Hawa ni washindi wa Ligi Kuu
Tanzania Bara tangu mwaka 1965. Katika rekodi hii klabu ya Yanga
imetwaa taji hilo mara 24, Simba mara 18 na mtibwa mara 2, nyingine zote
zilizopoa hapa zimetwaa mara moja. Tarehe 20 ligi itaanza tena ya msimu
wa 2014/15, Je Unadhani timu gani ipo katika nafasi ya kushinda taji
hilo msimu huu?
Thursday, September 11, 2014
WEKUNDU WA MSIMBAZI KUTIFUANA NA URA YA UGANDA
Simba Wekundu wa msimbazi SC kesho wanatarajia kushuka dimbani kuonyeshana kazi katika Mechi ya pili ya kimataifa ya kirafiki chini ya kocha Patrick Phiri
dhidi ya timu ya mamlaka ya ukusanyaji wa mapato nchini Uganda, URA katika uwanja wa Taifa jijini Dar es slaam katika mtanange utakao anza majira ya saa 11:00 jioni kwa saa za Afrika mashariki.
Wakati huo huo jumamosi jioni,
Simba itakuwa na mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Ndanda fc katika
uwanja wa Nangwanda Sijaona mk
oani Mtwara katika maadhimisho ya ‘Ndanda
fc Day’.
TAREHE NDONI YA TAIFA 2014 2014 YAPIGWA KALENDA
Shirikisho la ngumi Tanzania (BFT)
limesogeza tarehe ya kufanyika kwa mashindano ya ngumi ya Taifa na sasa
yatafanyika kuanzia tarehe 03-08/11/2014.Dar es salaam.
Awali mashindano hayo yalikuwa yamepangwa kufanyika tarehe 08-14/10/2014 Dar es salaam.
Sababu za kusogeza mashindano hayo
ni kuyapisha mashindano ya ngumi ya kimataifa yaliyoandaliwa na chama
cha ngumi wilaya ya Temeke yanayotarajia kuanza kufanyika mwishoni mwa
mwezi huu, lakini pia ni kutoa nafasi zaidi kwa mikoa ili kujiandaa
vizuri na kufanya mashindano ya kuwapata wawakilishi wa mikoa yao katika
mashindano ya taifa.
BFT tunawataki maandalizi mema na tunatoa wito kwa maafisa michezo
wa mikoa yote ya Tanzania bara kuhakikisha wanaleta wachezaji kutoka
katika mikoa yao ili kuleta upinzani utakaopelekea kupata timu ya taifa
iliyo bora kutoka katika mikoa yote ya Tanzania bara.
Aidha BFT inawapongeza kampuni ya
simu za mkononi ya Z antel kwa udhamini wa mashindano hayo kwa
kutoa kiasi cha Tsh. 10,000,000/=ambazo zitasaidia baadhi ya mahitaji ya
msingi ya kufanikisha mashindano hayo.
MWAMBUSI ASEMA PHIRI, MAXIMO, ASEMA NGOMA DAKIKA 90.

Akizungumza na mtandao huu,
Mwambusi amesema kocha Phiri ana historia ya kufundisha soka la Tanzania
kwa ngazi ya klabu wakati Maximo amefundisha timu ya Taifa, lakini wote
wataleta changamoto nzuri kwake.
Wednesday, September 10, 2014
JE TUFIKA KUHUSU TAIFA STARS HII AMA NDIO MWISHO
Hakuna kitu kinawaumiza watanzania kuhusu kilio kikubwa cha wadau na wapenzi wa soka nchini Tanzania ni kuitaka serikali, TFF na vyama wanachama wake pamoja na klabu zote kuwekeza katika soka la vijana kwa manufaa ya Taifa.

Aina ya wachezaji wanaopatikana Tanzania ni wale wasiokuwa na misingi ya mpira tangu utotoni, kwasababu hakuna akademi za kisasa na hata za kawaida kwa maeneo mengi ya nchi hii, hivyo vijana wenye vipaji vya soka hujikuta hawana kwa kujiendeleza.
Soka la vijana ni muhimu na lazima Taifa kama Taifa liandae mpango mkakati wa kitaifa kwa malengo ya kuwa na falsafa ya Taifa na mfumo sahihi wa kuibua, kukuza na kulinda vipaji vya soka.
Marsh aliachishwa kazi ya kuinoa Stars sambamba na kocha Mdenish, Kim Poulsen kwa madai ya wawili hao kushindwa kufikia malengo yaliyowekwa na Shirikisho la soka la Tanzania, TFF.
Hata hivyo wakati Kim anavunjiwa mkataba, Mashi alikuwa wodini akipata matibabu kutokana na kusumbuliwa na maradhi.
Usidhani huwa anakaa bure. Marsh ni moja ya watu wachache nchini wenye kiu ya kuona soka la nchi hii linapiga hatua.
Tangu mwaka 1991 anamiliki kituo chake cha kuibua, kulea na kukuza vipaji mkoani mwanza.
WADHAMINI WA VPL WAGAWA JEZI KWA TIMU ZA VPL KWA AJILI YA SEPT 20 VPL
Ikiwa zimebaki siku 10 kuanza kwa msimu mpya wa ligi kuu msimu wa 2014-2015 wadhamini wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Vodacom watoa jezi kwa vilabu vyote 14 vitakavyoshiriki ligi hiyo.
Katika hafla ya kukabidhi vifaa kwa timu za Ligi Kuu msimu mpya leo, Vodacom wamekabidhi jezi za rangi ya kijani na njano kwa Yanga na nyekundu na nyeupe kwa Simba, lakini muundo ni mmoja kila kitu.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) liliwakilishwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ ambaye alihakikisha timu zote 14 za Ligi Kuu zinapatiwa vifaa hivyo.
Timu zote 14 zilituma wawakilishi wao katika hafla hiyo iliyofanyika makao makuu ya Vodacom, Mlimani City, Dar es Salaam.
Ligi Kuu inatarajiwa kuanza Septemba 20, mwaka huu, mabingwa watetezi, Azam FC wakifungua dimba na Polisi Morogoro Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Mechi nyingine za ufunguzi za Ligi Kuu zitakuwa kati ya Stand United watakaoikaribisha Ndanda ya Mtwara Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Mgambo JKT wataikaribisha Kagera Sugar Uwanja wa Mkwakwani, Tanga na Ruvu Shooting watakuwa wenyeji wa Prisons Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.
Mabingwa wa zamani wa ligi hiyo, Simba SC wataanza kampeni ya kutwaa tena taji hilo Septemba 21 dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ligi hiyo itatanguliwa na mchezo wa Ngao ya Jamii utakaochezwa Jumapili wiki hii, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kati ya Azam FC na Yanga SC.
MAJIMAJI YAWEKA HADHARANI KIKOSI CHAKE KWA AJILI YA LIGI DARAJA LA KWANZA
ya zamani Tanzania, Majimaji FC WANALIZOMBE ya Songea mkoani Ruvuma imetaja kikosi cha wachezaji 26 iliyowasajili kwa ajili ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara msimu wa 2014-2015.

Amewataja wachezaji wa zamani 14 watakaoendelea kuitumikia klabu hiyo kuwa ni pamoja na Anthony Mwingira, Eliuta Ndunguru, Bahati Yussuf, Gerarrd Mbena, Abdallah Aus, Ditram Nchimbi, Filoteus Mahundi, Mpoki Mwakinyuke, Alex Zegega, Sadiq Gawaza, Odo Nombo, Frank Sekule, Marcel Boniventure na Freddy Mbuna.
Subscribe to:
Posts (Atom)