Saturday, June 29, 2013

ARSENAL WAMTAKA KIPA JULIO CESAR WA QPR ILIYOSHUKA DARAJA"

Wanted: Julio Cesar is set to join Arsenal following Queens Park Rangers' relegation to the Championship WASHIKA Bunduki wa jiji London Club ya Arsenal itaangalia uwezekano wa kukamilisha usajili wa kipa namba wa Brazil na klabu ya Queens Park Rangers, Julio Cesar baada ya Kombe la Mabara.
Arsene Wenger anataka kipa mzoefu atengeneze ushindani kwa Lukasz Fabianski na Wojciech Szczesny.
Mazungumzo baina ya wawakilishi wa Cesar na viongozi wa Gunners tayari yamefanyika, lakini hayajamalizika kwa kuwa kipa huyo yupo kwenye majukumu ya kimataifa.
Wanted: Julio Cesar is set to join Arsenal following Queens Park Rangers' relegation to the Championship
ARSENAL sasa inatarajiwa kumaliza dili hilo mara moja tu, baada ya kubainika Roma ya Italia nayo imeingia kwenye mbio za kuwania saini ya Cesar.
Kipa huyo wa kimataifa wa Brazil ambaye yupo huru kuondoka Loftus Road kufuatia kushuka kwa QPR hadi Championship, anataka kubaki London ambako amezoea maisha tangu awasili msimu uliopita akitokea Inter Milan.
Na The Gunners – ambayo inatumai kukamilisha pia usajili wa Gonzalo Higuain wiki ijayo, baada ya kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti kufungua njia kwa mshambuliaji huyo kuondoka  Hispania – inajiamini dili hilo litakamilishwa baada ya Fainali ya Kombe la Mabara Jumapili.
Wenger alitaka kusajili kipa wa Stoke, Asmir Begovic na wa Liverpool, Pepe Reina lakini, licha ya kuwa na fungu la bajeti ya usajili la Pauni Milioni 70, kocha huyo wa Arsenal ameona  hana sababu ya kutumia fedha nyingi kwa ajili ya kipa.
Rangers itasikiliza ofa ya kiasi cha Pauni Milioni 2 kwa Cesar, wakati mshahara wake wa Pauni 70,000 kwa wiki halitakuwa tatizo kwa The Gunners, ambayo imetuma waangalia vipaji wake nchini Brazil kumuangalia Cesar anachokifanya katika Kombe la Mabara.
Pamoja na mpango wa kuwasajili Cesar na Higuain, The Gunners pia wanataka kumsajili beki wa Swansea, Ashley Williams na kiungo wa Everton, Marouane Fellaini. Lakini masuala ya kifedha yanatia saka kama Arsenal itaweza kusajili wachezaji wote hao.
Hadi sasa, Arsenal imegoma kumpa Fellaini mshahara wa Pauni 100,000 kwa wiki na pia imeshindwa kufika dau la Pauni Milioni 24 za kumnunua.
Missing out? Arsenal look set to be priced out of moves for Marouane Fellaini and Ashley Williams (below) Amekosekana? Arsenal inataka kuwasajili Marouane Fellaini

MBEYA MWENYEJI WA NETIBOLI TENA KWA MARA YA PILI MFULULIZO".

Jiji la Mbeya kwa mara ya pili mfululizo,litakuwa mwenyeji wa ligi kuu ya Netiboli taifa ambapo  naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo anatarijiwa kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi kuanzia Agosti 24 hadi Septemba 7.
Mwenyekiti wa chama cha Netiboli Mkoa wa Mbeya, Mary Mung’ong’o ameumabia mtandao huu kuwa ligi hiyo inafanyika kwa mara nyingine kutokana na ombi la Waziri Mulugo kwa vile ligi hiyo haikuwa imefana, hivyo akaiomba CHANETA kuwapa Mbeya fursa nyingine ya uwenyeji.
Alisema maandalizi ya ligi yameanza na kusema zinahitajika sh milioni 16 kufanikisha na kuongeza kuwa hadi sasa, hawajajua timu ngapi zitashiriki kutokana na jukumu hilo kuwa chini ya Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA).
Hata hivyo, mwenyekiti huyo ametoa wito kwa viongozi wa ngazi mbalimbli wakiwemo wadau wenye mapenzi na mchezo kutoka mkoani hapa kujitoa kwa hali na mali kuyafanikisha ili yawe chachu ya kukua kwa mchezo huo nchini kwa maslahi ya vijana na taifa.
Aidha, mwenyekiti huyo alitamtambulisha Nwaka Mwakisu kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano hayo.
Akizungumzia mashindano hayo, Mwakisu alisema ni fursa kwa watu wa Mbeya kujitangaza kibiashara kupitia mchezo huo na kufuta makosa yaliyofanyika mwaka jana.
Alisema katika kufakisha mashindano hayo, nguvu ya pamoja inahitajika kuanzia viongozi wa kisiasa, serikari na vyombo vya habari.

MBASPO FC YATWAA UBINGWA WA AIRTEL RISING KWA MKOA WA MBEYA"

Kama kawaidaTimu ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Mbaspo imefanikiwa kuwa mabingwa wa Airtel Rising Stars mkoa wa Mbeya baada ya kukusanya pointi nne sawa na mahasimu wao Mbosa fc lakini wakiwa na magoli mengi ya kufunga. Timu ya Mbeya Secondari haikupata hata pointi moja katika michuano hiyo ya kusaka vipaji

Mbaspo walianza mbio zao za kutwaa ubingwa kwa kutoshana nguvu ya 3-3 dhidi ya Mbosa siku ya Jumatatu Juni 24 kabla ya kufanya mauaji makubwa ya 6-0 dhidi ya timu dhaifu ya Mbeya Sekondari siku ya Jumanne. Michezo yote imefanyika kwenye uwanja wa Magereza jijini Mbeya.
Mbosa walifikisha point nne juzi Jumatano walipoitandika Mbeya Sekondari 3-0 hivyo kumaliza wakiwa na point nne na magoli sita wakati wapinzani wao Mbaspo wakifikisha jumla ya magoli tisa ya kufunga. Katika mechi ya juzi, magoli ya Mbosa yalitiwa kwenye kamba na Michael Mwashilanga, Riziki Juma na Julius Landa.
Wakati huo huo, chama cha mpira wa miguu mkoa wa Mbeya kimetangaza kikosi cha wachezaji 18 kuuwakilisha mkoa huo kwenye michuano ya Taifa ya Airtel Rising Stars inayoanza kutimua vumbi kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam kuanzia Julai 2.

Wachezaji hao ni Ismail Yesaya, Emmanuel Alex, Gift Sanga, Jackson Mwaibambe, Boaz Mwangole, Costa Sanga, Seif Zubery, Stanley Angelo, Enock Sikaonga, Kaunda Malata, Joel Kasimila, Hamprey Nyeo, Elia Salengo, Peter Noah, Emmaneul Mtimbi, Michael Bosco, Richard Kalinga na Zamoyoni Mwashambwa. 

Katika mkoa wa Morogoro, mji kasoro bahari, timu ya Moro Kids imetoka sare ya bila kufungana na Techfort katika mchezo wa kushambuliana kwa zamu uliopigwa kwenye uwanja wa shule ya sekondari ya Morogoro juzi Jumatano na kushuhudiwa na mashabiki wengi wa mji huo
Airtel Rising Stars vile vile imeanza kutimua vumbi katika jiji la Mwanza ambapo timu ya Marsh Athletical imedhihirisha umwambe wake katika soka baada ya kuifunga Nyamagana United 2-0 kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana.
Timu za mikoa zimepangwa kuanza kuwasili jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki tayari kwa ajili ya kindumbwe ndumbwe cha Airtel Rising Stars ngazi ya taifa katika uwanja wa Kumbukumbu ya Karume. Wachezaji 16 watachaguliwa wakati wa mashindano hayo ili kuunda timu itakayoiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars. Nchi mwenyeji wa michuano hiyo itatangazwa baadaye mwezi ujao.

Friday, June 28, 2013

YANGA YAITAKA TFF IWALIPE KABLA JUMAPIL

YANGA_MJENGOWAKATI inasemekana TFF walishalipwa Shilingi Milioni 200 toka kwa Wadhamini wa Ligi Kuu ya Bara, VODACOM, tangu Mwezi uliopita zikiwa ni Zawadi kwa Washindi mbali mbali wa Ligi hiyo, Klabu zimelalamika kutolipwa Zawadi zao na Yanga wametaka walipwe Milioni 70 zao kabla Jumapili.
Zawadi hizo ni kwa ajili ya kumtunukia Bingwa, Yanga, pia wengine wanaostahili ni ni Azam FC, Simba, Kagera Sugar pamoja na Wachezaji mbali mbali wakiwemo Kipa Bora, Mfungaji Bora, ambae ni Kipre Tcheche wa Azam FC, Refa Bora, Kocha Bora na kadhalika.
Hata hivyo, Vodacom inasemekana wameshatangaza Zawadi hizo zitagawiwa mapema Mwezi ujao na hilo limegusiwa pia na TFF ambao wamesema wanaandaa Siku maalum ya kutoa Zawadi hizo ikiwa ni pamoja na kualika Maafisa wa Serikali pamoja na wale kutoka Wizara husika hasa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Msimu uliopita hata Simba walicheleweshwa kupata Zawadi yao kama Bingwa baada ya kusubiri karibu Miezi miwili tangu Ligi imalizike ili kupata Tuzo yao.
Yanga walitwaa Ubingwa wa Ligi Kuu Vodacom kwa Msimu wa 2012/13 uliomalizka Mwezi Mei lakini wao walitwaa Ubingwa huo mapema kabla Msimu huo haujafika tamati.

WAWILI WALA SHAVU WACHAGULIWA KITUO CHA VIPAJI ASPIRE

Wachezaji wawili kutoka Tanzania wamechaguliwa miongoni mwa 50 waliofanyiwa majaribio nchini Uganda kwa ajili ya kuingia katika kituo cha kuendeleza vipaji (centre of excellence) kilichoko Doha nchini Qatar kupitia mpango wa kukuza vipaji wa Aspire Football Dream.
Abdulrasul Tahir Bitebo (15) ambaye ni mshambuliaji kutoka Kituo cha Uwanja wa Karume, na Martin Omela Tangazi (14) ambaye ni beki kutoka Kituo cha Ukonga ndiyo waliochaguliwa kutoka Tanzania kuingia katika kituo ambapo watakaa kwa mwezi mmoja kabla ya kusaini mkataba rasmi wa kuendelezwa.

Wachezaji wengine walikuwa wakitoka katika nchi za Uganda na Kenya. Mchezaji mwingine aliyefuzu katika nafasi tatu zilizokuwepo ni kutoka nchini Kenya.

Mpango wa Aspire Football Dream unafadhiliwa na Mtoto wa Mfalme wa Qatar katika nchi 16 duniani, na kwa hapa nchini uko chini ya Idara ya Ufundi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

TFF ina jumla ya vituo 14 vya kuendeleza vipaji kupitia mpango huo wa Aspire Football Dream. Vituo hivyo ni Karume, Kigamboni, Tandika, Kawe, Ukonga, Kitunda, Mbagala, Magomeni, Makongo, na Tabata vilivyo katika Mkoa wa Dar es Salaam. Vingine ni Bagamoyo kilichopo mkoani Pwani, Morogoro, Arusha na Moshi mkoani Kilimanjaro.

Kituo kingine cha kuendeleza vipaji (centre of excellence) cha Aspire kipo Dakar nchini Senegal.

TFF KUENDESHA KOZI SITA KATI YA JULAI- SEPTEMBA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaendesha kozi sita tofauti za mpira wa miguu kati ya Julai na Septemba mwaka huu.

Kozi hizo ni FIFA 11 For Health itakayofanyika Hombolo mkoani Dodoma kuanzia Julai 8 hadi 19 mwaka huu. Julai 6 hadi 15 mwaka huu kutakuwa na kozi ya mpira wa miguu wa ufukweni (Beach Soccer) itakayofanyika jijini Dar es Salaam.

Waamuzi wa FIFA nao watakuwa na kozi itakayofanyika kati ya Agosti 22 hadi 26 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati kozi ya ukocha kwa ajili ya Copa Coca-Cola itafanyika jijini Dar es Salaam kati ya Agosti 12 na 17 mwaka huu.

Vilevile kutakuwa na kozi ya mpango wa grassroots unaolenga wachezaji mpira wa miguu (wasichana na wavulana) wenye umri kuanzia miaka 6-12 itafanyika kuanzia Septemba 9 hadi 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati tamasha (festival) la grassroots litafanyika Uwanja wa Karume, Septemba 14 mwaka huu.

RCL KUKAMILISHA HATUA YA NNE JUMAPILI
Mechi za marudiano za hatua ya nne ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) zitachezwa Jumapili (Juni 30 mwaka huu) kwenye viwanja vya Sokoine jijini Mbeya, na Kambarage mjini Shinyanga.

Friends Rangers ya Dar es Salaam ambayo katika mechi ya kwanza ilifungwa nyumbani mabao 3-0 itakuwa mgeni wa Stand United FC mjini Shinyanga wakati Kimondo SC itaikaribisha Polisi Jamii ya Mara jijini Mbeya. Katika mechi ya kwanza timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.

Hatua ya mwisho ya RCL itachezwa Julai 3 mwaka huu kwa mechi za kwanza wakati zile za marudiano zitafanyika Julai 7 mwaka huu. Timu tatu za kwanza zitapanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MAN UNITED USO KWA USO NDANI YA EVERTON WATAKA KUIBOMOA

Mabingwa wa BPL msimu uliopita Club ya soka ya Manchester United imeamua kumtengea kitita cha paundi milioni 15 kwa ajili ya kumnasa beki wa Everton, Leighton Baines. Baada ya kukataa ofa ya awali ya United ya Pauni Milioni 12, Everton imesisitiza kuwa beki huyo wa kushoto wa kimataifa wa England hauzwi. Lakini United imepania kupanda dau hadi paundi milioni 20 katika kuwania saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. Mrithi wa Moyes, Everton, Roberto Martinez anataka kumbakzia beki huyo na klabu hiyo inataka kumpa mkataba mpya ikimuongezea mshahara hadi paundi 70,000 kwa wiki. Mpango huu unamuweka shakani beki Mfaransa, Patrice Evra juu ya mustakabali wake Old Trafford na wazi sasa anaweza kuhamia Monaco au Paris Saint-Germain.

WAMSHANGAA MESSI BAADA YA KUTUA NCHIN SENEGAL-WAKANYAGANA

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Argentina Lionel Messi ametua nchini Senegal jana kwa ndege binafsi na kulakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Dakar na mashabiki wa soka na vijana wadogo waliotoka pembe mbalimbali za nchi hiyo. Nyota huyo anayecheza katika klabu ya Barcelona alialikwa na shule ya soka ya Qatar Aspire ambao wana tawi lao nchini humo kwa ajili ya kwenda kwenye kampeni ya kupiga vita ugonjwa wa malaria. Kwa mujibu wa waratibu ya ziara hiyo maelfu ya neti ambazo zitakuwa na picha ya Messi zitasambazwa kwa watoto na familia katika vijiji mbalimbali nchini humo. Messi atasafiri kwa helikopta kwenda Saly eneo la karibu na mji wa Dakar ambapo atatembelea nyumba za yatima na kuongea na wenyeji wa hapo jinsi watakavyoweza kujikinga na malaria.

HISPAIN YATINGA FAINALI SASA KUUMANA NA WENYEJI BRAZIL

Close shave: Spain moved through to the Confederations Cup final after beating Italy on penalties in FortalezaTimu ya taifa ya hispain imefanikiwa kutinga hatua ya fainali baada ya kuitooa Italia katika Kombe la Mabara kwa ushindi wa matuta wa 7-6 mjini Fortaleza, kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120 katika mchezo wa Nusu Fainali usiku huu.
Wataliano walifungwa na Waspanyola katika Fainali ya Euro mwaka jana wameshindwa kulipa kisasi na sasa Fainali ya michuano hiyo mwaka huu Jumapili Uwanja wa Maracana, itawakutanisha wenyeji La Roja na Brazil wenyeji.
Leonardo Bonucci wa Italia alikosa moja ya penalti 14 na Jesus Navas akaweka nyavuni mkwaju wa mwisho na kuipeleka Hispania Fainali.
 TUTAFAKARI KUELEKEA FAINALI JE NANI KUIBUKA NA UBINGWA"
USO KWA USO
JUMLA: Mechi 8
USHINDI: Brazil 4 Spain 2
SARE: 2
MAGOLI JUMLA: Brazil 11 Spain 8
Mechi zenyewe:
FIFA KOMBE LA DUNIA:
Jumla: Mechi 5
USHINDI: Brazil 3 Spain 1
SARE: 1
MAGOLI JUMLA: Brazil 10 Spain 5
1986  Spain 0 Brazil 1 {Guadalajara, Mexico}
1978  Brazil 0 Spain 0 {Mar Del Plata, Argentina}
1962  Brazil 2 Spain 1 {Vina Del Mar, Chile}
1950  Brazil 6 Spain 1 {Rio De Janeiro, Brazil}
1934  Spain 3 Brazil 1 {Genoa, Italy}
KIRAFIKI:
Jumla: Mechi 3
USHINDI: Brazil 1 Spain 1
SARE: 1
MAGOLI: Spain 3 Brazil 1
1999  Spain 0 Brazil 0 {Vigo, Spain}
1990  Spain 3 Brazil 0 {Gijon, Spain}
1981  Brazil 1 Spain 0 {Salvador, Brazil}

WAWILI WACHAGULIWA KITUO CHA VIPAJI ASPIRE

Wachezaji wawili kutoka Tanzania wamechaguliwa miongoni mwa 50 waliofanyiwa majaribio nchini Uganda kwa ajili ya kuingia katika kituo cha kuendeleza vipaji (centre of excellence) kilichoko Doha nchini Qatar kupitia mpango wa kukuza vipaji wa Aspire Football Dream.
Abdulrasul Tahir Bitebo (15) ambaye ni mshambuliaji kutoka Kituo cha Uwanja wa Karume, na Martin Omela Tangazi (14) ambaye ni beki kutoka Kituo cha Ukonga ndiyo waliochaguliwa kutoka Tanzania kuingia katika kituo ambapo watakaa kwa mwezi mmoja kabla ya kusaini mkataba rasmi wa kuendelezwa.

Wachezaji wengine walikuwa wakitoka katika nchi za Uganda na Kenya. Mchezaji mwingine aliyefuzu katika nafasi tatu zilizokuwepo ni kutoka nchini Kenya.

Mpango wa Aspire Football Dream unafadhiliwa na Mtoto wa Mfalme wa Qatar katika nchi 16 duniani, na kwa hapa nchini uko chini ya Idara ya Ufundi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

TFF ina jumla ya vituo 14 vya kuendeleza vipaji kupitia mpango huo wa Aspire Football Dream. Vituo hivyo ni Karume, Kigamboni, Tandika, Kawe, Ukonga, Kitunda, Mbagala, Magomeni, Makongo, na Tabata vilivyo katika Mkoa wa Dar es Salaam. Vingine ni Bagamoyo kilichopo mkoani Pwani, Morogoro, Arusha na Moshi mkoani Kilimanjaro.

Kituo kingine cha kuendeleza vipaji (centre of excellence) cha Aspire kipo Dakar nchini Senegal.

TFF KUENDESHA KOZI SITA KATI YA JULAI- SEPTEMBA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaendesha kozi sita tofauti za mpira wa miguu kati ya Julai na Septemba mwaka huu.

Kozi hizo ni FIFA 11 For Health itakayofanyika Hombolo mkoani Dodoma kuanzia Julai 8 hadi 19 mwaka huu. Julai 6 hadi 15 mwaka huu kutakuwa na kozi ya mpira wa miguu wa ufukweni (Beach Soccer) itakayofanyika jijini Dar es Salaam.

Waamuzi wa FIFA nao watakuwa na kozi itakayofanyika kati ya Agosti 22 hadi 26 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati kozi ya ukocha kwa ajili ya Copa Coca-Cola itafanyika jijini Dar es Salaam kati ya Agosti 12 na 17 mwaka huu.

Vilevile kutakuwa na kozi ya mpango wa grassroots unaolenga wachezaji mpira wa miguu (wasichana na wavulana) wenye umri kuanzia miaka 6-12 itafanyika kuanzia Septemba 9 hadi 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati tamasha (festival) la grassroots litafanyika Uwanja wa Karume, Septemba 14 mwaka huu.

RCL KUKAMILISHA HATUA YA NNE JUMAPILI
Mechi za marudiano za hatua ya nne ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) zitachezwa Jumapili (Juni 30 mwaka huu) kwenye viwanja vya Sokoine jijini Mbeya, na Kambarage mjini Shinyanga.

Friends Rangers ya Dar es Salaam ambayo katika mechi ya kwanza ilifungwa nyumbani mabao 3-0 itakuwa mgeni wa Stand United FC mjini Shinyanga wakati Kimondo SC itaikaribisha Polisi Jamii ya Mara jijini Mbeya. Katika mechi ya kwanza timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.

Hatua ya mwisho ya RCL itachezwa Julai 3 mwaka huu kwa mechi za kwanza wakati zile za marudiano zitafanyika Julai 7 mwaka huu. Timu tatu za kwanza zitapanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

TENGA ASEMA MKUTANO UPO PALEPALE"-MKUU WA TFF

TFF_LOGO12SHIRIKISHO la Soka Tanzania, TFF, limethibitisha kuwa Mkutano Mkuu wao uliopangwa kufanyika Julai 13 utaendelea licha ya kuwa Siku hiyo hiyo Tanzania inacheza Mechi ya kwanza ya Mchujo ya CHAN dhidi ya Uganda Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Wadau wengi wamekuwa wakihoji kufanyika kwa Mkutano huo wakati Nchi inakabiliwa na Mechi muhimu Siku hiyo hiyo huku wengine wakidiriki kudai kuna walakini ndani yake.
Lakini Rais wa TFF, Leodegar Tenga, amefafanua kuwa vitu hivyo viwili haviwezi kuleta mgongano kwani Mechi itachezwa kwa Dakika 90 na Mkutano Mkuu umepangwa kuwa wa Siku mbili.
Tenga alisema: “Hamna njama zozote. Vitu hivyo viwili vitaendelea kama ilivyopangwa.”
Akifafanua, Tenga alisema Wajumbe wa Mkutano Mkuu wamezoea kujadili Ajenda hadi 12 katika Siku moja lakini safari hii Ajenda ni moja tu na imepangiwa Siku mbili.
Ajenda ya Mkutano Mkuu huo ni kujadili na kupitisha Mabadiliko ya Katiba ili kuruhusu Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho hilo ufanyike kama ilivyoagizwa na FIFA.
Awali Uchaguzi ulikuwa ufanyike hapo Februari 24 lakini ukatokea mgongano mkubwa baada ya baadhi ya Wagombea kufutwa na pia madai kuwa Katiba ilibadilishwa bila kufuata taratibu.
Akifafanua zaidi, Tenga alisema upo uwezekano mkubwa kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu kumaliza Kikao chao kabla hata Mechi kuchezwa.
Katika Uchaguzi wa awali Tenga hakuwa Mgombea wa nafasi yake.

Thursday, June 27, 2013

FEDERER ASEMA BADO ATAENDELEA KUCHEZA MCHEZO HUO".

Mchezaji tenesi mahiri wa Switzerland, Roger Federer amesisitiza kuwa bado ataendelea kucheza mchezo huo kwa miaka mingi ijayo pamoja na kutolewa mapema katika michuano ya Wimbledon jana. Nyota huyo ambaye anashika namba tatu katika orodha za ubora duniani amesema hana hofu yoyote pamoja na kutolewa na Sergiy Stakhovisky wa Ukraine katika mzunguko wa pili wa michuano hiyo. Katika mchezo huo Federer aliburuzwa kwa kufungwa 6-7 7-6 7-5 7-6 na Stakhovsky anayeshika namba 116 katika orodha za ubora duniani. Baadhi ya wadau wa mchezo huo wamekuwa wakihoji kiwango cha Federer mwenye umri wa miaka 31 na kudai kuwa amekwisha lakini mwenye amesisitiza kuwa bado yuko fiti na ataendelea kucheza kwa miaka kadhaa ijayo. Kwa upande wa wanawake mwanadada nyota anayeshika namba mbili kwa ubora kwa upande wanawake Maria Sharapova wa Urusi naye aliyaaga mashindano hayo baada ya kukubali kipigo cha 6-3 6-4 kutoka kwa Michelle Larcher de Brito wa Ureno anayeshika namba 131 katika orodha hizo.

SCOLARI AMEKIRI KUWA TIMUYA BRAZIL BADO HAIKO FITI-DUNIA

KOCHA wa timu ya taifa ya Brazil, Luis Felipe Scolari amekiri kuwa kikosi chake bado hakiwezi kuanza kuweka matumaini ya kutwaa kombe lao la sita la Kombe la Dunia mwaka ujao lakini wamebakisha mechi moja kunyakuwa taji lao la tatu la Kombe la Shirikisho baada ya kuiengua Uruguay katika hatua ya nusu fainali. Scolari amesema anafikiri kikosi hicho kimefikia mahali pazuri lakini bado kuna vitu vingi vya kufanyia marekebisho mpaka kikamilike kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa wanahamishia nguvu zao katika mchezo wa fainali na baada ya hapo wataangalia mapungufu yalijitokeza ili kuhakikisha wanakuwa na kikosi imara kitakachoweza kulibakisha Kombe la Dunia nyumbani. Brazil kwasasa wanasubiri mshindi wa nusu fainali nyingine ya michuano hiyo itakayopigwa baadae leo kati ya mabingwa wa Ulaya na Dunia Hispania watakaochuana na Italia.

ABEL NA KISPANG WAJITOA TIMU YA WANARIADHA WA KENYA

BINGWA mara mbili wa dunia mashindano ya mbio ndefu Abel Kirui na mshindi wa medali ya shaba katika michuano ya olimpiki Wilson Kipsang wamejitoa katika timu ya wanariadha ya Kenya itakayoshiriki michuano ya riadha ya dunia itakayofanyika jijini Moscow. Makamu wa rais wa Chama cha Riadha cha nchi hiyo Paul Mutwii amedai kuwa Kurui aliwafahamisha kwamba amejitoa kwasababu ya kusumbuliwa na majeraha wakati Kipsang yeye amewaambia kuwa ana majukumu mengine. Kirui ambaye alishinda taji la dunia la mbio ndefu mwaka 2009 na 2011 amekuwa akisumbuliwa jeraha la kifundo cha mguu wake wa kulia na anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki sita. Kuziba nafasi hizo Mutwii amesema wamewaita Mike Kipyego ambaye alishinda mbio za marathon jijini Tokyo mwaka jana, Bernard Kipyego mshindi wa medali ya fedha mbio za nusu marathon 2009 na bingwa wa mbio za marathoni za Paris Peter Some. Kikosi cha mwisho kitakachokwenda Moscow kitatajwa mwezi ujao baada ya kufanyika mbioza mchujo.

JUVESTUS YATANGAZA RASMI KUMSAJILI TEVEZ

KLABU ya Juventus ya Italia jana ilimtangaza rasmi kumsajili mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Argentina, Carlos Tevez kutoka timu ya Manchester City kwa mkataba wa miaka mitatu. Taarifa zinadai kuwa klabu yenye maskani yake katika jiji la Turin wamelipa kiasi cha paundi milioni 10 kwa nyota huyo mwenye umri wamiaka 29. Lakini Tevez atatakiwa kumaliza adhabu yake ya kutumikia jamii kwa saa 250 ili kuondoka jijini London salama na kuepuka kuburuzwa tena mahakamani. Tevez alikatisha likizo yake huko Amerika Kusini na kupanda ndege kuelekea Italia jana lakini pia atatakiwa kumaliza adhabu yake aliyopewa na mahakama ya Macclefield April mwaka huu kwa kuendesha huku akiwa amefungiwa kufanya hivyo.

Tuesday, June 25, 2013

VALCKE-ASEMA BRAZIL NDIO MAHALA PA KOMBE LA DUNIA"

KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Jerome Valcke amesema kuwa hawana mpango wa kubadili mahali patakapochezwa michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Valcke alibainisha kwamba michuano hiyo itafanyika nchini Brazil katika miji 12 kama ilivyopangwa na hakuna mpango mwingine wowote wa kuhamisha mashindano hayo kwenda sehemu nyingine. Kauli ya Valcke imekuja kufuatia maandamano ambayo yamekuwa yakiendelea nchini humo wakati huu wa michuano ya Kombe la Shirikisho wakipinga gharama kubwa za matayarisho ya Kombe la Dunia wakati wananchi wake wana hali duni katika maisha yao ya kawaida. Valcke pia alipinga kauli ya Waziri wa Michezo wa Brazil, Aldo Rebelo aliyekuwa amekaa pembeni yake katika mkutano na waandishi wa habari aliyedai kwamba kuna nchi zimeonyesha nia ya kuwa mwenyeji wa mashindano hayo kama Brazil ikijitoa. Katibu mkuu huyo amesema hajapokea ofa yoyote kutoka katika nchi yoyote duniani kutaka kuandaa michuano hiyo ya 2014 na kumuondoa hofu Rebelo ambaye alidai amesoma katika vyombo vya habari kwamba nchi za Marekani, Uingereza, Ujerumani na Japan zinamendea nafasi hiyo.

EFF-LAMTIMUA KIBARUA KATIBU MKUU WAKE""

SHIRIKISHO la Soka la Ethiopia-EFF limemtimua kibarua katibu mkuu wake baada ya kukiri kumtumia mchezaji kimakosa katika mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 hatua ambayo inaweza kuigharimu timu nchi hiyo kukatwa alama tatu. Kamati ya Utendaji ya EFF ilipiga kura za kumtimua katibu huyo aitwaye Ashenafi Ejigu lakini walipinga barua ya kujiuzulu kwa makamu wa rais wa shirikisho hilo Berhanu Kebede ambaye ndiye alikuwa akilaumiwa kutokana na mkanganyiko huo. Baadhi ya wajumbe na waandishi wa habari za michezo waliokuwepo katika mkutano huo walikuwa wakitaka uongozi mzima wa shirikisho hilo ujiuzulu kwa kile walichokiita uzembe. Rais wa EFF, Sahilu Gebremariam alikiri kuwa suala hilo ni la kizembe na wanapaswa wote kujiuzulu na kudai kuwa atafanya hivyo katika mkutano mkuu utakaofanyika Septemba mwaka huu. Akihojiwa kuhusiana na suala la kumchezasha mchezaji aliyepewa kadi mbili za njano kocha wa Ethiopia Sewnet Bishaw alijitetea kuwa anapokuwa uwanjani huwa hatumii karatasi na kalamu anachofanya yeye ni kuhakikisha timu inapata matokeo mazuri.

YANGA WAJIPNGA NA MECHI ZA KIRAFIKI

Mabingwa wa soka Tanzania Bara , Afrika Mashariki na Kati, Klabu ya Dar Young Africans watacheza mechi za kirafiki  dhidi ya Rayon Sport ya Rwanda Julai 6 na 7, mwaka huu katika sehemu ya ziara yake ya kulitembeza Kombe lake la ubingwa wa Ligi Kuu mikoa ya kanda ya Ziwa inadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL)  kupitia bia yake, Kilimanjaro Premeum Lager.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa kaimu katibu mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako , Yanga maarufu kama Kwalalumpa Malysia itaondoka Dar es Salaam Julai 5, siku mbili tu baada ya kuanza  mazoezi Uwanja wa sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam kuelekea Mwanza tayari kwa mchezo wa kwanza dhidi ya mabingwa hao wa zamani wa Afrika Mashariki na Kati, Uwanja wa CCM Kirumba, Julai 6.
Baada ya kipute hicho, Julai 7, timu hizo ambazo zimewahi kufundishwa na kocha kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Raoul Jean Pierre Shungu kwa wakati tofauti na kwa mafanikio, zitarudiana kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
“Yanga tuna mipango mingi sana, bahati mbaya tumeshindwa kwenda Sudan kutetea ubingwa wetu wa Kagame, lakini bado tuna michuano mikubwa barani Afrika, ikiwa ni heshima kwa mashabiki wetu na wanachama wanaotuunga mkono, ni nafasi yao kuliona taji letu la ligi msimu uliopita, tutapita mikoani na kushangilia pamoja”. Alisema Mwalusako. Baada ya hapo , Yanga SC wataelekea mjini Tabora, kucheza mechi nyingine na wenyeji, Rhino FC waliopanda Ligi Kuu msimu huu Julai 11, mwaka huu Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi.
Katika ziara hizo, Yanga watatembeza Kombe lao la ubingwa wa Ligi Kuu, walilolitwaa kwa mara ya 24 msimu huu kwenye mitaa mbalimbali kushangilia na mashabiki wao. 
Yanga SC, imekuwa na mafanikio makubwa tangu ianze kudhaminiwa na TBL mnamo 2008, ikitwaa jumla ya mataji sita katika kipindi hicho, yakiwemo mawili ya Kagame, 2011 na 2012 na manne ya Ligi Kuu Bara, 2008, 2009, 2011 na 2013. Agosti 2, mwaka 2011, TBL ilisaini Mkataba wa udhamini na Yanga wa miaka minne sawa na kwa watani wao pia, Simba SC.
Katika mkataba huo mpya, uliotiwa saini kwenye hoteli ya Double Tree, Masaki, Dar es Salaam, TBL iliongeza dau la fedha za mishahara kwa wachezaji kutoka Sh. Milioni 16 hadi Milioni 25 kwa mwezi, ikaongeza basi moja kubwa, Yutong lenye uwezo wa kubeba abiria 54 na fedha kwa ajili ya kugharamia mikutano ya wanachama ya kila mwaka Sh. Milioni 20 kugharamia tamasha la mwaka la klabu na vifaa vya michezo vyenye thamani ya Sh. Milioni 35 kila msimu.
Yanga pia inapewa bonasi ya Sh. Milioni 25 ikitwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara au Milioni 15, ikishika nafasi ya pili katika Mkataba huo wenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 5 tangu Agosti 8, mwaka huu hadi Julai 31, mwaka 2016.

TETESI ZA MASTAA NA KITUO CHA REDIO CHA NAPOLI MARTE-CAVANI

KITUO cha Redio cha Napoli, Marte kimetangaza kuwa dau la Pauni Milioni 49.3 limetolewa na Chelsea kwa ajili ya mshambuliaji  Edinson Cavani ambaye muda wote anampasua kichwa mmiliki wa klabu ya Chelsea Bilionea Roman Abramovich mwenye lengo la kuimarisha kikosi chake chini ya kocha Jose Mourinho.
Katika taarifa ya jana usiku, Radio Marte ilitangaza: “Tumepokea taarifa kutoka ofisini kwa vyanzo vya kuaminika kwamba, Napoli imekubaliana dili la kuiuzia Chelsea Cavani.

Kitu moto: Chelsea sasa ipo katika nafasi ya kumnasa Edinson Cavani
“Rafa Benitez pia amebariki, lakini kabla ya kutangaza rasmi, Napoli inataka kupata mshambuliaji atakayeziba pengo la Il Matador.
“Aurelio De Laurentiis”, klabu itasomba kiasi cha Euro Milioni 58, sawa na dili la Ezequiel Lavezzi kwenda PSG mwaka jana.
“Mchezaji huyo atajiingizia mshahara wa Euro Milioni 8.5 kwa msimu pamoja na haki za picha,”. Habari zimevuja kama kwamba Cavani ametangaza anataka kukutana uso kwa uso na Rais, Aurelio de Laurentiis na kuna taarifa kwamba Manchester United nayo imo kwenye mbio hizo. 
Mshambuliaji huyo wa Uruguayna baba yake awali walionyesha nia ya kutaka kwenda Real Madrid. Klabu hiyo ya Hispani iliwasiliana na Napoli, lakini sasa itabidi waipiku ofa iliyotolewa na Chelsea.
                                  Hata Man United na PSG pia zinamtaka Cavani

Monday, June 24, 2013

RAMBIRAMBI MSIBA WA MATHIAS KISSA

Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mchezaji wa zamani wa timu za Cosmopolitan na Taifa Stars, Mathias Kissa (84) kilichotokea leo alfajiri (Juni 24 mwaka huu) kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.

Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani enzi zake, Kissa akiwa na timu ya Tabora alitamba katika michuano ya Kombe la Taifa wakati huo ikiitwa Sunlight Cup. Alikuwa akicheza katika nafasi ya ulinzi.

Baadaye alijiunga na Cosmoplitan ya Dar es Salaam, na pia kuwa mchezaji wa timu ya Taifa ambapo enzi zake akiwa na wachezaji kama Yunge Mwanansali wakiiwakilisha Tanganyika na baadaye Tanzania Bara walitamba katika michuano ya Kombe la Chalenji wakati huo ikiitwa Gossage, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.

Kissa ambaye alipata tuzo ya mchezaji bora wa karne kwa upande wa Tanzania, tuzo inayotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) alikuwa ndiye mchezaji msomi kupita wote wakati akichezea timu ya Taifa akiwa amehitimu elimu ya Darasa la Kumi.

Kwa mujibu wa binti yake, Erica, marehemu ambaye pia aliwahi kuwa mjumbe wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi (stroke) alioupata miaka mitano iliyopita, na kisukari. Baadaye alipata kidonda ambacho ndicho kilichosababisha kifo chake.

Msiba uko nyumbani kwa marahemu, Masaki, Mtaa wa Ruvu karibu na Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST). Maziko yatafanyika keshokutwa, Jumatano (Juni 26 mwaka huu) kwenye makaburi ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Kisa, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na klabu ya Cosmopolitan na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Mungu aiweke roho ya marehemu Kisa mahali pema peponi. Amina

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

TYSON AFUZU MBIO ZA DUNIA BAADA YA KUTUMIA SEKUNDE 19.74

Mwanariadha nyota wa Marekani, Tyson Gay amefanikiwa kufuzu kushiriki mbio za mita 200 za duniani zitakazofanyika jijini Moscow kwa kutumia muda wa sekunde 19.74 ambao ni muda wa haraka zaidi kwa mwaka huu. Gay ambaye ni bingwa wa dunia wa mwaka 2007, sasa atachuana na mwanariadha mwenye kasi zaidi duniani kutoka Jamaica, Usain Bolt katika mbio za mita 100 na 200 kwenye mashindano ya dunia yatakayofanyika jijini Moscow, Urusi Agosti mwaka huu. Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka aliwashinda Isiah Young aliyeshika nafasi ya pili na Curtis Mitchell alishika nafasi ya tatu. Kwa upnde wa wanawake mwanadada nyota katika mbio fupi kutoka Marekani Allyson Felix alishindwa kutamba kwenye mbio za mita 200 baada kushindwa na Kimberlyn Duncan.

ARSHAVIN SASA AFIKIRIA KURUDI ALIPOTOKA KISOKA CLUB YA "ZSP"

Baada ya kuitumikia Arsenal kwa muda wa miaka mitano nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Urussi, Andrei Arshavin anategemewa kukamilisha taratibu za kurejea klabu yake ya zamani ya Zenit Saint PetersburgKlabu hiyo ndio ilimuwezesha arshavin mwenye miaka 32 akiwa kinda kabla ya Arsenal kumuona na kumyakuwa. aidha Arshavin ambaye alikaa Zenit kwa mkopo kwa muda wakati wa msimu wa pili wa 2011-2012 kwa sasa yuko huru baada kuachwa na Arsenal mwishoni mwa msimu huu. hata hivyo nyotahuyo ni moja kati ya wachezaji waliokuwemo katika kikosi cha Zenit kilichonyakuwa taji la Europa League mwaka 2008 na pia katika kikosi cha Urusi kkilichoshiriki michuano ya Ulaya 2008 kabla ya kwenda Arsenal.

SUAREZ AWEKA REKODI YA KUWA MCHEZAJI ALITUPIA MABAO MENGI NA TIMU YA TAIFA.

MSHAMBULIAJI Mahiri wa kimataifa wa Uruguay, Luis Suarez ameweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi katika timu ya taifa ya nchi hiyo baada ya kufunga mabao mawili katika mchezo wa Kombe la Shirikisho ambao waliibigiza Tahiti kwa mabao 8-1. Nyota anayekipiga katika klabu ya Liverpool ya Uingereza alifunga bao lake la 35 na 36 na kumpita mchezaji mwenzake wa nchi hiyo Diego Forlan wakati timu hiyo ilipokata tiketi ya kucheza nusu fainali dhidi ya wenyeji Brazil Jumatano huko Belo Horizonte. Mabao mengine ya Uruguay katika mchezo huo yalifungwa na Abel Hernandez aliyefunga manne huku Diego Perez na Nicolas Lodeiro wakifunga bao moja kila mmoja na kupelekea Tahiti chovu kuaga mashindano hayo na mzigo wa magoli 24 ya kufungwa. Uruguay ilitinga uwanjani bila kuwaanzisha nyota wake kama Forlan, Edinson Cavani na Suarez ambaye aliingia kipindi cha pili kwa ajili ya kuwapumzisha kwa ajili ya mchezo wa Jumatano.

FIFA YASEMA RAVSHAN AKIRI KUWAPA ITALY BAO LA PILI-KOMBE LA MABARA

SHIRIKISHO la Soka Dunia-FIFA limedai kuwa mwamuzi Ravshan Irmatov amekiri kuwapa Italia bao la pili kwa makosa wakati wa mchezo wa Kombe la Shirikisho kati ya timu hiyo na Brazil ambao ndio wenyeji hao walitoa dozi ya mabao 4-2. Mabao hayo yalitiwa kimianina Giorgio Chiellini.
aidha bao hilo lilikubaliwa ingawa mwamuzi alishapuliza filimbi kuashiria penati kwenda kwa Italia kitendo ambacho kiliwaudhi wachezaji wa Brazil na kuzonga mwamuzi juu ya uwamuzi wake huo. FIFA imesema kuwa mwamuzi huyo wa Uzbekstan baadae alikiri kufanya kosa hilo na kukiri kupuliza filimbi kuashiria penati. Lakini pamoja na kukiri kutenda kosa kwa mwamuzi huyo FIFA hawajathibitisha kama watamrudisha nyumbani au ataendelea kuchezesha mechi za nusu fainali ya michuano hiyo.

JE?UNAMFAHAMU KWA UZURI DAVID SILVA KATIKA ULIMWENGU WA SOKA TAFAKARI ZAIDI".

             DAVID SILVA
David Silva Euro 2012 vs France 01.jpg
Taarifa kuhusu yeye
Full nameDavid Josué Jiménez Silva
Date of birth8 January 1986 (age 27)
Place of birthArguineguín, Spain
Height1.70 m (5 ft 7 in)
Playing positionAttacking midfielder / Winger
Taarifa kuhusu club
Current clubManchester City
Number21
Timu za Ujana
1995–2000UD San Fernando
2000–2003Valencia
Timu za Ukubwa
Mwaka   TimuMechiGoli
2003–2004Valencia B14(1)
2004–2010Valencia119(21)
2004–2005 Eibar (mkopo)35(4)
2005–2006Celta Vigo (mkopo)34(4)
2010–Manchester City103(14)
Timu ya Taifa
2001–2002Spain U166(2)
2002–2003Spain U1720(5)
2004–2005Spain U1914(5)
2005Spain U205(4)
2004–2006Spain U219(7)
2006–Spain74(20)
David Josué Jiménez Silva alizaliwa 8 Januari 1986 Arguineguín huko Las Palmas Hispain ni mchezaji mpira mhispania ambaye kwa sasa anachezea timu ya Man city na timu ya taifa ya Uhispania.Silva ana uwezo wa kucheza upande wowote au kama namba 10  na wakati mwingine kama mshambulizi msaidizi.Ni mchezaji mwenye mwili mdogo, na mara nyingi hulinganishwa na Aimar Pablo, alipochukua nafasi yake huko Valencia, akivalia nambari iliyohusishwa sana na Aimar; namba 21.
WASIFU WA KLABU
Silva alianza kucheza mpira wa kulipwa msimu wa 2004-05 katika Ngazi ya pili katika timu ya SD Eibar, akiwa amekopwa kutoka Valencia CF na alicheza mechi 35 katika daraja hilimna kufunga mabao matano.Msimu uliofuatia, alikopwa tena, lakini wakati huu alikopwa na timu ya Celta de Vigo, ambapo alicheza mechi 34, na kufunga mabao manne. 
Baada ya kucheza mechi mbili ambazo aliingia uwanjani katika dakika za mwisho za mechi hizo, ambapo mechi ya kwanza iliisha kwa Celta de Vigo kushinda 2-0 nyumbani dhidi ya Malaga CF tarehe 28 Agosti 2005.
Silva akamaalizia msimu huo kama mshambulizi bora huku timu hii ya Kigalisia ikifuzu katika kombe la UEFA moja kwa moja kutoka daraja la pili.Katika misimu miwili, alikosa kucheza mechi sita tu ilhali alifunga mabao 14 (bao la kwanza alilifunga tarehe 5 Novemba 2006 katika tasa ya 1-1 ugenini RCD Espanyol). Baada ya kutocheza kwa muda wa miezi mitatu kutokana na jeraha la kisigino ambapo alifanyiwa upasuaji,
Silva alirejea kikosini katikati mwa Desemba.Silva aliwakilishwa Uhispania akiwa na Cesc Fabregas mara ya kwanza mwaka wa 2003 katika michezo ya ubingwa duniani ya FIFA ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17 huko Finland, ambapo alifunga mabao matatu.
Mwaka wa 2006, alijiunga na timu ya Uhispania ya wachezaji wasiozidi umri wa 21 na alifunga mabao manne katika kombe la vijana duniani la FIFA mwaka 2005; hii ilimwezesha kunyakua nafasi ya 4 katika orodha ya wafungaji bora, pamoja na mshambulizi mwitaliano Graziano Pellè.
WASIFU WA TIMU YA TAIFA
Silva alichezea mara ya kwanza timu kuu ya Uhispania tarehe 15 Novemba 2006 katika mechi ya kirafiki dhidi ya Romania ambapo timu yake ilishindwa 1-0 nyumbani. Aliendelea kutajwa katika orodha ya timu ya Uhispania baada ya kuchangia vizuri katika mechi zake za kwanza.
Tarehe 22 Agosti 2007, Silva aliifungia Uhispania mabao yake ya kwanza kikosini mwa Uhispania, na alifunga mara mbili katika mechi hiyo ambapo waliishinda Ugiriki 3-2 katika mechi ya kirafiki.
Baadaye aliitwa ajiunge na kikosi cha wachezaji 23 ambao wangeiwakilisha nchi yao katika dimba la Euro 2008.
Katika nusu fainali Silva alifunga bao la tatu la Uhispania dhidi ya Urusi baada ya ushambulizi wa haraka ambayo Cesc Fabregas alimpigia krosi Silva, ambaye alitia mpira ndani ya lango la Igor Akinfeev kwa kutumia mguu wake wa kushoto.
Katika fainali, Silva alihusika katika tukio fulani na mjerumani Lukas Podolski. Baada ya kumvuta Podolski chini, Podolski alimwenedea Silva na kuzua ubishi mkali ambao haukuadhibiwa na mwamuzi.
Muda mfupi baadaye, kocha wa timu ya Uhispania, Luis Aragonés, alimwondoa Silva na kuleta Santi Cazorla ili kuzuia wezekano la vita.