Mechi
nyingine ya tiketi za elektroniki siku hiyo itachezwa Uwanja wa Kaitaba
mjini Bukoba kwa kuzikutanisha timu za Kagera Sugar na Geita Gold SC ya
mkoani Geita. Geita Gold iko Daraja la Kwanza
Kabla
ya mechi hizo, Ijumaa (Agosti 29 mwaka huu) saa 3 asubuhi kwenye
viwanja hivyo kutakuwa na mafunzo ya matumizi ya tiketi za elektroniki
pamoja na jinsi mfumo huo unavyofanya kazi.
Washiriki
wa mafunzo hayo ni wasimamizi wa vituo vya Tanga na Bukoba, viongozi wa
vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Kagera (KRFA) na Tanga (TRFA),
makatibu na maofisa habari wa klabu za Kagera Sugar, Mgambo Shooting,
African Sports na Geita Gold, mameneja wa viwanja vya Kaitaba na
Mkwakwani na wasaidizi wao, maofisa usalama wa TRFA na KRFA, wachanaji
tiketi, wasimamizi wa milangoni, wasaidizi (stewards) na waandishi wa
habari.
Thursday, August 28, 2014
RAIS TFF KUTUA MANYARA, KILIMANJARO, ARUSHA
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atatembelea mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara.
Katika
ziara hiyo atakutana na viongozi na kuangalia hali hali ya mpira wa
miguu katika mikoa hiyo na mahitaji yake. Pia atazungumzia maono
(vision) ya TFF katika mpira wa miguu.
Rais
Malinzi atawasili mkoani Manyara, Agosti 29 mwaka huu, na ataanza ziara
rasmi katika mkoa huo Agosti 30 mwaka huu. Agosti 31 mwaka huu atakuwa
Arusha, na kumalizia Septemba 1 mkoani Kilimanjaro.
Katika
ziara hiyo, Rais Malinzi atafuatana na Mkurugenzi Msaidizi (Wanachama)
wa TFF, Eliud Mvella. Pia Septemba 8 mwaka huu, Rais Malinzi ataanza
ziara ya mikoa ya Iringa, Mbeya na Njombe.
Wednesday, August 27, 2014
SIMBA YAMUWEKA KUNDINI MUSOTI AMPIGA BAO BUTOYI OKWI JE.
Rais
wa Simba, Evans Aveva amemaliza utata wa usajili wa wachezaji wa kigeni
uliokuwa umeigubika klabu hiyo kwa kusema Mkenya Donald Mosoti ndiye anabaki na Mrundi Butoyi
Hussein wamempiga chini huku Yanga nao wakimpiga chini Emmanuel Okwi raia wa
Uganda.
Simba
na Yanga zimelazimika kufanya uamuzi mgumu wa kupunguza idadi ya wachezaji wa
kigeni ambao wamezidi katika klabu zao kwa sababu usajili wa wachezaji katika
klabu za Ligi Kuu Bara unamalizika leo saa 6 usiku.
Mrundi huyo alimvutia Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia
Hans Poppe akiichezea Telecom ya Djibouti katika Klabu Bingwa Afrika Mashariki
na Kati, Kombe la Kagame mjini Kigali, Rwanda mwezi huu.
Maana yake wachezaji wa kigeni katika kikosi cha Simba SC watakuwa mabeki
Mganda Joseph Owino, Mkenya Mosoti, Warundi kiungo Pierre Kwizera, mshambuliaji
Amisi Tambwe na Mkenya Mkenya Paul Kiongera.
Kwa
upande wa Yanga ambapo nayo ilikuwa na wachezaji sita wa kigeni ambapo awali
Hamis Kiiza ambaye ni raia wa Uganda
ndiye aliyekuwa anadaiwa kuachwa, lakini habari za ndani kutoka katika klabu ya
Yanga zinasema panga limemwangukia Emmanueli Okwi ambaye hadi jana asubuhi
alikuwa hajajiunga na timu.
SIMBA YAIFUMUA MAFUNZO 2-0 MECHI YA KIRAFIKI
Kikosi
cha Simba SC kilikuwa; Ivo Mapunda/Hussein Sharrif ‘Cassilas’ dk80,
Miraj Adam/William Lucian ‘Gallas’ dk80, Issa Rashid ‘Baba
Ubaya’/Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ dk80, Joram Mgeveke/Donald Mosoti
dk80, Joseph Owino/Hussein Butoyi dk80, Pierre Kwizera/Said Ndemla dk42,
Haroun Chanongo/Uhuru Suleiman dk80, Amri Kiemba/Abdallah Seseme dk65,
Amisi Tambwe/Elias Maguri dk46, Shaaban Kisiga ‘Malone’/Ibrahim Hajibu dk80 na Ramadhani Singano ‘Messi’/Twaha Ibrahim.
AZAM FC KESHO YATARAJI KUANZA TIZI ZA VPL YA SEPT 20
Akizungumza na mkali wa dimba tz.blogspot.com afisa habari wa timu hiyo jaffari iddi maganga amesema kuwa wachezaji wote wataanza mazoezi kesho, kasoro wale ambao wameitwa timu ya taifa.
Maganga amesema kwamba wachezaji
wawili, Aishi Manula na Kevin Friday japokuwa hawapo kwenye kikosi cha Taifa
Stars, wao wamepewa mapumziko zaidi- hivyo si lazima waanze kesho.

Aidha Maganga amesema kwamba Simba
SC waliomba mchezo wa kirafiki na wao wikiendi hii, lakini imeshindikana kwa
sababu kocha Joseph Marius Omog amesema hawezi kuwa na mechi baada ya mazoezi
ya siku mbili.
Mwalimu
amesema mchezo wanaotaka Simba SC labda wiki ijayo, kwa sababu hawezi kufanya
mazoezi Alhamsi na Ijumaa halafu baada ya hapo awe na mechi ngumu.
Mcamreoon huyo ambaye aliipatia azam
Ubingwa msimu uliopita hivi karibuni ameifikisha Azam FC Robo Fainali ya Kombe
la Kagame mjini Kigali kabla ya kutolewa na El Merreikh ya Sudan, iliyoibuka
bingwa wa michuano hiyo mwaka huu.
|
MOROCCO YAIPOTEZEA TAIFA STAR MECHI YA KIRAFIKI YA FIFA.

Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa amesema Morocco imejitoa kwa sababu imesema haitaweza kuwapata wachezaji wake wa kimataifa.
Mwesigwa amesema sasa Taifa Stars itacheza na Burundi mjini Bujumbura siku hiyo hiyo. Kocha Mholanzi, Mart Nooij, tayari ameita kikosi cha wachezaji 26 kwa ajili ya mchezo huo.
Hao
ni makipa; Deogratias Munishi (Yanga) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni Said
Morad (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Shomari Kapombe (Azam), Nadir Haroub
(Yanga), Kelvin Yondani (Yanga SC), Aggrey Morris (Azam), Joram Mgeveke (Simba)
na Charles Edward (Yanga).
Viungo; Erasto Nyoni (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Amri Kiemba (Simba), Himid Mao (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Ndemla (Simba), Said Juma (Yanga) na Haruna Chanongo (Simba).
Washambuliaji; John Bocco (Azam), Khamis Mcha (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Yanga), Mwegane Yeya (Mbeya City) na Juma Liuzio 9ZESCO, Zambia).
Kikosi hicho kinatarajiwa kuingia kambini Jumapili (Agosti 31 mwaka huu) mchana katika hoteli ya Accomondia mjini Dar es Salaam na kitakuwa kikifanya mazoezi Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
ETO'O RASMI NA EVARTON,ASAINI MKATABA WA MIAKA

Klabu ya Everton imekamilisha usajili wa mchezaji wa kimataifa wa Cameroon Samuel Eto'o.
Mshambuliaji huyo mzoefu amesaini kandarasi ya miaka miwili katika hiyo ya Goodison Park, baada ya kuitumika msimu uliopita katika klabu ya Chelsea.
QPR na majirani zao Liverpool walikuwa pia na mawazo ya kumsajili Eto'o, ambaye anaweza kupatikana katika mchezo wa Premier League siku ya Jumamosi kati yake ya Everton na timu yake ya zamani Chelsea katika uwanja wa Goodison Park.
Subscribe to:
Posts (Atom)