Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza rasmi Mart Nooij kutoka Uholanzi
kuwa kocha mkuu mpya wa timu ya Taifa (Taifa Stars).
Rais
wa TFF, Jamal Malinzi amemtambulisha kocha huyo leo (Aprili 26 mwaka huu)
kwenye mkutano na waandishi
wa habari uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Akiwa
amefuatana na Makamu wake Wallace Karia, amesema anafurahi kumtangaza Nooij na
ana matarajio kuwa Tanzania itanufaika na uzoefu wake mkubwa wa ukocha, hasa
katika bara la Afrika.
“Nawaahidi
Watanzania kuwa sitomuingilia kocha katika kazi yake. Kama mimi sitomuingilia
kocha, basi hakuna mtu yeyote atakayemuingilia. Tumemwajiri yeye kwa vile ni
mtaalamu, hivyo hakuna sababu ya kumuingilia,” amesema Rais Malinzi.
Naye
Nooij ambaye amepewa mkataba wa miaka miwili amesema yeye ni mtu wa maneno
mafupi, hawezi kuahidi kitu lakini ana matarajio ya kuifanya Taifa Stars ifanye
vizuri katika mashindano mbalimbali.
Amesema
kabla ya kukubalia kufundisha Taifa Stars alikuwa na klabu ya St. Georges ya
Ethiopia, lakini vilevile amewahi kufundisha mpira wa miguu barani Afrika
katika nchi za Burkina Faso, Mali na Msumbiji.
Wasifu
wa Nooij umeambatanishwa (attached).
NGORONGORO
HEROES, KENYA UWANJANI DAR
Timu
ya vijana ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) na Kenya zinapambana kesho (Aprili 27
mwaka huu) katika mechi ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya
miaka 20 itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Matokeo
ya mechi hiyo ya marudiano itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili jioni ndiyo
yatakayoamua ni timu ipi kati ya hizo itakayocheza raundi inayofuata katika
michuano hiyo dhidi ya Nigeria.
Ngorongoro
Heroes inayofundishwa na John Simkoko ilitoka suluhu na Kenya katika mechi ya
kwanza iliyochezwa Machakos, Kenya wiki tatu zilizopita, na imekuwa kambini
jijini Dar es Salaam kwa wiki mbili kujiwinda kwa mechi hiyo.
Viingilio
katika mechi hiyo vitakuwa sh. 2,000 na sh. 5,000 ambapo Kenya iliyowasili
nchini jana (Aprili 25 mwaka huu) usiku imefanya mazoezi yake ya mwisho leo
(Aprili 26 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa..
Mechi
hiyo itachezeshwa na waamuzi kutoka Burundi wakiongozwa na Pacifique
Ndabihawenimana wakati Kamishna ni Tarig Atta Salih kutoka Sudan.
BEACH
SOCCER YAZINDULIWA RASMI
Michuano
ya mpira wa miguu ya ufukweni (Beach Soccer) inazinduliwa rasmi kesho (Aprili
27 mwaka huu) kwenye ufukwe wa Escape One uliopo Mikocheni, Dar es Salaam na
kushirikisha timu 13.
Uzinduzi
huo utaanza saa 2 asubuhi. Michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini
inashirikisha timu 13 kutoka vyuo mbalimbali vya jijini Dar es Salaam.
Vyuo
hivyo ni Chuo Kikuu cha Ardhi (AU), Chuo Kikuu cha St. Joseph Tanzania (SJUIT),
Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (TUDARCO), Chuo cha Ustawi wa Jamii (ISW),
Chuo cha Uandishi wa Habari Dar es Salaam (DSJ) na Chuo cha Kumbukumbu ya
Mwalimu Nyerere.
Vingine
ni Chuo cha Utumishi wa Umma Magogoni, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo
cha Elimu ya Biashara (CBE), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Taasisi
ya Uhasibu Tanzania (TIA), Chuo cha Utawala wa Kodi (ITA) na Chuo cha Taifa cha
Usafirishaji (NIT).
Michuano
hiyo itakuwa inachezwa Jumamosi na Jumapili kwenye fukwe za Escape One na
Gorilla Beach iliyopo Kigamboni, Dar es Salaam.
BONIFACE
WAMBURA
OFISA
HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO
LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
CURRICULUM
VITAE
Name:
Mart Nooij.
First
name(s): Martinus Ignatius Maria (Mart).
Nationality:
Dutch.
Age:
59 years (born 03.07.1954).
Profession:
Football Coach.
Euro
– pro licence 2010 – 2011.
Teacher
in Sports and Physical Education.
Coach
in Burkina
Faso:
From September 2001 until December 2003: National Technical Adviser of
FBF (FA), send out by KNVB (Holland FA).
Coach
of the National Team U 20 (Etalons Juniors).
Participation:
The
African Cup of Nations Juniors 2003 (4ième place) in Ouagadougou,
Burkina Faso.
The
Festival des Espoirs in Toulon (France) 2003.
The
Afro-Asiatic Games in October 2003, Hyderabad, India.
The
World Cup U 20 (EAU 2003) Burkina Faso reached the second round.
Coach
KNVB:
KNVB-
coach in the Dutch National Plan (1989 – 2001).
Responsible
for coach education in the western part of the country.
KNVB-
coach clinics abroad (1998 – 2005):
Seattle
(USA) in July 1998 (Lake Washington Youth Soccer Ass.).
Ouagadougou
(BF) in April 1999.
Maputo
(Mozambique) in July 1999.
Bobo-Dioulasso
(BF) in December 1999.
Preparation
of National Team of Kenya (The Harambe Stars) for
The
Castle Cup in Nairobi in October 2000.
KNVB-
course of the “CTR de la FBF” in Holland, May 2001.
International
KNVB coach clinic in Ouagadougou for French speaking African countries in
August 2003 (BF).
Willemstad,
Curaçao. Dutch Antilles (February- April 2004).
Bishkek,
Kyrgyzstan. October – November 2004.
Bishkek,
Kyrgyzstan July 2005.
Project
manager: Manager of the project “Reinforcement of the capacity INJEPS
Ouagadougou 2004 – February 2007“ send out by the Ministry of Sports in
Holland.
Coach
in
Mozambique:
Coach of the national team of Mozambique, February 2007 – October 2011.
Merdeka
Football tournament Malaysia 2008.
4
CAN qualifiers (CAN Ghana 2008).
12
CAN and WC qualifiers (CAN + WC 2010).
CAN
2010 (Angola 2010).
COSAFA
2007/2008/2009.
Mozambique
is the best mover up in FIFA ranking 2007.
6
CAN qualifiers (CAN 2012 Gabon).
All
African Games 2011 Mozambique.
Coach
of the National Team of Mozambique and the Olympic
Team
of Mozambique (U 23).
Contract
19/07/2010 – 31/10/2011.
Recently:
Head coach of Santos FC Cape
Town South Africa
(until
31 January 2013).
At
the moment: Head coach of St George FC in Addis Ababa, Ethiopia.