Sunday, June 15, 2014

STARS KWENDA BOTSWANA JUNI 24 KUJIWINDA DHIDI YA MSUMBIJI.

TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inatarajiwa kuondoka nchini wiki ijayo kwenda Botswana kuweka kambi ya mwezi mmoja kujiandaa na mchezo dhidi ya Msumbiji kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani Morocco.
Wachezaji wote wa Taifa Stars waliruhusiwa kurejea makwao jana kwa ajili ya kujiandaa na safari hiyo na watakutana tena kesho.
 Stars inayofundishwa na Mholanzi, Mart Nooij itaondoka nchini Juni 27 kwenda Gaborone, ambako itaweka kambi ya mazoezi hadi Julai 7 itakaporejea nchini.  
Taifa Stars itamenyana na Msumbiji ‘Mambas’ katika hatua ya mwisho ya mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani nchini Morocco baada ya kuitoa Zimbabwe juzi kwa jumla ya mabao 3-2, ikianza kwa ushindi wa 1-0  nyumbani na kumaliza kwa sare ya 2-2 juzi mjini hapa.
Mechi yake kwanza itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kati ya Julai 19 na 20 mwaka huu, wakati mechi ya marudiano itafanyika Msumbiji kati ya Agosti 2 na 3 mwaka huu. 
Stars pia inatarajiwa kuwa na mchezo wa kujipima nguvu na Uganda kabla ya kumenyana na Msumbiji.

TFF YASIMAMISHA UCHAGUZI SIMBA YAITAKA UENDE KAMATI YA MAADILI.



RAIS wa TFF, Jamal Malinzi, ametangaza kusimamishwa Uchaguzi Mkuu wa Simba hadi Klabu hiyo itakapounda Kamati ya Maadili kwa mujibu wa Katiba ya TFF.
Uchaguzi Mkuu Simba ulipangwa kufanyika Juni 29 na uamuzi huu wa TFF uliotangazwa Leo kwenye Mkutano wake na Wanahabari unaitaka Simba kuunda Kamati ya Maadili ifikapo Juni 30 na Kamati hiyo ndio itakayoshughulikia masuala yote ya Maadili kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu.
Uamuzi huu wa TFF unaendelea kumweka Madarakani Mheshimiwa Ismail Aden Rage hadi hapo Uchaguzi utakapofanyika baada ya Katiba yao kurekebishwa na kujumuisha Kamati ya Maadili.
Uchaguzi wa Simba umekumbwa na vuta nikuvute Klabuni hasa baada ya Mgombea Michael Wambura kuenguliwa kugombea Urais na Kamati ya Uchaguzi ya Simba na yeye kukata Rufaa TFF ambako Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF, chini ya Mwenyekiti wake Wakili Julius Lugaziya, ilimpitisha na kuamua aruhusiwe kugombea.
Hivi karibuni, Yanga walipitisha uundwaji wa Kamati ya Maadili ya Klabu yao ili kutii amri ya TFF kwenye Mkutano Mkuu wao huko Bwalo la Polisi –Oysterbay, Jijini Dar es Salaam.
Lakini hatua hiyo ililazimu Mkutano huo kumwongezea muda wa Mwaka mmoja Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Yusuf Manji, ili aweze kukamilisha masuala ya marekebisho ya Katiba yao na kujumuisha Kamati ya Maadili na pia kuweza kuandaa Mkutano wa Uchaguzi baada ya Katiba mpya kupitishwa na TFF.

Saturday, June 7, 2014

MASHABIKI WA YANGA MBEYA WAUTAKA UONGOZI WA YANGA KUMUELEZA MAXIMO KUZIBA PENGO LA KAVUMBAGU

Mashabiki na wadau wa soka mkoani mbeya wameutaka Uongozi wa Yanga sc kuhusu wameutaka uongozi huo kupendekeza kumweleza kocha mpya anayetarajiwa kuja kuinoa yanga kocha Marcio Maximo kumpata mshambuliaji mahiri wa kuziba nafasi ya Didier Kavumbagu, kabla ya kuanza kukinoa kikosi hicho kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi ya Tanzania Bara.

Wakizungumza na mtandano wa mkali wa dimba kupitia sayari ya michezo wames
ema kuwa kutokana habari zilizo tolewa katika Mkutano Mkuu wa marekebisho ya baadhi ya vipengele kwenye Katiba ya Yanga umefanyika na kumalizika salama na furaha kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi -Oysterbay huku wanachama wakipitisha kipengele cha kuundwa kwa kamati ya maadili.
katika kikao cha wanachama wa club ya yanga kilicho fanyika Juni 1 mwaka huu uongozi wa yanga Ulimtangaza kuwa Maximo kama kocha anayetarajiwa kuinoa Yanga.

Wamesema kuwa Maximo anatakiwa kutazama mchezaji sahihi atakae ziba pengo la mshambuliaji Didier Kavumbagu kwa ajili ya kuunda upya timu hiyo licha ya kuwa na Wachezaji wengi katika safu ya Ushambuliaji.
 Kwa mujibu wa chanzo cha karibu kutoka ndani ya yanga Taarifa zinasema mazungumzo na Kocha Maximo yamefikia sehemu nzuri kwa ajili ya kuja Tanzania kuinoa Yanga SC.

TFF YATOA RAMBIRAMBI MISIBA YA KANALI MWANAKATWE NA GEBO PETER!

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha aliyekuwa Katibu Mkuu wake (wakati huo ikiitwa FAT), Kanali mstaafu Ali Hassan Mwanakatwe kilichotokea leo asubuhi (Juni 7 mwaka huu) katika Hospitali Kuu ya Jeshi (GMH) Lugalo jijini Dar es Salaam.
TFF_LOGO12
Kwa mujibu wa binti wa marehemu, Sophia, baba yake alianguka bafuni nyumbani kwake Mbezi Beach ambapo alikimbizwa katika Hospitali ya Lugalo ambapo ndipo umauti ulipomfika wakati madaktari wakimpatia matibabu.
Kanali Mwanakatwe alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) katika uchaguzi uliofanyika mwaka 1993 mjini Kibaha mkoani Pwani.
Baada ya kuondoka FAT, aligombea nafasi ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na kufanikiwa kushinda katika uchaguzi uliofanyika mwaka 1997.
Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira wa miguu nchini na Afrika kwa ujumla kwani, Kanali Mwanakatwen enzi za uhai wake alitoa mchango mkubwa akiwa kiongozi, na mkufunzi wa utawala wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). Pia aliwahi kuwa Kamishna wa CAF.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Kanali Mwanakatwe, DRFA, na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa na familia yake nyumbani kwake Mbezi Beach karibu na hoteli ya Giraffe wakati ndugu wakisubiriwa kutoka mikoani. TFF tunasubiri taratibu hizo ili tujipange jinsi ya kushiriki katika msiba huo.
Sisi sote ni waja wake Mola. Hakika kwake tutarejea.

Friday, June 6, 2014

RAMBIRAMBI MSIBA WA GEBO PETER

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikiti
ko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya Simba na Taifa Stars, Gebo Peter kilichotokea usiku wa kuamkia leo (Juni 6 mwaka huu) katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Gebo aliyezaliwa mwaka 1961, pia aliwahi kuchezea timu za Sigara ya Dar es Salaam, CDA ya Dodoma na kombaini ya Mkoa wa Dar es Salaam (Mzizima United). Hadi mauti yanamkuta alikuwa akijishughulisha na biashara, kubwa ikiwa ya vifaa vya michezo.
Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu nchini kwani, Gebo enzi za uhai wake alitoa mchango mkubwa akiwa mchezaji na baadaye kiongozi katika timu ya Manyema ya jijini Dar es Salaam.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Gebo Peter, klabu ya Manyema na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Msiba upo nyumbani kwao Vingunguti karibu na Kanisa Katoliki ambapo taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa na familia.
Marehemu ambaye ameacha mjane na watoto watatu anatarajiwa kuzikwa kesho (Juni 7 mwaka huu) nyumbani kwao Kigurunyembe, mjini Morogoro.
Bwana alitoa, na Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe. Amina

Thursday, June 5, 2014

UBORA DUNIANI: SPAIN BADO 1, GERMANY 2, BRAZIL SASA 3, STARS YAKWEA HADI 113

Timu ya Taifa ya Brazil,ambao ni Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia wamepanda juu nafasi 1 na sasa wako Nafasi ya 3 katika Listi ya FIFA ya Ubora Duniani iliyotolewa Leo huku Mabingwa wa Dunia Spain wakibakia Nafasi ya 1, wakifuata Germany na Tanzania ikipanda Nafasi 9 na kukamata Nafasi ya 113.
England imerudi 10 Bora kwa kuishusha Greece wakati Argentina imepanda Nafasi 2 na ipo ya 5 na Uswisi ikoya 6 baada kupanda Nafasi 2.
Kwa Afrika, Timu ya juu kabisa ni Algeria iliyo Nafasi ya 22 baada kupanda Nafasi 3 na kuipiku Ivory Coast ambayo iko ya 23 baada kushuka Nafasi 2.
BRAZIL_SAMBA25 BORA:
1        Spain [Iko pale pale]
2        Germany [Iko pale pale]
3        Brazil [Imepanda Nafasi 1]
4        Portugal [Imeshuka Nafasi 1]
5        Argentina [Imepanda Nafasi 2]
6        Switzerland  [Imepanda Nafasi 2]
7        Uruguay [Imeshuka Nafasi 1]
8        Colombia [Imeshuka Nafasi 3]
9        Italy  [Iko pale pale]
10      England [Imepanda Nafasi 1]
11      Belgium [Imepanda Nafasi 1]
12      Greece [Imeshuka Nafasi 2]
13      USA   [Imepanda Nafasi 1]
14      Chile  [Imeshuka Nafasi 1]
15      Netherlands [Iko pale pale]
16      Ukraine[Imepanda Nafasi 1]
17      France [Imeshuka Nafasi 1]
18      Croatia [Imepanda Nafasi 2]
19      Russia [Imeshuka Nafasi 1]
20      Mexico [Imeshuka Nafasi 1]
21      Bosnia and Herzegovina [Imepanda Nafasi 4]
22      Algeria [Imepanda Nafasi 3]
23      Denmark [Iko pale pale]
23      Côte d'Ivoire [Imeshuka Nafasi 2]
25      Slovenia [Imepanda Nafasi 4]
TANZANIA-NAFASI ILIPO:
108    Kenya
109    Latvia
110    Bahrain
110    Canada
112    Niger
113    Tanzania [Imepanda Nafasi 9]
114    Namibia
115    Kuwait
116    Liberia
116    Rwanda

CECAFA NILE BASIN CUP: VICTORIA UNIVERSITY BINGWA, WAULA DOLA 30,000!!


UNI2
UNI1VICTORIA UNIVERSITY wamefanikiwa kuwa Mabingwa wa Mashindano mapya ya CECAFA NILE BASIN CUP baada kuichapa AFC Leopards ya Kenya Bao 2-1 katika Fainali iliyochezwa huko Khartoum International Stadium Jijini Khartoum Nchini Sudan hapo Jana.
Haya ni Mashindano ya kwanza kabisa ya Kombe hilo yaliyoshindaniwa na Klabu kadhaa toka Nchi za Afrika Mashariki na ya Kati ambao ni Wanachama wa CECAFA.
Kwa ushindi huo, Victoria University pia wamejinyakulia Donge nono la Dola 30,000 na ni baraka kwa Klabu changa iliyoshiriki michuano ya CECAFA kwa mara ya kwanza kabisa.
Victoria University ndio waliowatoa Wawakilishi wa Tanzania Bara, Mbeya City, kwenye Robo Fainali baada ya kuwafunga Bao 1-0 kwa Bao la Penati.
UNI3Kwa kuwa Washindi wa Pili, AFC Leopards walipewa Dola 20,000.
MAGOLI:
Victoria University 2
-Odongo Mathew Dakika ya 29
-Mutyaba Muzamir 90+2
AFC Leopards 1
-Ikene Austin Dakika ya 45

Nao, Timu ya Sudan, Al Shandy, ilinyakua Dola 10,000 kwa kumaliza Washindi wa Tatu baada ya kuifunga Academie Tchite ya Burundi Bao 4-1.
Klabu zilizoshiriki muchuano hii ni:
KUNDI A
-Polisi [Zanzibar]
-Victoria University Uganda]
-Malakia [South Sudan]
Al Merreikh [Sdan]
KUNDI B
-Mbeya City [Tanzania Bara]
-AFC Leopards [Kenya]
-Academie Tchite [Burundi]
-Enticelles [Rwanda]
KUNDI C
-Defence [Ethiopia]
-Dkhill FC [Djibouti]
-Al Shandy [Sudan]