Monday, August 12, 2013

AZAM FC YAMALIZA ZIARA YAKE NCHINI AFRIKA KUSINI KWA KIPONDO

Kikosi kabambe cha azam fc
Washindi wa pili mfululizo wa ligi kuu vodacom tanzania bara Azam FC leo imekamilisha ziara yake ya Afrika Kusini kwa kipigo cha bao 1-0 dhidi ya wenyeji, Moroka Swallows katika dimba la Uwanja wa Volkswagen Dobsonville mjini Soweto.
 
Aidha Katika Ziara hiyo huo unakuwa mchezo wao wa tatu kuambulia kipigo baada ya awali kuchapwa 3-0 na Kaizer Chiefs, 2-1 na Orlando Pirates.

Hata hivyo katika ziara hiyo wanarambaramba hao wamefanikiwa kuibuka na ushindi mchezo mmoja dhidi ya Mamelodi Sundowns baada ya kuichalaza bao 1-0.