Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho, ana
nia ya kuongeza safu yake ya Ushambuliaji na tayari ameshamnunua
Mchezaji wa Germany Andre Schurrle huku kukiwa na tetesi Mastraika wa
sasa, Fernando Torres na Demba Ba, huenda wakapigwa bei.
Katika Msimu wake wa kwanza na Zenit,
Hulk alifunga Bao 11 katika Mechi 30 na kabla hajahamia huko Urusi,
akiwa huko Portugal na FC Porto, Hulk aliifungia Klabu hiyo Bao 54
katika Mechi 99 za Primera Liga na Jumla ya Mabao yake kwa FC Porto ni
78.
Inadaiwa Chelsea imetoa Ofa ya kwanza ya Pauni Milioni 40 kwa Mchezaji alienunuliwa Septemba Mwaka Jana kwa Pauni Milioni 35.