Shirikisho la kandanda barani Ulaya-UEFA, limesema kuwa klabu za Fenerbahce na Besiktas za
Uturuki zimeshindwa rufani zao za kupinga adhabu ya kushiriki michuano
inayoandaliwa na shirikisho hilo. Fernabahce
ambao ilikuwa washiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu
walifungiwa kushiriki michuano yoyote ya Ulaya kwa misimu miwili huku
Besiktas ambao walifuzu kushiriki michuano ya Europa League wao
wamefungiwa msimu mmoja. Klabu
zote mbili zinatuhumiwa na kashfa ya upangaji matokeo katika baadhi ya
mechi za Ligi ya Kuu ya Soka nchini Uturuki mwaka 2011. Baada ya kugonga mwamba UEFA, klabu hizo bado zina haki ya kukata rufani katika Mahakama ya Usuluhishi ya Michezo-CAS.
Tuesday, July 16, 2013
FIFA BADO USO KWA USO NA CAMEROON KATIKA MICHEZO
Shirikisho la Soka
Duniani-FIFA limedai kuwa klabu ya Coton Sport ya Cameroon haitaruhusiwa
kucheza mechi yao ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika mwishoni mwa wiki
hii kwasababu ya adhabu iliyopewa Shirikisho la Soka la nchi
hiyo-Fecafoot na FIFA. Hatua
ya kuzuiwa kwa klabu hiyo kunazidi kuleta utata katika michuano hiyo
mikubwa kabisa ya vilabu barani Afrika huku mahasimu wa soka nchini
Misri klabu ya Zamalek na Al Ahly ambao ndio mabingwa watetezi nao
wakiwa hawajui hatma ya mechi baina yao kwasababu ya vrugu za kisiasa
zinazoendelea nchini humo. Timu
nane zilizofanikiwa kuvuka hatua ya makundi, ndio zinatarajiwa kuchuana
kutafuta washindi watakaocheza nusu fainali ya michuano hiyo katika
mechi zao za kwanza mwishoni mwa wiki hii. FIFA
imesema kuwa tayari wameshaanza mazungumzo kujaribu kutatua mgogoro wa
Cameroon lakini mpaka sasa hakuna lolote lililofikiwa mpaka kuwashawishi
kuondoa adhabu ya kuifungia nchi hiyo kushiriki michuano yoyote ya
kimataifa waliyoitoa Julai 4 mwaka huu. Kufungiwa
kwa Cameroon kumekuja kufuatia uchaguzi wa Juni 19 ambao Mohammed Iya
alichaguliwa tena kuongoza Fecafoot pamoja na kukamatwa kwa tuhuma za
matumizi mabaya ya fedha wakati akiongoza kampuni ya Cotton Development
Corporation inayomiliki timu ya Cotton Sport.
REAL MADRID YATAJWA KUWA CLUB YENYE THAMANI ZAIDI DUNIANI
CLUB ya Real Madrid ya
Hispania imetajwa kuwa klabu yenye thamani zaidi katika orodha ya timu
za michezo 50 zenye thamani zaidi duniani iliyotolewa na jarida Forbes
la nchini Marekani. Katika orodha hizo timu za Ligi Kuu ya Mpira wa Kimarekani-NFL ndizo zilizoonekana kutawala kwa kiasi kikubwa. Kwa
mujibu wa taarifa zilizochapishwa na jarida hilo Madrid ambao ni
mabingwa mara tisa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya wana utajiri unaofikia dola
bilioni 3.3, utajiri huo ukiwa umeongezeka kwa dola bilioni 1.88
kulinganisha na mwaka uliopita baada ya kuongeza mapato yao kwa kuingia
mikataba na kampuni za Adidas na Shirika la Ndege la Emirates. Manchester
United wamepigwa kikumbo na Madrid na kushuka mpaka nafasi ya pili
wakiwa na utajiri wa dola bilioni 3.17 wakati mabingwa wa Hispania
Barcelona wao wamekwea kutoka nafasi ya tano mpaka ya tatu wakiwa na
utajiri unaofikia dola bilioni 2.6. Nafasi
ya nne inashikiliwa na timu ya Baseball ya Marekani ya New York Yankees
ambao wana dola bilioni 2.3, wakifuatiwa na Dallas Cowboys ya NFL dola
bilioni 2.1 na New England Patriots dola bilioni 1.6. Nyingine
ni Los Angeles Dodgers ya baseball dola bilioni 1.6, timu za NFL
Washington Redskins na New York Giant pamoja na klabu ya soka ya Arsenal
ya Uingereza ambazo zote hizo zina utajiri wa dola bilioni 1.3.
KAMPUNI YA VIFAA VYA MICHEZO ADIDAS YA SIMAMISHA MKATABA WA TYSON GAY
Kampuni ya vifaa vya
michezo ya Adidas imesimamisha mkataba wake wa udhamini na mwanariadha
nyota wa mbio fupi Tyson Gay wa Marekani baada ya kukutwa na
chembechembe za dawa za kuongeza nguvu. Msemaji
wa kampuni alidai kuwa awameshtushwa na tuhuma hizo kwa Gay na hata
kama bado hajakutwa na hatia ya kosa hilo moja kwa moja kampuni
itasimamisha udhamini wake mpaka hapo hukumu itakapotolewa. Gay
mwenye umri wa miaka 30, ndio mwanariadha wa pili mwenye kasi zaidi
duniani katika mbio za mita 100 akiwa sambamba na Yohan Blake wa Jamaica
na pia ndiye mwanariadha aliyeweka rekodi ya kasi zaidi kwa mwaka huu. Nyota
huyo ambaye aliwahi kuwa bingwa wa dunia katika mbio za mita 100, 200
na mita 400 kupokezana vijiti mwaka 2007 alishindwa kukata tuhuma hizo
na kudai kuwa alimwamini mtu ambaye alimwangusha na hivyo atapokea
adhabu yoyote atakayopewa.
Sunday, July 14, 2013
Coastal Union yanasa saini ya Udula wa Bandari ya Kenya
Na Paul Mkai,Tanga.
UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga umesema tayari umeshamalizana na aliyekuwa mshambulizi wa timu ya Bandari ya Kenya,Christian Udula kwa mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuichezea timu kwenye msimu mpya ambao utaanza Agosti mwaka huu.
Akizungumza na Blogg hii,Katibu Mkuu wa timu ya Coastal Union ya Tanga,Kassim El Siagi alisema baada ya kumalizina na mchezaji huyo anatarajiwa kutua mkoani Tanga wiki ya leo akiwa na mchezaji mwengine wa timu hiyo Jerry Santos.
Siagi alisema msimu huu wamedhamiri kufanya usajili wa nguvu ambao utaifanya timu hiyo kuwa tishio kwenye mechi zao za Ligi kuu ya Tanzania bara kwani malengo yao ni kuchukua ubingwa wa mashindano hayo makubwa hapa nchini.
Aidha alisema timu hiyo itacheza mechi mbalimbali za majaribio nchini Kenya na timu za Sofapaka,Bandari na Goromahia lengo likiwa ni kukipa makali kikosi hicho ambacho kinatarajiwa kuwa tishio.
Katibu huyo aliwataka wapenzi na mashabiki wa timu hiyo kuendelea kujitokeza kuisapoti timu hiyo ili iweze kutimiza azma yao waliyojiwekea kwenye michuano hiyo.
Mwisho.
UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga umesema tayari umeshamalizana na aliyekuwa mshambulizi wa timu ya Bandari ya Kenya,Christian Udula kwa mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuichezea timu kwenye msimu mpya ambao utaanza Agosti mwaka huu.
Akizungumza na Blogg hii,Katibu Mkuu wa timu ya Coastal Union ya Tanga,Kassim El Siagi alisema baada ya kumalizina na mchezaji huyo anatarajiwa kutua mkoani Tanga wiki ya leo akiwa na mchezaji mwengine wa timu hiyo Jerry Santos.
Siagi alisema msimu huu wamedhamiri kufanya usajili wa nguvu ambao utaifanya timu hiyo kuwa tishio kwenye mechi zao za Ligi kuu ya Tanzania bara kwani malengo yao ni kuchukua ubingwa wa mashindano hayo makubwa hapa nchini.
Aidha alisema timu hiyo itacheza mechi mbalimbali za majaribio nchini Kenya na timu za Sofapaka,Bandari na Goromahia lengo likiwa ni kukipa makali kikosi hicho ambacho kinatarajiwa kuwa tishio.
Katibu huyo aliwataka wapenzi na mashabiki wa timu hiyo kuendelea kujitokeza kuisapoti timu hiyo ili iweze kutimiza azma yao waliyojiwekea kwenye michuano hiyo.
Mwisho.
Friday, July 12, 2013
KAMPUNI YA MADUKA NCHINI BRAZIL WATISHIA KWENDA MAHAKANI KUHUSU USAJILI NEYMAR

FIFA YA FUATILIA KWA KARIBU KASHFA YA UPANGAJI MATOKEO
SHIRIKISHO la Soka
Duniani-FIFA linafuatilia kwa karibu kashfa ya upangaji matokeo
inayozikabili vilabu viwili vya soka vya ridhaa nchini Nigeria
iliyotokea wiki iliyopita. Katika
matokeo ambayo yanaonekana kama ya mchezo wa kriketi, klabu ya Plateau
United Feeders iliibugiza Akurba FC kwa mabao 79-0 wakati Police Machine
wao waliitandika Bubayaro FC kwa mabao 67-0 mwishoni mwa wiki
iliyopita. Hatua uchunguzi kwa vilabu hivyo imekuja kutokana na timu hizo kuhitaji matokeo ya aina hiyo ili waweze kupanda daraja. Ambapo
katika taarifa yake FIFA imedai kuwa inafuatilia tukio hilo la tmu hizo
za Nigeria kwa karibu ili kuona jinsi gani Shirikisho la Soka la nchi
hiyo, NFF litatatua tatizo hilo. FIFA
inafanya hivyo kwa kutambua kuwa suala hilo ni la ndani hivyo NFF ina
wajibu wa kufanya uchunguzi na kuchukua hatua zinazostahiki kama
ikigundulika aina yoyote ya udanganyifu katika mechi hizo.
Subscribe to:
Posts (Atom)