Friday, November 28, 2014

GALATASARAY BAADA YA KUNTUPIA PRANDELLI SASA YAMCHUKUA HAMZAOGLU KUZIBA NAFASI.

KLABU kongwe jijini Instabul ya Galatasaray wanatarajia kumteua kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Uturuki Hamza Hamzaoglu kuwa meneja mpya wa klabu hiyo baada ya kutimuliwa kwa Muitaliano Cesare Prandelli. 
Klabu hiyo ilimtimua Prandelli baada ya kuitumikia chini ya nusu ya msimu kutokana na matokeo mabovu ambayo wamekuwa wakipata. 
Hamzaoglu amekuwa akiitumikia Uturuki chini ya kocha mkuu Fatih Terim toka mwaka 2013, na uamuzi wake huo umekuja baada ya kufanya mazungumzo na kocha huyo. 
Bodi ya klabu hiyo ilifikia uamuzi wa kumtimua Prandelli baada ya kutandikwa na Anderlecht kwa mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumatano usiku na kufuta matumaini yao ya kufuzu hatua ya mtoano. 
Prandelli alitua katika klabu hiyo Julai mwaka huu akichukua nafasi ya Muitaliano mwenzake Roberto Mancini na kupewa mkataba wa miaka miwili uliokuwa na thamani ya euro milioni 2.3.

DR SHEIN ASEMA KATIKA KUKUZA MPANGO WA UCHUMI NA KUONDOA UMASKINI ZANZIBAR SECTA YA UTALII NDIO SECTA YAKUUNGWA MKONO.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dokta, Ali Mohamed Shein amesema kuwa katika Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini Zanzibar (MKUZA), sekta ya utalii ndio sekta mama na nyegine zimekuwa zikiongeza nguvu hivyo inahitaji kuendelea kuungwa mkono ndani na nje ya nchi.
Dokta, Shein ameyasema hayo wakati alipofanya mazungumzo na Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada Jack Mugendi Zoka,  Ikulu mjini Zanzibar aliyefika kwa ajili ya kuaga kwenda katika kituo chake kipya cha kazi nchini humo  kufuatia uteuzi wa Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete hivi karibuni.
Katika maelezo yake Dokta Shein amemueleza Balozi huyo mpya wa Tanzania nchini Cadana kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imekuwa ikifanyaa juhudi za makusudi katika kuhakikisha sekta ya utalii inaimarika na inaendelea kuwa sekta mama na muhimu hapa nchini.
Akieleza juu ya sekta ya uwekezaji Dokta, Shein amemueleza Balozi Zoka kuwa mbali ya kutilia mkazo uwekezaji katika ujenzi wa mahoteli pia, Serikali imekuwa ikitilia mkazo uwekezaji katika Hospitali za kisasa za binafsi ambazo zinatibu maradhi maalum.

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU IMESEMA ITAENDELEA KUWAPATIA WANANCHI TAKWIMU SAHIHI ZINAZOHUSU SEKTA MBALIMBALI.

SERIKALI kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu imesema kuwa itaendelea kuwapatia wananchi takwimu sahihi zinazohusu sekta mbalimbali ili kuwajengea uwezo wa kushiriki katika ngazi za maamuzi na masuala mbalimbali nchini.
Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es salaam na Waziri wa Fedha wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  Omar Yussuf  Mzee wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yanaoongozwa na kauli mbiu isemayo Takwimu Huria kwa uwajibikaji na ushirikishwaji wa wadau wote.
Amesema upatikanaji wa taarifa na  takwimu sahihi kwa wananchi unaongeza ushiriki wao katika maamuzi na kuwajengea uwezo wa kutathmini utendaji wa Serikali katika masuala mbalimbali yakiwemo mapato na matumizi.
Amesema Ofisi ya Taifa ya Takwimu itaendelea kuhakikisha kuwa takwimu mbalimbali zinapatikana kwa urahisi kupitia mtandao, machapisho na mifumo rahisi ili kuwawezesha wananchi na wadau mbalimbali kuzipata pindi wanapozihitaji.

Thursday, November 27, 2014

FIFA YATOA LISTI YA UBORA DUNIANI TANZANIA YAPOROMOKA NAFASI 2 SAS YA 112.

SHIRIKISHO la soka Duniani FIFA Leo hii imetoa Listi ya Ubora Duniani na Mabingwa wa Dunia Germany wameendelea kushika Namba Moja huku Tanzania ikiporomoka Nafasi 2 na kukamata Nafasi ya 112.
Kulikuwa hamna mabadiliko yeyote ya Timu 7 za juu lakini England, iliyokuwa Nafasi ya 20, imepanda Nafasi 7 na sasa kukamata Nafasi ya 13.
Barani Afrika, Ageria imeendelea kuwa juu kabisa ikiwa Nafasi ya 18 baada kushuka Nafasi 3 ambapo Listi ya Ubora Duniani inayofuata itatolewa Tarehe 18 Desemba 2014.
20 BORA HII HAPA.
1.Germany               
2.Argentina   
3.Colombia    
4.Belgium      
5.Netherlands
6.Brazil
7.Portugal               
8.France
9.Spain          
10.Uruguay                
11.Italy           
12.Switzerland 
13.England                
14.Chile           
15.Romania                
16.Costa Rica  
17.Czech Republic      
18.Algeria       
19.Croatia       
20.Mexico

UONGOZI WA LIPULU FC YATUPIA VIRAGO BENCHI LA UFUNDI


Timu ya Lipuli FC ya Iringa kupitia uongozi wake umeamua kutitupilia virago benchi lake lote la ufundi kutokana na matokeo yasiyoridhisha ya timu yake katika Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
          
Mwenyekiti wa timu hiyo Abuu Changawa amesema wamefikia hatua hiyo baada ya timu yao kuwa na mwendo wa konokono katika ligi hiyo wakiwa nafasi ya tatu katika msimamo wa Kundi A.

Pamoja na kwamba wapo katika nafasi ya tatu kwenye         msimamo wa kundi letu, matokeo ya timu yetu hayaridhishi. Tumekuwa tukishinda 1-0 na kutoka sare ndiyo maana tumeaona tuachane na watendaji wote wa benchi la ufundi,” amesema Majeki.

Lipuli FC, aliyowahi kuifundisha Shadrack Nsajigwa (sasa kocha msaidizi Yanga), imekusanya pointi 21 katika mechi zote 11 za raundi ya kwanza ya FDL, pointi moja nyuma ya Friends Rangers walioko nafasi ya pili na tatu nyuma ya Majimaji FC wanaoshika usukani wa kundi hilo.

Aidha, Majeki amesema kuanzia Alhamisi wataanza msako wa kukamata watu wote wanaojihusisha na biashara haramu ya kutengeneza na kuuza jezi zenye nembo ya klabu yao kwa kuwa hadi sasa hakuna kampuni wala mtu aliyeidhinishwa kutengeneza na kuuza jezi zenye 

EMERSON AANZA TIZI LA KUJIUNGA NA YANGA CHINI YA MAXIMO.

Mbrazil, Emerson Roque ambae anacheza nafasi ya Kiungo leo ameanza kujifua katika kikosi cha Yanga.

Taarifa zilizopo Emerson atafanya majaribio kwa wiki mbili, ambapo leo imekuwa siku ya kwanza.
                 
Katika mazoezi hayo ya Yanga kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam kulikuwa na ulinzi mkali.

Emerson ambaye inaelezwa atachukua nafasi ya mshambuliaji, Jaja alionekana kama vile amezoeana na wachezaji wengine wa Yanga.


Pamoja naye, kiungo Coutinho na Kocha Marcio Maximo, nao walianza mazoezi yao kwa mara ya kwanza baada ya kurejea nchini, jana.

Wednesday, November 26, 2014

BARCA,MADRID,BAYERN YATAWALA ORODHA YA MABEKI FIFPRO WORD XI 2014


KLABU za Barcelona, Real Madrid na Bayern Munich zimetawala orodha ya mabeki wateule katika kikosi cha dunia cha FIFPro World XI 2014 chama cha wachezaji wakulipwa, baada majina 12 ya wachezaji wao kuingia katika orodha kati ya majina 20 yaliyoteuliwa.
Wachezaji wote wanne walioshinda nafasi ya kuwemo katika kikosi hicho mwaka jana wamejumuishwa wakiwemo Dani Alves, Philipp Lahm, Sergio Ramos na Thiago Silva. Leighton Baines, Ashley Cole, Dante na Nemanja Vidic ndio ambayo hayamo katika orodha hiyo ukilinganisha na ya mwaka jana. 
Kwa upande wa Madrid wamo Dani Carvajal, Pepe, Ramos, Raphael Varane na Marcelo wakati Barcelona wamo Jordi Alba, Alves, Javier Marscherano na Gerard Pique huku Bayern wakiwa na David Alaba, Lahm na Jerome Boateng. 
Mabeki wengine wnakamilisha orodha hiyo ni pamoja na David Luiz na Thiago Silva wa Paris Saint-Germain, Pablo Zabaleta na Vincent Kompany wa Manchester City, Branislav Ivanovic na Filipe Luis wa Chelsea, Diego Godin wa Atletico Madrid na Mats Hummels wa Borussia Dortmund. 
Majina manne ya washindi wa beki bora wa dunia yataamuliwa kwa kupiga kura miongoni mwa wachezaji ambapo zaidi ya wachezaji wa kulipwa 20,000 wanatarajiwa kushiriki zoezi hilo.