kati ya Ghana vs Chile.
Bao za France zilifungwa na Yaya Sanogo, Paul Pogba, Florian Thauvin naKurt Zouma.
RATIBA/MATOKEO:
ROBO FAINALI
06/07 France 4 Uzbekistan 0
06/07 Uruguay 1 Spain 0
07/07 muda 18:00 Iraq v South Korea
07/07 muda 21:00 Ghana v Chile
NUSU FAINALI
10/07 18:00 Bursa France vs Ghana or Chile
10/07 21:00 Trabzon Uruguay vs Iraq or South Korea
MSHINDI WA TATU
Tarehe 3/07 18:00 Uwanja Istanbul Kulingana na matokea
FAINALI
Tarehe 13/07 21:00 Uwanja Istanbul
World Youth Championship{Bingwaaaaaa}
TUKUMBUKE WASHINDI WALIOPITA:
2011 Brazil
2009 Ghana
2007 Argentina
2005 Argentina
2003 Brazil
2001 Argentina
1999 Spain
1997 Argentina
1995 Argentina
1993 Brazil
1991 Portugal
1989 Portugal
1987 Yugoslavia
1985 Brazil
1983 Brazil
1981 Germany
1979 Argentina
1977 U.S.S.R.
BOLT ATUMA SALAMU KWA WAPINZANI WAKE BAADA YA KUIBUKA NA USHINDI.
Usain Bolt Mwanariadha nyota wa
mbio fupi kutoka Jamaica,ametuma salamu kwa wapinzani wake
baada ya kufanikiwa kuibuka na ushindi katika mbio za mita 200 za Diamond League
zilizofanyika jijini Paris kwa kutumia muda wa sekunde 19.73 ukiwa ni
muda wa haraka zaidi kwa mwaka huu. Bolt
ambaye anashikilia rekodi ya dunia katika mbio hizo alifabnikiwa mbio
kirahisi na kuuzidi muda wa haraka zaidi uliowekwa kwa mwaka huu na
Tyson Gay wa Marekani mwezi mmoja kabla ya mashindano ya riadha ya dunia
yatakayofanyika jijini Moscow, Urusi. Akihojiwa
mara baada yam bio hizo Bolt amesema anajisikia vyema kwa kushinda mbio
hizo lakini bado bado ana kazi ya kufanya kuhakikisha anakuwa katika
kiwango chake ifikapo michuano ya dunia. Nafasi
ya pili katika mbio hizo ilikwenda kwa Warren Weir wa Jamaica
aliyetumia muda wa sekunde 19.92 huku nafasi ya tatu ikienda kwa
Christophe Lemaitre wa Ufaransa aliyetumia muda wa sekunde 20.07.
Subscribe to:
Posts (Atom)