Uongozi wa club ya Yanga
umewatupia virago Wabrazil, Marcio Maximo na Msaidizi wake, Leonardo Leiva na
kuwarejesha Mholanzi, Hans van der Pluijm na mzalendo, Charles Boniface Mkwasa.
Maximo ametupiwa virago na
baada ya kipindo cha mabao 2-0 kutoka kwa mahasimu Simba SC Jumamosi katika
mchezo wa Nani Mtani Jembe.
Pluijm atamewasili jana 8:38 usiku na kuweka kandarasi ya Mkataba wa kuanza kazi ambapo Mkwasa tayari
alisaini Mkataba wiki kadhaa zilizopita na ameridhika kufanya kazi chini ya
Pluijm tena.

Hata hivyo baada ya muda
usiozidi mwezi mmoja, Pluijm na Mkwasa waliacha kazi Uarabuni, wakidai kukerwa
na kuingiliwa na viongozi wa klabu yao katika masuala ya kiufundi.
Pluijm alirudi Ghana wakati
Mkwasa alirejea nyumbani Tanzania kabla ya kuajiriwa Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF) kama Mkufunzi Mkuu.
Hadi anaondoka Yanga SC,
Maximo ameiongoza timu hiyo katika mechi 14, kati ya hizo akishinda 10, sare
moja na kufungwa tatu dhidi ya Kagera Sugar 1-0, Mtibwa Sugar 2-0 sawa na Simba
SC katika Mtani Jembe.

Yanga SC ilikuwa tayari
kuendelea na Maximo iwapo angekubali kufanya kazi na Mkwasa, lakini baada ya
kukataa, klabu imeoana bora kuachana naye.
Maximo alikuwa anafanya kazi
kwa mara ya pili Tanzania, baada ya awali kuwa kocha wa timu ya soka ya taia,
Taifa Stars kuanzia mwaka 2006 hadi 2010.
REKODI YA PLUIJM AIKIWA NA YANGA SC
Yanga SC 0-0 KS Flamurtari
Vlore (Ziara ya Uturuki)
Yanga SC 2-2 na Simurq PIK
(Ziara ya Uturuki)
Yanga SC 2-1 Ashanti United
(Ligi Kuu Bara)
Yanga SC 0-0 Coastal Union
(Ligi Kuu Bara)
Yanga SC 1-0 Mbeya City
(Ligi Kuu Bara)
Yanga SC 7-0 Komorozine
(Ligi ya Mabingwa)
Yanga SC 5-2 Komorozine
(Ligi ya Mabingwa)
Yanga SC 7-0 Ruvu Shooting
(Ligi Kuu ya Bara)
Yanga SC 1-0 Al Ahly (Ligi
ya Mabingwa)
Yanga ilitolewa kwa penalti
4-3)
Yanga SC 0-0 Mtibwa
Sugar (Ligi Kuu Bara)
Yanga SC 1-1 Azam FC (Ligi
Kuu)
Yanga SC 2-0 Rhino Rangers
(Ligi Kuu)
Yanga SC 5-0 Prisons (Ligi
Kuu)
Yanga SC 1-2 Mgambo JKT
(Ligi Kuu)
Yanga SC 5-1 JKT Ruvu (Ligi
Kuu)
Yanga SC 2-1 Kagera Sugar
(Ligi Kuu)
Yanga SC 2-1 JKT Oljoro
(Ligi Kuu)
Yanga SC 1-1 Simba SC (Ligi
Kuu)