Friday, February 14, 2014

CHAMAZI NDIO HABARI YA MJINI-YANGA YAKUBALI KUWEKA KAMBI"

Dimba la Uwanja wa Azam Complex Chamazi
Yanga SC Kupitia Uongozi wake umetanabisha kuwa upo tayari kuweka kambi Chamazi kufuatia ofa waliyoitoa Azam ya kuwataka wakaweke kambi maeneo hayo kwa ajili ya kujiweka sawa na mchezo wa raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly ya Misri.
KAama unakumbuka wiki iliyopita uongozi wa Azam FC ulikataa ombi la Al Ahly kuweka kambi kwenye eneo lao hilo wakati watakapokuja nchini kucheza dhidi ya Yanga katika hatua hiyo baada ya kufanikiwa kuitoa Komorozine ya morroco.
Wachezaji Wa Yanga Wakiwa Katika Swimming Pool
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Bin Kleb amesema hawawezi kuiachia ofa kama hiyo kwa kuwa mtazamo wao ni kuona wanafanikiwa kufanya vizuri katika mechi hiyo.
"Katika hali ya kawaida hakuna mtu anaeweza kukataa ofa kama hiyo, iwapo Azam wameamua kutusaidia sisi tupo tayari ila tunamsikiliza upande wa benchi la ufundi kupitia Kocha Mkuu mwalimu Hans Van Pluijm anahitaji kambi ya aina gani ili kuweza kujiandaa.
"Hata hivyo Bin Kleb amesema Kocha ndiye anayejua aina ya timu anayotarajia kukutana nayo, hivyo uongozi unamwachia kila kitu na yeye ndiye atakayetoa maamuzi.

TFF YAWATAKA WANACHAMA WAKE KUFAVYA MAREKEBISHO YA KATIBA KABLA YA MACHI 20

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeamuru wanachama wake wote kufanya marekebisho ya katiba zao kabla ya Machi 20, mwaka huu, hivyo kutengua tarehe ya mkutano mkuu wa Simba.

Simba iliyo chini ya mwenyekiti wake, Ismail Aden Rage, ilipanga kufanya mkutano wake huo Machi 23, mwaka huu kwa ajenda moja ya marekebisho ya katiba yao ambapo sasa imeamua kufanya mkutano huo mapema, Machi 16 ili kwenda sawa na maagizo ya TFF.
Ofisa Habari wa Simba, Asha Muhaji alisema kuwa walitumiwa barua ya maagizo hayo na TFF wiki hii na hivyo wameamua kuurudisha nyuma ili marekebisho hayo yafanyike kabla ya Machi 20.
“Mkutano wa marekebisho hautafanyika tena Machi 23 kama wanachama na wadau wote wa Simba walivyokuwa wakifahamu, tumepata barua kutoka TFF inayotuelekeza kufanya mkutano huo kabla ya Machi 20, hivyo sasa mkutano utakuwa Machi 16.

NAPE ATOFAUTIANA NA JAJI WARIOBA BUNGE LA KATIBA.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema Bunge Maalumu la Katiba, litatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na si mawazo ya mtu yeyote.
Kauli hiyo ya Nape imekuja siku moja baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba kusema kuwa litakuwa jambo lisilo la kawaida kwa Bunge hilo kubadili hoja ya msingi iliyopo kwenye Rasimu ya Katiba, akisisitiza kuwa jukumu lake ni kuifanyia marekebisho.
Warioba alisema hayo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), kuhusu tafakuri na maridhiano kuelekea katika Katiba Mpya.
Alisema kama Bunge Maalumu la Katiba likipewa jukumu la kuandika Katiba linaweza kubadili mambo mengi, lakini kama Katiba itakuwa imeandaliwa na chombo kingine, Bunge hilo linatakiwa kutobadili hoja za msingi.
Akizungumza na gazeti hili jana, Nape alisema: “Mchakato wote wa Katiba Mpya unasimamiwa na sheria na sio maneno ya Warioba. Sheria inazungumzia haki, wajibu na mamlaka ya Bunge hilo, hivyo inawezekana kabisa kuboreshwa na hata kubadilishwa kwa hoja.”
Nape alisema kulingana na sheria hiyo, Bunge hilo lina mamlaka ya kufanya jambo lolote katika Rasimu hiyo, ikiwa ni pamoja na kuifanyia maboresho kadri itakavyoonekana kuwa inafaa.
“Bunge haliwezi kutishwa na mtu yeyote kwa sababu lipo kwa ajili ya kuwawakilisha wananchi. Ndiyo maana baada ya Bunge hilo kwisha wananchi watapiga kura ya maoni,” alisema.
Akitolea ufafanuzi kauli ya Jaji Warioba kwamba Bunge hilo lifanye maboresho na si kubadili hoja za msingi, Nape alisema: “Maboresho maana yake ni kubadili. Ukiwa na nyumba ya vyumba vinne na kuiboresha kwa kuweka chumba kimoja si umeibadili?”
Alisema Bunge hilo linatakiwa lisiingiliwe katika uamuzi wake.
Chanzo:Mwananchi".

DALADALA DAR ZATANGAZA MGOGORO NA SUMASTA.

    
Wamiliki wa daladala wametangaza mgogoro na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini nchini (Sumatra) wakipinga kile walichokiita upendeleo unaodaiwa kufanywa na Sumatra kwa mabasi ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda) na kuzikandamiza daladala katika utaratibu wa utoaji huduma ya usafiri jijini humo.
Wamedai upendeleo huo, mbali ya kuzikandamiza daladala, pia umekuwa ukiwanyonya wananchi kimapato, ambao wamekuwa wakijikuta wakilazimika kulipa nauli mara mbili (Sh. 800 na kuendelea) kwenye ruti, ambayo nauli yake halali ni Sh. 400.

Tamko la wamiliki hao lilitolewa kwa pamoja na Chama cha Wamiliki wa Daladala Mkoa (Darcoboa) na Umoja wa Wasafirishaji Abiria Dar es Salaam (Uwadar), kupitia viongozi wao wakuu, jana.
Mwenyekiti wa Darcoboa, Sabri Mabrouk, alisema mabasi ya Uda hayajapangiwa ruti kama ilivyo kwa daladala, na pia kuna habari kwamba, kuanzia wiki ijayo yataruhusiwa kuweka vibao vinavyoonyesha ruti yanakokwenda na hivyo kuwa na haki ya kwenda sehemu yanakotaka.
Alisema zaidi ya hivyo juzi mabasi hayo yaliruhusiwa peke yake kuchukua abiria kutoka kituo cha Mnazi Mmoja kwenda Kivukoni, huku daladala za Kivukoni zikitakiwa kuishia Mnazi Mmoja.

Alisema kama mabasi ya Uda yataendelea kupeleka abiria Kivukoni ifikapo Jumatatu wiki ijayo, daladala nazo pia zitafanya hivyo.

“Hili ni tangazo kwa madereva wetu wa daladala zinazokwenda Kivukoni. Tunawaambia wakiona Uda wanapeleka mabasi yao Kivukoni, nao pia wapeleke magari yote Kivukoni… Katika hili tunawaambia trafiki wasiingilie ugomvi huu.

Sisi tunadai haki za wanachama wetu kwa sababu haki haiombwi ikibidi inadaiwa kwa nguvu,” alisema Mabrouk.

Mabrouk alisema kimsingi hawana ugomvi na Uda kama ambavyo hawana haki ya kuwazuia kuingiza mabasi, lakini akasema wanachokitaka ni kuwapo na uwanja sawa katika utoaji wa huduma ya usafiri Dar es Salaam.


Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simon Group inayomiliki mabasi ya Uda, Robert Kisena, alipoulizwa kuhusiana na madai hayo, alisema wameshajipanga kwa hilo.
Alisema kuanzia wiki ijayo wataanza kutoa huduma ya usafiri jijini kwa kuzingatia ruti na kwamba, hakutakuwa na kuingiliana katika ruti.

“Haya siyo masuala ya kugombana, ni masuala ya kukaa na kuangalia tufanye vipi,” alisema Kisena. 
 Na:mwamdishi wetu Dar

KIA WAJIPANGA KUKABILIANA NA DAWA ZA KULEVYA

                                                       Uwanja cha Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)
Uongozi wa Uwanja cha Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), umeahidi kuongeza jitihada za kupambana na usafirishaji wa dawa za kulevya kutokana maboresho yaliyofanyika katika kitengo cha usalama cha uwanja huo.

Tamko hilo limekuja siku chache baada ya Mtanzania Mastura Makongoro, mwenye hati ya kusafiria namba AB26695, kukamatwa na dawa za kulevya zinazodhaniwa kuwa ni aina ya cocaine zenye uzito wa kilo 4.8 akielekea nchini Ghana.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Fedha na Huduma za Kibiashara wa Kampuni ya Uendelezaji Viwanja (Kadco), Bakari Murusuri, ilisema uwanja huo umejidhatiti kupambana na usafarishaji wa dawa za kulevya kupitia hapo.

Murusuri alisema maofisa usalama wa uwanja huo Jumanne usiku wa manane  wiki hii, walimkamata mwanamke huyo wakati akisubiri kupanda ndege ya Shirikia la Ethiopia kuelekea Addis Ababa.

“Mizigo yote ya abiria imekuwa ikichunguzwa kwa umakini mkubwa katika sehemu ya kuchunguza mizigo na safari hii tumefanikiwa mzigo mmoja uligundulika kuwa na shaka na vitu vilivyokuwa ndani kwa kuonyesha dalili ya kuwa ni dawa za kulevya," alisema.

Aliongeza: “Baada ya kuuchunguza mzigo huo kwa umakini, iligundulika ulikuwa na dawa za kulevya ambazo zilifungwa juu na chini kabisa ya begi lake yenye uzito wa kilo 4.8.”

Alisema wakati wa uchunguzi, mwanamke huyo alikiri kuwa aliambatana na mwenzake raia wa Nigeria aliyemtaja kwa jina la Mike Nwankwo (41), ambaye alimsindikiza mpaka uwanjani na alikuwa ni miongoni mwa mtandao wa wasafirishaji wa dawa hizo.

“Jeshi la Polisi na walinzi wa usalama hapa uwanjani waliunganisha nguvu ili kumsaka mtu huyo na baadaye alikutwa kwenye maegesho ya magari akisubiri kuhakikisha kuwa mwanamke huyo ameondoka nchini,” aliongeza.

Murusuri alisema tangu Machi, 2013 mpaka sasa, uwanja huo wa ndege umefanikiwa kukamata watu tisa wakihusishwa na usafirishaji wa dawa za kulevya na kuahidi kuwa uwanja huo sasa umejipanga kikamilifu kukabiliana na suala hilo.

“Tumeongeza ulinzi wa kutosha hapa KIA ili kuondoa mianya katika taratibu za kiusalama kwa upande wa mizigo na uchunguzi kwa ujumla.
Hili litatuwezesha kuhakikisha kuwa uwanja wetu wa ndege hauwi kitovu cha usafirishaji dawa za kulevya,” aliongeza.
Chanzo: Nipashe'.

Thursday, February 13, 2014

ENGLAND YAPOROMOKA VIWANGO VYA FIFA VS SPAIN 1

FIFA_LOGO_BESTShirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA leo limetoa Listi ya Ubora Duniani  huku Nchi 3 za Juu, Spain, Germany na Argentina, bado ziko pale pale na Portugal kupanda nafasi moja na kukamata Nambari ya 4 huku Tanzania ikipanda Nafasi mbili na kushika Nafasi ya 116.
Brazil, Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia hapo Juni, wamekwea Nafasi moja hadi Nafasi ya 9 lakini England imezidi kuporomoka na safari hii imeanguka Nafasi mbili na kuwa wa 15.
Nchi ya Afrika ambayo iko Juu kabisa ni Ivory Coast ambayo iko Nafasi ya 23 baada ya kuanguka Nafasi 6.
Listi nyingine ya Ubora itatolewa hapo Machi 13.
20 BORA:
1. Spain
2. Germany
3. Argentina
4. Portugal (+1)
5. Colombia (-1)
6. Switzerland (+2)
7. Uruguay (-1)
8. Italy (-1)
9. Brazil (+1)
10. Netherlands (-1)
11. Belgium
12. Greece
13. United States (+1)
14. Chile (+1)
15. England (-2)
16. Croatie
17. Bosnia-Herzegovina (+2)
18. Ukraine
18. France (+2)
20. Denmark (+5)

JESHI LA POLISI MKOANI SINGIDA LANASA PEMBE ZA NDOVU

Jeshi la polisi mkoani SINGIDA limekamata vipande 21 vya meno ya Tembo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 43.


Nyara hizo za serikali zimekamatwa katika  kijiji cha MWAMAGEMBE  wilayania MANYONI  zikisafirishwa kwenda ITIGI mkoani SINGIDA.



Vitendo vya ujangili vimeendelea kukithiri nchini ambapo Jeshi la POLISI Mkoani SINGIDA limemtia mbaroni  GEORGE JAMES kwa tuhuma za kukutwa na meno ya TEMBO yakiwa yamehifadhiwa katika mabegi mawili ya kusafiria.


Mtuhumiwa huyo alikamatwa katika kizuizi cha idara ya maliasili kilichoko katika kijiji UKIMBU ,kata ya MGANDU wilayania MANYONI akiwa katika gari aina ya TOYOTA HIACE lenye namba za usajili T797CQL akiwa amehifadhi men o hayo katika mabegi ya nguo.


Kamanda wa polisi mkoa wa SINGIDA ,GEOFREY KAMWELA amesema vipande hivyo 21 vina thmani ya zaidi ya shilingi milioni 43 na vyote vimehifadhiwa katika kituo cha polisi wilayani ITIGI.


vitendo vya ujangili wilayani MANYONI vimekuwa vikiongezeka ambapo mwaka 2013 askari mmoja wa jeshi  polisi alipoteza maisha katika mapambano na majangili wilayani humo.