Wednesday, July 17, 2013

NURI SAHIN APATA FARAJA KWA USAJILI WA BORUSSIA DORTMUND"

Kiungo nyota wa Club ya Borussia Dortmund, Nuri Sahin ameonyesha furaha na shauku kwa usajili uliofanywa na klabu hiyo huku akiwa na matumaini ya kupiku utawala wa wapinzani wao Bayern Munich katika soka la Ujerumani. 
Ujio wa wachezaji kama Pierre-Emerick Aubameyang, Henrikh Mikhitaryan na Sokratis Papastathopoulous katika kikosi cha Jurgen Klopp kunategemewa kuisimamisha Bayern kurudia mafanikio ya kushinda mataji yote matatu nchini humo.  
Sahin, ambaye amebakisha miezi 12 ya mkopo kutoka klabu ya Real Madrid ana matumaini usajili huo unaweza kuwaongezea nguvu ili kupambana na Bayern ambao kwasasa wametawala soka la nchi hiyo. Dortmund walitolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na DFB-Pokal na Bayern msimu uliopita huku pia wakimaliza nyuma kwa alama 25 mbele ya Bayern ambayo ndio walikuwa mabingwa wa Bundesliga.

LIGI KUU NCHINI MISRI YAWEKWA KAPUNI KWA SABABU ZA KIUSALAMA"

Ligi Kuu ya kandanda nchini Misri imesimamishwa kwasababu za kiusalama kufuatia jeshi la nchi hiyo kumuondoa rais Mohamed Mursi madarakani mapma mwezi huu. Shirikisho la Soka la nchi hiyo lilitangaza rasmi kusitisha msimu wa ligi wa 2012-2013 huku kukiwa kumebaki mzunguko mmoja msimu kumalizika na timu nne kucheza hatua ya mtoano kwa ajili ya kumpata bingwa. Kwa zaidi ya wiki mbili toka jeshi limuondoe Mursi baada ya maandamano makubwa ya kumpinga, kumekuwa na vurugu huku watu zaidi ya saba wakiripotiwa kufa katika mapigano baina waislamu waliokuwa upande wa Mursi na wengine waliokuwa wakimpinga rais huyo. Hii ni mara ya pili katia kipindi cha miaka miwili ligi kusimamishwa katikati ya msimu baada ya mapema mwaka jana ligi hiyo kusitishwa tena kutokana na vurugu zilizotokea Port Said na kusababisha vifo vya mashabiki wapatao 74.

MARTINA ATARAJI KUREJEA TENA KAZINI KATIKA MCHEZO HUU"

Martina Hingis ambae ni mwanadada nyota wa tenisi wa zamani,  kutoka Switzerland anatarajiwa kurejea tena katika ulingo wa tenisi baada ya kustaafu mchezo huo mwaka 2007. Hingis mwenye umri wa miaka 32 amekubali mwaliko wa kucheza michuano ya wazi ya California ya wawili wawili akiwa sambamba na Daniela Hantuchova baadae mwezi huu. Nyota huyo ambaye amewahi kushinda mataji matano ya Grand Slam kwa mchezaji mmoja mmoja likiwemo taji la Wimbledon mwaka 1997 akiwa na umri wa miaka 16, Jumamosi iliyopita alichaguliwa kuwa mmoja wa wachezaji mashuhuri wa mchezo huo kuwahi kutokea. Akihojiwa kuhusiana na uamuzi huo wa kurejea uwanjani baada ya kupita kipindi kirefu, Hingis ambaye pia amewahi kushika namba moja katika orodha za ubora duniani kwa upande wa wanawake amesema bado anahisi kuwa na ari ya ushindani ndani ya nafsi yake. Mara ya kwanza Hingis alistaafu mchezo huo akiwa na miaka 22 baada ya kusumbuliwa na majeraha lakini alirejea tena mwaka 2006 kabla ya kustaafu tena mwaka 2007 baada ya kukutwa na chembechembe ya dawa za kusisimua misuli ingawa mwenyewe alikana tuhuma hizo.

CAF YATANGAZA KUSOGEZA MBELE MCHEZO WA LIGI YA MABINGWA KATI YA WATANI WA JADI"

Shirikisho la kandanda Barani Afrika-CAF limesogeza mbele mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Afrika ambao unawakutanisha watani wa jadi nchini Misri timu za Zamalek na Al Ahly mpaka Jumatatu ijayo.  
Vigogo hao wa soka nchini humo walitarajiwa kucheza Jumapili katika mji wa El Gouna ambao uko kilometa 500 kutoka mji mkuu wa Cairo kutokana na sababu za kiusalama. Katika taarifa iliyotolewa katika mtandao wa Zamalek, wamethibitisha kuwa FIFA imekubali mchezo huo kuchezwa El Gouna pamoja na kwamba uwanja huo haukuwepo katika ratiba za michuano hiyo na kuamua kuchelewesha mchezo huo kwa siku moja kwasababu za kibiashara. Wizara ya mambo ya ndani ya nchi hiyo ilikataa mapema kuhakikisha usalama wa mechi hiyo kuchezwa jijini Cairo au Alexandria kabla ya Zamalek kuchagua El Gouna.

WAKALA WA SUAREZ ASEMA KAMA KUNA CLUB INAMTAKA MCHEZAJI HUYO IWEKE MEZANI KITITA CHA NGUVU

Wakala wa mshambulaij  nyota wa klabu ya Liverpool na timu ya taifa ya Uruguay" Luis Suarez’ amebainisha na kuweka wazi kama kuna klabu inahitaji kumsajili nyota huyo lazima iandae dau la nono la pauni miliaoni 40 ili kupata huduma yake.

Klabu ya Liverpool imesema itasikiliza ofa ya pauni milioni 40, lakini kuna uwezekano wa ofa hiyo kupanda mpaka kufikia pauni milioni 50 kumnunua nyota huyo mwenye matukio ya aina yake nchini England, likiwemo la kumng`ata beki wa Chelsea,  Ivanovic na kusimamishwa mechi kumi, pamoja na tuhuma za ubaguzi wa rangi kwa beki wa mabingwa wa soka nchini Englanda, Manchester United, Mfaransa Patrick Evra.

Wakala wa Suarez bwana Pere Guardiola, ambaye ni kaka yake kocha wa wekundu wa kusini mwa Ujerumani, The Bavarian, klabu ya Bayern Munich , Joseph Pep Guardiola , amasema atakaa mezani na klabu yoyote yenye uwezo wa kuweka mezani mzigo wa pauni milioni 40.

Ambapo sasa Baadhi ya Klabu kubwa barani Ulaya zinataka kuinasa saini ya Luis Suarez kutoka kwa majogoo wa jiji.

Arsenal ni klabu pekee yenye mpango wa nguvu zaidi kutaka kumsajili Suarez kwa pauni milioni 35, lakini ofa hiyo inaonkana haina maana kwa wekundu wa Anfield waliotangaza pauni milioni 40.

Awali Asernal walituma ofa ya pauni milioni 30, Liver wakatupilia mbali, wakaongeza tano, bado wakagomewa kabisa kwani wanataka 40 tu, huna mzigo huo basi amekosa huduma ya nyota huyo.

Saurez ambaye atajiunga na Liverpool waliopo  Melbourne jumatatu ijayo, ana mkataba na Liverpool mpaka mwaka 2016. Lakini Liver wameonekana kuwa na msimamo wa kumbakisha, huku klabu za Arsena, Real Madrid na Chelsea zakiimarisha rada zao kutaka kumsajili.

UONGOZI WA YANGA WAWATAKA MASHABIKI KUJITOKEZA KWA WINGI"

Club ya Yanga ya jangwani kupitia uongozi wake waumewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi katika mechi ya kimataifa ya kirafiki itakayochezwa Julai 18 mwaka huu.
Mechi hiyo kimataifa ya Kirafiki dhidi ya timu ya 3 Pillars ya Nigeria inataraji kutimua vumbi Julai 18 mwaka huu katika uwanja wa Taifa.
Mechi hiyo ni sehemu ya maandalizi ya klabu zote mbili kabla ya ligi kuu kuanza mwezi ujao  ambapo Yanga pia inajinoa kwa ajili ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika.
Mratibu wa mechi Salum Mkemi amesema kikosi cha wachezaji 17 na viongozi na makocha wao wapo jijini Dar es Salaam wakijifua kwa ajili mtanange huo utakaochezwa katika uwanja wa Taifa.
Mkemi amesema pia timu ya 3 Pillars ambayo imepanda daraja la ligi kuu nchini Nigeria inataraji kujipima na Coastal Union ya Tanga huku wakifanya mazungumzo na Mbeya City kwa ajili ya mechi nyingine za Kirafiki.
Katibu mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako amesema wachezaji wako kambini kujiwinda na michuano ya ligi kuu na kuongeza kuwa wana morali kuelekea mchezo huo.
Mratibu wa mechi ametangaza Viingilio vya mechi hiyo vitakuwa kati ya shilingi elfu tatu na elfu 15 ili kuwawezesha mashabiki wengi zaidi kuhudhuria kipute hicho.
Timu ya 3 Pillars inataraji kurejea nchini Nigeria Julai 30 mwaka huu.

Tuesday, July 16, 2013

KUTOA OFA PAUNI MILIONI 40 KUMNUNUA HULK--CHELSEA

Katika harakati za usajili baada ya kuikosa saini ya kumnasa Straika hatari wa Uruguay, Edinson Cavani, ambae sasa yuko njiani kukamilisha ku

hamia PSG kutoka Napoli, Chelsea sasa imemgeukia Straika wa Klabu ya Urusi Zenit St Petersburg, Hulk, anaetoka Brazil.
Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho, ana nia ya kuongeza safu yake ya Ushambuliaji na tayari ameshamnunua Mchezaji wa Germany Andre Schurrle huku kukiwa na tetesi Mastraika wa sasa, Fernando Torres na Demba Ba, huenda wakapigwa bei.
Katika Msimu wake wa kwanza na Zenit, Hulk alifunga Bao 11 katika Mechi 30 na kabla hajahamia huko Urusi, akiwa huko Portugal na FC Porto, Hulk aliifungia Klabu hiyo Bao 54 katika Mechi 99 za Primera Liga na Jumla ya Mabao yake kwa FC Porto ni 78.
Inadaiwa Chelsea imetoa Ofa ya kwanza ya Pauni Milioni 40 kwa Mchezaji alienunuliwa Septemba Mwaka Jana kwa Pauni Milioni 35.