Thursday, February 13, 2014

MESSI AWEKA REKODI FC BARCA JANA ATUPIA 1

Mshambuliaji mahiri wa argentina na club ya barcelona Lionel Messi amefanikiwa kuweka rekodi nyingine ya mabao wakati Barcelona ikitinga fainali ya Kombe la Hispania kuelekea mechi na Manchester City wiki ijayo Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Messi alifanikiwa kuifungia timu yake jana katika sare ya 1-1 na Real Sociedad na kufikisha mabao 335 hivyo kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi katika klabu hiyo ya Hispania.

Barca imeingia fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-1 baada ya awali kushinda 2-0 na sasa itakutana na Real Madrid katika mechi ya kuwania Kombe.
COPA del REY
NUSU FAINALI

{Saa za Bongo}

Marudiano

Jumanne Februari 11

Atletico de Madrid 0          Real Madrid CF 2 {0-5}

Jumatano Februari 12

Real Sociedad 1 FC Barcelona 1 {1-3}

FAINALI

Aprili 19

Real Madrid v Barcelona

LIVER YAICHAPA FULHAM 3-1-TOURE AENDELEA KUJIFUNGA:

Timu ya Liverpool imefanikiwa kupanda hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kuifunga mabao 3-2 Fulham jana usiku .

Kolo Toure alijifunga dakika ya nane kuipatia Fulham bao la kwanza na Richardson akaifungia timu hiyo bao la pili dakika ya 63.

Mabao ya Liverpool yalifungwa na Daniel Sturridge dakika ya 41, Coutinho dakika ya 40 na mkongwe Steven Gerrard dakika ya 90 kwa penalti.

Liverpool sasa imetimiza pointi 53 baada ya kucheza mechi 26 na inabaki nafasi ya nne.
MATOKEO
Jumatano Februari 12
Arsenal 0 Man United 0

Everton v Crystal Palace {Imeahirishwa}

Man City v Sunderland     {Imeahirishwa}

Newcastle 0 Tottenham 4

Stoke 1 Swansea 1

Fulham 2 Liverpool 3

MSIMAMO:TIMU

NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 Chelsea 26 17 6 3 48 21 27 57
2 Arsenal 26 17 5 4 48 26 22 56
3 Man City 25 17 3 5 68 27 41 54
4 Liverpool 26 16 5 5 66 32 34 53
5 Tottenham 26 15 5 6 36 32 4 50
6 Everton 25 12 9 4 37 26 11 45
7 Man United 26 12 6 8 41 31 10 42
8 Southampton 25 10 9 7 37 29 8 39
9 Newcastle 26 11 4 11 32 38 -6 37
10 Swansea City 26 7 7 12 33 36 -3 28
11 West Ham 26 7 7 12 28 33 -5 28
12 Aston Villa 26 7 7 12 27 36 -9 28
13 Hull 26 7 6 13 25 31 -6 27
14 Stoke 26 6 9 11 27 41 -14 27
15 Crystal Palace 25 8 2 15 18 34 -16 26
16 Norwich 26 6 7 13 19 39 -20 25
17 West Brom 26 4 12 10 30 38 -8 24
18 Sunderland 25 6 6 13 25 38 -13 24
19 Cardiff 26 5 7 14 19 44 -25 22
20 Fulham 25 6 2 18 26 58 -32 20
    TAZAMA MAPUNGUFU YA TOURE
Mchoro Kuhusu Toure Jinsi ilivyo Kuwa
TOURE AKIJIFUNGA

RAGE ASEMA APOKEA BARUA TATU TOKA FIFA-IPO YA OKWI

SHIRIKISHO la Soka la Kimataifa (Fifa), limetuma barua tatu tofauti kwa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, moja ikiwa ni ile inayomhusu Emmanuel Okwi ambaye sasa yuko Yanga.

Moja ya barua ambazo Rage amepewa kopi na Fifa ni ile ambayo Shirikisho la Soka la Uganda (Fufa), limemuomba Okwi kurejea Uganda na kuitumikia timu ya taifa katika michuano ya kimataifa.
Pamoja na barua hiyo, Rage amethibitisha kupokea barua hizo tatu kutoka Fifa ikiwemo ile ya Etoile du Sahel ya Tunisia kuomba kuongezewa muda wa kulipa deni la dola 300,000 wanazodaiwa na Simba kutokana na mauzo ya Okwi.
“Kweli nimepokea barua hizo, moja ni ile ambayo Etoile ambao mwezi huu ndiyo ulikuwa mwisho kulipa dola 300,000, sasa wameomba waongezewe muda hadi Septemba, mwaka huu ili waweze kulipa.
“Fifa wao wamenitumia kopi lakini barua hiyo ni kutoka kwao Etoile kwenda Fifa na wamethibitisha kwamba ni kweli Simba inawadai,” alisema Rage.
Barua ya tatu kati ya hizo kwa mujibu wa Rage ni ile ambayo inaonyesha namna klabu hiyo ya Tunisia ilivyomshitaki Okwi kwa Fifa kutokana na kuonyesha kukiuka mambo kadhaa wakati akijua mkataba wake nao unamalizika mwaka 2016.
“Katika ile barua ya kuhusiana na suala la kulipa, Fifa wametaka tusaini na kukubali kwamba sasa mwisho utakuwa Septemba 30 na tayari barua hiyo nimeikabidhi kwa Hans Pope,” aliongeza Rage.
Tayari Okwi yuko nchini na Yanga imemsajili ingawa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeamua kusimamisha usajili wake hadi litakapopata ufafanuzi kuhusiana na usajili wake.
Wakati Fifa ilitoa kibali kwa Okwi kucheza SC Villa ya Uganda kwa miezi sita, lakini Yanga ikamnunua na kuingia naye mkataba wa miaka miwili, suala ambalo limezua mzozo mkubwa huku Simba wakiendelea kusisitiza kulipwa fedha zao ambazo mwanzo walimuuza na hawakulipwa. 
Okwi amekuwa akisisitiza kwamba anataka kuichezea Yanga ambayo imemsajili, huku akieleza amekuwa akiumia moyoni kuona wenzake wakicheza naye akiwa jukwaani kama mtazamaji.
SOURCE: CHAMPIONI

KOCHA TWIGA STAR ASEMA WAPO VIZURI VS ZAMBIA

Kocha Mkuu wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage amesema kikosi chake kiko tayari kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Zambia itakayochezwa keshokutwa (Ijumaa) jijini Lusaka.
Akizungumza kwenye hafla ya kuiaga timu hiyo iliyofanyika leo (Februari 12 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF jijini Dar es Salaam, Kocha Kaijage amesema wachezaji wake wako vizuri, ingawa hakuwa tayari kutoa ahadi kuhusu matokeo.
“Vijana wako vizuri, lakini sitaki kutoa ahadi. Watanzania watuombee, watuunge mkono ili tuweze kufanya vizuri,” amesema Kocha Kaijage katika hafla hiyo ambayo mgeni rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi.
Twiga Stars inaondoka na kikosi cha wachezaji 19 na benchi la ufundi lenye watu watano kwa ndege ya Fastjet kwa ajili ya mechi hiyo itakayooanza saa 9 kamili kwa saa za Zambia. Msafara wa timu hiyo unaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Wachezaji waliopo kwenye kikosi hicho chini ya nahodha Sophia Mwasikili ni Amina Ali, Anastazia Katunzi, Asha Rashid, Donisia Minja, Esther Chabruma, Etoe Mlenzi, Everine Sekikubo, Fatuma Issa, Fatuma Makusanya, Fatuma Mwisendi, Fatuma Omari, Happiness Mwaipata, Maimuna Mkane, Mwapewa Mtumwa, Sherida Boniface, Therese Yona, Vumilia Maarifa na Zena Said.
Wakati huo huo, timu ya Azam imeondoka leo alfajiri (Februari 12 mwaka huu) kwenda Beira, Msumbiji kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi Ferroviario da Beira itakayochezwa Jumamosi. Msafara wa timu hiyo unaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, James Mhagama.

Naye mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Nassib Ramadhan ataongoza msafara wa timu ya Yanga inayoondoka kesho mchana kwenda Comoro kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Komorozine itakayochezwa Jumamosi.

Wednesday, February 12, 2014

REAL MADRID KUISUBIRI MSHINDI KATI YA REAL SOCIEDAD v BARCELONA LEO:

Nyota Mahiri Duniani Cristiano Ronaldo Jana Usiku Aliiwezesha Real Madrid kutingaFainali ya Copa del Rey baada ya kuibwaga Atletico Madrid  kwenye Mechi ya Marudiano ya Nusu Fainali iliyochezwa Estadio Vicente Calderon.
Penati hizo za Ronaldo zilipatikana katika Dakika ya 7 na 16 na kuwabwaga nje Atletico Madrid ambao ndio walikuwa Mabingwa Wateteza wa Kombe hili.
hivyo basi Real wametinga Fainali kwa Jumla ya Bao 5-0 baada kushinda Mechi ya Kwanza 3-0 huko Santiago Bernabeu Wiki iliyopita.
Kwenye Fainali Real itacheza na Mshindi wa Leo kati ya Real Sociedad na Barcelona ambao wanarudiana huko Estadio Anoeta huku Barcelona wako mbele kwa Bao 2-0 walizopata huko Nou Camp Wiki iliyopita.
COPA_DEL_REY-FP
COPA del REY
NUSU FAINALI
[Saa za Bongo]
Marudiano
Jumanne Februari 11
Atletico de Madrid 0 Real Madrid CF 2 [0-5] [Estadio Vicente Calderon]
Jumatano Februari 12
24:00 Real Sociedad v FC Barcelona [0-2] [Estadio Anoeta]
FAINALI
Aprili 19
Real Madrid v Real Sociedad/Barcelona

KAZI IPO LEO ARSENAL VS MAN UNITED-UWANJANI EMIRATES

Jumatano Februari 12

2245 Arsenal v Man United

2245 Everton v Crystal Palace

2245 Man City v Sunderland

2245 Newcastle v Tottenham

2245 Stoke v Swansea

2300 Fulham v Liverpool

MSIMAMO:

NA TIMU P W D L F A PTS GD
1 Chelsea FC 26 17 6 3 48 21 27 57
2 Arsenal FC 25 17 4 4 48 26 22 55
3 Man City 25 17 3 5 68 27 41 54
4 Liverpool 25 15 5 5 63 30 33 50
5 Tottenham 25 14 5 6 32 32 0 47
6 Everton FC 25 12 9 4 37 26 11 45
7 Man United 25 12 5 8 41 31 10 41
8 Southampton 26 10 9 7 37 29 8 39
9 Newcastle 25 11 4 10 32 34 -2 37
10 Swansea 25 7 6 12 32 35 -3 27
11 Hull City 26 7 6 13 25 31 -6 27
12 West Ham 26 7 7 12 28 33 -5 28
13 Aston Villa 26 7 7 12 27 36 -9 28
14 Stoke City 25 6 8 11 26 40 -14 26
15 Crystal Palace 25 8 2 15 18 34 -16 26
16 Norwich City 26 6 7 13 19 39 -20 25
17 West Brom 26 4 12 10 30 38 -8 24
18 Sunderland 25 6 6 13 25 38 -13 24
19 Cardiff City 26 5 7 14 19 44 -25 22
20 Fulham FC 25 6 2 17 24 55 -31 20

RATIBA MECHI ZIJAZO:

Jumamosi Februari 22

1545 Chelsea v Everton

1800 Arsenal v Sunderland

1800 Cardiff v Hull

1800 Man City v Stoke

1800 West Brom v Fulham

1800 West Ham v Southampton

2030 Crystal Palace v Man United

Jumapili Februari 23

1630 Liverpool v Swansea

1630 Newcastle v Aston Villa

1900 Norwich v Tottenham

RIPOTI YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA WAKAZI WA PWANI UKANDA WA PWANI WATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI:


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI 
         MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Simu: 255 22 2460735/2460706
FAKSI: 255 22 2460735/2460700
Barua pepe: met@meteo.go.tz
Tovuti: Tanzania Meteorological Agency - Admin -

S.L.P. 3056
DAR ES SALAAM
Unapojibu tafadhali nakili:
Kumb. Na.: TMA/1622

10 Februari, 2014

Taarifa kwa Umma: Matarajio ya kuwa naVipindi vya Mvua kubwa, Upepo Mkali na Mawimbi Makubwa.
Taarifa Na.
201402-01
Muda wa Kutolewa: Saa za Afrika Mashariki
Saa 11 Jioni
Daraja la Taarifa:
Tahadhari
Kuanzia: Tarehe
11 Februari, 2014
Mpaka: Tarehe
13 Februari, 2014
Aina ya Tukio Linalotarajiwa
1. Vipindi vya mvua kubwa (zaidi ya mm 50 ndani ya saa 24)
2. Hali ya Upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa
pamoja na mawimbi makubwa zaidi ya mita 2.0
Kiwango cha uhakika:
Wastani (60%)
Maeneo yanayotarajiwa
kuathirika
1. Vipindi vya Mvua Kubwa: Ukanda wa pwani mikoa ya Tanga,
Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara pamoja na visiwa vya
Unguja na Pemba, Mbeya , Njombe, Ruvuma pamoja na kusini
mwa mkoa wa Morogoro
2. Upepo Mkali na Mawimbi Makubwa: Pwani ya mikoa ya Tanga,
Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba
Maelezo:
Hali hii inatokana na kuwepo kwa kimbunga “FOBANE” kusini
magharibi mwa Bahari ya Hindi. Mfumo huu unatarajiwa kuvuta upepo kutoka Pwani ya Somalia na misitu ya Congo kuelekea maeneo ya nchi yetu.
Angalizo:
Watumiaji wa bahari na wakazi wa maeneo hatarishi wanashauriwa kuchukua tahadhari.
Maelezo ya Ziada
Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa
mrejeo pale itakapobidi