Tuesday, September 23, 2014

MSIMAMO NA RATIBA MSIMU MPYA WA LIGI KUU TANZANIA BARA VPL 2014-2015

RATIBA
Septemba 27
Simba v Polisi Moro {Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam}
Mtibwa Sugar v Ndanda FC {Manungu, Morogoro}
Azam F
C v Ruvu Shooting {Azam Complex, Dar es Salaam}
Mbeya City v Coastal Union {Sokoine, Mbeya}
Mgambo JKT v Stand United {Mkwakwani, Tanga}
VODAcom_na_kabumbu_lianze
Septemba 28
JKT Ruvu v Kagera Sugar {Azam Complex, Dar es Salaam}
Yanga v Prisons {Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam}
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Ndanda FC
1
1
0
0
4
1
3
3
2
Azam FC
1
1
0
0
3
1
2
3
3
Mtibwa Sugar
1
1
0
0
2
0
2
3
4
Tanzania Prisons
1
1
0
0
2
0
2
3
5
Mgambo JKT
1
1
0
0
1
0
1
3
6
Coastal Union
1
0
1
0
2
2
0
1
7
Simba
1
0
1
0
2
2
0
1
8
Mbeya City
1
0
1
0
0
0
0
1
9
JKT Ruvu
1
0
1
0
0
0
0
1
10
Kagera Sugar
1
0
0
1
0
1
-1
0
11
Polisi Moro
1
0
0
1
1
3
-2
0
12
Yanga
1
0
0
1
0
2
-2
0
13
Ruvu Shooting
1
0
0
1
0
2
-2
0
14
Stand United
1
0
0
1
1
4
-3
0

CAF YAITIA KITANZI MIAKA 2 JS KABYLIE KWA KIFO CHA MCHEZAJI EBOSSE

CAF_CHAMPIONS_LEAGUE_LOGOKLABU ya Algerian JS Kabylie  imefungiwa Miaka Miwili kutocheza Mashindano ya Afrika kwa sababu ya Kifo cha Mchezaji wake kutoka Cameroon Albert Ebosse.
Albert Ebosse, mwenye Miaka 24, alipigwa Kichwani na Mawe wakati akitoka Uwanjani baada ya Timu yake JS Kabylie kufungwa Nyumbani kwao na USM Alger Bao 2-1 huko Tizi Ouzou0 huku Bao pekee la JS Kabylie likifungwa na Ebosse.
JS Kabylie  imefuzu kucheza CAF CHAMPIONZ LIGI Mwakani baada ya kumaliza Ligi ya Algeria ikiwa Nafasi ya Pili lakini sasa watayakosa Mashindano hayo.
Uamuzi huo wa CAF umetolewa huko Ethiopia kwenye Kikao chao ambacho pia kimeamua kutoa Tuzo ya kila Mwaka ya Mchezo wa Haki kwa Jina la Ebosse kwa Chama cha Soka kitakachoshinda viwango vya Uchezaji Haki ambavyo vitaamuliwa na Kamati Kuu ya CAF kufuatia utendaji wao kwenye Mashindano ya CAF.
Mbali ya Adhabu hii ya Kifungo toka CAF, Viongozi wa Soka huko Algeria tayari wameshaiadhibu JS Kabylie  kwa kuizuia kucheza Mechi zao za Nyumbani za Msimu wa 2014/15 kwenye Uwanja wao, 1st November 1954, na pia kuwapiga marufuku Washabiki wao kuhudhuria Mechi yeyote ya Klabu hiyo hadi mwanzoni mwa Mwaka ujao.
Mara baada ya maafa ya Kifo cha Ebosse, Shirikisho la Soka Algeria lilitoa Dola 100,000 kwa Familia ya Ebosse na pia kulipa Fedha zote ambazo angelipwa kwa muda wake wote wa Mkataba wake na Klabu ya JS Kabylie.
Pia kila Mchezaji wa JS Kabylie alijitolea Mshahara wake wa Mwezi mmoja kwa Familia ya Mchezaji huyo.

KIONGERA NJE KUIKOSA YANGA KATIKA MTANANGE WATANI WA JADI OCT 12 MWAKA HUU.

MSHAMBULIAJI Mahiri Wa Simba Mkenya, Paul Raphael Kiongera yupo katika hatari ya kukosa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya wapinzani wa jadi, Yanga SC Oktoba 12, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Hiyo inafuatia kuumia katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu Jumapili Uwanja wa Taifa, Simba SC ikilazimishwa sare ya 2-2 na Coastal Union, licha ya kuongoza kwa 2-0 hadi mapumziko.

Kiongera alitokea benchi dakika ya 67, lakini dakika mbili kabla ya mpira kumalizika  alimpisha Amri Kiemba baada ya kuumia, kufuatia kugongana na kipa wa Coastal Union, Shaaban Kado.

Kiongera ameumia goti ambapo leo alikuwa Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili kwa ajili ya kufanyiwa vipimo, ila inasemekana mchezaji huyo ana maumivu sugu ya goti hilo baada ya kuumia awali kwao, Kenya.
Taarifa za awali zinasema Kiongera anaweza kuwa nje ya Uwanja kwa muda wa kati ya wiki sita hadi miezi miwili kabla ya kuanza mazoezi mepesi, maana yake hataweza kucheza Oktoba 12 pambano la watani.

Baada ya taarifa hiyo kuna hali ya wasiwasi ndani ya Simba SC kwamba huenda wameingia mkenge’ kumsajili Mkenya huyo bila kumfanyia vipimo vya afya, kufuatia habari kwamba ana maumivu sugu ya goti.

KOCHA MWAMWAJA ASEMA TZ PRISON ITAENDELEZA VIPIGO TU VPL

Baada ya Kuifumua Tanzaania Prison Kocha Mkuu wa Prisons ya Mbeya, David Mwamwaja amesema kuwa mpango mkubwa walionao ni kuendeleza vipigo kwa lengo la kujiimarisha kileleni.

Mwamwaja Kocha mzoefu aliyewahi kuifundisha Simba, amesema ushindi wao wa kwanza wa ligi katika mechi ya kwanza, umewapa motisha na nguvu za kutaka kuendelea kujinyakulia pointi tatu.

Prisons iliitandika Ruvu Shooting kwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Mabatini Mlandizi, Pwani.

Mwamwaja amesema kuwa Mechi na Ruvu shooting ilikuwa ngumu lakini tumefurahia kushinda ambapo amesema lengo kuu Tunataka kushinda zaidi na tumeanza kucheza mechi kadhaa za kirafiki kujiimarisha.


WAGOSI WA KAYA COASTAL UNIONI WAFURAHIA MAJERUHI WA MBEYA CITY 3 NJE.

Kuelekea Mtanange wa Juma mosi Timu ya mbeya city itawakosa baadhi ya wachezaji wake watatu baada ya kuumia katika mechi ya jumamosi iliyopita dhidi ya JKT Ruvu  iliyomalizika kwa suluhu ya bila kufungana, uwanja wa Sokoine, Mbeya, na watakaa nje ya uwanja kwa wiki mbili.
Akizungumza na Mkali wa dimba tz.blogspot Afisa habari wa mbeya city Dismas Ten amesema kuwa baada ya mechi iliyopita, wachezaji watano walipata majeruhi, lakini wawili kati yao watarejea uwanjani jumamosi ya septemba 27 kuchuana na Coastal Union.
Wachezaji hao ni Kabanda, Alex Seth na Eric Mawala, hawataweza kucheza kabisa siku ya jumamosi kwasababu watakaa nje kwa majuma mawili, kwa mujibu wa daktari wa timu
Dismas aliongeza kuwa maandalizi ya mechi ya pili nyumbani yanakwenda vizuri na wachezaji wana morali ya kutafuta ushindi na kuendeleza rekodi yao ya msimu uliopita ambapo walimaliza katika nafasi ya tatu nyuma ya Yanga na mabingwa Azam fc.
sanjari na hayo Dismas amesema kuwa Hali ya kambi ni nzuri, tunajiandaa vizuri na tunaamini tutaibuka na ushindi. Tulicheza mpira mkubwa sana dhidi ya JKT Ruvu.

Monday, September 15, 2014

MOURINHO ASEMA AMTUPIA LAWAMA CRISIANO RONALDO

KOCHA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amemtupia lawama Cristiano Ronaldo kwa kushindwa kwake kunyakuwa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati akiinoa Real Madrid. 
Mourinho alijiunga na na Madrid mwaka 2010 baada ya kuisaidia Inter Milan kunyakuw ataji hilo lakini katika msimu mitatu aliyokuwa Santiago bernabeu alishindwa kabisa kupata mafanikio barani Ulaya akiwa ameambulia kuingoza timu hiyo mpaka hatua ya nusu fainali katika kipindi chote hicho. 

Mara ya mwisho Mourinho kukaribia kutinga fainali ya michuano ya hiyo ilikuwa msimu wa mwaka 2011-2012 wakati walipokwenda katika hatua ya changamoto ya mikwaju ya penati baada ya muda wa nyongeza katika nusu fainali ya pili lakini walitolewa baada ya nyota wake akiwemo Ronaldo, Kaka na Sergio Ramos kukosa penati muhimu. 

Akihojiwa Mourinho ametamba kuwa kushinda taji la michuano hiyo mara mbili kama imefanya kazi yake hiyo kuwa ya kipekee. 

Mourinho amesema amekuwepo katika nusu fainali kadhaa na baadhi imekuwa ngumu kukubali kushindwa kama goli walilofungwa na Liverpool wakati akiwa na Chelsea mwaka 2005 pamoja matuta ya mwaka 2011 wakati mchezaji wao tegemeo Ronaldo alipokosa penati ya kwanza.

WEKUNDU WA MSIMBAZI WAREJEA ZANZIBAR KUWEKA KAMBI KWA MARA YA PILI.

Klub ya simba wekundu wa Msimbazi , Simba SC wamerejea tena Visiwani Zanzibar kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya ligi kuu soka  Tanzania bara inayotarajia kuanza kutimua vumbi septemba 20 mwaka huu.
20140913_160508Simba chini ya kocha Mzambia Patrick Phiri wataanza kampeni za kusaka ubingwa walioukosa kwa misimu miwili dhidi ya Wagosi wa ya, Coastal Union, septemba 21 mwaka huu uwanja wa Taifa , Dar es salaam.
Hii itakuwa mara ya pili Simba kujificha Zanzibar kwa sabababu ilikuwa huko kabla ya kuja Dar es salaam kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya, septemba 6 mwaka huu uwanja wa Taifa na kuitandika 3-0.
Ijumaa ya wiki iliyopita, Simba ilicheza mechi ya pili ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya URA ya Uganda na kulala bao 1-0.
jumamosi ya wiki iliyopita, Simba ilisafiri kwenda Mtwara ambapo ilicheza mechi ya kirafiki na Ndanda fc katika uwanja wa Nangwanda Sijaona na kutoka suluhu pacha ya bila kufungana.
Baada ya mechi hiyo, jana wachezaji walipewa mapumzikio, na leo jumatatu wanaanza mazoezi kabla ya kuelekea Zanzibar.
Simba wamekuwa wakiijenga timu upya chini ya kocha Phiri na usajili wao unawafanya wapinzani wawe na wasiwasi.
Wachezaji wa kigeni waliopo Simba wameonekana kuwa na ubora wa kutosha, hivyo kujenga imani kwa mashabiki wao.
Warundi, Amissi Tambwe, Pierre Kwizera, Mkenya, Paul Kiongera na Waganda Joseph Owino na Emmanuel Okwi wameonekana kuwa na msaada mkubwa kwa Simba.
Pia wapo wazawa waliosajiliwa kama, kipa Hussein Sharrif, Shaaban Kisiga, Elius Maguli,Joram Mgeveke, Tshabalala, na wengineo.
Wachezaji hawa wameonakana kuelewana na kucheza mpira mzuri kama walivyoonekana kwenye mechi dhidi ya Gor Mahia na URA.