Tuesday, May 28, 2013

TAIFA STARS YAANZA KUJINOA ADDIS ABABA.

  1. Taifa Stars imetua jijini Addis Ababa, Ethiopia leo (Mei 28 mwaka huu) alfajiri kwa ndege ya EgyptAir ambapo itaweka kambi ya wiki moja kujiandaa kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco (Lions of the Atlas) itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech. Stars iliyotua na kikosi cha wachezaji 21 imefikia hoteli ya Hilton, na imeanza mazoezi leo (Mei 28 mwaka huu) saa 12 jioni kwenye Uwanja wa Addis. Kwa mujibu wa Kocha Kim Poulsen, Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itakuwa na vipindi (sessions) vinne vya mazoezi kabla ya kucheza mechi ya kirafiki na Sudan (Nile Crocodile). Mechi dhidi yan Sudan itachezwa Jumapili kuanzia saa 11 jioni kwenye Uwanja wa Addis. Sudan ambayo pia imeweka kambi yake Addis Ababa kujiandaa kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia ilicheza mechi yake ya kwanza jana (Mei 27 mwaka huu) dhidi ya wenyeji Ethiopia na kulala mabao 2-0. Wachezaji wanaounda Stars ni nahodha Juma Kaseja, nahodha msaidizi Aggrey Morris, Mwadini Ally, Ally Mustafa, Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Erasto Nyoni, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd, Haruni Chanongo na Zahoro Pazi. Kikosi hicho kinatarajiwa kuondoka Addis Ababa kwenda Marrakech alfajiri ya Juni 3 mwaka huu kwa ndege ya EgyptAir. Stars itatua siku hiyo hiyo Casabalanca na kuunganisha moja kwa moja kwenda Marrakech.

KING KIBADEN MPUTA AANZA KUINOA RASMI SIMBA SC LEO KATIKA UWANJA WA KINESI

KOCHA mpya wa wekundu wa msimbazi simba sc alhaj abdallah athumani seif "King kibaden mputa" leo asubuhi ameanza rasmi kazi ya kuinoa timu hiyo katika uwanja wa kinesi Urafiki jijini Dar es salaam.

Kabla ya kuanza usaili Kibadeni alianza kutoa mazoezi kwa wachezaji wa simba mara baada ya hapo usaili ukafuata kwa wachezaji waliojitokeza kuomba kusajiliwa katika timu hiyo.

Kibadeni ataanza  rasmi leo na atasaini mkataba kesho ikumbukwe kibadeni alikuwa akiifundisha Kagera Sugar ambapo katika msimu uliomalizika wa ligi kuu vodacom tanzania bara ameiwezesha Kagera Sugar kushika nafasi ya nne ikiwa na jumla ya point 43.

aidha ikumbukwe kibadeni amechuwa nafasi ya mfaransa patric liewig alitupiwa virago clubuni hapo baada ya kuyashindwa maisha ya msimbazi.

hivyo kwa sasa simba itakuwa chini ya kocha mkuu king kabadeni mputa akisaidiwa na jamhuri kihwelu julio pamoja na suleimani abdallah matola.

WASIFU WA KING KIBADEN
1949- Oktoba 11; Alizaliwa Mbagala Kiburugwa Dar es Salaam.
1959- Alitungwa jina Kibadeni na watoto wenzake kutokana kucheza soka ya nguvu akiwa mdogo na mfupi, ambalo limefunika jina lake halisi la Abdallah Athumani Seif. Mwenyewe anasema Kibadeni maana yake ni kitu cha baadaye. Kwamba kila siku alikuwa akionekana bado kwa umri na umbo wakati anaweza soka.
1969- Februari 2; Alijiunga na Simba SC ikiitwa Sunderland akitokea Kahe Republic ya Mtaa wa Kongo na Mchikichi, Kariakoo.
1974- Alifunga bao la pili katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Hearts Of Oak ya Ghana nchini Ghana katika Robo Fainali ya Kwanza ya Klabu Bingwa Afrika.
1974- Aliiongoza Simba kuwa klabu ya kwanza na pekee Tanzania kufika Nusu Fainali ya Klabu Bingwa Afrika hadi sasa.
1975- Aliiongoza Simba kuwa klabu ya kwanza kutwaa Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati Dar es Salaam.
1977- Alifunga mabao matatu peke yake katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Yanga SC.
1993- Aliiwezesha Simba SC kufika Fainali ya Kombe la CAF akiwa Kocha, rekodi ambayo haijavunjwa hadi leo ikiwa ni miaka 20 baadaye
1978-Aling’atuka Simba SC na kwenda kuwa kocha mchezaji Majimaji ya Songea.
2011- Alikwenda Hijja.

NEYMAR ATANGAZA RASMI KUWA MCHEZAJI RASMI WA BARCELONA.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Brazil, Neymar amemwaga wino na rasmi kuwa mchezaji rasmi wa klabu ya Barcelona ya Hispania. Neymar amesema amesaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo jana, zikiwa zimepita siku mbili baada ya kutangaza kuwa ameamua kuchagua timu hiyo badala ya mahasimu wao Real Madrid. Nyota huyo amesema anaondoka Santos huku akiwa na majonzi lakini pia ni heshima kwake kusajiliwa na klabu kama Barcelona ambapo katika hali ya kawaida amepata fursa ya kucheza na baadhi ya wachezaji bora kabisa duniani. Neymar mwenye umri wa miaka 21 atajiunga na nyota wenzake Barcelna akiwemo mshindi wan ne mfululizo wa tuzo ya mchezaji bora wa dunia Lionel Messi, Xavi Hernandez na Andres Iniesta. Sio Neymar wala Barcelona walioweka wazi ada halisi ya uhamisho huo lakini vyombo vya habari nchini Brazil vimedai kuwa Barcelona watalipa kiasi cha euro milioni 30 kwa nyota huyo.

MFAHAMU KWA UZURI TORREZ ELININYOOO MKALI WA MABAOOO

Fernando Torres
TorresFinale12 cropped.jpg
Taarifa kuhusu yeye
Jina kamiliFernando José Torres Sanz
Kuzaliwa20 March 1984 (age 29)
NchiFuenlabrada, Spain
Urefu1.83 m (6 ft 0 in)
Nafasi Mshambuliaji
Timu ya sasa
Current clubChelsea
Number9
Timu ya ujana
1995–2001Atlético Madrid
Timu za ukubwa
YearsTeamMechiGoli
2001–2007Atlético Madrid214(82)
2007–2011Liverpool102(65)
2011–Chelsea82(15)
Timu ya taifa
2000Spain U151(0)
2001Spain U169(11)
2001Spain U174(1)
2002Spain U181(1)
2002Spain U195(6)
2002–2003Spain U2110(3)
2003–Spain101(31)
KLABU ALIZOCHEZA NA KUPATA MATAJI
Atletico Madrid
Segunda Division: 2001-02 
Chelsea
Kombe la FA: 2011-12 
Ligi ya Mabingwa: 2011-12 
UEFA Europa Ligi: 2012-13 
Timu ya Taifa
Hispania U-16
Kombe la Ulaya la Chini- michuano miaka 16 : 2001
Hispania U-19
Kombe la Ulaya la Chini ya miaka 19 Kandanda michuano: 2002
Timu kubwa Hispania
Soka Ulaya UEFA michuano ya (2): 2008, 2012
Kombe la Dunia: 2010 
TUZO BINAFSI
1.Mfungaji bora Kombe la nike : 1999
2.Algarve cup Mchezaji wa Mashindano: 2001
3.Algarve mashindano mfungaji bora: 2001
4.Kombe la Ulaya la Chini-16 Mchezaji wa bora wa Mashindano: 2001
5.Kombe la Ulaya la Chini-16  mfungaji bora: 2001
6.Kombe la Ulaya la Chini ya 19 Mchezaji bora wa Mashindano: 2002 
7.Kombe la Ulaya la Chini ya 19 mfungaji bora wa michuano Soka: 2002.
8.Ligi Kuu ya PFA Timu ya Mwaka (2): 2007-08, 2008-09
9.Ligi Kuu ya Mchezaji wa Mwezi (2): Februari 2008, Septemba 2009.
10.Ligi Kuu mfungaji bora wa Mwezi (2): Aprili 2009,  Machi 2010.
11.UEFA Euro Timu ya mashindano: 2008
12.UEFA Timu ya Mwaka: 2008
13.FIFPro World XI mchezaji bora  (2): 2008, 2009
14.FIFA World Mchezaji bora  wa Mwaka : 2008
15.Ballon d'Or Nafasi ya tatu: 2008
16.Kombe la Shirikisho la Silver Boot: 2009
17.FIFA Confederations Cup Timu ya mashindano: 2009 
18.UEFA Euro Golden Boot: 2012 
TUZO ZA KIENYEJI"
1.Mkuu wa Asturias tuzo kwa ajili ya Michezo: 2010
2.Medali ya dhahabu ya Mpango Royal ya Michezo kiutamaduni: 2011. 

RAFAEL BENITEZ ATEULIWA KUWA KOCHA MPYA NAPOLI

Klabu ya Italy Napoli imemteuwa Rafael Benitez, Miaka 53 kuwa Meneja mpya wa klubu hiyo ambayo katika Msimu huu imeshika Nafasi ya Pili nyuma ya Mabingwa Juventus.
Msimu ujao wa 2013/14, Napoli itacheza UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI.
katika suala nzima la benitez kutua hapo ni kutokana na aliyekuwa Meneja wa club hiyo Walter Mazzarri, alitangazwa kuiacha Napoli na kuhamia Inter Milan.
Uteuzi huo wa Benitez ulithibitishwa na Rais wa Napoli Aurelio De Laurentiis ambae alimsifia Benitez na kumwita Kocha mwenye ujuzi wa Kimataifa.
aidha Benitez ndio kwanza amemaliza Kibarua cha kuwa Meneja wa muda Klabuni Chelsea na, Wiki mbili zilizopita, hapo Mei 15, aliiwezesha Chelsea kutwaa Kombe la EUROPA LIGI baada ya kuichapa Benfica Bao 2-1 kwenye Fainali.
hata hivyo Benitez aliteuliwa Meneja wa muda wa Chelsea Novemba Mwaka jana baada ya kufukuzwa Roberto Di Matteo.

LEWANDOWSKI ANANAFASI KUBWA KWENDA MUNICH-WAKALA

WAKALA wa mshambuliaji nyota wa klabu ya Borussia Dortmund, Robert Lewandowski amesema kuna uwezekano mkubwa wa mshambuliaji huyo kujiunga na mabingwa wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya Bayern Munich. Hata hivyo, wakala huyoaitwaye Cezary Kucharski aliiambia luninga moja nchini Ujerumani kwamba Bayern bado hawajafikia makubaliano ya mambo binafsi ya nyota huyo wa kimataifa wa Poland. Wakala huyo aliendelea kusema kuwa wao wako tayari lakini badi hawajasaini chochote kwasababu klabu nayo inatakiwa iafiki makubaliano hayo. Bayern ambao ni mabingwa wapya wa Ujerumani tayari wamemnyakuwa kiungo wa Dortmund Mario Gotze mwenye umri wa miaka 20 kwa ada ya euro milioni 37.

TORRES VS CASILLAS WAITWA TIMU YA TAIFA

KOCHA wa timu ya taifa ya Hispania, Vicente del Bosque amemuita golikipa Iker Casillas na mshambuliaji Fernando Torres katika kikosi cha wachezaji 26 ambacho kitaanza maandalizi ya Kombe la Shirikisho linalotarajiwa kuanza mwezi ujao nchini Brazil. Orodha hiyo ya wachezaji 26 itapunguzwa na kufikia 23 baada ya mzunguko wa mwisho wa mechi za Ligi Kuu nchini Hispania mwishoni mwa wiki ijayo. Hispania ambao ni mabingwa wa Dunia na Ulaya wana mechi mbili za kimataifa za kirafiki dhidi ya Haiti Juni 8 na Ireland siku tatu baadae kabla ya kuelekea nchini Brazil. Katika michuano ya Kombe la Shirikisho, Hispania imepangwa katika kundi B sambamba na Uruguay, Tahiti na Nigeria ambapo mchezo wa ufunguzi utachezwa Juni 16 dhidi ya Uruguay. 
Michuano hiyo ambayo inashirikisha timu nane inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 15 mpaka 30. 
Goalkeepers: Iker Casillas (Real Madrid), Victor Valdes (Barcelona), Pepe Reina (Liverpool)

Defenders: Alvaro Arbeloa (Real Madrid), Sergio Ramos (Real Madrid), Gerard Pique (Barcelona), Cesar Azpilicueta (Chelsea), Jordi Alba (Barcelona), Ignacio Monreal (Arsenal), Raul Albiol (Real Madrid), Javi Garcia (Manchester City)

Midfielders: Javi Martinez (Bayern Munich), Xavi (Barcelona), Andres Iniesta (Barcelona), Sergio Busquets (Barcelona), Santi Cazorla (Arsenal), Xabi Alonso (Real Madrid), Benat Etxebarria (Real Betis)
Forwards: Cesc Fabregas (Barcelona), David Villa (Barcelona), David Silva (Manchester City), Roberto Soldado (Valencia), Pedro (Barcelona), Juan Mata (Chelsea), Jesus Navas (Sevilla), Fernando Torres (Chelsea).

Monday, May 27, 2013

FRANK RIBERY ATANABAISHA KULALA NA KOMBE LA UEFA LIGI.

WINGA maarufu wa klabu ya Bayern Munich, Franck Ribery ametanabaisha kuwa alichukua Kombe la Ligi ya Mabingwa na kwenda nalo kitandani kufuatia ushindi wa timu yao wa mabao 2-1 dhidi ya Borussia Dortmund. Bayern wamefanikiwa kutinga fainali ya michuano hiyo mara tatu katika kipindi cha  miaka minne lakini walifanikiwa kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza toka mwaka 2001 kwa ushindi waliopata katika Uwanja wa Wembley Jumamosi. Na Ribery alibainisha hilo katika sherehe za kulitembeza kombe hilo mtaani huko Ujerumani kwamba alichukua kombe hilo na kwenda nalo nyumbani. Nyota huyo raia wa Ufaransa amesema alikuwa macho mpaka alfajiri na baadae kwenda kulala akiwa na mke wake pamoja na kombe hilo. Bayern sasa wana nafasi ya kushinda matatu matatu kwa mkupuo kama wakifanikiwa kushinda taji la DFB Pokal Juni mosi mwaka huu.

BENITEZ ATAKA KUIFUNDISHA TIMU INAYOSHIRIKI LIGI YA MABINGWA ULAYA.

MENEJA wa muda wa klabu ya Chelsea Rafael Benitez ametanabaisha kuwa anataka kufundisha timu inayoshiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao baada ya kumaliza kazi yake katika klabu hiyo.
Katika kipindi kifupi kijacho Benitez ataondoka Stamford Bridge akiwa ameisimamia klabu hiyo kwa mara ya mwisho Jumamosi iliyopita wakati walipocheza na Manchester City katika mchezo wa kirafiki uliofanyika jijini New York Marekani.
Kocha huyo raia wa Hispania ameiongoza Chelsea kushinda taji la Europa League pamoja na kuisadia kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao baada ya kuajiriwa kwa muda mfupi kuziba nafasi ya Roberto Di Matteo Novemba mwaka jana. 
Banitez anaondoka Chelsea kumpisha Jose Mourinho na kocha huyo sasa anaweza kuangalia mstakabali wake wa kuhusishwa na tetesi za kwenda Napoli na Paris Saint-Germain ambapo klabu zote hizo zinakidhi matakwa yake ya kushiriki Ligi ya Mabingwa.

RADAMEL FALCAO HATIMAYE ATUA KATIKA CLUB YA MONACO

STRAIKA MAHIRI wa Atletico Madrid, Radamel Falcao, atapimwa afya yake kwenye Klabu ya Monaco ambayo imepanda Daraja Msimu huu kurudi Ligue 1 ya France na Uhamisho wake unatarajiwa kugharimu Dau la Pauni Milioni 51.
Habari hizi zimevuja huko Spain na kudaiwa kuwa Atraika huyo kutoka Colombo atapimwa afya yake siku ya Jumatatu Mei 27.
Monaco, ambayo imenunuliwa na Tajiri wa Kirusi Dmitry Rybolovlev, tayari imeshawanunua Mastaa wa FC Porto Joao Moutinho na James Rodriguez kwa Dau la Jumla ya Pauni Milioni 60 na kutua kwa Falcao kutawafanya watatu hao wakutane tena kwani waliwahi kuchezea Klabu moja.
Kuhama kwa Falcao kulidokezwa na Meneja wa Atletico Madrid Diego Simeone ambae ameshasema hatakuwa na kinyongo ikiwa Falcao, mwenye Miaka 27, atahama.
Hivi Juzi, Kocha Msaidizi wa Monaco, Jean Petit, alidokeza wanatarajia Falcao na Wachezaji wengine wanne au watano wa kiwango chake kununuliwa na Klabu yao.
Mwezi Desemba 2011, Dmitry Rybolovlev alinunua Hisa za Asilimia 60 za Klabu ya Monaco na kuanza kuibadili wakati huo ikiogelea Daraja la chini huko France, Ligue 2, na Mwezi Mei 2012 alimteua Kocha wa zamani wa Chelsea Claudio Ranieri kuiongoza Monaco na amefanya hilo kwa mafanikio kwa kuirudisha Monaco Daraja la juu huko France.

NEYMAR HATIMAYE SASA ATUA FC BARCELONA

CLUB ya soka FC Barcelona imefikia Makubaliano na Klabu ya Brazil, Santos, ya kumsaini Neymar ambapo leo Jumatatu Mei 27 atasaini Mkataba ili kukamilisha Dili hiyo ya Uhamisho.
Klabu ya Barcelona imetoa Taarifa rasmi ya kuthibitisha kufikia makubaliano ya kumsaini Nyota huyo wa Brazil mwenye Miaka 21.
WASIFU:
Neymar da Silva Santos Junior
KUZALIWA: 5 Februari 1992, Nchini Brazil
Santos: Mechi 229 Magoli 138
Brazil: Mechi 32 Magoli 20
Na Mwenyewe Neymar alitoa Ujumbe kwenye Mtandao wa Instagram uliosema  kuwa jumatatu nasaini Mkataba na Barcelona. Nataka kuwashukuru Mashabiki wa Santos kwa Miaka hii 9 ya ajabu.
Juzi Klabu ya Santos ilitoa Taarifa kuwa imepokea Ofa mbili za kumnunua Neymar na ilisadikiwa zimetoka toka mbili kati ya Klabu za Barcelona, Real Madrid au Chelsea.
Mkataba wake na Santos ulitarajiwa kumalizika mwishoni mwa Msimu ujao, Mwezi Juni 2014.
Neymar anatarajiwa kujiunga na Barcelona mara baada ya kuiwakilisha Brazil kwenye Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara yatakayochezwa Nchini Brazil kuanzia Juni 15 hadi 30.
Neymar ndie ameiongoza Santos kupata mafanikio makubwa tangu Nguli Pele aache kuichezea Klabu hiyo kwenye Miaka ya 1970 kwa kuisaidia kutwaa Kombe la Brazil Mwaka 2010, Copa Libertadores Mwaka 2011 na Ubingwa wa Jimbo la Sao Paolo kwa mara 3 mfululizo.
Nayo Klabu ya Santos imesema kuwa ilijaribu kila njia ili Neymar abaki kwao lakini Ofa za nje zimewafanya wasiweze kushindana.
Hata hivyo, Santos imekataa kutaja Dili hiyo ya Uhamisho imegharimu kiasi gani kwa vile kila upande umekubaliana kuwa iwe siri.
             
WASIFU WA NEYMAR
Taarifa kuhusu yeye
Full name Neymar da Silva Santos Júnior
Date of birth 5 February 1992 (age 21)
Place of birth Mogi das Cruzes, Brazi
Height 1.74 m (5 ft 9 in)
Playing position Mshambuliaji
Club ya sasa
Current club Santos
Number 11
Timu za ujana
1999–2003 Portuguesa Santista
2003–2009 Santos
Timu ya ukubwa
Years Team Mechi Goli
2009– Santos 103 (54)
Timu ya Taifa
2009 Brazil U17 3 (1)
2011 Brazil U20 7 (9)
2012 Brazil U23 7 (4)
2010– Brazil 32 (20)

AGUERO BADO NIPO NIPO MAN CITY MPAKA 2017.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Manchester City, Sergio Aguero ameongeza mkataba wa mwaka mmoja ambao utamuweka katika klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu nchini Uingereza mpaka mwaka 2017. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 24 amefunga mabao 12 katika mechi 30 za ligi alizocheza msimu uliopita na kufunga bao la ushindi dhidi ya Queens Park Rangers lililowapa taji la ligi katika msimu wa 2011-2012. Mara baada ya kusaini mkataba huyo Aguero aliuambia mtandao wa klabu hiyo kwamba anajisikia furaha na kuhitajika hivyo atafanya kila awezalo ili aendelee kufanya kazi vyema na kuipa mataji klabu hiyo. Vyombo vya habari nchini Uingereza vilikuwa vikiripoti kuwa mchezaji huyo anaweza kutimkia Real Madrid lakini tetesi hizo zitakwisha baada ya kuwa mchezaji mwingine wa timu hiyo kuongeza mkataba baada ya Gael Clichy, Yaya Toure na David Silva kufanya hivyo.

KLOPP ASEMA TUTAIMARISHA KIKOSI FAINALI ZIJAZO

MENEJA wa klabu ya Borussia Dortmund, Jurgen Klopp ametanabaisha kuwa ataimarisha kikosi chake na kufikia fainali nyingine ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kipigo walichopata dhidi ya Bayern Munich. Dortmund walipoteza mchezo huo ulizikutanisha timu zote kutoka Ujerumani kwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Wembley baada ya bao la dakika za mwisho lililofungw ana Arjen Robben. Lakini kocha huyo ametamba kuwa pamoja na kushindwa katika fainali hiyo ya Wembley lakini anaamini atafikia fainali nyingine katika kipindi kifupi kijacho. Klopp amesema kwasasa ana kazi kubwa ya kuimarisha kikosi chake baada ya wachezaji kadhaa tegemeo kutaka kuondoka mwishoni mwa msimu huu lakini anaamini mpaka kufikia msimu mpya tayari atakuwa na kikosi imara. Kiungo tegemeo wa klabu hiyo Mario Gotze tayari imeshathibitishwa kwenda Bayern Msimu ujao huku mshambuliaji wake nyota Robert Lewandowski naye akijipanga kuelekea huko.

TAIFA STARS YAELEKEA ADDIS ABABA LEO.

TIMU ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajia kuondoka leo (Mei 26 mwaka huu) usiku kwenda Addis Ababa, Ethiopia ambapo itaweka kambi na kucheza mechi moja ya kirafiki kabla ya kwenda Morocco. Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itaondoka saa 5 usiku kwa ndege ya EgyptAir ikiwa na kikosi cha wachezaji 21 chini ya nahodha wake kipa Juma Kaseja. Timu hiyo ikiwa Ethiopia, Juni 2 mwaka huu itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan ambapo siku inayofuata itaondoka kwenda Marrakech, Morocco kwa kupitia Cairo, Misri. Mechi hiyo ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech.

Mbali ya nahodha Kaseja, wachezaji wengine wanaoondoka katika kikosi hicho ambacho kina wiki sasa tangu kingie kambini jijini Dar es Salaam ni Mwadini Ally na Ally Mustafa ambao wote ni makipa. Wengine ni Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Aggrey Morris, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd na Haruni Chanongo. Wachezaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu ambao wako na timu yao ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo watajiunga moja kwa moja na Stars jijini Marrakech, Juni 4 mwaka huu wakitokea Maputo, Msumbiji mara baada ya mechi yao ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Liga Muculumana ya huko. Katika msafara huo wa Ethiopia benchi la ufundi la Stars linaundwa na Kim Poulsen (Kocha Mkuu), Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi),Juma Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja wa timu), Dk. Mwanandi Mwankemwa (Daktari), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred Chimela (Mtunza vifaa).

Saturday, May 25, 2013

30 TWIGA STARS WAITWA KAMBINI KESHO MEI 26 MWAKA HUU

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu (Twiga Stars), Rogasian Kaijage amewaita kambini wachezaji 30 ikiwa ni mwendelezo wa kuijenga na kuiimarisha timu hiyo.

Twiga Stars itakuwa na kambi ya siku kumi kuanzia Jumapili (Mei 26 mwaka huu) ambapo baadaye inatarajia kucheza mechi moja ya kirafiki kabla ya wachezaji kurudi kwenye klabu zao.

Kambi hiyo ni mwendelezo wa programu iliyopendekezwa na kocha kuijenga na kuiimarisha timu hiyo kwa vile haina mashindano mwaka huu, na itakuwa kambi ya pili baada ya ile iliyofanyika Machi mwaka huu.

Wachezaji walioitwa na klabu zao kwenye mabano ni Asha Rashid (Mburahati Queens), Aziza Mwadini (Zanzibar), Belina Julius (Lord Barden), Ester Chabruma (Sayari), Ester Mayala (TSC Academy), Eto Mlenzi (JKT), Evelyn Sekikubo (Mburahati Queens) na Fatuma Bushiri (Mburahati Queens).

Fatuma Hassan (Mburahati Queens), Fatuma Omari (Sayari), Flora Kayanda (Tanzanite), Hamisa Athuman (Marsh Academy), Hellen Peter (JKT), Maimuna Said (JKT), Mwajuma Abdallah (Tanzanite), Mwanahamisi Omari (Mburahati Queens), Mwanaidi Tamba (Mburahati Queens) na Mwapewa Mtumwa (Sayari).

Nabila Ahmed (Marsh Academy), Pulkeria Charaji (Sayari), Rehema Abdul (Lord Barden), Rukia Khamis (Uzuri Queens), Semeni Abeid (Tanzanite), Sharida Boniface (Makongo Sekondari), Sophia Mwasikili (Sayari), Therese Yona (TSC Academy), Vumilia Maarifa (Evergreen) na Zena Khamis (Mburahati Queens).

RCL KUENDELEA KUTIMUA VUMBI KESHO
Raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) inaendelea kesho (Mei 26 mwaka huu) kwa mechi sita za kwanza zitakazochezwa katika miji sita tofauti.


Abajalo ya Dar es Salaam na Kariakoo ya Lindi zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam wakati Machava FC ya Kilimanjaro itakuwa mwenyeji wa Mpwapwa Stars ya Dodoma kwenye Uwanja wa Ushirika mjini Moshi.

Nayo Stand United FC ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida huku Polisi Jamii ya Bunda mkoani Mara ikimenyana na Biharamulo FC ya Kagera kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.

Mjini Kigoma kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika ni kati ya wenyeji Saigon FC na Katavi Warriors ya Katavi wakati Njombe Mji itaikaribisha Kimondo SC ya Mbeya kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.

Leo (Mei 25 mwaka huu) Friends Rangers ya Kinondoni, Dar es Salaam inacheza na African Sports ya Tanga kwenye Uwanja wa Azam Chamazi. Mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu.

Timu zitakazofuzu kucheza raundi ya tatu zitacheza mechi za kwanza kati ya Juni 8 na 9 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitakuwa kati ya Juni 15 na 16 mwaka huu.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Friday, May 24, 2013

UCL: WATOTO WA BABA MMOJA USO KWA USO WEMBLEY

NI FAINALI ya kukata na shoka  hapo Kesho katika dimba la  uwanja wa wembley uliopo jijini london nchini uingereza watoto wa baba mmoja kutoka ujerumani watavaana  kucheza Fainali ya Klabu Bingwa Ulaya  ambapo Borussia Dortmund na Bayern Munich watakukutana hapo  kesho Jumamosi Mei 25 na kila upande imejipanga kuhakikisha inaibuka na ushindi hasa kisaikolojia
Hii ni mara ya kwanza kwa Klabu za Germany kukutana Fainali ya UCL, hii itakuwa mara ya 4 kwa Klabu za Nchi moja kukutana Fainali hizi.
Mwaka 2000, Klabu za Spain, Real Madrid na Valencia, zilivaana, Mwaka 2003 AC Milan na Juventus za Italy zilipigana na 2008 ni Man United v Chelsea za England.
Kwa Bayern Munich hii ni Fainali yao ya 10 ya Klabu Bingwa Ulaya wakiwa nyuma ya Real Madrid, waliofika Fainali 12, na AC Milan, Fainali 11,
Hii itakuwa Fainali ya 3 kwa Bayern ndani ya Misimu minne iliyopita lakini mara ya mwisho kutwaa Kombe la UCL ni Mwaka 2001.
Kwa Borussia Dortmund, hii ni Fainali ya Pili kwao ambapo walishinda ile ya kwanza ya Mwaka 1997.
Baada ya kutwaa Ubingwa wa Ulaya Mwaka 1997, Msimu uliofuata, 1997/98, Borussia Dortmund na Bayern Munich zilikutana Robo Fainali ya UCL na Borussia kusonga kwa Jumla ya Bao 1-0.

KLABU ZA NCHI MOJA KUUMANA FAINALI ULAYA

UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI
1999/2000 Real Madrid 3-0 Valencia CF
2002/03 AC Milan 0-0 Juventus (AC Milan washinda kwa Penati 3-2)
2007/08 Manchester United 1-1 Chelsea FC (Man United washinda kwa Penati 6-5)
UEFA CUP
1979/80 VfL Borussia Mönchengladbach 3-2 Eintracht Frankfurt

WAPI WAMETOKA MPAKA KUFIKA FAINALI:
FAHAMU:  -N: Nyumbani -U: Ugenini
BORUSSIA DORTMUND BAYERN MUNICH
KUNDI  D: KUNDI  F:
MSHINDI MSHINDI
-Ajax: 1-0 [N] 4-1 [U] -Valencia: 2-1 [N] 1-1 [U]
-Man City: 1-1 [U]] 1-0 [N] -BATE Borislov:1-3 [U] 4-1 [N]
-Real Madrid: 2-1 [N] 2-2 [U] Lille: 1-0 [U] 6-1 [N]
RAUNDI ZA MTOANO: RAUNDI ZA MTOANO:
-Donetsk: 2-2 [U] 3-0 [N] -Arsenal: 3-1 [U] 0-2 [N]
-Malaga: 0-0 [U] 3-2 [N] -Juventus: 2-0 [N] 2-0 [U]
-Real Madrid: 4-1 [N] 2-0 [U] -Barcelona: 4-0 [N] 3-0 [U]

DONDOO MUHIMU:
REFA:
-Nicola Rizzoli [Italy] akisaidiwa na wenzake toka Italy Renato Faverani na Andrea Stefani na Refa wa Akiba, Damir Skomina, wa Slovenia.
BALOZI MAALUM:
-Steve McManaman, Mshindi mara mbili wa UCL, ni Mchezaji wa zamani wa Kimataifa wa England
SHERIA ZA FAINALI:
-Baada Dakika 90 kama Sare, zitachezwa Dakika za Nyongeza 30 na kama bado Sare ni Mikwaju ya Penati kuamua Bingwa.
-Kila Timu itakuwa na Wachezaji wa Akiba 7
-Kila Timu inaruhusiwa kubadili Wachezaji Watatu tu.
UWANJA: Wembley Stadium
-Ndio Uwanja wa Nyumbani wa Timu ya Taifa ya England.
-Ingawa ndio ilichezwa Fainali ya UCL Mwaka 2011, UEFA imeuteua tena kwa kuadhimisha Miaka 150 ya uhai wa FA, Chama cha Soka England.
-Ni mara ya 7 kwa Wembley kutumika kwa Fainali za Klabu Bingwa Ulaya nyingine zikiwa za Miaka ya 1963, 1968, 1971, 1978, 1992 na 2011.
-Katika Fainali za Miaka ya 1968 na 1978, Klabu za England zilitwaa Ubingwa kwa Mwaka 1968 Manchester United kuichapa Benfica Bao 4-1 na Liverpool kuifunga Club Brugge 1-0 Mwaka 1978.
MATOKEO MICHIZO ZA HIVI KARIBUNI
[BUNDESLIGA PAMOJA NA DFB POKAL]
04/05/13      Borussia Dortmund v Bayern Munich       1 : 1
27/02/13      Bayern Munich v Borussia Dortmund       1 : 0
01/12/12      Bayern Munich v Borussia Dortmund       1 : 1
12/08/12      Bayern Munich v Borussia Dortmund       2 : 1
12/05/12      Borussia Dortmund v Bayern Munich       5 : 2
11/04/12      Borussia Dortmund v Bayern Munich       1 : 0
19/11/11      Bayern Munich v Borussia Dortmund       0 : 1
26/02/11      Bayern Munich v Borussia Dortmund       1 : 3
03/10/10      Borussia Dortmund v Bayern Munich       2 : 0
13/02/10      Bayern Munich v Borussia Dortmund       3 : 1
12/09/09      Borussia Dortmund v Bayern Munich       1 : 5
08/02/09      Bayern Munich v Borussia Dortmund       3 : 1
23/08/08      Borussia Dortmund v Bayern Munich       1 : 1
23/07/08      Borussia Dortmund v Bayern Munich       2 : 1
19/04/08      Borussia Dortmund v Bayern Munich       1 : 2
13/04/08      Bayern Munich v Borussia Dortmund       5 : 0
28/10/07      Borussia Dortmund v Bayern Munich       0 : 0
26/01/07      Borussia Dortmund v Bayern Munich       3 : 2
11/08/06      Bayern Munich v Borussia Dortmund       2 : 0
13/05/06      Bayern Munich v Borussia Dortmund       3 : 3
17/12/05      Borussia Dortmund v Bayern Munich       1 : 2
19/02/0        Bayern Munich v Borussia Dortmund       5 : 0
18/09/04      Borussia Dortmund v Bayern Munich       2 : 2
17/04/04      Borussia Dortmund v Bayern Munich       2 : 0
09/11/03      Bayern Munich v Borussia Dortmund       4 : 1
19/04/03      Borussia Dortmund v Bayern Munich       1 : 0
Ukitazama kuelekea mchezo wa kesho Bayen munich inanafasi kubwa kutwaa kombe hili lakini ukitazama zaidi timu hizi zinaupinzani wa hali ya juu hivyo timu ambayo itakuwa imejipanga na kufanya maandalizi mazuri basi inanafasi ya kutwaa ubingwa msimu wa UCL UEFA CHAMPION LIGI MSIMU WA 2012-2013

 TAZAMA MSIMO WA BUNDASLIGA
*FAHAMU NI BINGWA BAYERN MUNICH BUNDASLIGA
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Bayern Munich
34
28
4
1
94
18
82
92
2
BV Borussia Dortmund
34
19
9
5
80
42
41
66










MABINGWA WALIOPITA WA UCL

MWAKA               BINGWA


1955–56 Real Madrid
1956–57 Real Madrid
1957–58 Real Madrid
1958–59 Real Madrid
1959–60 Real Madrid
1960–61 Benfica
1961–62 Benfica
1962–63 Milan
1963–64 Internazionale
1964–65 Internazionale
1965–66 Real Madrid
1966–67 Celtic
1967–68 Manchester United
1968–69 Milan
1969–70 Feyenoord
1970–71 Ajax
1971–72 Ajax
1972–73 Ajax
1973–74 Bayern Munich
1974–75 Bayern Munich
1975–76 Bayern Munich
1976–77 Liverpool
1977–78 Liverpool
1978–79 Nottingham Forest
1979–80 Nottingham Forest
1980–81 Liverpool
1981–82 Aston Villa
1982–83 Hamburg
1983–84 Liverpool
1984–85 Juventus
1985–86 Steaua București
1986–87 Porto
1987–88 PSV Eindhoven
1988–89 Milan
1989–90 Milan
1990–91 Red Star Belgrade
1991–92 Barcelona
1992–93 Marseille
1993–94 Milan
1994–95 Ajax
1995–96 Juventus
1996–97 Borussia Dortmund
1997–98 Real Madrid
1998–99 Manchester United
1999–2000 Real Madrid
2000–01 Bayern Munich
2001–02 Real Madrid
2002–03 Milan
2003–04 Porto
2004–05 Liverpool
2005–06 Barcelona
2006–07 Milan
2007–08 Manchester United
2008–09 Barcelona
2009–10 Internazionale
2010–11 Barcelona
2011–12 Chelsea