Monday, September 15, 2014

MINZIRO ASEMA TUNAWAKATI MGUMU LIGI KUU LAKINI TUTAPAMBANA TU" WACHEZAJI 7 NJE

Maafande wa Jkt Ruvu kutoka kibaha mkoani pwani kushuka kitaanza Ligi Kuu Bara bila ya wanandinga wake saba wa kikosi cha kwanza.
Kocha Mkuu wa JKT Ruvu, Felix Minziro, amethibitisha kutokuwepo kwa wachezaji hao ambao wamekwenda kushiriki michuano ya Majeshi ya Afrika Mashariki iliyokuwa ikifanyika mjini Zanzibar.
Wachezaji wangu takribani saba wa kikosi cha kwanza, hawapo kwa sasa, hili linanipa wakati mgumu sana.
Minziro amesema ligi inaanza siku ya Jumamosi, uwepo wao una mchango mkubwa katika timu na wako Msumbiji kwa sasa kulitumikia jeshi katika masuala la michezo.

KAMATI YA SHERIA YAPITISHA USAJILI KLAB ZA VPL NA FDL MSIMU 2014

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imepitisha usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza huku wenye kasoro ndogondogo klabu zao zikitakiwa kuziondoa ili waweze kupatia leseni za kucheza ligi msimu huu wa 2014/2015.
Kasoro hizo ni kufikia makubaliano na klabu ambazo wachezaji husika wametoka, kuwafanyia uhamisho (transfer) na kulipa ada za uhamisho. Kamati vilevile ilibaini wachezaji wengi hawakufanyiwa uhamisho kama kanuni za ligi hizo zinavyoelekeza.
Hivyo, klabu ambazo hazitakuwa zimeondoa kasoro hizo kwa wachezaji wao leseni zao zitazuiliwa mpaka watakapokuwa wamekamilisha kila kitu. Ni wachezaji wenye leseni tu ndiyo watakaoruhusiwa kucheza mechi za ligi.

Klabu za African Lyon, African Sports, Ashanti United, Coastal Union, Kiluvya United, Majimaji, Mji Mkuu, Polisi Dodoma, Polisi Morogoro, Red Coast na Stand United ziliwawekea pingamizi wachezaji mbalimbali kwa kutofanyiwa uhamisho.
Kuhusu Ike Bright Obina wa Nigeria aliyewekewa pingamizi na African Lyon dhidi ya Coastal Union, Kamati imezitaka klabu hizo kufikia makubaliano, na zikishindwa mchezaji huyo atabaki African Lyon.

Kamati vilevile ilijadili malalamiko ya Kocha wa zamani wa Simba, Zdravko Logarusic dhidi ya klabu hiyo, na kuzipa pande hizo mbili siku 14 kufikia muafaka juu ya malalamiko hayo, na zikishindwa ndipo zirejee tena mbele ya Kamati.
Logarusic aliyewakilishwa na mwanasheria wake Dickson Sanga anailalamikia klabu hiyo kwa kuvunja mkataba kinyume cha taratibu, hivyo kutaka Simba imlipe dola 6,000 kwa kuvunja mkataba, na pia kulipa dola 50,000 ikiwa ni fidia maalumu ya madhara yaliyotokana na uvunjwaji huo.
BONIFACE WAMBURA
KNY KATIBU MKUU
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Friday, September 12, 2014

MCHEZO WA KIRAFIKI WA KIMATAIFA MBEYA CITY VS VIPERS FC

Jumamosi hii kwenye uwanja wa Sokoine  kutakuwa na mchezo wa kirafiki kati ya Mbeya City Fc na Vipers FC (Zamani Bunamwaya Fc)ya Uganda . 

Mchezo huo unamepangwa kuanza saa       10:00. 

Vipers Fc inatarajiwa kuwasili Mbeya jioni ya leo ikitokea Entebbe kupitia  Dar Es Salaam ambapo Kiingilio kitakuwa Sh.3000
Hii ikiwa ni mabadiliko kutoka kiingilio  kilichotangazwa  awali cha sh.  5000

DISMAS  TEN
OFISA HABARI
MBEYA CITY COUNCIL FC.

Thursday, September 11, 2014

TAZAMA WASHINDI WA LIGI KUU TZ BARA TANGU MWAKA 1965-HADI LEO

Hawa ni washindi wa Ligi Kuu Tanzania Bara tangu mwaka 1965. Katika rekodi hii klabu ya Yanga imetwaa taji hilo mara 24, Simba mara 18 na mtibwa mara 2, nyingine zote zilizopoa hapa zimetwaa mara moja. Tarehe 20 ligi itaanza tena ya msimu wa 2014/15, Je Unadhani timu gani ipo katika nafasi ya kushinda taji hilo msimu huu?
Washindi wa Ligi Kuu Tanzania Bara Tangu 1965 hadi leo
    1965 Sunderland (Sasa Simba SC)
    1966 Sunderland
    1967 Cosmopolitan
    1968 Yanga
    1969 Yanga
    1970 Yanga
    1971 Yanga
    1972 Yanga
    1973 Simba SC
    1974 Yanga
    1975 Mseto SC
    1976 Simba SC
    1977 Simba SC
    1978 Simba SC
    1979 Simba SC
    1980 Simba SC
    1981 Yanga
    1982 Pan Africans
    1983 Yanga
    1984 Simba SC
    1985 Yanga
    1986 Tukuyu Stars
    1987 Yanga
    1988 Coastal Union
    1989 Yanga
    1990 Simba SC
    1991 Yanga
    1992 Yanga
    1993 Yanga
    1994 Simba SC
    1995 Simba SC
    1996 Yanga
    1997 Yanga
    1998 Yanga
    1999 Mtibwa Sugar
    2000 Mtibwa Sugar
    2001 Simba SC
    2002 Yanga
    2003 Simba SC
    2004 Simba SC
    2005 Yanga
    2006 Yanga
    2007 Simba SC
    2007/08 Yanga
    2008/09 Yanga
    2009/2010 Simba SC
    2010/2011 Yanga
    2011/2012 Simba SC
    2012/2013 Yanga
    2013/2014 Azam FC
    2014/2015 ??.

WEKUNDU WA MSIMBAZI KUTIFUANA NA URA YA UGANDA

Simba Wekundu wa msimbazi SC kesho wanatarajia kushuka dimbani kuonyeshana kazi katika Mechi ya pili ya kimataifa ya kirafiki chini ya kocha Patrick Phiri dhidi ya timu ya mamlaka ya ukusanyaji wa mapato nchini Uganda, URA katika uwanja wa Taifa jijini Dar es slaam katika mtanange utakao anza majira ya saa 11:00 jioni kwa saa za Afrika mashariki.

Wakati huo huo jumamosi jioni, Simba itakuwa na mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Ndanda fc katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mk
oani Mtwara katika maadhimisho ya ‘Ndanda fc Day’.

TAREHE NDONI YA TAIFA 2014 2014 YAPIGWA KALENDA

Shirikisho la ngumi Tanzania (BFT) limesogeza tarehe ya kufanyika kwa mashindano ya ngumi ya Taifa na sasa yatafanyika kuanzia tarehe 03-08/11/2014.Dar es salaam.
Awali mashindano hayo yalikuwa yamepangwa kufanyika tarehe 08-14/10/2014 Dar es salaam.
Sababu za kusogeza mashindano hayo ni kuyapisha mashindano ya ngumi ya kimataifa yaliyoandaliwa na chama cha ngumi wilaya ya Temeke yanayotarajia kuanza kufanyika mwishoni mwa mwezi huu, lakini pia ni kutoa nafasi zaidi kwa mikoa ili kujiandaa vizuri na kufanya mashindano ya kuwapata wawakilishi wa mikoa yao katika mashindano ya taifa.
BFT tunawataki maandalizi mema na tunatoa wito kwa maafisa michezo wa mikoa yote ya Tanzania bara kuhakikisha wanaleta wachezaji kutoka katika mikoa yao ili kuleta upinzani utakaopelekea kupata timu ya taifa iliyo bora kutoka katika mikoa yote ya Tanzania bara.
Aidha BFT inawapongeza kampuni ya simu za mkononi ya Z         antel kwa udhamini wa mashindano hayo kwa kutoa kiasi cha Tsh. 10,000,000/=ambazo zitasaidia baadhi ya mahitaji ya msingi ya kufanikisha mashindano hayo.

MWAMBUSI ASEMA PHIRI, MAXIMO, ASEMA NGOMA DAKIKA 90.

KOCHA mkuu wa Mbeya City fc na kocha bora wa ligi kuu Tanzania bara msimu uliopita, Juma Mwambusi, amewakaribisha makocha Patrick Phiri wa Simba na Marcio Maximo wa Yanga.
Akizungumza na mtandao huu, Mwambusi amesema kocha Phiri ana historia ya kufundisha soka la Tanzania kwa ngazi ya klabu wakati Maximo amefundisha timu ya Taifa, lakini wote wataleta changamoto nzuri kwake.