
Thursday, July 4, 2013
ISCO ASEMA LENGO KUU NI KUISAIDIA MADRID KUTWAA UEFA

GIGGS NAYE AWA KOCHA MCHEZAJI SAFU YA BENCH LA UFUNDI.

RYAN GIGGS NA MAN U
-UMRI: 39
-MECHI: 941
-MAGOLI: 168
-MATAJI YA LIGI: 13
-FA CUP: 4
-LIGI CUP: 4
-UEFA CHAMPIONZ LIGI: 2
HISPAIN BADO NAMBARI MOJA DUNIANI VIWANGO VYA FIFA
Ivory Coast ndiyo Nchi ambayo iko juu kupita zote Afrika na inakamata Nafasi ya 13.
Brazil, ambao Jumapili iliyopita walitwaa Kombe la Mabara, wamerudi 10 Bora na sasa wapo Nafasi ya 9.
20 BORA:
1 Spain
2 Germany
3 Colombia (Imepanda Nafasi 4)
4 Argentina (Imeshuka 1)
5 Holland
6 Italy (Imepanda 2)
7 Portugal (Imeshuka 1)
8 Croatia (Imeshuka 4)
9 Brazil (Imepanda 13)
10 Belgium (Imepanda 2)
11 Greece (Imepanda 5)
12 Uruguay (Imepanda 7)
13 Ivory Coast
14Bosnia-Herzegovina (Imepanda 1)
15 England (Imeshuka 6)
16Switzerland (Imeshuka 2)
17 Russia (Imeshuka 6)
18 Ecuador(Imeshuka 8)
19 Peru (Imepanda 11)
20 Mexico (Imeshuka 3).
WACHINA WAKABIDHI UWANJA WA TAIFA KWA SERIKALI.

Makabidhiano hayo ya Uwanja huo
uliochukua Miaka 7 kujengwa yalifanyika Jana kwa kutia saini na
kubadilishana Vyeti kati ya Balozi wa China Nchini Tanzania, Li Youqing,
na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Sihaba Mkinga.
Akizungumza, Waziri wa Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo, Dr. Fenella Mukangara, aliishukuru China
kwa msaada wao mkubwa wa Fedha na Ujenzi.
Pia, Waziri Mukangara, alisifu Usimamizi
wa China wa Uwanja huo tangu ujenzi ulipokamilika na tangu Uwanja huo
ulipofunguliwa rasmi hapo Tarehe 25 Februari 2009 na Rais wa zamani wa
China, Hu Jintao, na Rais Jakaya Kikwete.
Uwanja wa Taifa, unaochukua Washabiki
60,000 wote wakiwa Vitini, umegharimu Shilingi Bilioni 56 na kati ya
hizo China ilitoa Bilioni 33.4 na Tanzania ilitoa Fedha zilizobaki.
Uwanja huu ni wa kisasa na upo katika Viwango vinavyokubalika na FIFA na Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki.
Serikali imedokeza kuwa hivi sasa wapo
kwenye mazungumzo ya kutafuta Fedha ili kugharamia Ujenzi wa Awamu ya
Pili na inatarajiwa Serikali ya China itahusishwa na pia Mkandarasi
aliejenga Awamu ya Kwanaza, Beijing Construction Engineering Company
Limited, ndio watashughulikia Awamu hii.
Baada ya kukamilika kwa Ujenzi wa Awamu
ya Pili, Tanzania itakuwa iko tayari kuwa Mwenyeji wa Mashindano makubwa
ya Michezo ya kila aina.
CHELSEA YAFIKIA MAKUBALIANO NA MARCO VAN GINKEL WA VITESSE FC YA UHOLANZI".
WAKALI wa Darajani Club ya soka ya Chelsea imefikia makubaliano ya kumsajili kiungo wa klabu ya Vitesse Arnhem ya Uholanzi, Marco van Ginkel. Kiungo
huyo mwenye miaka 20 ambaye ametokea katika shule ya watoto ya Vitesse
kabla ya kupata namba katika kikosi cha kwanza April mwaka 2010
atajiunga na Chelsea baada ya kukamilisha taratibu za vipimo vya afya. Van
Ginkel amekuwa akicheza katika kikosi cha timu ya taifa ya vijana chini
ya miaka 21 ya Uholanzi na mara moja ameshaitwa katika kikosi cha timu
ya wakubwa akiingia kama mchezaji wa akiba katika mchezo dhidi ya
Ujerumani Novemba mwaka jana. Kiungo
huyo anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na meneja mpya wa Chelsea Jose
Mourinho kufuatia kusajiliwa kwa mshambuliaji Andre Schuerrle ktoka
Leverrkusen mwezi uliopita.
YONDAN AWA MCHEZAJI BORA WA LIGI KUU TZ 2012-2013
INJINI ya Yanga Sc beki Kevin
Patrick Yondan amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara msimu wa 2012/2013 na kuzawadiwa kitita cha Sh. Milioni
5. Hata hivyo,
katika hafla ya kutoa zawadi za washindi wa Ligi Kuu msimu uliopita
kutoa wadhamini, Vodacom Tanzania zilizofanyika katika hoteli ya Double
Tree, Dar es Salaam jana usiku, Yondan hakuwepo na tuzo yake alipokelewa
na Ofisa Habari wa klabu hiyo, Baraka Kizuguto, kutoka kwa mgeni rasmi,
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara. Yondan
ambaye alikuwa katika msimu wake wa kwanza Yanga SC, yuko kwenye kambi
ya timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inayojiandaa na mchezo
dhidi ya Uganda Julai 13, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Kipa
chipukizi wa Tanzania Prisons FC ya Mbeya, David Burhan alishinda tuzo
ya kipa bora wa Ligi Kuu na kupewa Sh. Milioni 5, wakati mfungaji bora,
Kipre Herman Tchetche raia wa Ivory Coast wa Azam FC alipewa Milioni 5
pia na Fully Maganga wa JKT Mgambo alipewa tuzo ya mchezaji mwenye
nidhamu na kuzawadiwa Milioni 5. Kocha
mpya wa Simba, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibadeni’ ameshinda
tuzo ya kocha bora kwa kazi nzuri aliyoifanya akiwa na Kagera Sugar
msimu uliopita na kuzawadiwa Milioni 7.5 sawa na refa bora, Simon
Mbelwa. Yanga SC
pamoja na kuzawadiwa Sh. Milioni 70 za kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu,
waliongezewa Milioni 15 kwa kuwa timu yenye nidhamu zaidi kwenye ligi
hiyo msimu uliopita, hivyo kuondoka na jumla ya kiasi cha Sh. Milioni
85. Azam FC
washindi wa pili kwa msimu wa pili mfululizo, walizawadiwa Sh. Milioni
35, Simba SC washindi wa tatu Milioni 25 na Kagera Sugar washindi wa nne
walipewa Milioni 20. Kwa
upande wa zawadi za wachezaji wa timu za vijana za klabu za Ligi Kuu,
Hamisi Saleh (JKT Ojoro), Abdulrahman Mussa (Ruvu Shooting), Hassan
Dilunga (Ruvu Shooting), Chande Magoja (Mgambo JKT), Tonny Kavishe
(Mgambo JKT) na Rajab Zahir (Mtibwa Sugar), wote wamezawadiwa Sh.
Milioni 1 kila mmoja. Zawadi
za wachezaji wa timu za vijana, walizozawadiwa kwa kuzichezea mechi
nyingi timu zao za wakubwa katika Ligi Kuu, zimetoka Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF).
Rajab Zahir amesaini Yanga SC na tayari amejiunga nayo.
Rajab Zahir amesaini Yanga SC na tayari amejiunga nayo.
Wednesday, July 3, 2013
USAJILI WAPAMBA MOTO BARANI ULAYA
Stoke City wamemsaini Beki wa Kimataifa wa Timu ya Spain U-21 Marc Muniesa anaecheza Barcelona kwa Uhamisho wa bure.
Muniesa, Miaka 21, ni mmoja wa Wachezaji
wa Spain ambayo ilitwaa Ubingwa wa EURO 2013 kwa U-21 hivi karibuni na
anajiunga na Stoke kwa Mkataba wa Miaka minne.
Huyu ni Mchezaji wa pili kuchukuliwa na
Meneja mpya wa Stoke, Mark Hughes, baada ya Wiki iliyopita kumsaini Erik
Pieters kutoka PSV Eindhoven.
SWANSEA YAKUBALIANA NA LIVERPOOL KUHUSU JONJO
Swansea City imeafikiana na Liverpool
Ada ya Pauni Milioni 6 ya kumhamisha Kiungo Jonjo Shelvey na Mchezaji
huyo sasa atakutana na Swansea ili kukamilisha makubaliano ya Maslahi
yake binafsi.
Jonjo Shelvey, Miaka 21, alisainiwa na
Liverpool kutoka Charlton Athletics kwa Dau la Pauni 1.7 Miaka mitatu
iliyopita lakini akiwa Anfield kupata namba kwake kumekuwa nadra na
Meneja Brendan Rodgers amemruhusu kutafuta Klabu nyingine.
Shelvey aliichezea England kwa mara ya
kwanza Novemba Mwaka jana ilipofungwa na Sweden na pia amecheza Mechi 17
za Ligi huko Anfield Msimu uliopita.
Jana Swansea ilitangaza kuwasaini
Wachezaji watatu wengine ambao ni Alejandro Pozuelo, Miaka 21, kutoka
Real Betis ya Spain, Kipa wa Miaka 17, Gregor Zabret kutoka Klabu ya
Slovenia NK Domzale na Alex Gogic, Kiungo wa Miaka 19 kutoka Klabu ya
Greece, Olympiakos.

Katika azma yao ya kukiimarisha Kikosi
chao kuwa na nguvu na Misuli inayostahili kwa ajili ya Msimu mpya, Klabu
ya Arsenal imemuajiri Mchezaji wa zamani wa Kimataifa wa Ireland wa
Mchezo wa Raga, Jerry Flannery, kuwa Kocha wao mpya wa kujenga nguvu,
musili na stamina kwa Wachezaji wao.
Flannery, Miaka 34, alistaafu mapema kucheza Raga baada ya kuumia Misuli za Mguu.
MOURINHO AZUNGUMZA NA MARCO VAN GINKEL
Chelsea imefanya mazungumzo na Kiungo wa Vitesse Arnhem, Marco van Ginkel, ili ahamie Stamford Bridge.
Van Ginkel, Miaka 20, ameshakutana na Jose Mourinho na Alhamisi ataongea na Klabu yake ya Uholanzi ili apate baraka za Uhamisho.
Marco van Ginkel alijiunga na Vitesse
Arnhem akiwa na Miaka 7 tu na kupanda kwenye Vyuo vya Klabu hiyo hadi
Aprili 2010 alipocheza Timu ya Kwanza kwa mara ya kwanza.
Van Ginkel anathaminiwa kuwa na Dau la Pauni Milioni 8 na Mkataba wake na Klabu yake unamalizika Juni 2015.
Ikiwa Uhamisho huu utakamilika, huu
utakuwa ni usajili wa pili kwa Jose Mourinho baada ya Wiki iliyopita
kumnasa Mchezaji wa Kimataifa wa Germany, Andre Schurrle, kutoka Klabu
ya Bundesliga, Bayer Leverkusen.
Subscribe to:
Posts (Atom)