Kiungo nyota wa kimataifa wa
Mexico, Giovani Dos Santos amekamilisha usajili wake wa kujiunga na
klabu Villareal ambayo imepanda ligi msimu huu akitokea klabu ya Real
Mallorca zote za Hispania. Dos
Santos mwenye umri wa miaka 24 ambaye alikuwa sehemu ya kikosi cha
Mexico kilichonyakuwa medali ya dhahabu katika michuano ya olimpiki
jijini London mwaka jana, amesaini mkataba wa miaka minne na klabu
hiyo. Kiungo huyo
mshabuliaji aliibukia katika shule ya watoto ya Barcelona kabla ya
kwenda katika klabu ya Tottenham Hotspurs mwaka 2008 kwa uhamisho wa
euro milioni sita. Hata
hivyo Dos Santos alishindwa kung’aa sana katika kikosi cha kwanza na
kujikuta akipelekwa kwa mkopo katika timu ya daraja la pili ya Ipswich
Town na baadae kwenda Galatasaray ya Uturuki na Racing Santander.
Wednesday, July 10, 2013
WANNE KUTOKA BAYEN MUNICH NAO KATIKA ORODHA YA FIFA
Club
ya Bayern Munich ya ujerumani imefanikiwa kutoa wachezaji wa nne walioteuliwa katika orodha ya wachezaji 10 na
Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA kugombea tuzo ya mchezaji bora wa
bara hilo kwa msimu wa 2012-2013. Wachezaji
hao ni Franck Ribery, Thomas Mueller, Arjen Robben na Bastian
Schwainsteiger ambao wote walikuwemo katika kikosi cha Bayern ambacho
kilifanikiwa kunyakuwa mataji matatu msimu uliopita. Mbali
na hao wengine waliotajwa katika orodha hiyo ni mchezaji bora wa mwaka
katika Ligi Kuu nchini Uingereza, Gareth Bale pamoja na mfungaji bora wa
ligi hiyo Robin van Persie huku Lionel Messi na Cristiano Ronaldo
wakiwa wachezaji pekee kutoka La Liga ya nchini Hispania kwenye orodha
hiyo. Hii itakuwa
ni mara ya tatu kufanyika sherehe za tuzo hizo ambapo mwaka 2011 Messi
ndiye aliyeshinda huku mchezaji mwenzake wa Barcelona Andres Iniesta
akishinda tuzo hiyo mwaka jana. Wachezaji
wengine ni Mshambuliaji nyota wa klabu ya Paris Saint-Germain-PSG,
Zlatan Ibrahimovic na Robert Lewandowski anayekipiga Borussia Dortmund
ambapo orodha ya mwisho ya wachezaji watatu itatajwa Agosti 6 kabla ya
sherehe za kumjua mshindi ambazo zitafanyika wakati wa upangaji wa
ratiba ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Agosti 29 mwaka huu jijini Monaco.
Tuesday, July 9, 2013
MURRAY APONGEZWA NA CAMEROON VS MALIKIA ELIZABETH
Waziri Mkuu David
Cameron pamoja na Malkia Elizabeth wa pili wa Uingereza wamekuwa miongoni mwa
watu mashuhuri waliotoa pongezi kwa mchezaji tenisi nyota wan chi hiyo
Andy Murray kwa kunyakuwa taji la michuano ya Wimbledon. Wachezaji
nyota na watu wengine maarufu nchini humo pia walitoa pongezi zao kwa
Murray mwenye umri wa miaka 26 baada ya kuwa Muingereza wa kwanza
kunyakuw ataji la michuano hiyo toka Fred Perry alipofanya hivyo mwaka
1936, kwa kumfunga Novak Djokovic kwa seti 3-0.
Cameron ambaye alikuwepo
uwanjani kushuhudia mtanange huo alimpongeza Murray kwa kuonyesha
kiwango cha juu kwenye mchezo huo na kuweka historia mpya katika mchezo
huo nchini Uingereza. Mwandishi
wa BBC katika kasri ya kifalme nchini humo, Peter Hunt alibainisha kuwa
Malkia alimtumia ujumbe binafsi Murray kumpongeza kwa kufanikiwa
kushinda taji hilo.
LIVERPOOL YAIBWAGA CHINI OFA YA ARSENAL KUHUSU SUAREZ
Majogoo wa jiji london Club ya soka ya Liverpool
imepiga chini ofa ya paundi milioni 30 waliyotoa Arsenal kwa ajili ya
kumsajili mshambuliaji wa klabu hiyo Luis Suarez. Kumekuwa
na tetesi za muda mrefu za Suarez kutaka kuuzwa baada ya kufungiwa
mechi 10 kwa kumng’ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic katika Uwanja
wa Anfield msimu uliopita. Klabu
ya Real Madrid ya Hispania ndio wanaotegemewa kumsajili mshambuliaji
huyo wa kimataifa wa Uruguay baada ya kutamka wazi kwamba ameyachoka
maisha ya Uingereza. Mwishoni
mwa wiki hii Arsenal nao walidaiwa kuingia katika kinyang’anyiro cha
kumuwania lakini Liverpool walikataa kutoa kauli yoyote kuhusiana na
tetesi hizo huku wakisisitiza kwamba bado wanamhitaji mshambuliaji huyo.THIERRY HENRY NAYE YUMO KIKOSI CHA WACHEZAJI 10 WA MLS
Mshambuliaji nyota wa
zamani wa Ufaransa, Thierry Henry ni moja kati ya wanadinga nyota 10
watakaounda kikosi kutoka katika Ligi Kuu ya Soka nchini Marekani-MLS
ambacho kitapambana na AS Roma ya Italia Julai 31 huko jijini Kansas. Henry
mwenye umri wa miaka 35 mshambuliaji wa klabu ya New York Red Bull
ambaye aliisadia Ufaransa kushinda Kombe la Dunia mwaka 1998, amefunga
mabao sita katika mechi 17 alizoichezea timu hiyo msimu huu. Kabla ya kwenda Marekani mwaka 2010 akitokea klabu ya Barcelona, henry amewahi kucheza katika vilabu vya Juventus na Arsenal. Golikipa
wa FC Dallas ambaye ni raia wa Peru Raul Fernandez, kiungo wa timu ya
taifa ya Canada Will Johnson na Beki wa Kansas City Aurelien Collin
ambaye ni raia wa Ufaransa ni miongoni mwa wachezaji wasiokuwa raia wa
Marekani walioteuliwa katika kikosi hicho cha nyota wa MLS.
FIFA-SEPP BRATTER ATARAJI KUZUNGUMZA NA MAOFISA WA ISRAEL
![]() |
| Bratter akiyatafakari mazungumzo |
MESSI RASMI ATARAJIWA KUREJEA BARCA MAZOEZINI JULAI 15
Mshambuliaji nyota wa kimataifa wa argentina na club ya fc Barcelona, Lionel Messi anatarajiwa kurejea mazoezini Julai 15
baada ya kupumzika kwa wiki moja pekee katika likizo yake kutokana na
majukumu mbalimbali ambayo yamekuwa yakimtinga. Masimu
wa 2012-2013 kwa mchezaji huyo nyota ulimalizika Juni 15 baada ya
Argentina kuigaragaza Guatemala kwa mabao 4-0 katika mchezo wa kimataifa
wa kirafiki, hivyo kumanisha kwamba nyota huyo angekuwa na mwezi mzima
wa kupumzika kabla ya kuanza kwa msimu mpya. Hata
hivyo Messi mwenye umri wa miaka 26 alitumia nafasi hiyo kucheza mechi
mbalimbali za hisani kuzunguka dunia na kumaliza ziara yake hiyo
mwishoni mwa wiki iliyopita huko Chicago, Marekani. Jumla
ya ziara zote hizo Messi amesafiri kilimita zaidi ya 90,000 toka msimu
wa ligi ulipomalizika akitembelea nchi za Argentina, Ecuador, Guatemala,
Italia, Senegal, Colombia, Peru na Marekani. Nyota
huyo amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya msuli mwishoni mwa msimu
uliopita na mapumziko mafupi aatakayopata yatawapa uhakika mdogo
madaktari juu ya afya yake kabla ya kuanza msimu mpya wa 2013-2014.
Subscribe to:
Posts (Atom)





