YaYa Toure kiungo mahiri
wa kimataifa wa Ivory Coast na club ya man city ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwaka
wa nchi hiyo katika msimu wa 2012-2013 baada ya kupata asilimia 32 ya
kura zilizopigwa na waandishi wa habari za michezo na watumiaji wa
mtandao. Toure mwenye umri wa miaka 30 anayecheza katika klabu ya
Manchester City anafuatia na mshambuliaji nyota wan chi hiyo Didier
Drogba aliyepata asilimia 24 wakati nafasi ya tatu inashikiliwa na Bony
Wilfried aliyepata asilimia 17. Wengine ni Aroune Kone ambaye amejiunga
na timu ya Everton akitokea Wigan mwezi uliopita pamoja na Gervino
aliyejiunga na AS Roma akitokea Arsenal ambao wote kwa pamoja wamepata
asilimia 15 ya kura zilizopigwa. Hiyo inakuwa mara ya tatu Toure
kushinda tuzo hiyo mara nyingine ikiwa mwaka 2008 na 2009.