Saturday, August 16, 2014

MAN UNITED YAPOLEA KIPONDO NYUMBANI 2-1 SWANSEA CITY

MENEJA mpya wa klabu ya Manchester United ameanza vibaya kampeni zake za Ligi Kuu baada ya kushuhudia kikosi chake kikitandikwa mabao 2-1 dhidi ya Swansea city katika mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Old Trafford mchana wa leo.
Wageni Swansea ndio waliokuwa wa kwanza kuchukuliwa wavu wa United kwa bao lililofungwa na Ki Sung-yueng katika dakika ya 28 lakini bao hilo lilisawazishwa muda mfupi baada ya kuanza kipindi cha pili kupitia kwa nahodha wake Wayne Rooney.
Swansea walifunga bao lao la ushindi katika dakika ya 72 kupitia kwa Gyfi Sigurdsson hivyo kuifanya timu hiyo kupoteza mchezo wake wa ufunguzi nyumbani kwa mara ya kwanza toka mwaka 1972.
United walionekana kushindwa kabisa kutengeneza mipango ya kusawazisha bao hilo hatua ambayo mashabiki wake walionnekana kukata tamaa na kuanza kuondoka mapema uwanjani kabla ya mchezo kumalizika.
 Mashabiki wa United duniani kote kabla ya mchezo walionekana kuwa na imani kubwa na kikosi chao toka alipotua Van Gaal akichukua mikoba ya David Moyes ambaye alifanikiwa kushinda mechi zake zote za kirafiki alizocheza.

AZAM FC YAIFUMUA 4-1 ADAMA CITY KOMBE LA KAGAME CUP



Mabingwa wa tanzania bara 2013-2014 azam fc imekamilisha hayau ya makundi imemaliza katika klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame baada ya kuichalaza mabao 4-1 Adama City ya Ethiopia Uwanja wa Nyamirambo mjini hapa.

Kwa matokeo hayo Azam
FC ya Tanzania Bara, imekwea kileleni mwa Kundi A kwa kufikisha pointi nane baada ya mechi nne, ikishinda mbili na sare mbili na hatimaye kutinga hatua ya bRobo Fainali.

Dakika 45 za kwanza zilimalizika timu hizo zikiwa zimefungana bao 1-1, Azam wakitangulia kupitia kwa Nahodha John Bocco ‘Adebayor’ akiunganisha krosi ya Khamis Mcha ‘Vialli’ kabla ya Desaleny Debesh kuisawazishia Adama dakika ya 39.

Refa Mohamed Hassan kutoka Somalia alikataa bao la Kipre Herman Tchetche dakika ya 42, akidai kipa alibughudhiwa na kipindi cha pili Azam iliingia na moto mkali
na kufanikiwa kuongeza mabao matatu.

Kocha Mcameroon Joseph Marous Omog alifurahia matokeo hayo na akasema sasa anajipanga kwa Robo Fainali.
Kikosi cha Azam FC; Mwadini Ali, Erasto Nyoni, Gardiel Michael/Said Mourad dk51, David Mwantika, Aggrey Morris, Kipre Balou, Khamis Mcha ‘Vialli’/Farid Mussa dk61, Salum Abubakar ‘Sure Boy’/Mudathir Yahya dk72, John Bocco ‘Adebayor’, Didier Kavumbangu na Kipre Tchetche.

MAXIMO ATOA NENO KWA PATRIC PHIRI KUHUSU VPL SEPT 20

Mbrazil Marcio Maximo Kocha Mkuu wa klabu Yanga ametoa ya moyoni kwa kumkaribisha nchini kocha wa Simba Timu pinzani wa jadi, Mzambia, Patrik Phiri aliyetua hivi karibuni na kuanza kazi ya kukinoa kikosi cha Wanamsimbazi.
Maximo alichukua nafasi ya Mholanzi, Hans van Der Pluijm huku Phiri akiwa amesaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuitumikia Simba baada ya kuchukua mikoba iliyoachwa na  Mcroatia, Zdravko Logarusic aliyetimuliwa Jumapili iliyopita.
Katikamkutano na waandishi wa habari, Maximo amesema kuwa amemkaribisha kocha huyo ambaye anafahamu kuwa ni mzuri lakini amemtaka kutambua ushindani uliopo wa ligi ya Tanzania.
Maximo amesema napenda kumwambia kocha mpya wa Simba (Patrick Phiri),  karibu Tanzania lakini ajue kuwa ligi ina ushindani wa hali ya juu japo natambua kuwa yeye ni kocha mzuri na anayeifahamu ligi ya hapa”, alisema Maximo.
Phiri ametua nchini siku chache zilizopita na kusaini mkataba wa mwaka
mmoja kuinoa Simba, hii ikiwa ni mara ya tatu tofauti kuionoa timu hiyo.
Kwa upande mwingine, Maximo alisema kuwa kikosi chake kinaendelea vizuri na mazoezi ambapo kinamchanganyiko wa vijana na wakongwe ambao wengine walikuwa kwenye timu zao za Taifa.
Maximo aliongeza kuwa beki aliyesajiliwa na timu hiyo, Edward Charles ni mchezaji mzuri anayeamini ataisaidia Yanga kwa muda mrefu kutokana na umri  wake kuwa mdogo.
Maximo anatarajia kutaja majina ya wachezaji ataokwenda nao kwenye kambi kisiwani Pemba na watakaa huko kwa takribani siku kumi na baadae kurudi Dar tayari kwa kuanza msimu mpya wa Ligi Kuu Bara.

Friday, August 15, 2014

SIMBA SC YA DAR YATUA VISIWANI ZANZIBAR KUWEKA KAMBI



Simba sc baada ya kumnasa kocha Mzambia Patrick Phiri na kusaini Mkataba wa mwaka mmoja jana, kikosi cha Simba SC leo kimekwendavisiwani Zanzibar leo kuweka kambi rasmi ya kujiandaa na msimu.

Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuanza Septemba 20, mwaka huu na ratiba itatoka wiki moja kabla.

Tayari SImba SC imekamilisha usajili wake na wachezaji wote walikuwa wanahudhuria mazoezi mjini Dar es Salaam.


Phiri amerejea Simba SC baada ya miaka minne tangu aondoke mwaka 2010, akirithi mikoba ya Mcroatia Zdravko Logarusic aliyetupiwa virago mwishoni mwa wiki.

Haijulikani mshahara wa Phiri utakuwa kiasi gani, lakini mara ya mwisho aliondoka Simba SC akiwa analipwa dola za Kimarekani 5,000 (zaidi ya Sh. Milioni 7.5) kwa mwezi. 

Kocha huyo bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2009/2010, aliyezaliwa Mei 3 mwaka 1956, alifanya kazi kwa awamu tatu tofauti akiwa na Wekundu hao wa Msimbazi kati ya mwaka 2004 na 2010 kwa mafanikio makubwa- na sasa anataka kurejesha enzi za wana Simba ‘kutembea vifua wazi’.

Mzambia huyo alishinda mataji mawili ya Ligi Kuu akiwa na Simba SC, misimu ya 2004/2005 na 2009/2010 na pia alishinda Makombe ya Tusker mwaka 2005 la Tanzania na Kenya.

MBOFA YASEMA MWISHO WA KULIPA ADA YA LIGI YA WILAYA NI AGOSTI 30

Chama cha mpira wa miguu wilaya ya mbozi kinatoa taarifa kwa vilabu ambavyo bado havijalipa ada ya ligi ya wilaya kwa mwaka 2014.
Vilabu hivyo vinatakiwa kulipa ada ya shillingi laki moja na mwisho wa kulipa ada hiyo ni agosti 30 mwaka huu ambapo hakutakuwa na muda wa nyongeza tena kutokana na awali ilikuwa ni tarehe 30 mwezi wa 7 mwaka huu.
Akizungumza na mtandao huu katibu wa chama cha wilaya mbozi MBOFA Willium Mwamlima amesema hiyo ni nafasi ya pekee kwa timu zilizochelewa kufika katika ofisi za chama hicho kuchukua fomu za usajili.

CLUB 12 ZA MAVETERANI WA TZ KUCHUANA TAMASHA LA MIAKA 16 YA HOME GYM

CLUB 12 za timu za soka za maveterani zinazooundwa na nyota wa zamani wa kandanda nchini zinatarajiwa kuchuana katika michezo maalum ya Tamasha la Miaka 16 ya Home Gym, itakayofanyika Septemba 6 kwenye uwanja wa Mwenge, Dar es Salaam.
Aidha zaidi ya klabu 30 za Jogging nazo zinatarajiwa kupamba tamasha hilo ambalo litahusisha pia michezo mbalimbali ikiwamo ya netiboli, kuvuta kamba, kukimbia kwenye magunia na kukimbiza kuku.
Kwa mujibu wa mratibu wa tamasha hilo, Andrew Mangomango, klabu za maveterani zilizothibitisha kushiriki tamasha hilo ambalo litapambwa na burudani ya muziki na shoo ya watunisha misuli, wanyanyua vitu vizito, ngumi na karateka ni Mbagala Veterani, Boko, 501, Break Point, Survey, Mwenge na Msasani.
Mangomango alizitaja nyingine kuwa ni Biafra Veterani, Meeda, Mikocheni, Mbezi, Mabenzi, Segerea na Ukonga Veterani ambazo zinaundwa na nyota wa zamani wa kandanda waliowahi kutamba na timu kama za Simba, Yanga na Taifa Stars.
Juu ya klabu za Jogging mratibu huyo alizitaja kuwa ni pamoja na Temeke Jogging, Mwananyamala, Kingungi, Amani, Magenge, Makuka, 501, Ndiyo Sisi, Wastaarab, Makutanom, Pasada, FBI, Kongowe, Oysterbay Police, Zakheem, Kwa Nyoka, Kawe Beach, Satojio, Kawe Mkwamani na nyingine.
Mangomango aliongeza kuwa baada ya michezo yote wanamichezo washiriki watajumuika pamoja kuwatembelea yatima wanaolelewa kituo cha Chakuhama kwa ajili ya kuwapeleka misaada mbalimbali.
“Ni tamasha ambalo litaambatana na michezo mbalimbali kama ya kuvuta kamba, kukimbiza kuku, kukimbia kwenye magunia, na shoo za watunisha misuli, wanamieleka, mabondia na karateka kisha kwenda kutembelea yatima,” alisema.
Mangomango alisema mgeni rasmi wa shughuli zote hizo anatarajiwa kuwa Mkuu wa Kikosi cha Jeshi cha 501, J.B Kapumbe.
Hii ni mara ya pili kwa tamasha hilo kufanyika mwaja jana lilifanyika wakati Home Gym ikiadhimisha miaka 15 tangu kuasisiwa kwake ambapo shughuli zake kuu ni kufanyisha mazoezi na kutoa ushauri juu ya afya ya mwili.

KIUNGO WA GOR MAHIA ATUA KWA WAGOSI WA TANGA ASAINI MKATABA WA MWAKA 1.

UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga umeizidi kete klabu ya Simba SC baada ya kumsajili kiungo kati wa timu ya Gormahia ya nchini Kenya,Rama Saluma Mohamed aliyekuwa akiwaniwa na klabu hiyo.
Rama ametua kwenye klabu ya Coastal Union  akitokea nchini Kenya na kusaini  mkataba wa kuitumikia timu hiyo kwa kipindi cha mwaka
mmoja.