MENEJA mpya wa klabu ya
Manchester United ameanza vibaya kampeni zake za Ligi Kuu baada ya
kushuhudia kikosi chake kikitandikwa mabao 2-1 dhidi ya Swansea city katika mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Old Trafford
mchana wa leo.
Wageni Swansea ndio waliokuwa wa kwanza kuchukuliwa wavu
wa United kwa bao lililofungwa na Ki Sung-yueng katika dakika ya 28
lakini bao hilo lilisawazishwa muda mfupi baada ya kuanza kipindi cha
pili kupitia kwa nahodha wake Wayne Rooney.

United walionekana
kushindwa kabisa kutengeneza mipango ya kusawazisha bao hilo hatua
ambayo mashabiki wake walionnekana kukata tamaa na kuanza kuondoka
mapema uwanjani kabla ya mchezo kumalizika.
Mashabiki wa United duniani
kote kabla ya mchezo walionekana kuwa na imani kubwa na kikosi chao toka
alipotua Van Gaal akichukua mikoba ya David Moyes ambaye alifanikiwa
kushinda mechi zake zote za kirafiki alizocheza.