Tuesday, June 11, 2013

WAALGERIA KUCHEZESHA TAIFA STARS, IVORY COAST


Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limeteua waamuzi kutoka Algeria kuchezesha mechi kati ya Taifa Stars na Ivory Coast itakayofanyika Jumapili saa 9 alasiri kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Waamuzi hao watakaochezesha mechi hiyo ya kundi C kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil wataongozwa na Charef Mehdi Abid atakayepuliza filimbi. Atasaidiwa na Hamza Hammou na Bouabdallah Omari wakati mezani atakuwa Sofiane Bousseter.

Abdi na wezake wanatarajiwa kutua nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 12 asubuhi kwa ndege ya EgyptAir. Mtathmini wa waamuzi ni Athanase Nkubito kutoka Rwanda ambaye atatua nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 12 jioni kwa ndege ya RwandAir.

Kamishna wa mechi hiyo ni Bernard Mfubusa kutoka nchini Burundi ambapo atawasili nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 3.35 asubuhi kwa ndege ya Kenya Airways. Maofisa wote hao wa mechi hiyo watarejea makwao Jumatatu (Juni 17 mwaka huu).

HATUA YA TATU RCL KUCHEZWA JUMAMOSI
Mechi za kwanza za hatua ya tatu ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kuwania nafasi tatu za kupanda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao zitachezwa Jumamosi (Juni 15 mwaka huu) wakati za marudiano zitachezwa Jumatano ya Juni 19 mwaka huu.


Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana leo (Juni 11 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kupitia ripoti za michezo iliyopita na kufanya uamuzi mbalimbali ikiwemo mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars na Machava FC ambayo haikuchezwa.

Machava FC ambayo ilishinda mechi ya kwanza iliyochezwa mjini Moshi kwa mabao 2-0 inaendelea katika hatua ya tatu kwa vile haikuhusika katika kukwamisha mchezo wa marudiano uliopangwa kuchezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma (DOREFA) kiliuhamishia mchezo huo kwenye Uwanja wa Mgambo mjini Mpwapwa kinyume na maelekezo ya Kamati ya Mashindano ya TFF. Kamati katika kikao chake cha awali iliekeleza kuwa mechi zote za RCL zitachezwa makao makuu ya mikoa isipokuwa kwa Morogoro ambapo timu ya Techfort FC iliruhusiwa kutumia Uwanja wa CCM Mkamba mjini Ifakara.

Hivyo timu nane zilizofuzu kucheza raundi hiyo ni Friends Rangers ya Dar es Salaam, Kariakoo ya Lindi, Katavi Warriors ya Katavi, Kimondo SC ya Mbeya, Machava ya Kilimanjaro, Njombe Mji ya Njombe, Polisi Jamii ya Mara na Stand United FC ya Shinyanga.

Wakati timu nyingine zimefuzu kwa kushinda mechi zao za raundi ya mbili, Njombe Mji imeingia hatua hiyo kwa kuwa timu yenye uwiano mdogo wa kufungwa (best looser) katika hatua ya pili.

Katika hatua hiyo mechi ni ifuatavyo; Kariakoo vs Friends Rangers, Machava FC vs Stand United FC, Polisi Jamii vs Katavi Warriors, na Kimondo SC vs Njombe Mji. Timu zilizoanza kutajwa ndizo zinazoanzia nyumbani.

Vilevile Kamati ya Mashindano imeagiza Kamishna wa mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars vs Machava FC, Mwijage Rugakingira wa Tanga ambaye alikwenda Uwanja wa Mgambo badala ya Uwanja wa Jamhuri kinyume na maelekezo ya TFF aondolewe kwenye orodha ya makamishna.

Pia waamuzi wa mechi hiyo ambao nao walikwenda Mpwapwa badala ya Dodoma Mjini wamepelekwa Kamati ya Waamuzi ya TFF kwa ajili ya kuchukuliwa hatua kutokana na tukio hilo.

Kamati ya Mashindano imekumbusha kuwa RCL ni mashindano yanayosimamiwa na TFF, hivyo maelekezo yoyote kuhusiana na mashindano hayo pia yatatoka TFF na si mahali pengine popote. Hivyo, msimamizi wa kituoa hana mamlaka ya kubadili uwanja.

Hatua ya nne ya RCL itachezwa kati ya Juni 23 na 23 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 29 na 30 mwaka huu.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MOYES AWEKA NIA YA DHATI KWA FABREGAS VS LEWANDOWSKI.

Mabingwa wa ligi kuu BPL nchini uingereza Msimu 2012-2013 hivi karibuni Club ya Manchester United imeongeza hali  na kasi ya kujiamini kuwa wanaweza kuwatwaa wachezaji Cesc Fabregas na Robert Lewandowski  kutua Old Trafford majira haya ya joto.
Kocha mpya wa United, David Moyes ametanabaisha kuwa angependa kuwasajili wote.
 kiungo wa Barcelona na mshambuliaji wa Kipoland wa Borussia Dortmund katika klabu yake kabla ya kikosi chake hakijakwenda katika ziara ya Asia na Australia katikati ya mwezi ujao.
Inafahamika kwamba, wachezaji wote hao wameonyesha nia zao za kuhamishia cheche zao kwa mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England, hivyo United wanaweza kufanikisha dili hizo.
Double strike: Man United believe they can land Cesc Fabregas and Robert Lewandowski (below)

Man United wanaamini wanaweza kumnasa Cesc Fabregas na Robert Lewandowski (chini)
Robert Lewandowski
Robert Lewandowski

Klabu yake ya zamani Fabregas, Arsenal haijaonyesha nia na malengo ya  kumsajili tena iwapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ataondoka Nou Camp, lakini United inafahamika wanamtaka kwa dhati kiungo huyo aliyeichezea kwa miaka nane timu hiyo ya London kabla ya kurejea Hispania miaka miwili iliyopita.
 
Lewandowski anaweza kuhamia England baada ya matumaini yake kuhamia kwa mabingwa wapya wa Ulaya, Bayern Munich kukatwa wiki hii.
United wamekuwa wakimfuatilia mshambuliaji huyo wa Poland kwa miezi kadhaa na wanaamini anaweza kuzalisha ushindani mzuri kwa Robin van Persie, ambaye atatimiza miaka 30 muda mfupi kabla timu haijaanza kutetea ubingw awake Agosti.

Changamoto: Robin van Persie anaweza kukabiliana na changamoto kubwa mwanzoni mwa msimu ujao Man United
Kuwasili kwake pia kunaweza kukuza shinikizo kwa Wayne Rooney ambaye ameomba kuondoka Old Trafford tangu mwishoni mwa msimu uliopita.

MOURINHO KWA MARA NYINGINE ATAMBULISHWA RASMI DARAJANI.

Kocha jose mourinho rasmi  ametambulishwa darajani ambapo amesisitiza  na kuweka wazi kuwa hajawahi kuwa na bifu na mmiliki wa club hiyo Roman Abramovich na lengo lake kuu ni kumrejesha John Terry uwanjani huku akiwataka wachezaji kucheza kwa uzalendo mkubwa.
mourinho2 7c61aMreno Jose Mourinho jana ametambulishwa rasmi kuwa kocha mpya wa wazee wa darajani, klabu ya Chelsea. 
Akizungumza na waandishi wa habari, Mourinho ambaye miaka ya nyuma akiwa na Chelsea alikuwa anajiita “The Speacial one” kwa tafsiri isiyo rasmi,  akimaanisha mtu maalumu, leo hii ametoa kali ya mwaka baada ya kubadili jina hilo na kujiita “The Happy One kwa tafsiri isiyo rasmi unaweza kusema “Mtu mwenye furaha pekee”.
Mreno huyo ambaye ametokea klabu ya Real Madridi ya Hispania leo mchana ametambulishwa jijini London na kujibu maswali mengi kutoka kwa wanahabari waliohitaji kujua mambo mengi kutoka kwake likiwemo suala la uhusiano na bosi wake Abramovich.
Mourinho ambaye miaka ya nyuma alitimuliwa na mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich baada ya kushindwa kuelewana, leo hii amesema kipindi cha nyuma alikuwa na mahusiano mazuri na bosi wake, endapo wangekuwa na mahusiano mabaya asingerejea kwa mara ya pili darajani.
Akiongea na wanahabari wapatao 250 leo katika uwanja wa Stamford Bridge, aliulizwa kama ataendelea kujiita “The Special one”, kocha huyo mwenye umri wa miaka 50 kwa sasa alisema “I am the Happy One” na kumalizia maneno yake kwa kusema “nina furaha sana”.
mourinho3 f5edf
Mourinho alisema ” Mambo mengi sana yametokea katika maisha yangu ya kufundisha soka na kazi yangu miaka tisa iliyopita, lakini ni mtu yule yule, nina moyo uleule, nina hisia zile zile za kupenda mpira na kazi yangu, lakini kwa sasa ni mtu mwingine kabisa baada ya kurudi nyumbani Chelsea, nina furaha sana”.

Mourinho amewataka wachezaji wake kujituma zaidi na kuongeza kuwa klabu ni muhimu kuliko wao, kwani isingekuwepo wao pia wasingekuwepo. Chanzo: Baraka Mpenja

SNEIJDER ASIKITISHWA KUNYANG'ANYWA UNAHODHA:

KIUNGO nyota wa klabu ya Galatasaray  na timu ya taifa ya Uholanzi Wesley Sneijder amekiri kusikitishwa na kitendo cha kunyang’anywa kitambaa cha unahodha wa timu yake ya taifa. Kiungo huyo alipewa unahodha wa Uholanzi wakati Louis van Gaal alipochukua nafasi ya Bert van Marwijk baada ya michuano ya Ulaya 2012. Akihojiwa Sneijder amesema ni jambo lililomuumiza sana na sio sababu hakutambua hilo ila kwasababu amekua akijitoa kwa uwezo wake wote toka akabidhiwe majukumu hayo lakini inabidi akubaliane na uamuzi wa kocha. Baada ya kumvua unahodha kiungo huyo kutokana na kutofurahishwa na kiwango chake, Van Gaal alimkabidhi majukumu hayo mshambuliaji nyota wa Manchester United Robin van Persie ambaye ameisadia klabu yake kushinda taji la Ligi Kuu msimu uliopita.

ZINEDINE ZIDANE AWEKA WAZI KUWA WATAKA KUVUNJA REKODI YA USAJILI.

Mkurugenzi wa michezo wa klabu ya REAL MADRID ambaye alikuwa kiungo wa wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa na klabu ya Real Madrid, Zinedine Zidane amekiri kuwa lengo kuu ni kuvunja rekodi ya uhamisho kama watkuwa na nia ya kumsajili Gareth Bale. 
Bale ambaye ni winga wa klabu ya Tottenham Hotspurs ya Uingereza amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Madrid ambapo kuna taarifa kuwa klabu hiyo imetenga kitita cha paundi milioni 85 kwa ajili yake.
Kama uhamisho huo ukifanyika utakuwa umevunja rekodi aliyoweka Cristiano Ronaldo wakati aliposajiliwa kutoka Manchester United kwa ada ya paundi milioni 80 miaka minne iliyopita. 
Zidane amesema kwa kiwango cha mchezaji huyo alichokionyesha msimu uliopita sio ajabu vilabu vingi kumuwania ndio maana anadhani itakuwa gharama kubwa kupata saini yake. 
Nyota huyo wa zamani aliendelea kusema kuwa kama klabu yoyote yenye uwezo wa kifedha itahitaji saini ya mchezaji huyo lazima watoe dau kubwa na hata kufikia kuvunja rekodi ili Tottenham waweze kumuachia.

Monday, June 10, 2013

PEREIRA RASMI KUIFUNDISHA AL AHLI YA SAUDI ARABIA.

KLABU ya Al Ahli ya Saudi Arabia imethibitisha na kuweka wazi kuwa imemteua Vitor Pereira kuwa kocha mpya wa klabu hiyo baada kocha huyo kuondoka Porto mwishoni mwa msimu huu. Pereira ameifundisha Porto kwa kipindi cha misimu miwili baada ya kuchukua nafasi ya Andre Villas-Boas Juni mwaka 2011 na kuisadia klabu hiyo kushinda mataji mawili ya Ligi Kuu nchini Ureno. Katika taarifa iliyotolewa katika mtandao wa klabu hiyo, Pereira mwenye umri wa miaka 44 atajiunga rasmi na klabu hiyo Juni 27 kabla ya kuiandaa timu kwa ajili ya msimu ujao siku mbili baadae. Pia zimekuwepo taarifa kuwa atatua katika klabu hiyo na wasaidizi wake wa watatu kutoka Ureno kwa ajili ya kuimarisha benchi lake la ufundi.

MMOJA APOTEZA MAISHA KATIKAMICHUANO YA LANGALANGA YA CANADIAN.

MASHINDANO ya langalanga ya Canadian Grand Prix jana yalimalizika kwa Majonzi makubwa baada ya mmoja wa wafanyakazi mwenye umri wa miaka 38 kufariki baada ya kukanyagwa na winji. Ajali hiyo ilitokea wakati gari la dereva Esteban Gutierrez wa timu ya Sauber lilipokuwa likiondolewa barabara za Montreal baada ya kupata ajali.

Mashuhuda wanasema wakati winji hilo likijaribu kuliondoa gari hilo ndipo mfanyakazi huyo aliangusha radio yake na wakati akiiokota ndipo alipokanyagwa kwasababu dereva wa winji hakumuona. Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter Gutierrez alituma salamu zake za rambirambi kwa familia ya mfanyakazi huyo kwa kumpoteza mtu wao karibu. Mbali na Gutierrez madereva wengine waliotoa rambirambi zao ni pamoja na Sebastian Vettel wa Red Bull aliyeshinda mbio hizo pamoja na Fernando Alonso wa Ferrari aliyeshika nafasi ya pili. Hilo ni tukio la pili kutokea katika mashindano hayo kwani mwaka jana katika michuano ya Grand Prix ya Italia mfanyakazi wa kujitolea wa zimamoto Paolo Ghislimberti alifariki kutoka na amejraha aliyopata kichwani na kifuani baada ya kupigwa na tairi lililochomoka kutoka katika gari la Heinz-Harald Frentzen wa timu ya Jordan.