Thursday, February 6, 2014

KANEMBWA JKT NA WACHEZAJI WAO KUJITETEA KAMATI YA NIDHAMU!

TFF_LOGO12TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 6, 2014
Wachezaji tisa wa Kanembwa JKT pamoja na timu yao wanaolalamikiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kumpiga mwamuzi Peter Mujaya wanatakiwa kujitetea mbele ya Kamati ya Nidhamu itakayokutana Jumapili (Februari 9 mwaka huu).
Utetezi huo unaweza kuwa wa mdomo kwa walalamikiwa kufika wenyewe mbele ya kamati itakayokutana saa 4 kamili asubuhi au kuuwasilisha kwa njia ya maandishi.
Kamati ilikutana jana Jumatano (Februari 5 mwaka huu) kusikiliza malalamiko dhidi ya wachezaji hao na timu yao kwa tukio hilo lililotokea Novemba 2 mwaka jana kwenye mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) dhidi ya Stand United FC iliyochezwa Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Wachezaji hao ni Abdallah Mgonja, Bariki Abdul, Philipo Ndonde, Mbeke Mbeke, Mkuba Clement, Mrisho Mussa, Nteze Raymond, Ntilakigwa Hussein na Uhuru Mwambungu. Mlalamikiwa mwingine ambaye naye anatakiwa kujitetea ni timu ya Kanembwa JKT.
Ikiwa chini ya Mwenyekiti wake Tarimba Abbas, Kamati hiyo baada ya kusikiliza malalamiko dhidi ya wahusika na kupokea ushahidi wa aina mbalimbali kutoka kwa mlalamikaji imesema ili iweze kutenda haki katika shauri hilo ni lazima walalamikiwa wapate fursa ya kusikilizwa.
Katika hatua nyingine, Kamati hiyo iliyokutana kwa mara ya kwanza tangu ilipoundwa imesema imesikitishwa na vitendo vya fujo ndani ya mpira wa miguu, na kuwataka watu wasijihusishe na aina yoyote ya fujo.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Wednesday, February 5, 2014

LOGARUSIC AFUNGUKA KUHUSU MTIBWA

Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, ametanabaisha na kufunguka kuwa, anahofia kikosi chake kupata majeruhi katika kipindi hiki cha lala salama kwani watamharibia mipango yake.
 
Simba ipo nafasi ya nne ya msimamo wa ligi kuu kufuatia kuwa na pointi 30, nyuma ya Mbeya City yenye pointi 31, ambapo inahitaji kujipanga ili iweze kufanikiwa kusonga mbele.
Loga alisema anahofia majeruhi katika kikosi chake kwani wanaweza kusababisha kutokuwa na kikosi kizuri kwa kuwa kila mchezaji anamtumia kulingana na mfumo.
Ligi ni ngumu na hakuna timu kubwa wala ndogo katika kipindi hiki kwani kila timu imejiandaa vya kutosha, hivyo tunahitaji kujipanga pindi tunapokutana na timu yoyote.
Kwa sasa sina kikosi cha kwanza na ninatumia mchezaji kulingana na mechi kwani kuna baadhi wanajua mfumo huu na wengine wanajua mfumo mwingine, hivyo wote wapo sawa.
Wachezaji ambao ni majeruhi kwa sasa ni Said Nassoro ‘Chollo’ ambapo Donald Musoti alikuwa anasumbuliwa na malaria, pia kuna baadhi ya wachezaji wanacheza huku wakisumbuliwa na majeraha madogo-madogo.

PAWASA NA WENGINE WATEULIWA KUSAKA VIPAJI KWA AJILI YA TAIFA STAR

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeteua kikosi cha makocha 40 kutoka sshehemu mbalimbali, Tanzania Bara na Zanzibar ili kung’amua vipaji katika mpango wa kuboresha timu ya Taifa (Taifa Stars).
Makocha hao ambao watafanya kazi hiyo katika michuano maalumu ya mikoa wanatakiwa kuripoti katika ofisi za TFF siku ya Jumamosi (Februari 8 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwa ajili ya kupewa maelekezo zaidi.
Walioteuliwa ni Abdallah Hussein (Kilimanjaro), Abdul Mingange (Dar es Salaam), Ali Bushiri (Zanzibar), Ali Mayay (Dar es Salaam), Ally Mtumwa (Arusha), Ayoub Selemani (Zanzibar), Boniface Pawasa (Dar es Salaam), Dan Korosso (Mbeya), Dk. Mshindo Msolla (Dar es Salaam) na Edward Hiza (Morogoro).
Elly Mzozo (Dar es Salaam), Fred Minziro (Dar es Salaam), George Komba (Dodoma), Hafidh Badru (Zanzibar), Hamimu Mawazo (Mtwara), Idd Simba (Mwanza), Jabir Seleman (Zanzibar), John Tegete (Mwanza), Juma Mgunda (Tanga) na Kanali mstaafu Idd Kipingu (Dar es Salaam).
Kenny Mwaisabula (Dar es Salaam), Khalid Abeid (Dar es Salaam), Madaraka Bendera (Arusha), Madaraka Selemani (Dar es Salaam), Mbarouk Nyenga (Pwani), Mohamed Mwameja (Dar es Salaam), Musa Kissoki (Dar es Salaam), Nicholas Mihayo (Dar es Salaam), Patrick Rweyemamu (Dar es Salaam) na Peter Magomba (Singida).
Peter Mhina (Songea), Salvatory Edward (Dar es Salaam), Salum Mayanga (Morogoro), Sebastian Nkoma (Dar es Salaam), Sekilojo Chambua (Dar es Salaam), Shaban Ramadhan (Zanzibar), Steven Nemes (Dar es Salaam), Sunday Manara (Dar es Salaam), Tiborowa Jonas (Dar es Salaam), Yusuf Macho (Dar es Salaam), Zamoyoni Mogela (Dar es Salaam).

OKWI ATINGA KAMBINI BAGAMOYO

Mshambuliajih hatari Emmanuel Okwi amejiunga na kambi ya Yanga mjini Bagamoyo.
Okwi ambaye usajili wake umesimamishwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ameanza mazoezi na wenzake.

Akizungumza na mkali wa dimba Okwi amesema ameanza mazoezi na wenzake baada ya kufanya pekee kwa zaidi ya wiki.

TFF imesimamisha usajili wake kwa madai kwamba kuna kesi tatu za msingi ambazo ni Simba kuishitaki Etoile du Sahel ikitaka kulipwa dola 300,000, Okwi kuishitaki timu hiyo na yenye pia imemshitaki Fifa.
Okwi alikuwa jukwaani akiishuhudia Yanga ikivunja mwisho wa msimu kwa kuifunga Mbeya City bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Sunday, February 2, 2014

AZAM YAITANDIKA KAGERA, YAKAA KILELENI!

Ligi kuu Vodacom Tanzania bara imeendelea leo Jijini Dar es Salaama ambapo Mechi mbili zimepigwa zikihusisha Timu 3 za juu na Azam FC kubaki kileleni baada kuinyuka Kagera Sugara Bao 4-0 huko Azam Complez, Chamazi na Yanga kuipa kipigo cha kwanza kwenye Ligi Mbeya City na kubaki Nafasi ya Pili.
YANGA 1 MBEYA CITY 0
Goli la Dakika ya 16 la Supastraika, Mrisho Ngassa, liliwashushia Mbeya City kipigo cha kwanza kwenye Ligi na kuifanya Yanga izidi kujichimbia Nafasi ya Pili ikiwa Pointi 1 nyuma ya Azam FC.
Mbeya City, ambao walipigana kiume, walipata pigo mara tu baada Kipindi cha Pili kuanza baada ya Mchezaji wao Steven Mazanda kutolewa kwa Kadi Nyekundu.
AZAM FC 4 KAGERA SUGAR 0
Huko Azam Complex, Chamazi kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salamm, Wenyeji na Vinara wa VPL, Azam FC, waliendelea kukaa kileleni baada kuinyuka Kager Sugar Bao 4-0.
Bao za Azam FC zilifungwa na Brian Umony, Bao mbili, na nyingine kupitia Jabir Aziz Stima na Kevin Friday.
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumatano  Februari 5
Tanzania Prisons vs Coastal Union (Uwanja wa Sokoine, Mbeya)
Mgambo Shooting vs Ruvu Shooting (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga)
Rhino Rangers vs Oljoro JKT (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora)
JKT Ruvu vs Ashanti United (Uwanja wa Azam Complex, Chamazi)


MSIMAMO:
NO
TEAMS
P
W
D
L
GF
GA
GD
PTS
1
Azam FC
16
10
6
0
29
10
19
36
2
Young Africans
16
10
5
1
34
12
22
35
3
Mbeya City
16
8
7
1
22
13
9
31
4
Simba SC
15
8
6
1
31
13
18
30
5
Mtibwa Sugar
15
5
6
4
19
18
1
21
6
Kagera Sugar
16
5
6
5
15
15
0
21
7
Coastal Union
15
3
9
3
11
8
3
18
8
Ruvu Shootings
14
4
6
4
16
16
0
18
9
JKT Ruvu
14
6
0
8
13
18
-5
18
10
Rhino Rangers
15
2
5
8
9
18
-9
11
11
JKT Oljoro
15
2
5
8
10
15
-5
11
12
Ashanti United
15
2
4
9
13
28
-15
10
13
Tanzania Prisons
13
1
6
6
6
16
-10
9
14
Mgambo JKT
15
2
3
10
7
26
-19
9

MENEJA WA AC-MILAN SEEDORF ASEMA MILAN ITAKUWA POA TU

MENEJA wa klabu ya AC Milan, Clerence Seedorf amedai kuwa klabu hiyo inaendelea kuimarika pamoja na kupata sare ya kufungana mabao 1-1 na Torino katika mchezo wa Serie A uliofanyika jana. Katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa San Siro wageni Torino ndio walioanza kupata bao kipindi cha kwanza kupitia kwa Ciro Immobile lakini wenyeji walirudisha bao hilo katika kipindi cha pili kupitia kwa Adil Rami. Sare hiyo inaonekana kumfurahisha Seedorf ambaye anadai kuwa wachezaji wake wameanza kuzoea mfumo anaofundisha. Seedorf amesema ni jambo jema kuona kikosi chake kikianza kuelewana taratibu na kudai kuwa ni dalili nzuri za kufanya vyema huko mbele. Sare hiyo imeiacha Milan katika nafasi ya tisa ya Serie A, wakiwa wanajikongoja toka alipotimuliwa kocha Massimiliano Allegri Januari mwaka huu.

LIBYA WATWAA UBINGWA WA CHAN KWA MARA YA KWANZA VS GHANA

TIMU ya taifa ya Libya wametawadhwa mabingwa wapya wa michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani, CHAN baada ya kuifunga Ghana kwa changamoto ya mikwaju ya penati katika mchezo wa fainali uliochezwa katika Uwanja wa Cape Town nchini Afrika Kusini. Libya walinyakuwa taji lao hilo la kwanza la kihistoria kwa kuigaragaza Ghana kwa penati 4-3 baada ya mchezo huo kumalizika bila ya kufungana mpaka katika muda wa nyongeza. Hiyo inakuwa mechi ya tatu kwa Libya kushinda kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada ya kuziengua Gabon na Zimbabwe katika hatua ya robo fainali na nusu fainali. Kwa wa mechi ya kutafuta mshindi wa tatu Nigeria walifanikiwa kuibuka kidedea baada ya kuifunga Zimbabwe kwa bao 1-0.