Kiungo nyota wa Club ya
Borussia Dortmund, Nuri Sahin ameonyesha furaha na shauku kwa usajili uliofanywa
na klabu hiyo huku akiwa na matumaini ya kupiku utawala wa wapinzani wao
Bayern Munich katika soka la Ujerumani.
Ujio
wa wachezaji kama Pierre-Emerick Aubameyang, Henrikh Mikhitaryan na
Sokratis Papastathopoulous katika kikosi cha Jurgen Klopp kunategemewa
kuisimamisha Bayern kurudia mafanikio ya kushinda mataji yote matatu
nchini humo.
Sahin, ambaye amebakisha miezi 12 ya mkopo kutoka klabu ya Real Madrid ana matumaini usajili huo unaweza kuwaongezea nguvu ili kupambana na Bayern ambao kwasasa wametawala soka la nchi hiyo. Dortmund walitolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na DFB-Pokal na Bayern msimu uliopita huku pia wakimaliza nyuma kwa alama 25 mbele ya Bayern ambayo ndio walikuwa mabingwa wa Bundesliga.

Sahin, ambaye amebakisha miezi 12 ya mkopo kutoka klabu ya Real Madrid ana matumaini usajili huo unaweza kuwaongezea nguvu ili kupambana na Bayern ambao kwasasa wametawala soka la nchi hiyo. Dortmund walitolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na DFB-Pokal na Bayern msimu uliopita huku pia wakimaliza nyuma kwa alama 25 mbele ya Bayern ambayo ndio walikuwa mabingwa wa Bundesliga.