Wednesday, July 17, 2013

CAF YATANGAZA KUSOGEZA MBELE MCHEZO WA LIGI YA MABINGWA KATI YA WATANI WA JADI"

Shirikisho la kandanda Barani Afrika-CAF limesogeza mbele mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Afrika ambao unawakutanisha watani wa jadi nchini Misri timu za Zamalek na Al Ahly mpaka Jumatatu ijayo.  
Vigogo hao wa soka nchini humo walitarajiwa kucheza Jumapili katika mji wa El Gouna ambao uko kilometa 500 kutoka mji mkuu wa Cairo kutokana na sababu za kiusalama. Katika taarifa iliyotolewa katika mtandao wa Zamalek, wamethibitisha kuwa FIFA imekubali mchezo huo kuchezwa El Gouna pamoja na kwamba uwanja huo haukuwepo katika ratiba za michuano hiyo na kuamua kuchelewesha mchezo huo kwa siku moja kwasababu za kibiashara. Wizara ya mambo ya ndani ya nchi hiyo ilikataa mapema kuhakikisha usalama wa mechi hiyo kuchezwa jijini Cairo au Alexandria kabla ya Zamalek kuchagua El Gouna.

WAKALA WA SUAREZ ASEMA KAMA KUNA CLUB INAMTAKA MCHEZAJI HUYO IWEKE MEZANI KITITA CHA NGUVU

Wakala wa mshambulaij  nyota wa klabu ya Liverpool na timu ya taifa ya Uruguay" Luis Suarez’ amebainisha na kuweka wazi kama kuna klabu inahitaji kumsajili nyota huyo lazima iandae dau la nono la pauni miliaoni 40 ili kupata huduma yake.

Klabu ya Liverpool imesema itasikiliza ofa ya pauni milioni 40, lakini kuna uwezekano wa ofa hiyo kupanda mpaka kufikia pauni milioni 50 kumnunua nyota huyo mwenye matukio ya aina yake nchini England, likiwemo la kumng`ata beki wa Chelsea,  Ivanovic na kusimamishwa mechi kumi, pamoja na tuhuma za ubaguzi wa rangi kwa beki wa mabingwa wa soka nchini Englanda, Manchester United, Mfaransa Patrick Evra.

Wakala wa Suarez bwana Pere Guardiola, ambaye ni kaka yake kocha wa wekundu wa kusini mwa Ujerumani, The Bavarian, klabu ya Bayern Munich , Joseph Pep Guardiola , amasema atakaa mezani na klabu yoyote yenye uwezo wa kuweka mezani mzigo wa pauni milioni 40.

Ambapo sasa Baadhi ya Klabu kubwa barani Ulaya zinataka kuinasa saini ya Luis Suarez kutoka kwa majogoo wa jiji.

Arsenal ni klabu pekee yenye mpango wa nguvu zaidi kutaka kumsajili Suarez kwa pauni milioni 35, lakini ofa hiyo inaonkana haina maana kwa wekundu wa Anfield waliotangaza pauni milioni 40.

Awali Asernal walituma ofa ya pauni milioni 30, Liver wakatupilia mbali, wakaongeza tano, bado wakagomewa kabisa kwani wanataka 40 tu, huna mzigo huo basi amekosa huduma ya nyota huyo.

Saurez ambaye atajiunga na Liverpool waliopo  Melbourne jumatatu ijayo, ana mkataba na Liverpool mpaka mwaka 2016. Lakini Liver wameonekana kuwa na msimamo wa kumbakisha, huku klabu za Arsena, Real Madrid na Chelsea zakiimarisha rada zao kutaka kumsajili.

UONGOZI WA YANGA WAWATAKA MASHABIKI KUJITOKEZA KWA WINGI"

Club ya Yanga ya jangwani kupitia uongozi wake waumewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi katika mechi ya kimataifa ya kirafiki itakayochezwa Julai 18 mwaka huu.
Mechi hiyo kimataifa ya Kirafiki dhidi ya timu ya 3 Pillars ya Nigeria inataraji kutimua vumbi Julai 18 mwaka huu katika uwanja wa Taifa.
Mechi hiyo ni sehemu ya maandalizi ya klabu zote mbili kabla ya ligi kuu kuanza mwezi ujao  ambapo Yanga pia inajinoa kwa ajili ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika.
Mratibu wa mechi Salum Mkemi amesema kikosi cha wachezaji 17 na viongozi na makocha wao wapo jijini Dar es Salaam wakijifua kwa ajili mtanange huo utakaochezwa katika uwanja wa Taifa.
Mkemi amesema pia timu ya 3 Pillars ambayo imepanda daraja la ligi kuu nchini Nigeria inataraji kujipima na Coastal Union ya Tanga huku wakifanya mazungumzo na Mbeya City kwa ajili ya mechi nyingine za Kirafiki.
Katibu mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako amesema wachezaji wako kambini kujiwinda na michuano ya ligi kuu na kuongeza kuwa wana morali kuelekea mchezo huo.
Mratibu wa mechi ametangaza Viingilio vya mechi hiyo vitakuwa kati ya shilingi elfu tatu na elfu 15 ili kuwawezesha mashabiki wengi zaidi kuhudhuria kipute hicho.
Timu ya 3 Pillars inataraji kurejea nchini Nigeria Julai 30 mwaka huu.

Tuesday, July 16, 2013

KUTOA OFA PAUNI MILIONI 40 KUMNUNUA HULK--CHELSEA

Katika harakati za usajili baada ya kuikosa saini ya kumnasa Straika hatari wa Uruguay, Edinson Cavani, ambae sasa yuko njiani kukamilisha ku

hamia PSG kutoka Napoli, Chelsea sasa imemgeukia Straika wa Klabu ya Urusi Zenit St Petersburg, Hulk, anaetoka Brazil.
Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho, ana nia ya kuongeza safu yake ya Ushambuliaji na tayari ameshamnunua Mchezaji wa Germany Andre Schurrle huku kukiwa na tetesi Mastraika wa sasa, Fernando Torres na Demba Ba, huenda wakapigwa bei.
Katika Msimu wake wa kwanza na Zenit, Hulk alifunga Bao 11 katika Mechi 30 na kabla hajahamia huko Urusi, akiwa huko Portugal na FC Porto, Hulk aliifungia Klabu hiyo Bao 54 katika Mechi 99 za Primera Liga na Jumla ya Mabao yake kwa FC Porto ni 78.
Inadaiwa Chelsea imetoa Ofa ya kwanza ya Pauni Milioni 40 kwa Mchezaji alienunuliwa Septemba Mwaka Jana kwa Pauni Milioni 35.

SIMBA YAJA NA MKUTANO MKUU JALAI 20 MWAKA HUU VS TBL"

Club ya soka ya Simba, inatarajia kufanya wake Mkutano Mkuu Jumamosi Julai 20 na Mdhamini wao, TBL, Tanzania Breweries Limited ambapo mdhamini huyo ametoa Shilingi Milioni 20 ili kuendesha Mkutano huo.
Mkutanno Mkuu huo ni fursa safi kwa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, kuwasilisha Ripoti ya shughuli za Klabu hiyo.
TBL, ambayo ina Mikataba ya Miaka mitano mitano ya kuzidhamini Yanga na Simba kuanzia Miaka miwili iliyopita, inawajibika kuzipa Klabu hizo Shilingi Milioni 20 kila mmoja ili kuendesha Mikutano Mikuu ya Vilabu vyao.
Akiongea wakati akikabidhi Cheki ya Shilingi Milioni 20 kwa Simba, George Kavishe, Meneja wa Bia ya aina ya Kilimanjaro Premium Lager, alisema: "Kama Wadhamini wakuu, tunatoa Fedha hizi kama jukumu letu kwa Klabu ili iwajibike, ipate mafanikio nje na ndani ya Uwanja. Tunaamini Mkutano huu utaimarisha uhusiano kati ya Simba na Wanachama wake kwa kuwapa nafasi kupitia masuala ya Klabu yao waipendayo."
Nae Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, aliishukuru TBL kwa kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa Mkataba na akaahidi Fedha hizo zitatumika kama ilivyokusudiwa.
Kwa baadhi ya Wadau wa Simba Mkutano Mkuu huu unasubiriwa kwa hamu kubwa hasa baada ya Klabu hiyo kugubikwa na mfarakano na Mwezi Machi Kikundi kimoja cha waliodaiwa kuwa Wanachama kujaribu kumpindua Rage kwa madai ya kushindwa kuongoza lakini jaribio hilo halikufua dafu.
Pia, inasemekana ipo Kambi ya Wanachama itakayoshika bango waelezwe kinagaubaga nini kimetokea kuhusu kuuzwa kwa Straika wao kutoka Uganda, Emmanuel Okwi, kwa Klabu ya Tunisia Etoile Sportive Du Sahel Mwezi Januari kwa Dau linalodaiwa kuwa Dola Laki 3 na Klabu kutolipwa Fedha hizo hadi sasa.
Wengine watapenda wajue nini kiliwasibu Msimu uliopita na kumalizika Mwezi Mei huku Simba ikinyang’anywa Taji lao la Ubingwa na Mahasimu wao wakubwa, Yanga, na pia kujikuta wakibwagwa hadi Nafasi ya 3 nyuma ya Yanga na Azam na hivyo kutopata fursa ya kucheza Mashindano ya Klabu Barani Afrika Mwakani.

FABREGAS ASEMA AMWAMBIA VILANOVA NATAKA KUBAKI HAPA"

Meneja wa Manchester United,  David Moyes huenda akapata pigo lingine baada ya kiungo wa FC Barcelona, Cesc Fabregas kumweleza kocha wake  Tito Vilanova kuwa anataka kubakia ndani ya club ya Barcelona wazee wa Katalunya.

Ambapo Jana julai 15 Man united walithibitisha kutuma ofa ya pauni milioni 26 ili kumsajili Febregas,  nahodha wa zamani wa washika bunduki wa kaskazini mwa London, klabu ya Asernal.

Dili la kumhitaji Febregas limekuja baada ya  Thiago Alcantara kujiunga na kocha wake wa zamani Pep Guardiola  
Wachezaji wa Barcelona wakiwa mazoezini kwa ajili ya msimu mpya wa La Liga
katika klabu ya Bayern Munich badala ya kujiunga ma mabingwa wa ligi kuu soka nchini England, Manchester United.

Mambo yamekuwa magumu kwa United baada ya kocha wa Barca Tito Vilanova kuweka wazi kuwa amezungumza na Febregas ambaye amesema anataka kubakia Camp Nou.

Vilanova alisema: ‘Cesc amepokea ofa kutoka klabu nyingine. Nilizungumza naye na ameniambia anataka kubakia hapa. Ndoto yake ni kutwaa makombe hapa”

“Tunafurahi kuwa na Cesc. Nafahamu amepata ofa nyingi, lakini ameniambia kuwa, ana furaja ya kuwepo Barca, hakuna haja ya kuondoka.’

FIFA YASEMA CLUB YA FENERBAHCE NA BASIKTAS ZIMESHINDA RUFANI YAO

Shirikisho la kandanda barani Ulaya-UEFA, limesema kuwa klabu za Fenerbahce na Besiktas za Uturuki zimeshindwa rufani zao za kupinga adhabu ya kushiriki michuano inayoandaliwa na shirikisho hilo. Fernabahce ambao ilikuwa washiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu walifungiwa kushiriki michuano yoyote ya Ulaya kwa misimu miwili huku Besiktas ambao walifuzu kushiriki michuano ya Europa League wao wamefungiwa msimu mmoja. Klabu zote mbili zinatuhumiwa na kashfa ya upangaji matokeo katika baadhi ya mechi za Ligi ya Kuu ya Soka nchini Uturuki mwaka 2011. Baada ya kugonga mwamba UEFA, klabu hizo bado zina haki ya kukata rufani katika Mahakama ya Usuluhishi ya Michezo-CAS.