Club
ya Bayern Munich ya ujerumani imefanikiwa kutoa wachezaji wa nne walioteuliwa katika orodha ya wachezaji 10 na
Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA kugombea tuzo ya mchezaji bora wa
bara hilo kwa msimu wa 2012-2013. Wachezaji
hao ni Franck Ribery, Thomas Mueller, Arjen Robben na Bastian
Schwainsteiger ambao wote walikuwemo katika kikosi cha Bayern ambacho
kilifanikiwa kunyakuwa mataji matatu msimu uliopita. Mbali
na hao wengine waliotajwa katika orodha hiyo ni mchezaji bora wa mwaka
katika Ligi Kuu nchini Uingereza, Gareth Bale pamoja na mfungaji bora wa
ligi hiyo Robin van Persie huku Lionel Messi na Cristiano Ronaldo
wakiwa wachezaji pekee kutoka La Liga ya nchini Hispania kwenye orodha
hiyo. Hii itakuwa
ni mara ya tatu kufanyika sherehe za tuzo hizo ambapo mwaka 2011 Messi
ndiye aliyeshinda huku mchezaji mwenzake wa Barcelona Andres Iniesta
akishinda tuzo hiyo mwaka jana. Wachezaji
wengine ni Mshambuliaji nyota wa klabu ya Paris Saint-Germain-PSG,
Zlatan Ibrahimovic na Robert Lewandowski anayekipiga Borussia Dortmund
ambapo orodha ya mwisho ya wachezaji watatu itatajwa Agosti 6 kabla ya
sherehe za kumjua mshindi ambazo zitafanyika wakati wa upangaji wa
ratiba ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Agosti 29 mwaka huu jijini Monaco.
Wednesday, July 10, 2013
Tuesday, July 9, 2013
MURRAY APONGEZWA NA CAMEROON VS MALIKIA ELIZABETH
Waziri Mkuu David
Cameron pamoja na Malkia Elizabeth wa pili wa Uingereza wamekuwa miongoni mwa
watu mashuhuri waliotoa pongezi kwa mchezaji tenisi nyota wan chi hiyo
Andy Murray kwa kunyakuwa taji la michuano ya Wimbledon. Wachezaji
nyota na watu wengine maarufu nchini humo pia walitoa pongezi zao kwa
Murray mwenye umri wa miaka 26 baada ya kuwa Muingereza wa kwanza
kunyakuw ataji la michuano hiyo toka Fred Perry alipofanya hivyo mwaka
1936, kwa kumfunga Novak Djokovic kwa seti 3-0.
Cameron ambaye alikuwepo
uwanjani kushuhudia mtanange huo alimpongeza Murray kwa kuonyesha
kiwango cha juu kwenye mchezo huo na kuweka historia mpya katika mchezo
huo nchini Uingereza. Mwandishi
wa BBC katika kasri ya kifalme nchini humo, Peter Hunt alibainisha kuwa
Malkia alimtumia ujumbe binafsi Murray kumpongeza kwa kufanikiwa
kushinda taji hilo.
LIVERPOOL YAIBWAGA CHINI OFA YA ARSENAL KUHUSU SUAREZ

THIERRY HENRY NAYE YUMO KIKOSI CHA WACHEZAJI 10 WA MLS
Mshambuliaji nyota wa
zamani wa Ufaransa, Thierry Henry ni moja kati ya wanadinga nyota 10
watakaounda kikosi kutoka katika Ligi Kuu ya Soka nchini Marekani-MLS
ambacho kitapambana na AS Roma ya Italia Julai 31 huko jijini Kansas. Henry
mwenye umri wa miaka 35 mshambuliaji wa klabu ya New York Red Bull
ambaye aliisadia Ufaransa kushinda Kombe la Dunia mwaka 1998, amefunga
mabao sita katika mechi 17 alizoichezea timu hiyo msimu huu. Kabla ya kwenda Marekani mwaka 2010 akitokea klabu ya Barcelona, henry amewahi kucheza katika vilabu vya Juventus na Arsenal. Golikipa
wa FC Dallas ambaye ni raia wa Peru Raul Fernandez, kiungo wa timu ya
taifa ya Canada Will Johnson na Beki wa Kansas City Aurelien Collin
ambaye ni raia wa Ufaransa ni miongoni mwa wachezaji wasiokuwa raia wa
Marekani walioteuliwa katika kikosi hicho cha nyota wa MLS.
FIFA-SEPP BRATTER ATARAJI KUZUNGUMZA NA MAOFISA WA ISRAEL
![]() |
Bratter akiyatafakari mazungumzo |
MESSI RASMI ATARAJIWA KUREJEA BARCA MAZOEZINI JULAI 15

ROLNADO NAYE KUWANIA TUZO YA UNYAYO WA DHAHABU:
Mshambuliaji nyota mahiri wa club ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametajwa katika orodha ya
wachezaji 10 watakaowania tuzo ya kiatu cha Dhahabu kwa mwaka 2013. Mshambuliaji
huyo wa kimataifa wa ureno atakuwa mchezaji wa kwanza wan chi hiyo
kushinda tuzo hiyo ambayo ilianza kutolewa mwaka 2003 mahsusi kwa
wachezaji waliozidi umri wa miaka 28. Mchezaji
mwenzake wa Madri Iker Casillas na kiungo mahiri wa Barcelona Andres
Iniesta ni miongoni wa nyota wengine walioteuliwa kugombea tuzo hiyo. Wachezaji
waliwahi kushinda tuzo hiyo ambayo hutolewa kwa kuangalia uwezo wake wa
kipindi chote alichocheza soka na kiwango chake cha sasa, ni pamoja na
Roberto Carlos, Ronaldinho, Francesco Totti na mshindi wa mwaka uliopita
Zlatan Ibrahimovic. Wachezaji
wanaweza kushinda tuzo hiyo mara moja pekee, ambapo sherehe zake
hufanyika jijini Monaco kila mwaka toka ilipoanzishwa. Mbali
na hao wengine waliokuwemo katika orodha ya mwaka huu ni pamoja na
Samuel Eto'o kutoka Anzhi Makhachkala, Andrea Pirlo anayekipiga
Juventus, Didier Drogba kutoka Galatasaray, Frank Lampard-Chelsea,
Miroslav Klose-Lazio, David Trezeguet-River Plate and David
Beckham-Paris Saint-Germain.
Subscribe to:
Posts (Atom)