Wednesday, April 30, 2014

MALAWI KUTUA NCHINI KESHO MEI 1 MWAKA HUU.

Kiungo mshambuliaji wa timu ya Taifa, Taifa Stars, Mrisho Ngassa (kushoto) akiangalia namna ya kumtoka mlinzi wa timu ya Taifa ya Mawali, Wisdom Ndhlovu wakati timu hizo zilipochuana katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki uliochezwa katika uwanja mpya wa taifa jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Henry Joseph wa Taifa Stars. (Picha na Mroki Mroki).TIMU ya Taifa ya Malawi inatarajiwa kuwasili nchini kesho Mei 1 mwaka huu kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Mei 4 mwaka huu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
Flames yenye msafara wa 31 utakaoongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Mpira wa Miguu cha Malawi (FAM) utaingia Mbeya kwa usafiri wa barabara. Wachezaji katika msafara huo ni 20.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ikiwa chini ya Kocha mpya, Mart Nooij tayari ipo jijini Mbeya kujiwinda kwa mechi hiyo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya mashindano dhidi ya Zimbabwe itakayochezwa jijini Dar es Salaam kati ya Mei 16 na 18 mwaka huu.

KATIBU MKUU WA FIFA AWASILI KESHO DAR

Valcke ambaye atafuatana na maofisa wengine saba wa FIFA baadaye kesho hiyo hiyo (Mei 1 mwaka huu) atakuwa na mkutano na waandishi wa habari. Mkutano huo utafanyika saa 4 kamili asubuhi kwenye hoteli ya Double Tree by Hilton iliyopo Oysterbay, Dar es Salaam.

Tuesday, April 29, 2014

KAVUMBAGU ATUA AZAM KWA MKATABA WA MWAKA MMOJA.

Mshambuliaji Didier Kavumbagu mchana wa leo amesaini mkataba wa mwaka mmoja na mabingwa wapya wa ligi kuu soka Tanzania bara, klabu ya Azam fc.
Mtandao wa Mkali wa dimba tz umafanikiwa kuthibitisha Taarifa hii kwa afisa habari wa  Azam fc, wana Lambalamba, Jafari iddi maganga 
Maganga amesema Kavumbagu tumem
alizana nae na amesaini rasmi mkataba wa mwaka mmoja, hivyo basi tutakuwa nae msimu ujao kwenye kampeni ya kutetea ubingwa wetu pamoja na michuano ya klabu bingwa ya Afrika.
Kavumbagu ambae ni Mshambuliaji mahiri na nahodha wa timu ya Taifa ya Burundi ameamua kumwaga wino Azam baada ya Uongozi wa Yanga kusuasua kumpa mkataba mwingine baada ya ule wa miaka miwili kumalizika.
Maganga amesema kuwa lengo la kuanza usaji mapema ni kuweka mipango mathubuti katika kuhakikisha azam fc inakuwa timu bora na kuweza kukiweka imara kikosi hicho katika msimu ujao pamoja na ligi ya mabingwa barani africa

MALAWI KUWASILI MEI 1 KUIVAA STARS

Timu ya Taifa ya Malawi (Flames) inatarajiwa kuwasili nchini Mei 1 mwaka huu kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Mei 4 mwaka huu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
malawi-teamFlames yenye msafara wa 31 utakaoongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Mpira wa Miguu cha Malawi (FAM) utaingia Mbeya kwa usafiri wa barabara. Wachezaji katika msafara huo ni 20.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ikiwa chini ya Kocha mpya, Mart Nooij tayari ipo jijini Mbeya kujiwinda kwa mechi hiyo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya mashindano dhidi ya Zimbabwe itakayochezwa jijini Dar es Salaam kati ya Mei 16 na 18 mwaka huu.

LIGI YA MABINGWA WA MIKOA KUANZA KUTIMUA VUMBI MEI 10

Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) msimu wa 2013/2014 itakayochezwa kwa mkondo mmoja inaanza kutimua vumbi Mei 10 mwaka huu katika vituo vitatu vya timu tisa kila kimoja.
Tmu itakayoongoza katika kila kituo cha ligi hiyo itakayomalizika Juni 2 mwaka huu ndiyo itakayopata tiketi ya kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa msimu ujao wa 2014/2015. Vituo hivyo ni Mbeya, Morogoro na Shinyanga.
Kituo cha Morogoro ambapo mechi zitachezwa Uwanja wa Jamhuri kitakuwa na timu za Abajalo FC ya Dar es Salaam, African Sports (Tanga), Bulyanhulu FC (Shinyanga), Kariakoo SC (Lindi), Kiluvya United (Pwani), Mji Mkuu FC (Dodoma) Mshikamano FC (Dar es Salaam), Navy FC (Dar es Salaam) na Pachoto FC (Mtwara).  
Uwanja wa Sokoine ndiyo utakaotumika katika kituo cha Mbeya chenye timu za AFC ya Arusha, Magereza FC (Iringa), Mpanda United SC (Katavi), Njombe Mji FC (Njombe), Panone FC (Kilimanjaro), Tanzanite SC (Manyara), Town Small Boys (Ruvuma), Ujenzi (Rukwa) na Volcano FC (Morogoro).
Timu za Eleven Stars ya Kagera, Geita Veterans (Geita), JKT Rwamkoma FC (Mara), Mbao FC (Mwanza), Milambo SC (Tabora), Mvuvumwa FC (Kigoma), Simiyu United (Simiyu), Singida United (Singida) na Wenda FC (Mbeya) zitacheza katika kituo cha Shinyanga kwenye Uwanja wa Kambarage.
Orodha ya usajili wa wachezaji wa timu zote kwa ajili ya RCL imetumwa kwa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa na klabu zote za RCL, FDL na Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kwa ajili ya kipindi cha pingamizi ambacho kinamalizika Mei 4 mwaka huu.
Hata hivyo, katika usajili uliowasilishwa na baadhi ya klabu imebainika kuwa kuna wachezaji walioshiriki VPL, FDL na wale U20 za VPL waliocheza ligi msimu wa 2013/2014.
Kiongozi yeyote atakayebainika katika udanganyifu kwenye usajili huo, awe wa klabu au chama cha mpira wa miguu cha mkoa atachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni ikiwemo kufikishwa katika vyombo vya kimaadili vya TFF kwa hatua zaidi.
Ligi ya Mabingwa haina mdhamini, hivyo timu shiriki zitajitegemea kwa kila kitu, na zinakumbushwa kuwahi vituoni.

UEFA CHAMPIONZ LIGI LEO UWANJA KUWAKA MOTO

NUSU FAINALI:
Marudiano
[Mechi zote Saa 3 Dakika 45 Usiku]
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
UCL-NUSU_FAINALI-MARUDIANOJumanne Aprili 29
Bayern Munich v Real Madrid [0-1]
Jumatano Aprili 30
Chelsea v Atletico Madrid [0-0]

DONDOO MUHIMU:
-Rekodi ya Bayern Munich wakiwa Nyumbani kwao dhidi ya Real Madrid ni Ushindi: 8, Sare: 1 Kufungwa: 0.
-Real Madrid wameshinda mara 2 tu katika safari zao 27 Nchini Germany, mojawapo ikiwa ni ushindi wa Bao 6-1 dhidi ya FC Schalke katika Raundi ya Mtoano ya Timu 16 Msimu huu.

Monday, April 28, 2014

KLABU AFRIKA: DROO ZA MAKUNDI KUFANYIKA KESHO

DROO za kupanga Makundi ya CAF CHAMPIONZ LIGI na Kombe la Shirikisho itafanyika Jumanne Aprili 29 huko Makao Makuu ya CAF Jijini Cairo Nchini Misri.
CAF_DROO
Kwenye CAF CHAMPIONZ LIGI zipo Timu 8 zilizofuzu hatua hii na Droo hiyo itapanga Makundi mawili ya Timu 4 kila moja ambayo yatacheza mtindo wa Ligi, Nyumbani na Ugenini, ili kupata Timu mbili za juu toka kila Kundi kucheza Nusu Fainali.
Timu hizo 8 ni:
-Al-Ahly Benghazi ya Libya
-Al-Hilal ya Sudan
-AS Vita Club ya Congo DR
-CS Sfaxien ya Tunisia
-Espérance de Tunis ya Tunisia
-ES Sétif ya Algeria
-TP Mazembe ya Congo DR
-Zamalek ya Egypt
Mechi za Makundi zitaanza Wikiendi ya Mei 16 hadi 18.
CAF Kombe la Shirikisho
Kwenye CAF Kombe la Shirikisho, Droo ya hapo kesho Jumanne pia itashirikisha Timu 8 ambazo nazo zitagawanywa Makundi mawili ya Timu 4 kila moja ambayo yatacheza mtindo wa Ligi, Nyumbani na Ugenini, ili kupata Timu mbili za juu toka kila Kundi kucheza Nusu Fainali.
Timu hizo 8 ni:
-Sewe Sport - Ivory Coast
-Al Ahly – Egypt
-AS Real de Bamako – Mali
-AC Leopards de Dolisie – Congo
-ASEC Mimosas Abidjan - Ivory Coast
-Coton Sport FC – Cameroon
-E.S. Sahel – Tunisia
Mechi za Makundi zitaanza Wikiendi ya M
ei 16 hadi 18.
CAF Kombe la Shirikisho
Marudiano
[Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili]
Jumamosi Aprili 26
Bayelsa United – Nigeria 0 Sewe Sport - Ivory Coast 1 [0-3]
Difaa Hassani El Jadidi – Morocco 2 Al Ahly – Egypt 1 [2-2, Al Ahly yasonga kwa Bao la Ugenini]
Jumapili Aprili 26
Djoliba AC – Mali 0 AS Real de Bamako – Mali 0 [1-2]
Medeama – Ghana 2 AC Leopards de Dolisie – Congo 0 [2-2, Penati 4-5]
ASEC Mimosas Abidjan - Ivory Coast 1 Kaizer Chiefs - South Africa 0 [3-1]
Petro Atlético de Luanda - Angola 2 Coton Sport FC – Cameroon 2 [3-4]
E.S. Sahel – Tunisia 1 Horoya Athlétique Club – Guinea 0 [1-0]
C. A. Bizertin – Tunisia 1 Nkana FC – Zamba 1 [1-1]

BRENDAN RODGRERS ASEMA CHELSEA WALIPAKI MABASI 2 GOLINI.

Wakati Jose Mourinho akijisifia kwamba timu bora imeshinda, kocha wa Liverpool Brendan Rodgers akiongea na waandishi wa habari ameipaka timu ya Chelsea kwa aina ya uchezaji wao.
morhoChelsea wamepunguza kasi za Liverpool kushinda taji la ubingwa wa EPL baada ya miaka mingi kwa kuwafunga magoli 2 bila huku wakililinda goli lao kwa idadi kubwa ya wachezaji wakiwa ndani ya 18.
Kocha wa Liverpool amesema Chelsea walipaki mabasi mawili golini kwao na ilikuwa ni vigumu kwa wao kupita kujaribu kupata goli.
Licha ya ushindi huo mashabiki wengi wa soka kwenye mtandao wa goal.com wakati post hii inawekwa wameipa nafasi kubwa Manchester city(44.4%) kuchukua taji hilo. Kura hizo zimeipa Liverpool(41%) nafasi ya pili na kumaliza na Chelsea(14.6%).

PFA-LUIS SUAREZ TUZO YA MCHEZAJI BORA WA MWAKA:

Mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez ametwaa Tuzo ya England ya Mchezaji Bora wa Mwaka ya PFA [Professional Footballers' Association], Chama cha Wanasoka wa Kulipwa, hapo Jana.
Msimu uliopita, kipindi kama hiki, Luis Suarez alikuwa akianza kutumikia Adhabu ya Kifungo cha Mechi 10 baada kumuuma Meno Mchezaji wa Chelsea, Branislav Ivanovic, lakini safari hii ni kidedea.
Suarez alikabidhiwa Tuzo yake Jana Usiku kwenye Hoteli ya Kifahari, Grosvenor House, Jijini London mara baada ya kuruka kutoka Jijini Liverpool baada ya Mechi yao Uwanjani kwao Anfield walikofungwa Bao 2-0 na Chelsea.
Msimu huu, Suarez amefunga Bao 30 katika Mechi 31 za Ligi licha ya k
uzikosa Mechi za mwanzo wa Msimu akiwa bado Kifungoni.
Mchezaji wa Chelsea, Eden Hazard, ambae hakucheza hiy
o Jana huko Anfield, alitwaa Tuzo ya England ya Mchezaji Bora Kijana wa Mwaka ya PFA.
Kwenye Timu Bora ya Mwaka ya PFA ya Ligi Kuu England, Suarez alijumuika na wenzake wa Liverpool, Daniel Sturridge na Nahodha wao Steven Gerrard.
Chelsea pia walikuwa na Wachezaji watatu ambao ni Petr Cech, Gary Cahill na Hazard.
Manchester City inawakilishwa na Vincent Kompany na Yaya Toure huku Southampton ikiwa na wawili, Luke Shaw na Adam Lallana.
Mabingwa Watetezi, Manchester United nar Arsenal, haina hata Mchezaji mmoja.
PFA-LIGI KUU ENGLAND-TIMU YA MWAKA: Petr Cech (Chelsea); Luke Shaw (Southampton), Vincent Kompany (Manchester City), Gary Cahill (Chelsea), Seamus Coleman (Everton); Eden Hazard (Chelsea), Yaya Toure (Manchester City), Steven Gerrard (Liverpool), Adam Lallana (Southampton); Luis Suarez (Liverpool), Daniel Sturridge (Liverpool)

WANASOKA BORA WA MWAKA ENGLAND

Mchezaji Bora wa Mwaka: Luis Suarez (Liverpool).
Mchezaji Bora Chipukizi wa mwaka: Eden Hazard (Chelsea).
Mchezaji Bora wa kike wa Mwaka: Lucy Bronze (Liverpool Ladies).
Mchezaji Bora chipukizi wanawake: Martha Harris (Liverpool Ladies).

Sunday, April 27, 2014

AFCON 2015-MOROCCO: DROO YAWEKWA HADHARANI

DROO ya Mashindano ya Mataifa ya Africa, rasmi kama Orange Africa Cup of Nations Morocco 2015, ambayo Fainali zake zitachezwa huko Morocco kati ya Tarehe 17 Januari hadi 8 Februari 2015, imefanyika hii Leo huko Cairo, Egypt.
Nchi 51 zitashiriki Mashindano haya ambapo Mauritania na South Sudan zilishinda toka Raundi ya Kwanza na kutinga Raundi ya Pili ya Mtoano ambayo Tanzania itacheza na Zimbabwe.
AFCON_2015_LOGO-MOROCCOWashindi 14 wa Raundi ya Pili ya Mtoano wataingia Raundi ya Tatu ya Mtoano ili kupata Timu 7 zitakazosonga kwenye Makundi ambayo hii Leo pia yamepangwa.
Ikiwa Tanzania itaitoa Zimbabwe basi kwenye Raundi ya Tatu ya Mtoano itacheza na Mshindi kati ya Mozambique na South Sudan na Tanzania ikipita hapo itaingia 
KUNDI F ambako ziko Zambia, Cape Verde na Niger.
Yapo Makundi 7 ambapo Mshindi wa Kila Kundi na Mshindi wa Pili wa Kila Kundi pamoja na Timu moja iliyofuzu Nafasi ya 3 Bora katika Makundi ndizo zitaingia Fainali kuungana na Morocco na kufanya idadi ya Timu 16 kwenye Fainali.
RATIBA/MAKUNDI:
Nchi ambazo zimeingia Makundi moja kwa moja: Nigeria, Ghana, Ivory Coast, Zambia, Burkina Faso, Mali, Tunisia, Algeria, Angola, Cape Verde, Togo, Egypt, South Africa, Cameroon, DR Congo, Ethiopia, Gabon, Niger, Guinea, Senegal and Sudan.
RAUNDI YA PILI YA MTOANO

Mechi Na 1: Liberia vs Lesotho

Mechi Na 2: Kenya vs Comoros
Mechi Na 3: Madagascar vs Uganda
Mechi Na 4: Mauritania vs Equatorial Guinea
Mechi Na 5: Namibia vs Congo
Mechi Na 6: Libya vs Rwanda
Mechi Na 7: Burundi vs Botswana
Mechi Na 8: Central African Republic vs Guinea Bissau
Mechi Na 9: Swaziland vs Sierra Leone
Mechi Na 10: Gambia vs Seychelles 
Mechi Na 11: Sao Tome e Principe vs Benin
Mechi Na 12: Malawi vs Chad
Mechi Na 13: Tanzania vs Zimbabwe
Mechi Na 14: Mozambique vs South Sudan

**Mechi za Kwanza 16,17,18 Mei 2014

**Mechi za Marudiano 30,31 Mei au 1 Jun1 2014

RAUNDI YA TATU YA MTOANO
**WASHINDI 14 wa Raundi ya Pili ya Mtoano watacheza Raundi hii
TIMU MECHI NA TIMU Mechi ya Kwanza Mechi ya Pili
Mshindi Mechi Na 1 1/2 Mshindi Mechi Na 2 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 3 3/4 Mshindi Mechi Na 4 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 5 5/6 Mshindi Mechi Na 6 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 7 7/8 Mshindi Mechi Na 8 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 9 9/10 Mshindi Mechi Na 10 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 11 11/12 Mshindi Mechi Na 12 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 13 13/14 Mshindi Mechi Na 14 18–20 Julai 1–3 Agosti
MAKUNDI:
KUNDI A
-Nigeria
-South Africa
-Sudan
-Mshindi 5/6
KUNDI B
-Mali
-Algeria
-Ethiopia
Mshindi 11/12
KUNDI C
-Burkina Faso
-Angola
-Gabon
-Mshindi 1/2
KUNDI D
-Ivory Coast
-Cameroun
-Congo DR
-Mshindi 9/10
KUNDI E
-Ghana
-Togo
-Guinea
Mshindi 3/4
KUNDI F
-Zambia
-Cape Verde
-Niger
-Mshindi 13/14
KUNDI G
-Tunisia
-Egypt
-Senegal
-Mshindi 7/8

TANZANIA YAITWANGA KENYA U20 KUFUZU FAINALI ZA AFRIKA

TIMU ya soka ya taifa ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes imeitoa Kenya katika Raundi ya Kwanza ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika mwakani nchini Senegal kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya jumla ya bila kufungana nyumbani na ugenini.
Kwa matokeo hayo, Ngorongoro inayofundishwa na kocha mzalendo John Simkoko sasa itamenyana na Nigeria katika hatua inayofuata.
Penalti za Tanzania zilikwamishwa nyavuni na Mohammed Hussein, Kevin Friday, Mange Chagula na Iddi Suleiman, wak
ati Mudathir Yahya alikosa.
Penalti za Kenya zilifungwa na Geoffrey Shiveka, Timonah Wanyonyi na Victor Ndinya, wakati Evans Makari na Harison Nzivo walipoteza.
Hakuna kipa aliyeokoa penalti bali wapigaji waliokosa walipiga nje.
Ilikuwa mechi kali na ya ushindani na makipa wa timu zote mbili, Aishi Manula wa Tanzania na Farouk Shikhalo wa Kenya aliyeanza kabla ya kumpisha Boniface Barasa dakika ya 88 walifanya kazi nzuri ya kuokoa michomo ya hatari.

MART NOOIJ AONGEZA 9 TAIFA STARS, KUIVAA MALAWI HUKO MBEYA!!

Kocha mpya wa Taifa Stars, Mart Nooij ameongeza wachezaji tisa katika kikosi hicho kinachojiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Malawi (The Flames) itakayochezwa Mei 4 mwaka huu katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Wachezaji walioongezwa ni Edward Charles Manyama (JKT Ruvu), Elias Maguli (Ruvu Shooting), Hassan Dilunga (Yanga), Hussein Javu (Yanga), John Bocco (Azam), Kelvin Friday (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Nadir Haroub (Yanga) na Shomari Kapombe (AC Cannes, Ufaransa).
Martinus_Ignatius_Maria_maarufu_kama_Mart_Nooij
Naye beki Kelvin Yondani wa Yanga ambaye aliitwa awali ameondolewa katika kikosi hicho kwa vile ameshindwa kuripoti kambini.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Pemium Lager inaingia kambini kesho (Aprili 28 mwaka huu) jijini Mbeya kujiandaa kwa mechi dhidi ya Malawi.
Wakati huo huo, Tanzania (Taifa Stars) imepangiwa kucheza na Zimbabwe katika raundi ya pili ya mechi za mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika (AFCON) zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.
Stars itaanzia nyumbani ambapo mechi ya kwanza itachezwa kati ya Mei 16 na 18 wakati ile ya marudiano itachezwa Harare kati ya Mei 30 na Juni 1 mwaka huu.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Saturday, April 26, 2014

TAIFA Star ya Tanzania,yapokea kipigo ambapo imeleta simanzi kwa wananchi kuwafanya wamalizie vibaya sherehe za miaka 50 za Muungano baada ya kufungwa mabao 3-0 na Burundi katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa jioni hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Stars iliyotumia wachezaji wengi chipukizi waliopatikana kwa njia ya maboresho ya timu hiyo, leo ilionekana kuzidiwa katika idara na Burundi iliyotumia wachezaji wake wazoefu.

Mshambuliaji wa Yanga SC na Nahodha wa Int’hamba Murugamba, Didier Kavumbangu alifungua pati la mabao ya Burundi dakika ya 45 akifunga kwa ustadi wa hali ya juu baada ya kumalizia pasi nzuri ya Ndarusanze Claude aliyeingia dakika ya 32 kuchukua nafasi ya Paschal Hakizimana.

Burundi walikwenda kupumzika wakiwa wanaongoza kwa bao hilo 1-0 na kipindi cha pili Stars ilidhoofika zaidi na kuongezwa mabao mawili ndani ya dakika nne.
Alianza mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Bara, Amisi Tambwe anayechezea Simba SC dakika ya 56 aliyefumua shuti akiwa ndani ya eneo la hatari baada ya kutengewa mpira kwa kifua na Kavumbangu kufuatia koris ya Cedric Amisi

Yussuf Ndikumana alifunga bao la tatu dakika ya 60 kwa shuti la umbali wa mita 50 baada ya kukutana na mpira akiwa katikati ya Uwanja na kumtazama kipa Deo Munishi ‘Dida’ aliyekuwa ametoka langoni mwake na kumtungua kiulaini.
Bao hilo liliamsha Stars na kutoka wote kushambulia kusaka japo bao la kufutia machozi na Simon Msuva alitengeneza nafasi tatu nzuri na zote wenzake wakashindwa kuzitumia vizuri.
Nafasi nzuri zaidi ilikuja dakika ya 85 baada ya Msuva kuteleza kulia mwa Uwanja na kuingia hadi kwenye boksi akamkatia pande safi Ramadhani Singano ‘Messi’ ambaye alipiga nje.
Mchezo wa leo umeonyesha Tanzania bado ina safari ndefu na ngumu kuweza kupata timu bora ya taifa.

Kikosi cha Tanzania leo kilikuwa; Deo Munishi ‘Dida’, Omar Kindamba/Himid Mao, Edward Peter, Aggrey Morris, Said Mourad, Said Juma/Jonas Mkude, Simon Msuva, Frank Domayo, Ayoub Lipati/Omar Nyenje, Mohamed Seif/Haroun Chanongo na Ramadhani Singano ‘Messi’.


Burundi; Arthur Arakaza/Biha Omar, Kiza Fataki, Rugonumugabo Stephane, Issa Hakizimana, Rashid Leon, Yusuf Ndikumana/Nahimana Chasil, Steve Nzigamasabo, Amisi Cedric, Didier Kavumbangu, Paschal Hakizimana/Ndarusanze Claude na Amisi Tambwe/Shaaban Hussein. 

MART NOOIJ AKABIDHIWA RASMI MIKOBA TAIFA STARS



Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza rasmi Mart Nooij kutoka Uholanzi kuwa kocha mkuu mpya wa timu ya Taifa (Taifa Stars).
Rais wa TFF, Jamal Malinzi amemtambulisha kocha huyo leo (Aprili 26 mwaka huu) kwenye mkutano na waandishiMartinus_Ignatius_Maria_maarufu_kama_Mart_Nooij wa habari uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Akiwa amefuatana na Makamu wake Wallace Karia, amesema anafurahi kumtangaza Nooij na ana matarajio kuwa Tanzania itanufaika na uzoefu wake mkubwa wa ukocha, hasa katika bara la Afrika.
“Nawaahidi Watanzania kuwa sitomuingilia kocha katika kazi yake. Kama mimi sitomuingilia kocha, basi hakuna mtu yeyote atakayemuingilia. Tumemwajiri yeye kwa vile ni mtaalamu, hivyo hakuna sababu ya kumuingilia,” amesema Rais Malinzi.
Naye Nooij ambaye amepewa mkataba wa miaka miwili amesema yeye ni mtu wa maneno mafupi, hawezi kuahidi kitu lakini ana matarajio ya kuifanya Taifa Stars ifanye vizuri katika mashindano mbalimbali.
Amesema kabla ya kukubalia kufundisha Taifa Stars alikuwa na klabu ya St. Georges ya Ethiopia, lakini vilevile amewahi kufundisha mpira wa miguu barani Afrika katika nchi za Burkina Faso, Mali na Msumbiji.
Wasifu wa Nooij umeambatanishwa (attached).
NGORONGORO HEROES, KENYA UWANJANI DAR
Timu ya vijana ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) na Kenya zinapambana kesho (Aprili 27 mwaka huu) katika mechi ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Matokeo ya mechi hiyo ya marudiano itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili jioni ndiyo yatakayoamua ni timu ipi kati ya hizo itakayocheza raundi inayofuata katika michuano hiyo dhidi ya Nigeria.
Ngorongoro Heroes inayofundishwa na John Simkoko ilitoka suluhu na Kenya katika mechi ya kwanza iliyochezwa Machakos, Kenya wiki tatu zilizopita, na imekuwa kambini jijini Dar es Salaam kwa wiki mbili kujiwinda kwa mechi hiyo.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 2,000 na sh. 5,000 ambapo Kenya iliyowasili nchini jana (Aprili 25 mwaka huu) usiku imefanya mazoezi yake ya mwisho leo (Aprili 26 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa..
Mechi hiyo itachezeshwa na waamuzi kutoka Burundi wakiongozwa na Pacifique Ndabihawenimana wakati Kamishna ni Tarig Atta Salih kutoka Sudan.
BEACH SOCCER YAZINDULIWA RASMI
Michuano ya mpira wa miguu ya ufukweni (Beach Soccer) inazinduliwa rasmi kesho (Aprili 27 mwaka huu) kwenye ufukwe wa Escape One uliopo Mikocheni, Dar es Salaam na kushirikisha timu 13.
Uzinduzi huo utaanza saa 2 asubuhi. Michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini inashirikisha timu 13 kutoka vyuo mbalimbali vya jijini Dar es Salaam.
Vyuo hivyo ni Chuo Kikuu cha Ardhi (AU), Chuo Kikuu cha St. Joseph Tanzania (SJUIT), Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (TUDARCO), Chuo cha Ustawi wa Jamii (ISW), Chuo cha Uandishi wa Habari Dar es Salaam (DSJ) na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.
Vingine ni Chuo cha Utumishi wa Umma Magogoni, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Chuo cha Utawala wa Kodi (ITA) na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).
Michuano hiyo itakuwa inachezwa Jumamosi na Jumapili kwenye fukwe za Escape One na Gorilla Beach iliyopo Kigamboni, Dar es Salaam.
BONIFACE WAMBURA

OFISA HABARI NA MAWASILIANO

SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
CURRICULUM VITAE
Name:                  Mart Nooij.
First name(s):      Martinus Ignatius Maria (Mart).
Nationality:                   Dutch.
Age:                     59 years (born 03.07.1954).
Profession:                    Football Coach.
Euro – pro licence 2010 – 2011.
Teacher in Sports and Physical Education.
Coach in Burkina
Faso: From September 2001 until December 2003: National Technical Adviser of  FBF (FA), send out by KNVB (Holland FA).
Coach of the National Team U 20 (Etalons Juniors).
Participation:
The African Cup of Nations Juniors 2003 (4ième place) in Ouagadougou, Burkina Faso.
The Festival des Espoirs in Toulon (France) 2003.
The Afro-Asiatic Games in October 2003, Hyderabad, India.
The World Cup U 20 (EAU 2003) Burkina Faso reached the second round.
Coach KNVB:
KNVB- coach in the Dutch National Plan (1989 – 2001).
Responsible for coach education in the western part of the country.
KNVB- coach clinics abroad (1998 – 2005):
Seattle (USA) in July 1998 (Lake Washington Youth Soccer Ass.).
Ouagadougou (BF) in April 1999.
Maputo (Mozambique) in July 1999.
Bobo-Dioulasso (BF) in December 1999.
Preparation of National Team of Kenya (The Harambe Stars)  for
The Castle Cup in Nairobi in October 2000.
KNVB- course of the “CTR de la FBF” in Holland, May 2001.
International KNVB coach clinic in Ouagadougou for French speaking African countries in August 2003 (BF).
Willemstad, Curaçao. Dutch Antilles (February- April 2004).
Bishkek, Kyrgyzstan.  October – November 2004.
Bishkek, Kyrgyzstan July 2005.
Project manager: Manager of the project “Reinforcement of the capacity INJEPS Ouagadougou 2004 – February 2007“ send out by the Ministry of Sports in Holland.
Coach in
Mozambique:       Coach of the national team of Mozambique, February 2007 – October 2011.
Merdeka Football tournament Malaysia 2008.
4 CAN qualifiers (CAN Ghana 2008).
12 CAN and WC qualifiers (CAN + WC 2010).
CAN 2010 (Angola 2010).
COSAFA 2007/2008/2009.
Mozambique is the best mover up in FIFA ranking 2007.
6  CAN qualifiers (CAN 2012 Gabon).
All African Games 2011 Mozambique.
Coach of the National Team of Mozambique and the Olympic
Team of  Mozambique (U 23).
Contract 19/07/2010 – 31/10/2011.
Recently:             Head coach of Santos FC Cape Town South Africa
(until 31 January 2013).
At the moment:   Head coach of St George FC in Addis Ababa, Ethiopia.