Sunday, July 21, 2013

WAGOSI WA KAYA WAJIPANGA NA MECHI YA KIRAFIKI VS URA YA UGANDA

TIMU ya Wagosi wa wakaya Coastal Union ya Tanga Mabingwa ya ligi kuu mnamo mwaka 1988 inataraji kushuka dimbani kucheza mechi ya Kirafiki ya Kimataifa na Mabingwa wa soka Uganda URA Jumatano wiki ijayo kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mkoani Tanga.
Athibtisha taarifa hizo,Mwenyekiti wa timu hiyo,Hemed Aurora "Mpiganaji"alisema ni kweli mechi hiyo ipo na kinachofanyika hivi sasa ni kufanya mazungumzo ya mwisho na uongozi wa timu hiyo ili iweze kutua mkoani hapa kwa ajili ya mchezo huo.
Aurora alisema baada ya kumalizika mechi hiyo kikosi cha timu hiyo kitaondoka mkoani Tanga kuelekea Mombasa nchini Kenya kucheza mechi ya kirafiki na timu ya Bandari lengo likiwa ni kukiimarisha kikosi hicho kabla ya kuanza msimu mpya wa Ligi kuu.
Licha ya kucheza na Bandari lakini pia wapo kwenye mikakati ya kuzungumza na uongozi wa Yanga ili kuweza kucheza nao mechi ya majaribio siku ya Iddi Pili kwenye dimba hilo la Mkwakwani ambapo alisema anaamini mazungumzo hayo yatafanikiwa.

Mwenyekiti huyo amebainisha kuwa lengo la timu hiyo msimu ujao ni kuhakikisha wanafanya vizuri ili kuweza kurudisha heshima yao ya mwaka 1988 ya kuchukua ubingwa wa Ligi hiyo na kueleza hilo linawezekana kutokana na mshikamano uliopo baina ya wapenzi,wanachama na uongozi wao.
Akizungumzia maandalizi ya mechi hiyo ,Meneja wa uwanja wa CCM Mkwakwani,Mbwana Msumari alisema kwa mara ya mwisho uwanja huo kulichezwa mechi ya kimataifa mwaka 1988 kati ya African Sports na timu kutoka nchini Swithland wakati huo African Sports ni mabingwa wa Kombe la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Msumari alisema na mwaka huo huo ,Coastal Union wakacheza na Cost De Solver ya Msumbuji ambayo ilikuwa ikishiriki mashindano ya Klabu bingwa kwa hiyo anaamini mechi hiyo itakuwa na mvuto wa aina yake kutokana na historia ya timu hiyo.

NAPOLI YATANGAZA KUMSAJILI BEKI WA MADRID YA HISPANIA RAUL ALBIOL

Club ya Napoli ya nchin Italia imetangaza kumsajili beki mahiri wa klabu ya Real Madrid ya Hispania Raul Albiol. Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo imeeleza kuwa beki huyo wa kati mwenye umri wa miaka 27 amesajiliwa kwa mkataba wa miaka minne ambapo taarifa hiyo haikufafanua thamani halisi waliyomnunulia mchezaji huyo. 
Napoli kwasasaiajipanga kuimarisha kikosi chake kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu nchini Italia na Ligi ya Mabingwa Ulaya huku wakiwa na fedha za kutosha kutumia baada ya kumuuza mshambuliaji wa kimataifa wa Uruguay Edinson Cavani kwenda Paris Saint Germain kwa ada ya euro milioni 64. Albion ambaye ametoka katika shule ya soka ya Valencia akiwa kama mchezaji wa kiungo aliibuka katika kikosi cha kwanza cha klabu hiyo mwaka 2003 wakati huo ikifundishwa na kocha wa mpya wa Napoli Rafa Benitez kabla ya kuhamia Madrid mwaka 2009 ambako muda mwingi alitumika kama mchezaji wa akiba. Pamoja na kukosa namba klabuni kwake alifanikiwa kupata nafasi katika kikosi cha timu ya taifa ya Hispania katika michuano ya Kombe la Dunia 2010 na michuano ya Ulaya mwaka jana.

CAF YATEU MUAMUZI KUTOKA MADAGASCAR KUCHEZESHA MECHI KATI YA TANZANIA VS UGANDA

Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Madagascar kuchezesha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Uganda (The Cranes) itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja wa Mandela ulioko Namboole nje kidogo ya Jiji la Kampala. Waamuzi wataongozwa na Kanoso Abdoul Ohabee wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Andirvoavonjy Pierre Jean Eric. Mwamuzi msaidizi namba mbili ni Jinoro Velomanana Ferdinand huku Andriamiharisoa Hubert Marie Bruno akiwa mwamuzi wa mezani (fourth official). Kamishna wa mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya mwisho kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) ni Ismail Kamal kutoka Ethiopia. Mechi hiyo namba 38 itachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki. Taifa Stars ilipoteza mechi ya kwanza iliyochezwa Julai 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa bao 1-0. Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini jijini Mwanza ikijiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza Fainali za CHAN mwakani nchini Afrika Kusini.

Friday, July 19, 2013

WENGER ARUSIWA KUONGEZA DAU KUHUSU SUAREZ

KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger ameruhusiwa kuongeza ofa kufikia paundi milioni 40 kwa ajili ya kuiwinda saini ya mshambuliaji nyota wa Liverpool Luis Suarez. Mshambulijai huyo wa kimataifa wa Uruguay ndiye mchezaji anayepewa kipaumbele kusajiliwa na Arsenal msimu huu wa majira ya kiangazi ambapo tayari ofa yao ya kwanza ya paundi milioni 30 ilikataliwa na klabu hiyo.  
Mapema wiki hii kulikuwa na tetesi kuwa Arsenal walianzisha mazungumzo na maofisa wa Liverpool kwa kutoa ofa ya paundi milioni 35 lakini nayo ilikataliwa na kuweka wazi kuwa kiasi hicho hakikutosha. Lakini ofa mpya ya paundi milioni 40 inatarajiwa kutikisa mkataba wa Suarez huku wakala wake akidai kuwa ofa hiyo inashawishi hivyo Liverpool wanatakiwa kuisikiliza.

DAVID MOYES ASISITIZA KUHUSU ROONEY-USAJILI

KOCHA wa klabu ya Manchester United, David Moyes kwa mara nyingine tena amesisitiza kuwa Wayne Rooney hawezi kuuzwa baada ya Chelsea kudai kuwa mshambuliaji wa kimataifa wa Uingereza ndio chaguo lao katika kipindi hiki cha usajili majira ya kiangazi. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Sydney, Australia katika ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya, Moyes amesema msimamo wa klabu kuhusiana na mustakabali wa nyota huyo bado haujabadilika. Akitupiwa swali lingine kuhusiana na suala ofa iliyotolewa na United kwa ajili ya kumnasa kiungo wa Barcelona, Cesc Fabregas, Moyes amesema hajajua suala hilo linaendeleaje lakini anategemea katika siku mbili zijazo atafahamishwa na maofisa wa United maendeleo yake. Ofa ya kwanza ya meneja mpya wa Chelsea Jose Mourinho kutaka kumsajili nyota huyo tayari imekataliwa na United lakini klabu hiyo bado imeendelea kufuatilia nyendo za nyota huyo.

MBUYU TWITE "MAJERUHI KUIKOSA URA'

Beki mahiri mwenye nguvu na kasi Mbuyi Twite ataikosa mechi ya keshokutwa wakati Yanga itakapowavaa URA, timu inayomilikiwa na kampuni ya watoza kodi ya mapato ya Uganda.

URA itakuwa nchini kucheza mechi mbili za kirafiki, ikianza na Simba kesho kabla ya kuivaa Yanga, keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Twite amesema ataikosa mechi hiyo kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya goti ingawa amekuwa akifanya mazoezi taratibu.

Awali Yanga ilikuwa icheze mechi ya kirafiki dhidi ya 3 Pillars ya Nigeria, jana lakini ikagundulika timmu hiyo ilikuwa bagumashi kupita kiasi.

TFF ikapoga stop mchezo huo kwa kuwa Wanigeria hao walikuwa wameokotana lakini walitaka kucheza na mabingwa wa Tanzania.

TFF YAIPIGA STOPU TIMU ‘FEKI’ TOKA NIGERIA!!


KATIBU MKUU wa TFF, Angetilie Osiah, amesema wamefuta Mechi za Klabu kutoka Nigeria, FC 3 Pillars, walizokuwa wacheze Nchini baada ya Shirikisho la Soka la Nigeria, NFF, kusema haijui lolote kuhusu Timu hiyo na Ziara yake.

Kwa mujibu wa Osiah, imebidi TFF waifute Ziara hiyo ya Klabu hiyo ya Nigeria kwa sababu Kanuni za FIFA haziruhusu Timu kucheza nje ya Nchi zao bila Kibali toka kwa Mamlaka ya Soka ya Nchini kwao.

Vile vile TFF imesema FC 3 Pillars haijapandishwa Daraja kucheza Ligi Kuu ya Nigeria, NPL [Nigeria Premier League] kama vile tamko la Waandaaji wa Ziara yao Nchini, SportLink International, walivyodai kwenye Matangazo yao.

Jana FC 3 Pillars ilikuwa icheze na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam na pia Timu hiyo ilipangiwa kucheza na Coastal Union na Mbeya City, ambayo Msimu huu unaokuja itacheza Ligi Kuu Vodacom baada ya kupanda Daraja.

Licha ya kuifuta Ziara ya FC 3 Pillars, pia Katibu Mkuu wa TFF, Angetiilie Osiah, alibainisha kuwa hata hao Waandaaji, SportLink International, hawajasaliwa na FIFA kwa ajili ya kuandaa Mechi za Kimataifa kama vile taratibu zinavyotaka.

Akiongeza, Osiah alivitaka Vyama vya Soka vya Mikoa viwe waangalifu wasidanganywe na Wajanja wanaoleta Timu toka nje bila ya kufuata taratibu zilizowekwa.