Tuesday, December 16, 2014

LIGI KUU VODACOM TZ BARA DIMBA DEC 26 TIMU KUUMANA DIMBANI

Timu zinazoshiriki ligi kuu vodacom tanzania bara kila moja tayari imekamilisha usajili ili kuimarisha vikiosi vyao kwa ajili ya Raundi ya nane ya ligi hiyo.
LIGI KUU VODACOM
RATIBA
Ijumaa Desemba 26
Simba v Kagera Sugar
Jumamosi Desemba 27
Mtibwa Sugar v Stand United               
Prisons v Coastal Union             
JKT Ruvu v Ruvu Shootings
Jumapili Desemba 28
Mbeya City v Ndanda FC            
Polisi Moro v Mgambo JKT          
Yanga v Azam FC   
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Mtibwa Sugar
7
4
3
0
10
3
7
15
2
Yanga
7
4
1
2
9
4
4
13
3
Azam FC
7
4
1
2
8
4
4
13
4
Coastal Union
7
3
2
2
8
6
2
11
5
Kagera Sugar
7
2
4
1
5
3
1
10
6
JKT Ruvu
7
3
1
3
7
7
0
10
7
Simba
7
1
6
0
7
6
1
9
8
Polisi Moro
7
3
2
2
6
7
-1
9
9
Mgambo JKT
7
3
0
4
4
7
-3
9
10
Stand United
7
2
3
2
5
9
-4
9
11
Ruvu Shooting
7
2
1
4
4
7
-3
7
12
Tanzania Prisons
7
1
3
3
5
6
-1
6
13
Ndanda FC
7
2
0
5
8
12
-4
6
14
Mbeya City
7
1
2
4
3
5
-2
5

SIMBA YAFUNGA USAJILI KWA KUMNASA BEKI WA MTIBWA HASSAN KESSY RAMADHANI

Wekundu wa Msimbazi Simba imetua nanga baada ya kufunga usajili wake wa dirisha dogo kwa kumsaini beki kijana wa kulia wa Mtibwa Sugar ya Morogoro, Hassan Ramadhani Kessy.
Kessy amesaini usiku huu Mkataba wa miezi 18 baada ya mvutano wa muda mrefu na klabu hiyo juu ya dau.
Zaidi ya mara tatu, Kessy alikwishakutana mezani na uongozi wa Simba SC bila kufikia maafikiano na baada ya mvutano huo uliodumu kwa takriban mwezi mzima, leo mambo yameisha.
Kaburu amesema kwamba baada ya kumpata Kessi wanadhani sasa kikosi chao kimekamilika na wanaelekeza nguvu zao katika maandalizi kwa ajili ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Kessy anakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Simba SC katika dirisha dogo, baada ya Waganda beki Juuko Murushid na washambuliaji Dan Sserunkuma na Simon Sserunkuma.
Murushid amesaini miaka mitatu, wakati akina Sserunkuma wamesaini miaka miwili kila moja.
Simba SC imewatema Warundi kiungo Pierre Kwizera na mshambuliaji Amisi Tambwe aliyehamia kwa mahasimu, Yanga SC baada ya kuwasajili Waganda hao.
Simba SC ililazimika kuwatema Warundi hao ili kukidhi matakwa ya kanuni ya Usajili ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ya wachezaji watano wa kigeni.
Murushid na akina Sserunkuma wanaungana na Waganda wenzao, beki Joseph Owino na mshambuliaji Emmanuel Okwi kukamilisha idadi ya wachezaji watano wa kigeni.

YANGA WAKALI KWELI KWELI YAMTUPIA VIRAGO EMERSON NA KIIZA

Baada ya Mvutano wa hapa na pale nani aachwe kati ya Emerson kiiza na Coutinho Yanga sasa imeamua kuwaacha kuwatupia virago Mbrazil, Emerson de Oliviera Roque na Mganda Hamis Kiiza na kumsajili mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Mrundi Amisi Tambwe.
Tambwe amesaini Mkataba wa mwaka mmoja baada ya kuachwa na klabu yake, Simba SC aliyoichezea msimu mmoja uliopita akitokea Vital’O ya Burundi.
Yanga SC imeamua kumuacha Mbrazil Emerson baada ya kushindwa kupata Hati yake ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC).
Tambwe anaungana na Mliberia, Kpah Sherman, Wanyarwanda Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Mbrazil Andrey Coutinho kukamilisha idadi ya wachezaji watano wa kigeni Yanga SC.
Wakati dirisha la usajili limefungwa jana Saa 6:00 usiku.
Yanga SC imesajili jumla ya wachezaji watatu wapya baada ya kumuacha Emerson, mwingine ni Danny Mrwanda. 
Katika kipindi cha msimu mmoja, Tambwe ameichezea Simba SC jumla ya mechi 43 na kuifungia mabao 26.
Maisha yake yalianza kuwa magumu Simba SC baada ya ujio wa kocha Mzambia, Patrick Phiri kuchukua mikoba ya Mcroatia, Zdravko Logarusic.

UONGOZI WA CLUB YANGA WASAMBARATISHA BENCHI LAKE LA UFUNDI

Uongozi wa club ya Yanga umewatupia virago Wabrazil, Marcio Maximo na Msaidizi wake, Leonardo Leiva na kuwarejesha Mholanzi, Hans van der Pluijm na mzalendo, Charles Boniface Mkwasa.
Maximo ametupiwa virago na baada ya kipindo cha mabao 2-0 kutoka kwa mahasimu Simba SC Jumamosi katika mchezo wa Nani Mtani Jembe.
Pluijm atamewasili  jana 8:38 usiku na kuweka kandarasi ya Mkataba wa kuanza kazi ambapo Mkwasa tayari alisaini Mkataba wiki kadhaa zilizopita na ameridhika kufanya kazi chini ya Pluijm tena.
Maximo na Leonardo walitua Yanga SC Julai mwaka huu kurithi mikoba ya Pluijm na Mkwasa ambao walipata kazi Uarabuni.
Hata hivyo baada ya muda usiozidi mwezi mmoja, Pluijm na Mkwasa waliacha kazi Uarabuni, wakidai kukerwa na kuingiliwa na viongozi wa klabu yao katika masuala ya kiufundi.
Pluijm alirudi Ghana wakati Mkwasa alirejea nyumbani Tanzania kabla ya kuajiriwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kama Mkufunzi Mkuu.
Hadi anaondoka Yanga SC, Maximo ameiongoza timu hiyo katika mechi 14, kati ya hizo akishinda 10, sare moja na kufungwa tatu dhidi ya Kagera Sugar 1-0, Mtibwa Sugar 2-0 sawa na Simba SC katika Mtani Jembe. 
Pluijm aliiongoza Yanga SC katika mechi 19, akishinda 11, sare sita na kufungwa mbili dhidi ya Al Ahly 1-0 Cairo na Mgambo JKT 2-1 Tanga.
Yanga SC ilikuwa tayari kuendelea na Maximo iwapo angekubali kufanya kazi na Mkwasa, lakini baada ya kukataa, klabu imeoana bora kuachana naye.
Maximo alikuwa anafanya kazi kwa mara ya pili Tanzania, baada ya awali kuwa kocha wa timu ya soka ya taia, Taifa Stars kuanzia mwaka 2006 hadi 2010.
REKODI YA PLUIJM AIKIWA NA YANGA SC
Yanga SC 0-0 KS Flamurtari Vlore (Ziara ya Uturuki)
Yanga SC 2-2 na Simurq PIK (Ziara ya Uturuki)
Yanga SC 2-1 Ashanti United (Ligi Kuu Bara)
Yanga SC 0-0 Coastal Union (Ligi Kuu Bara)
Yanga SC 1-0 Mbeya City (Ligi Kuu Bara)
Yanga SC 7-0 Komorozine (Ligi ya Mabingwa)
Yanga SC 5-2 Komorozine (Ligi ya Mabingwa)
Yanga SC 7-0 Ruvu Shooting (Ligi Kuu ya Bara)
Yanga SC 1-0 Al Ahly (Ligi ya Mabingwa)
Yanga SC 0-1 Al Ahly (Ligi ya Mabingwa.
Yanga ilitolewa kwa penalti 4-3)
Yanga SC 0-0 Mtibwa Sugar  (Ligi Kuu Bara)
Yanga SC 1-1 Azam FC (Ligi Kuu)
Yanga SC 2-0 Rhino Rangers (Ligi Kuu)
Yanga SC 5-0 Prisons (Ligi Kuu)
Yanga SC 1-2 Mgambo JKT (Ligi Kuu)
Yanga SC 5-1 JKT Ruvu (Ligi Kuu)
Yanga SC 2-1 Kagera Sugar (Ligi Kuu)
Yanga SC 2-1 JKT Oljoro (Ligi Kuu)

Yanga SC 1-1 Simba SC (Ligi Kuu)

Sunday, December 14, 2014

VARANE AWEKA WAZI KUWA ILIKUWA KIDOGO ATUE MAN UNITED

BEKI wa Real Madrid, Raphael Varane amabainisha kuwa ilibaki kidogo ajiunge na Manchester United kabla ya kukamilisha usajili wake Santiago Bernabeu.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa, alijiunga na Madrid akitokea klabu ya Lens mwaka 2011 kwa kitita cha euro milioni 10.
Hata hivyo, Varane amekiri kuwa alikuwa akifikiria kwenda Old Trafford lakini akaamua kwenda Maddrid kwani aliona ndio mahali pazuri kwa kuimarika kama mchezaji.

Varane amesema walikuwa wamekaribia kukubaliana na United kwnai mama yake anazungumza lugha ya kiingereza hivyo ndio alikuwa kama mkalimani lakini baada ya kufikiri sana akaona bora aende Madrid.

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA HAPA NA PALE

Arsenal na Liverpool wanachuana Juventus katika kuwania saini ya beki wa kulia wa Barcelona Martin Montoya, mwenye 23 ambae amekosa namba kwenye kikosi cha barca.
Mshambuliaji Fernando Torres anaweza kurejea katika klabu yake ya Chelsea mwezi januari,Ac Milan wanampango wa kusitisha mkataba wake.
WENGER
Klabu yaNapol ya itali wanaangalia uwezekano wa kumsajili winga Yannick Bolasie, mwenye miaka 25 kutoka klabu ya Crystal Palace.
Brendan Rodgers
Timu ya Man United wako tayari kupamba na Real Madrid ili kuweza kupata saini ya kiungo Christoph Kramer anaekipiga na klabu ya Borussia Monchengladbach, pia kukiwa na tetesi beki.

ROGERS
Winga wa Chelsea Thorgan Hazard yuko tayari kujiunga na Borussia Monchengladbach kwa mkataba kamili baada ya kufanya vizuri katika msimu wake wa kwanza anakocheza kwa mkopo toka Chelsea.