Kiungo mahiri wa
kimataifa wa Brazil, Luiz Gustavo anatarajiwa kukubali uhamisho wake
kwenda Arsenal ili aweze kucheza zaidi katika kikosi cha kwanza kwa
ajili ya michuano ya Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil. Kiungo
huyo mkabaji wa Bayern Munich ambaye amejikuta akishindwa kupata namba
ya moja kwa moja katika kikosi cha kwanza anakaribia kukamilisha usajili
wake wa paundi milioni 14 kwenda Emirates wiki hii. Gustavo
anaamini kuwa nafasi yake itazidi kuwa finyu chini ya kocha mpya Pep
Guardiola ambaye ameonyesha kumtumia sasa Javi Martinez ambaye naye
anacheza nafasi hiyo ndio maana anaona uhamisho wake kwenda Arsenal
unaweza kumsadia. Akihojiwa
jijini Basel kabla ya mchezo wa kirafikiwa kimataifa baina ya Brazil na
Switzerland kesho, Gustavo amesema mkataba wake na Bayern unamalizika
2015 lakini ni muhimu kwake kucheza katika kikosi cha kwanza ili aweze
kuitwa katika timu ya taifa.
Tuesday, August 13, 2013
NASRI AOMBA RADHI KUHUSU TABIA YAKE YA LAKINI ASEMA HAJAUWA MTU
Kiungo nyota wa
kimataifa wa Ufaransa, Samir Nasri ameomba radhi kwa tabia yake lakini
amesisitiza kuwa hajaua mtu hivyo anapaswa kupewa nafasi nyingine ya
kujirekebisha. Kiungo
huyo anayecheza katika klabu ya Manchester City alifungiwa mechi tatu
na Shirikisho la Soka la Ufaransa kufuatia kumtukana mwandishi katika
michuano ya Ulaya 2012 na hajaitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya
nchi hiyo toka kipindi hiko. Hatahivyo
Nasri sasa yuko tayari kurejea katika mchezo wa kirafiki kati ya
Ufaransa na Ubelgiji baada ya kocha Didier Deschamps kuridhishwa na
tabia ya mchezaji huyo. Nasri
mwenye umri wa miaka 26 aliomba radhi kwa tukio alilofanya katika
michuano hiyo mwaka jana na kudai kuwa angetakiwa kukabiliana na tatizo
hilo kwa weledi zaidi kuliko alivyofanya. Nyota
aliendelea kudai kuwa anashukuru kupewa nafasi nyingine ya
kujirekebisha na ana mategemeo yaliyotokea hayatajirudia kwasababu hivi
sasa anajua jinsi gani ya kumudu hasira zake tofauti na ilivyokuwa
kipindi cha nyuma.
KAMATI KUTANGAZA MCHAKATO WA UCHAGUZI TFF

Mwenyekiti
wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Hamidu Mbwezeleni atakutana na Waaandishi
wa Habari kwenye ofisi za TFF saa 6 kamili mchana ambapo mbali ya
mchakato utakavyokuwa anatarajia kutangaza tarehe mpya ya uchaguzi huo
ambao awali ulitarajiwa kufanyika Septemba 29 mwaka huu.
Kamati
ya Uchaguzi ya TFF ilikutana Jumapili (Agosti 11 mwaka huu) na
inatarajia kuwa na kikao kingine leo (Agosti 12 mwaka huu) ambapo pamoja
na mambo mengine itazungumzia maandalizi ya uchaguzi huo.
Mbali
ya Mbwezeleni, wajumbe wengine wa Kamati hiyo ni Moses Karuwa (Makamu
Mwenyekiti), Mohamed Sinani, Chabanga Dyamwale na Kitwana Manara.
MAGORI, LINA WAINGIA KAMATI ZA CAF
Watanzania
Crescentius Magori na Lina Kessy wameteuliwa kuwa wajumbe kwenye kamati
ndogondogo (standing committees) mpya za Shirikisho la Mpira wa Miguu
Afrika (CAF) zilizotangazwa juzi na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo
Hicham El Amrani.
Magori
na Lina ambao ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF watakuwa kwenye
kamati hizo kwa kipindi cha miaka miwili (2013-2015). Magori ameteuliwa
kuwa mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano ya Mpira wa Miguu wa
Ufukweni (Beach Soccer) wakati Lina ameingia kwenye Kamati ya Maandalizi
ya Mpira wa Miguu kwa Wanawake.
Makamu
wa Rais wa TFF, Athuman Nyamlani ameteuliwa tena kuwemo kwenye Bodi ya
Rufani ya CAF yenye wajumbe 12 kwa kipindi kingine cha miaka miwili.
Nyamlani alikuwepo kwenye bodi iliyopita, na itaendelea kuwa chini ya
uenyekiti wa Prosper Abega kutoka Cameroon.
Rais
wa TFF, Leodegar Tenga ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya
CAF yuko kwenye kamati tano za Shirikisho hilo. Kamati hizo ni Kamati ya
Fedha ambayo ni Makamu Mwenyekiti na Kamati ya Maandalizi ya Fainali za
Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).
Kamati
nyingine ni Kamati ya Masoko na Televisheni ambayo ni Mwenyekiti,
Kamati ya Ufundi na Maendeleo, na Kamati ya Ushauri na Vyama Wanachama
wa CAF.
KAMATI YA SHERIA KUPITIA USAJILI
Kamati
ya Sheria na Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa
inakutana leo jioni (Agosti 13 mwaka huu) na kesho (Agosti 14 mwaka
huu) kupitia na kufanyia uamuzi usajili wa wachezaji wenye matatizo.
Hatua
ya kwanza ya usajili imeshamalizika wakati hatua ya pili ya usajili
inaanza kesho (Agosti 14 mwaka huu) ikihusisha wachezaji ambao watakuwa
hawajasajiliwa katika Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu na wale kutoka nje
ya Tanzania.
Hivyo,
dirisha la uhamisho kwa wachezaji wa kimataifa litafungwa baada ya
hatua ya pili ya usajili kumalizika Agosti 29 mwaka huu.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Monday, August 12, 2013
LOPEZ AONYESHA KIWANGO CHA JUU ZAIDI KATIKA NAFASI YAKE"
Lopez ameonyesha
kiwango cha juu katika mechi za kirafiki za timu hiyo ambazo imecheza.
Hali inayomfanya Ancelotti azidi kuchanganyikiwa kuwa yupi hasa awe kipa namba moja kati ya hao wawili.
Lopez alianza
kupata nafasi ya kudaka baada ya kocha wa zamani wa Real Madrid, Jose Mourinho kukorofishana
na Casillas.
Hali inayomfanya Ancelotti azidi kuchanganyikiwa kuwa yupi hasa awe kipa namba moja kati ya hao wawili.

KOCHA MPYA WA BARCA ASEMA BADO KIKOSI CHANGU HAKIJA KIDHI HITAJI LANGU
Meneja mpya
Barcelona, Gerardo Martino amekiri kuwa kikosi chake bado hakijawa katika
hali anayoitaka.
“Kweli tumecheza na kushinda katika mechi za majaribio, lakini kiwango haikuwa kizuri.
“Hata mashabiki waliokuja katika mechi zetu watakubaliana nasi kwamba hatukuwa katika fomu nzuri.
“Lakini tutajipanga, mambo yatakuwa tifauti tutakapoanza msimu na mechi yetu na Levante hakika tutafanya vizuri sana,” alisema kocha huyo maarufu Tata.
Kocha huyo amechukua nafasi ya Tito Vilanova ambaye ameshindwa kuendelea na kazi kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kansa.
“Kweli tumecheza na kushinda katika mechi za majaribio, lakini kiwango haikuwa kizuri.
“Hata mashabiki waliokuja katika mechi zetu watakubaliana nasi kwamba hatukuwa katika fomu nzuri.
“Lakini tutajipanga, mambo yatakuwa tifauti tutakapoanza msimu na mechi yetu na Levante hakika tutafanya vizuri sana,” alisema kocha huyo maarufu Tata.
Kocha huyo amechukua nafasi ya Tito Vilanova ambaye ameshindwa kuendelea na kazi kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kansa.
AZAM FC YAMALIZA ZIARA YAKE NCHINI AFRIKA KUSINI KWA KIPONDO
![]() |
Kikosi kabambe cha azam fc |
Aidha Katika Ziara hiyo huo unakuwa mchezo wao wa tatu kuambulia kipigo baada ya awali kuchapwa 3-0 na Kaizer
Chiefs, 2-1 na Orlando Pirates.
Hata hivyo katika ziara hiyo wanarambaramba hao wamefanikiwa kuibuka na ushindi mchezo mmoja dhidi
ya Mamelodi Sundowns baada ya kuichalaza bao 1-0.
NADAL ATWAA TAJI LA MICHUANO YA KOMBE LA ROGER
Mchezaji tenisi nyota
Rafael Nadal amefanikiwa kutawadhwa bingwa mpya wa michuano ya Kombe la
Rogers baada ya kugaragaza Milos Raonic wa Canada. Nadal mwenye umri wa
miaka 27 kutoka Hispania alitumia dakika 68 pekee kushinda mchezo huo
kwa 6-2 6-2 na kunyakuwa taji lake la nane kwa mwaka huu. Toka arejee
tena uwanjani Februari mwaka huu baada ya kupona majeraha, Nadal
amefanikiwa kushinda michezo 48 kati ya 51 aliyocheza na kufanikiwa
kushinda taji lake la nane katika michuano ya wazi ya Ufaransa. Kwa
upande wa wanawake mwanadada anayeshika namba moja katika orodha za
ubora Serena Williams wa Marekani naye alifanikiwa taji la michuano hiyo
kwa kumgaragaza Sorana Cirstea wa Romania. Williams mwenye umri wa
miaka 31 alihitaji dakika 65 pekee kummaliza mpinzani wake kwa 6-2 6-0
na kunyakuwa taji hilo kwa mara ya tatu.
Subscribe to:
Posts (Atom)