Wednesday, November 19, 2014

KIMBE ASEMA DEUS KASEKE BADO NI MALI YA MBEYA CITY

Uongozi wa Mbeya City umesema kuwa bado inatambua kuwa Deus Kaseke ni mwanandinga wao na kukanusha uvumi wa kwamba mchezaji huyo anatarajiwa kujiunga na Simba ama Yanga kupitia dirisha dogo lililoanza kufunguliwa mnamo Nov 15/2014.
Kiungo huyo mshambuliaji wa kikosi hicho cha Mbeya City, hivi karibuni jina lake limeoneka kuchukuwa nafasi katika vyombo vya habari ikionyesha kwamba mchezaji huyo anakwenda Msimbazi Simba sanjari na mshambuliaji wa Mtibwa Sugar Ame Ali ambapo mpaka sasa mtibwa imekanusha kupitia afisa habari wake Tobias kifaru akisema hawana mpango wakuuza mchezaji lakini kama kunatimu inataka mcheza ifike katika mashamba ya miwa.
Aidha taarifa hizo zimekuwa zikidai kuwa mchezaji huyo huenda akamwaga wino katika klabu ya Yanga kwa ajili ya kukipiga katika duru la pili .
Akiweka bayana kupitia Kapu la habari .blogspot.com Katibu mkuu wa klabu ya Mbeya ciity Emmanuel Kimb amesema mpaka sasa uongozi huo haujapata  ofa yoyote kutoka kwenye vilabu hivyo.
Amesema,  hivyo mchezaji Deus Kaseke anaendelea kuwa mchezaji halali wa klabu ya Mbeya City lakini Kimbe, hakuwa tayari kuweka wazi mkataba walioingia na mchezaji huyo.
Katibu huyo ameweka wazi kuwa Mpaka sasa bado klabu  hiyo inauhalali wa kuendelea kumtumia mchezaji Deus Kaseke kwani mkataba wake haujamalizika na pia uongozi haujapokea ofa yoyote kutoka klabu za Yanga na Simba.
Sanjari na hayo Timu ya mbeya city inatarajia kuingia kambini mwishoni mwa mwezi huu kujiweka sawa michezo inayofuata ya ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara itakayo Endelea Dec 26/2014.
Timu hiyo ambayo itafungua dimba na timu ya Ndanda kutoka Mkoani Mtwara, mchezo unaotaraji kupigwa kwenye dimba la kumbukumbu ya hayati Edward Moringe Sokoine Jijini Mbeya kwa sasa mbeya city ipo nafasi ya mwisho ya 14 ikiwa na point 5 katika Msimamo ya ligi hiyo kwa Mechi Saba zilizochezwa.
Tazama Matokeo ya Mbeya  city:
    Mechi                                  Dimba
1. Mbeya City 0-0  Jkt Ruvu  Sokoine
2. Mbeya City1-0  Coastal     Sokoine
3. R'Shooting 0-0   Mbeya     Mabatini
4. Mbeya City0-1  Azam       Sokoine
5. Mbeya City 0-2  Mtibwa   Sokoine
6. Mgambo Jkt 2-1 Mbeya    Mkwakwani
7. Stand United1-0  Mbeya    Kambarage

POLISI MJINI MOMBASA YANASA SILAHA NYINGINE.

Jeshi la Polisi mjini Mombasa Pwani ya Kenya wanasema wamepata silaha nyingine zaidi ikiwemo mabomu katika msikiti wa tatu ambao ulifanyiwa msako.
Msako huo katika msikiti wa Swafaa mtaani Kisauni unakuja baada ya msako mwingine wa Jumatatu ambapo polisi pia walipata silaha gutu ndani ya msikiti ambao wanasema hutumika kutoa mafunzo yenye itikadi kali.
Mtaa wa Kisauni ndiko vijana waliokuwa wamejihamu kuwadunga visu watu wanne na kuwaua. Pia waliwashambulia kwa silaha nyingine gutu.
Waziri wa usalama wa ndani, Joseph Ole Lenku anasema kuwa msako huo ulifanywa katika misikiti ambayo hutumiwa na watu wanaoeneza itikadi kali za kiisilamu kwa vijana ambao inadaiwa wanajiunga na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Al Shabaab nchini Somalia.
Viongozi wa kiisilamu wamelanaani misako hiyo katika msikiti wakisema kuwa itachochea zaidi vijana kuendeleza itikadi kali za kidini.

kENYA YAPEWA NAFASI KUANDAA RIADHA YA VIJANA 2017

NCHI ya Kenya imetangazwa rasmi kuwa mwenyeji wa mashindano ya dunia ya riadha kwa vijana mwaka 2017, hiyo ni baada ya mji wa Greenboro wa Marekani kujiondoa na kuachia nafasi ya wazi nchi hiyo ya Afrika Mashariki yenye kusifika duniani kwa watimuaji hodari wa mbio.
Tangu awali Kenya ilianza kupata unafuu wa ushindani baada ya mji wa Bunos Aires wa Argentina kujitoa mapema.
Kenya iliwahi kuandaa mashindano ya dunia ya mbio ndefu za Cross Country mjini Mombasa mwaka 2007.
Wakati Kenya ikijiandaa kwa mashindano hayo, Uganda imeshinda ombi la kuandaa mashindano ya dunia ya mbio za Cross Country kwa mwaka 2017 baada ya kuushinda mji wa Manama wa Bahrain.
Wakati ambapo mji wa Doha Qatar wenyewe umeshinda kuwa mwenyeji wa mbio za dunia za mwaka 2019.

KUUUZA KIPRE NA KUMLETA TRAORE INAHITAJI MOYO JE ANAWEZA KUZIBA PENGO

Mabingwa wa ligi kuu Msimu uliopita Azam fc Azam FC imekubali kumuuza mshambulizi wake bora zaidi, Muivory Coast, Kipre Tchetche kwa timu ya Kelntan FC ya nchini Malasyia ambapo nafasi yake ikitarajiwa kuzibwa na mshambulizi wa mali, Mohammed Traore. 
Tunaweza kusema toa kifaa pata kifaa wakati mwingine huzaa majibu mabaya kutokana na uwezo wa mtu alieondoka hatari sana i nahitaji maamuzi kumtoa mtu kama kipre. 
Hivyo kitendo cha kumuuza, Kipre mwenye kasi na kumsaini mchezaji anayetegemea kutengenezewa mipira tu kinaweza kuifanya timu hiyo kupooza kabisa katika safu ya ushambulizi.
Didier Kavumbagu, John Bocco, Gaudensi Mwaikimba, Leonel Saint wote hawa ni washambuliaji ambao hawana kasi sana uwanjani tofauti na Kipre alikuwa na uwezo binafsi katika uchezaji wake, alikuwa akishambulia vizuri kutokea pembeni ya uwanja na alikuwa hatari kutokana na kasi yake. 
Benchi la ugfundi la timu hiyo linakabiliwa na changamoto kubwa, lakini watalazimika kukubali changamoto kuishi bila msaada wa mabao ya Kipre’ mchezaji ambaye alijiunga na Azam FC miaka minne iliyopita na kushinda tuzo ya ufungaji bora msimu wa 2012/14 huku akishinda tuzo ya mchezaji bora wa msimu uliopita.

KAMATI YA MAREFA TFF YAWAFUNGIA MAREFAWA FDL KESHO NI VPL

KAMATI ya Waamuzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imewaondoa kwenye ratiba za kuchezesha mechi za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) marefa 8 huku ikiwaweka kando makamisaa wawili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) akiwamo Fulgenzi Novatus kutoka Mwanza aliyesimamia mechi ya Kagera Sugar dhidi ya Yanga kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Kagera Novemba Mosi, mwaka huu.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Saloum Umande Chama ameyasema hayo jijini Dar es Salaam leo kuwa wamefikia uamuzi huo kutokana na makosa mbalimbali yaliyofanywa na marefa na makamisaa hao.
Amesema wumebaini kuna tatizo katika uandikaji wa ripoti za mechi kwa waamuzi na marefa. Pia tumebaini baadhi ya makamisaa wamekuwa wakidai posho kubwa kutoka kwa wasimamizi wa vituo. 
Kamisaa anasafiri kwa nauli ya Sh. 20,000 lakini huku anataka msimamzi amlipe Sh. 30,000 au mara mbili ya nauli halali. Tunaanza kwa kutoa onyo kwao kabla ya kuwashughulikia.
Amesema makamisaa wawili walioondolewa ni pamoja na John Kiteve kutoka Iringa ambaye ameponzwa na taarifa yake kuhusu mechi ya Mbeya City dhidi ya Coastal Union kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini Mbeya ambayo wenyeji walishinda kwa bao 1-0, bao likifungwa kwa penalti.
Mwingine ni Novatus ambaye taarifa yake kuhusu mechi ya Kagera Sugar dhidi ya Yanga iliyomalizika kwa wageni kuchapwa bao 1-0 imeonekana kukosa umakini katika kueleza kilichojitokeza uwanjani.
Taarifa ya Kiteve kuhusu mechi ya Mbeya City na Coastal inapishana na maelezo yaliyomo kwenye taarifa ya na refa (Israel Nkongo) pamoja na ofisa wa TFF aliyekwenda kusimamia mchezo huo. 
Mara mpira ulishikwa, mara kuna faulo. Halafu anasema refa alichezesha vibaya lakini mwishoni mwa ripoti anampa alama 8 ambazo ni kiwango kizuri kwa refa wa VPL (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara).
“Fulgence katika ripoti yake anasema mechi ya Yanga na Kagera Sugar iliisha kwa amani na watu walishikana mikono wakati kulitokea fujo na watu kupigana uwanjani.
Amewataja marefa waliofungiwa kuwa ni pamoja na Said Mbege, Hamis Ramadhani na Kalina Kabala (wote kutoka Dar es Salaam). Wengine ni Nassoro Mwinchui, Aloyce Mayombo (wote kutoka Pwani), Thomas Mkombozi (Kilimanjaro), Philimon Mboje (Mwanza) na Mohamed Keyala (Mtwara).

KESHO MAREFA VPL KUWEKWA KITI MOTO.
Aidha, Chama amesema kamati yake kesho itaendelea kupitia mikanda ya mechi zote 49 za raundi saba zilizopita za VPL pamoja na ripoti za marefa, makamisaa na maofisa wa TFF waliotumwa kusimamia mechi hizo.
Malalamiko dhidi ya marefa yamepungua, lakini lengo letu ni kuhakikisha yanaisha. 
aidha kesho tutapitia ripoti na mikanda ya mechi za VPL na waamuzi watakaofanya vizuri tutawapa zawadi, na wale watakaofanya vibaya, tutawapatia wanachostahili pia,” amesema zaidi kiongozi huyo.

MWOMBEKI ATUA RUVU SHOOTING DIRISA DOGO LA USAJILI

Maafande wa Ruvu shootingi wa kibaha Mkoani Pwani imefanikiwa kumnasa aliyekuwa Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Betram Mwombeki  na kumpatia kitanzi cha  mkataba wa mwaka mmoja.
Straika huyo msimu uliopita alikuwa akiitumikia Simba akitokea Pamba na aliweza kufanya vyema katika mzunguko wa kwanza lakini wa pili hakuweza kupata nafasi ya uhakika, hivyo akaumaliza msimu akiwa na mabao manne tu.

Akizumgumza na mkali wa dimba Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire amethibitisha hilo huku akidai kuwa wakati ukifika ataweka hadharani huku akihitaji siku muda ili kulitanabaisha hadharani.
Baada ya kuondoka Simba, Mwombeki alikwenda Oman na kufanya majaribio katika kikosi cha Oman Club FC linachoshiriki daraja la kwanza. Lakini mambo yalikwenda kombo.

Saturday, November 8, 2014

YANGA YAKWEA MPAKA NAFASI YA PILI MBEYA CITY BADO HALI TETE YAPIGWA 1 NA STEND UNITED.


MATOKEO MECHI ZA VPL
Stand United 1 Mbeya City 0       
Yanga 2 Mgambo JKT 0             
Mtibwa Sugar v Kagera Sugar (Mvua yavunja yaleta balaa Mtibwa 1 Kagera 0)             
Azam FC 2 Coastal Union 1                 
Polisi Moro 1 Prisons 0
Katika Mtanange wa Vinara wa Ligi Kuu Vodacom, Mtibwa Sugar, na Kagera Sugar huko Morogoro umevunjika kutokana na mvua kunyesha ambapo Mtibwa wakiwa mbele kwa Bao 1-0 na katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam baada ya kupoteza dhidi ya kagera sugar Yanga leo imefanikiwa kuibuka na ushindi wa 2-0 zikiwekwa kimiani na Saimon Msuva kunako Dakika za 74 na 90 na kuipandisha Yanga hadi Nafasi ya Pili. .
na huko katika Viunga vya Azam Complex, Chamazi Mabingwa Azam FC walifunga mabao yao katika dakika za mwishoni na kushinda 2-1 wakiumana na Coastal Union.
Mabao Azam FC wamefunga Kipre Tchetche Dakika ya 88 kwa Azam FC na Rama kuisawazishia Coastal lakini Shomari Kapombe akaipa ushindi Azam FC kwa Bao la Dakika ya 90.
LIGI KUU VODACOM
RATIBA
Jumapili Novemba 9
Simba v Ruvu Shootings             
JKT Ruvu v Ndanda FC
Ijumaa Desemba 26
Simba v Kagera Sugar
Jumamosi Desemba 27
Mtibwa Sugar v Stand United               
Prisons v Coastal Union             
JKT Ruvu v Ruvu Shootings
Jumapili Desemba 28
Mbeya City v Ndanda FC            
Polisi Moro v Mgambo JKT          
Yanga v Azam FC             
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Mtibwa Sugar
6
4
2
0
9
2
7
14
4
Yanga
7
4
1
2
9
5
4
13
3
Azam FC
7
4
1
2
8
4
4
13
2
Coastal Union
7
3
2
2
8
6
2
11
5
Kagera Sugar
6
2
3
1
4
2
1
9
12
Polisi Moro
7
3
2
2
6
7
-1
9
6
Mgambo JKT
7
3
0
4
4
7
-3
9
13
Stand United
7
2
3
2
5
9
-4
9
7
JKT Ruvu
6
2
1
3
5
7
-2
7
8
Ruvu Shooting
6
2
1
3
4
6
-2
7
9
Simba
6
0
6
0
6
6
0
6
10
Tanzania Prisons
7
1
3
3
5
6
-1
6
11
Ndanda FC
6
2
0
4
8
10
-2
6
14
Mbeya City
7
1
2
4
3
5
-2
5