Meneja wa Manchester United, David Moyes huenda akapata pigo lingine baada ya
kiungo wa FC Barcelona, Cesc Fabregas kumweleza kocha wake Tito
Vilanova kuwa anataka kubakia ndani ya club ya Barcelona wazee wa Katalunya.
Ambapo Jana julai 15 Man united walithibitisha kutuma ofa ya pauni milioni 26 ili kumsajili
Febregas, nahodha wa zamani wa washika bunduki wa kaskazini mwa London,
klabu ya Asernal.
Dili
la kumhitaji Febregas limekuja baada ya Thiago Alcantara kujiunga na
kocha wake wa zamani Pep Guardiola
katika klabu ya Bayern Munich badala
ya kujiunga ma mabingwa wa ligi kuu soka nchini England, Manchester
United.
![]() |
Wachezaji wa Barcelona wakiwa mazoezini kwa ajili ya msimu mpya wa La Liga |
Mambo
yamekuwa magumu kwa United baada ya kocha wa Barca Tito Vilanova kuweka
wazi kuwa amezungumza na Febregas ambaye amesema anataka kubakia Camp
Nou.
Vilanova
alisema: ‘Cesc amepokea ofa kutoka klabu nyingine. Nilizungumza naye na
ameniambia anataka kubakia hapa. Ndoto yake ni kutwaa makombe hapa”
“Tunafurahi
kuwa na Cesc. Nafahamu amepata ofa nyingi, lakini ameniambia kuwa, ana
furaja ya kuwepo Barca, hakuna haja ya kuondoka.’