Tuesday, August 26, 2014

KOCHA WA POLISI MORO AWATAKA WACHEZAJI WAKE KUJITUMA VPL.


Kocha Mkuu wa Polisi Morogoro Adolf’ Rishard ameweka wazi kuhusu timu yake timu yake ifanye vizuri msimu huu, wachezaji wanatakiwa wajitume, washikamane na kucheza kama timu moja.

Adolf ameyasema hayo wakati akizungumza na mtandao huu ambapo amesema ushindi unawezekana kama wachezaji wake watakuwa wanazingatia maelekezo wanayopewa.
Adolf amesema malengo yetu makubwa msimu ujao ni kufanya vizuri, na hayo yote yatawezekana kutokana na jinsi wachezaji watakavyojituma na kucheza kiushindani.
Katika kuhakikisha lengo linatimia tayari imeshafanya usajili wa wachezaji kadhaa wakiwamo Salum Machaku, Edward Chistopher aliyekuwa Simba, Dan Mrwanda, Labana Kambone wa Rhino Rangers, Toni Kavishe wa Mgambo JKT, Seleman Selembi wa Coastal Union na Mohamed Mpopo wa Villa Squad.

NOOIJ AITA 26 STARS KUIKABILI MOROCCO SEPTEMBA 5 MWAKA HUU.

Kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij ametangaza kikosi cha wachezaji 26 kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya FIFA Date dhidi
ya Morocco itakayochezwa Septemba 5 mwaka huu nchini Morocco.
Wachezaji walioitwa ni makipa Deogratias Munishi (Yanga) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni Said Morad (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Shomari Kapombe (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondani (Azam), Aggrey Morris (Azam), Joram Mgeveke (Simba) na Charles Edward (Yanga).
Viungo ni Erasto Nyoni (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Amri Kiemba (Simba), Himid Mao (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Ndemla (Simba), Said Juma (Yanga) na Haruna Chanongo (Simba).
Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Khamis Mcha (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Yanga), Mwegane Yeya (Mbeya City) na Juma Liuzio 9ZESCO, Zambia).
Timu hiyo itaingia kambini Jumapili (Agosti 31 mwaka huu) mchana katika hoteli ya Accomondia.
                      Mart Nooij
Taarifa Binafsi
Full nameMartinus Ignatius Nooij 
Date of birthJune 3, 1954 (age 60)
Place of birthHeemskerkNetherlands
Timu anayofundisha
Current team
Tanzania
Timu alizofundisha
YearsTeam
2003Burkina Faso U20
2007–2011Mozambique
2012Santos Cape Town
2013–2014Saint George
2014–Tanzania

Monday, August 25, 2014

KUFUATIA KIFO CHA MCHEZAJI ALGERIA YASIMAMISHA LIGI

SHIRIKISHO la Soka nchini Algeria limesimamisha Ligi Kuu kufuatia kifo cha mchezaji wa Cameroon Albert Ebosse ambaye alipigwa na jiwe lililorushwa na mashabiki. Uamuzi huo umefikiwa jana katika kikao kilichofanyika jana. Ebosse mwenye umri wa miaka 24 alipigwa na jiwe kichwani wakati akitoka uwanjani baada ya timu yake ya JS Kabylie kufungwa na USM Alger huko Tizi Ouzou juzi. Tayari mamlaka inayohusika imeshaufungia Uwanja wa 1st Novemba 1954 kulikotokea tukio hilo. Shirikisho hilo pia limeamua kutoa ubani wa dola 100,000 kwa familia ya Ebosse kiwango ambacho kinaaminika angeweza kukipata katika kipindi cha mkataba wake huku wachezaji wa Kabylie nao wakitoa mishahara yao ya mwezi kama rambirambi ya kufariki kwa mwenzao. Imegundulika kuwa uwanja wa 1st Novemba 1954 ulikuwa katika matengenezo wakati wa mchezo huo na mashabiki walitumiwe mawe ya ujenzi yaliyokuwa yamewekwa maeneo hayo.

Albert Ebossé Bodjongo
Taarifa binafsi
Full nameAlbert Dominique Ebossé Bodjongo Dika
Date of birth6 October 1989
Place of birthDoualaCameroon
Date of death23 August 2014 (aged 24)
Place of deathTizi OuzouAlgeria
Height1.85 m (6 ft 1 in)
Playing positionForward
Timu ya ukubwani
YearsTeamMechiGoli
2008–2010Coton Sport FC
2010–2011Unisport Bafang
2011–2012Douala AC10(9)
2012–2013Perak FA16(11)
2013–2014JS Kabylie32(19)
Timu ya taifa
2009Cameroon U20

RONALDO YUKO POA SANA KUIKABILI CORDOBA.

MSHAMBULIAJI mahiri wa klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo anaweza kuanza katika mchezo wa ufunguzi wa La Liga dhidi ya timu iliyopanda daraja ya Cordoba pamoja na kushambuliwa na majeruhi. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno alitokea benchi katika mchezo wa Super Cup uliochezwa Ijumaa iliyopita na kufungwa na Atletico Madrid. Meneja wa Madrid Carlo Ancelotti amesema Ronaldo amefanya mazoezi vyema hivyo anaweza kumpanga katika kikosi chake. Ancelottio alikiri kuwa wakati wa maandalizi ya msimu alikuwa akisumbuliwa na majeruhi hivyo anahitaji kufanya jitihada ili aweze kurejea katika kiwangop chake. Ronaldo mwenye umri wa miaka 29 ambaye anashikilia tuzo ya mchezaji bora wa dunia alipata majeruhi ya mgongo wakati timu hizo mbili zilipotoa sare ya bao 1-1 katika mchezo wa mkondo wa kwanza.
Cristiano Ronaldo
Cristiano Ronaldo - Croatia vs. Portugal, 10th June 2013.jpg
Ronaldo playing for Portugal in 2013
Taarifa Binafsi
Full nameCristiano Ronaldo dos Santos Aveiro
Date of birth5 February 1985 (age 29)[1]
Place of birthFunchalMadeira, Portugal
Height1.85 m (6 ft 1 in)[2]
Playing positionForward
Club anayocheza
Current team
Real Madrid
Number7
acadaemy
1992–1995Andorinha
1995–1997Nacional
1997–2002Sporting CP
Timu za ukubwani
YearsTeamMechiGoli
2002–2003Sporting CP25(3)
2003–2009Manchester United196(84)
2009–Real Madrid165(177)
Timu ya taifa
2001Portugal U159(7)
2001–2002Portugal U177(5)
2003Portugal U205(1)
2002–2003Portugal U2110(3)
2004Portugal U233(2)
2003–Portugal114(50)

TFF YAOMBA KUANDA MECHI ZA MASHINDANO YA AFCON 2017

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) chini ya Rais wake, Jamal Malinzi, limeomba kuadaa mashindano ya Kombe la Taifa Africa (Afcon).
TFF imetuma barua kwa Shirkisho la Soka Afrika (Caf) kuomba kuandaa mashindano yatakayofanyika 2017.

TFF imechukau uamuzi huo baada ya Caf kuifuta Libya iliyopanga kuandaa michuano hiyo mwaka 2017 kutokana na vurugu.

TFF imesema inaamini kuna miundombinu ya kutosha kuandaa michuano hiyo na tayari barua imetumwa Caf.
Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Celestine amesema barua ya maombi kwenda imeshatumwa. 

WAMBURA HUYOO SASA MKURUGENZI WA MASHINDANO TFF

Aliyekuwa Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura Nyota emeendelea kunga’aa katika anga la kichezo ambapo sasa atakuwa Mkurugenzi wa Mashindano wa shirikisho hilo.

Wambura amepata nafasi hiyo baada ya TFF kuamua kumpandisha cheo na sasa anaicha ile nafasi yake ya ofisa habari.


Katibu Mkuu wa TFF, Mwesugwa Celestine ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar.