Saturday, November 22, 2014

BASI LINALOTUMIA KINYESI LIMEANZA SAFARI YAKE YA KWANZA.

Basi la kwanza nchini Uingereza linalotumia kinyesi na uchafu unaotokana na chakula limeanza safari yake ya kwanza.
Bio Bus,lenye viti 40 na ambalo linatoa huduma ya uchukuzi kati ya Bath na uwanja wa ndege wa Bristol ,linaweza kusafiri hadi maili 186 kwa kutumia tangi moja la gesi.
Gesi hiyo hupatikana kupitia kutibu maji taka na uchafu wa chakula usiofaa kwa matumizi ya binaadamu.
Uchafu unaopatikana katika abiria wa basi moja unaweza kutumiwa kutoa kawi ya kulisafarisha basi hilo kutoka Lands End hadi John O'Groats.
Basi hilo ambalo limepewa majina kadhaa ya kutungwa likiwemo lile la Basi la pili linapongezwa kama njia mojawapo ya kuchochea usafiri wa uma huku ukiimarisha ubora wa hewa jijini.
Gasi inayotumiwa kuliendesha gari hilo hutoka katika mradi wa maji taka wa Bristol ambao husimamiwa na GENeco ambyo ni kampuni tanzu ya Wassex Water.
Mohammed saddiq,meneja mkurugenzi wa kampuni ya GENeco ,anaamini chakula na maji taka yanaweza kutoa kawi ya Biomethane inayotoa gesi katika shirika la kitaiafa la gesi inayoweza kutoa gesi yenye uwezo wa kutumika katika nyumba 8,500 mbali na kuliendesha basi hilo la Bio.

HENRY ATARAJIWA KUTUA KWA WENGER KUWA MKUFUNZI.

Timu ya Arsenal ipo katika harakati za kumpatia aliyekuwa mshambulizi wa timu hiyo Thiery Henry fursa ya ukufunzi katika timu hiyo kulingana na gazeti la daily mail.
Kandarasi ya raia huyo wa Ufaransa katika kilabu ya New York Red Bulls inatarajiwa kuisha mwisho wa msimu wa ligi ya soka ya marekani MLS mwezi ujao na hajasema ni hatua gani anayotarajia kuchukua.
Wengi wanaamini kwamba kampeni hiyo itakamilisha harakati zake kama mchezaji na huenda Arsene Wenger akamchukua katika klabu hiyo.
Na alipoulizwa iwapo Henry anaweza kurudi katika klabu hiyo kama kocha ,Wenger alijibu kwamba hakuna lisilowezekana.''Mimi huwakaribisha watu ambao wameichezea timu hii''.
Nimewaona wengi ambao wana uwezo lakini wameshindwa katika fursa yao ya kwanza kwa kuwa hawakuwa tayari.

CAF YAMTEUA SAM MPENZU KUTOKA TZ MCHUZO WA AFCON 2015.

Shirikisho la Soka Africa (Caf) limemteua mwamuzi kutoka nchini Tanzania, Samwel Mpenzu kushiriki kwenye mchujo wa kuwapata waamuzi watakaochezesha michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon 2015) inayotarajiwa kufanyika mwakani nchini Equatorial Guinea.

Iwapo Mpenzu atafuzu mchujo huo, atakuwa ni Mtanzania wa tatu kuchezesha michuano mikubwa kama hiyo barani Afrika, waamuzi wengine waliowahi kuchezesha ni Omar Abdulkadir na Ferdinand Chacha aliyechezesha Afcon (U-21).

Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Salumu Umande, amesema kuwa wameshapokea taarifa hizo za kuteuliwa kwa Mpenzu na tayari ameshawasili nchini Misri kwa ajili ya mchujo huo ambao unatarajiwa kufanyika kati ya leo (Jumamosi) na kesho.

Amesema kuwa iwapo atafanikiwa kufuzu kwenye mchujo huo, atapata nafasi ya moja kwa moja ya kuchezesha fainali hizo, kitu ambacho kitakuwa ni hatua kubwa kwa waamuzi wa Tanzania kwani kwa miaka mingi hakuna mwamuzi hata mmoja kutoka Tanzania aliyepata nafasi hiyo.

JE WAJUA:MBEYA CITY,PRISON,STAND HAZINA MCHEZAJI ALICHEZA SIMBA WALA YANGA

Tanzani Prisons,Mbeya City na Stand United ndizo timu pekee ambazo hazijafanikiwa kutwaa mchezaji yeyote aliyewahi kucheza Yanga ama Simba katika vikosi vyao msimu huu.
Baada ya kuchezwa mechi saba, uchunguzi umeonyesha kuwa Yanga ina wachezaji 20 na Simba 19 wanaocheza katika timu 11 kati ya 14 zinazoshiriki ligi hiyo.
Timu ambazo zina wachezaji waliowahi kucheza Simba na Yanga kwa vipindi tofauti na sasa wapo timu hizo ni Azam, JKT Ruvu, Kagera Sugar, Mgambo Shooting, Mtibwa Sugar, Ndanda, Polisi Morogoro, Ruvu Shooting , Simba na Yanga.
Hali hiyo inawapa nafuu Yanga na Simba katika baadhi ya michezo yao kwani kuna kasumba ya baadhi ya wachezaji kuwa na unazi uliopitiliza kwa vigogo hao.
Madai ya mapenzi ya Usimba na Uyanga yamewakuta  wachezaji wengi wanapocheza dhidi ya timu zao za zamani huku baadhi yao wakituhumiwa kucheza chini ya kiwango kisa walitoka kwenye mojawapo ya timu hizo.
Hata hivyo, Simba imeonekana kuwa na wachezaji wengi wa Yanga wakati watani zao, Yanga wameonyesha wana idadi kubwa ya wachezaji kwenye kikosi cha JKT Ruvu na Azam.
Wachezaji waliowahi kuichezea Simba ambao sasa wapo Yanga ni Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Kaseja, Ali Mustapha ‘Barthez’ na beki Kelvin Yondani, wakati wachezaji waliopo Simba na ambao wamewahi kupita Yanga ni Amri Kiemba, Ivo Mapunda na Emmanuel Okwi.
Simba pia ina wachezaji wawili JKT Ruvu ambao ni Ramadhan Shamte na Jabir Aziz, wakati Yanga katika kikosi cha maafande hao ina wachezaji watatu ambao ni Benjamin Haule, Jackson Chove na  Reliant Lusajo.
Yanga ina wachezaji watatu Azam, Frank Domayo, Gaudence Mwaikimba na Didier Kavumbagu, wakati watani zao Simba pia wana wachezaji wawili kwenye kikosi cha mabingwa hao, ambao ni Said Morad na Shomari Kapombe.
Katika kikosi cha Mtibwa Sugar, Simba ina wachezaji wawili, Mussa Hassan Mgosi na Abdallah Juma, wakati Yanga wana Vicent Barnabas, Said Mohamed na David Luhende. Kwenye kikosi cha Kagera Sugar, Yanga wana wachezaji Abubakary Mtiro na Atupele Green, wakati Simba wana Adam Kingwande na Salum Kanoni.
Polisi Morogoro, Simba inajivunia wachezaji Edward Christopher, Danny Mrwanda na Salum Machaku, wakati Yanga inajivunia Chacha Marwa na Lulanga Mapunda.
Yanga pia ina wachezaji wawili Coastal Union ambao ni Hussein Sued na Razack Khalfan, wakati watani zao Simba hawana mchezaji yeyote kwenye kikosi hicho, lakini wanawazidi Yanga kwani wana wachezaji wawili Ndanda ambao ni Paul Ngalema na Wilbert Mweta na wapinzani wao hawana mchezaji ndani ya kikosi hicho.
Source:Mwananchi

Friday, November 21, 2014

FIFA KUPITIA KWA UHAKIKA UPYA RIPOTI YA GARCIA.


SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limethibitisha kamati yake ya ukaguzi itapitia upya taarifa yote ya mchakato wa uenyeji wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 na 2022 baada ya kikao kati ya wakili Michael Garcia na jaji wa maadili Hans-Joachim Eckert. 
Taarifa ya mapitio ya ripoti ya uchunguzi wa Garcia kuhusiana na masuala ya rushwa ilitolewa na jaji Eckert wiki iliyopita huku Urusi na Qatar zikisafishwa kuwa wenyeji halali wa michuano hiyo ya mwaka 2018 na 2022. 
Jaji Eckert alikiri kuwepo matukio kadha katika ripoti hiyo lakini hayakuingilia mchakato wa kutafuta wenyeji katika michuano hiyo. 
Haraka taarifa hiyo iliyokuwa na kurasa 42 ilipingwa vikali na wakili Garcia alioongoza uchunguzi huo kwa miaka miwili akisisitiza kumekuwa na makosa kadhaa kadhaa kulinganisha na ripoti yake iliyokuwa na kurasa 430.
Jaji Eckert na Garcia alikutana ili kusawazisha mambo na kufikia uamuzi huo wa kupeleka ripoti yote kwa kamati ya ukaguzi kwa ajili ya kufanyiwa kazi zaidi.

NDANDA YAJIWEKA FITI LIGI KUU YAJIPANGA KUSAJILI WA NGUVU.

Timu ya Ndanda FC katika kuhakikisha inatoa dozi Ligi Kuu Bara ya imeamua kusajili wachezaji kutoka Burundi na katika timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes.

Ndanda inayoshika nafasi ya pili kutoka mkiani katika msimamo wa ligi kuu, tayari imeshaingia mkataba na kiungo wa zamani wa Mtibwa Sugar, Masoud Ally Mohamed ‘Chille’ ambaye kwa sasa anaichezea Zanzibar Heroes.

Klabu hiyo imeanza mazungumzo na mashambuliaji, Indeshyme Dumu raia wa Burundi ambaye alikuwa anacheza soka la kulipwa nchini Djibouti.

Selemani Kachele Katibu wa Ndanda, akizunghumza na mtandao huu amesema kuwa nia yao ni kusajili wachezaji sita wakati huu wa dirisha dogo.

Ndanda inayoshika nafasi ya pili kutoka mkiani katika msimamo wa ligi kuu  ikiwa na point 6, tayari imeshaingia mkataba na kiungo wa zamani wa Mtibwa Sugar, Masoud Ally Mohamed ‘Chille’ ambaye kwa sasa anaichezea Zanzibar Heroes.

Klabu hiyo imeanza mazungumzo na mashambuliaji, Indeshyme Dumu raia wa Burundi ambaye alikuwa anacheza soka la kulipwa nchini Djibouti.

Katibu wa Ndanda, Selemani Kachele amesema nia yao ni kusajili wachezaji sita wakati huu wa dirisha dogo.

TAARIFA KWA MASHABIKI KUHUSU KOCHA JUMA MWAMBUSI-UONGOZI.

Uongozi wa Halmashauri ya jiji la Mbeya unapenda kuwaarifu mashabiki na wadau wa Timu ya Mbeya City Fc kuwa suala lililojitokeza wiki iliyopita kuhusiana na kocha mkuu wa timu hii Juma Mwambusi kujiuzulu, litatolewa maelezo na ufafanuzi wiki ijayo.
Hivyo basi mashabiki na wadau wa timu ya Mbeya City Fc  mnaombwa  kutulia mpaka  ufafanuzi  au taarifa  rasmi juu ya jambo hili itakapotolewa, pia  mashabiki mnaombwa kuwa makini na baadhi ya watu ambao wanataka kutumia mwanya huu  kuzusha  chokochoko nyingi kwa lengo la kuleta mgawanyiko na kuvuruga umoja wetu.
Kwa sasa Juma Mwambusi bado ni mwalimu wa Mbeya City Football Club{Vikao vya ndani vinaendelea kuhusu suala hili}.