Sunday, November 30, 2014

BENO NJOVU AWASHUKURU WANACHAMA WA CLUB YA YANGA

Katibu Mkuu wa Yanga Beno Njovu ambaye anamalizia muda wake kuitumikia Timu ya yabga amesema anawashukuru wanachama na mashabiki wa klabu hiyo.

Njovu amesema anawashukuru kwa ushirikiano wao kwa kipindi chote alichokuwa Jangwani.

Njovu amesema yanga ni klabu kubwa, changamoto ni nyingi sana. Lakini nawashukuru wanachama na mashabiki kwa ushirikiano wao.

Hata hivyo amesema ataendelea kuwa mwanachama wa Yanga tena mwaminifu. Nimejifunza mengi, lakini sasa ni wakati wa kukabili changamoto nyingine.

Njovu amekuwa mmoja wa makatibu wa Yanga waliofanya vizuri katika kipindi wakiwa madarakani.

Ameamua kutoongeza mkataba baada ya ule aliokuwa nao kwisha muda wake.

Friday, November 28, 2014

TFF YAKIRI KUFANYA MAKOSA KURUHUSU KUFUNGULIWA DIRISHA DOGO LA USAJILI.


Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limekiri kufanya makosa kuruhusu kufunguliwa kwa dirisha dogo la usajili kabla ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL).

VPL ilisimama kwa wiki saba Novemba 9 baada ya kuchezwa kwa mechi 49 za raundi ya kwanza hadi ya saba kupisha usajili wa dirisha dogo, mashindano ya Kombe la Uhai yanayoshirikisha Timu B za klabu za Ligi Kuu na michuano ya Kombe la Chalenji.
TFF ilifungua dirisha dogo la usajili Novemba 15 na litafungwa Desemba 15 huku mechi za raundi ya nane hadi ya 13 ya mzunguko wa kwanza wa VPL bado hazijachezwa, hivyo kutoa mwanya kwa baadhi ya wachezaji watakaozihama timu zao kipindi hiki cha usajili kucheza mechi tatu dhidi ya timu moja.


Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa amekiri shirikisho hilo kujisahau katika suala hilo lakini akasisitiza kuwa hakuna tatizo kubwa mchezaji kucheza mechi tatu dhidi ya timu moja.
Mwesigwa amesema haijawahi kutokea hapa kwetu (Tanzania), tumejifunza kitu lakini mchezaji kucheza mechi tatu dhidi ya timu moja VPL haina tatizo, tatizo kubwa ni mchezaji kusajiliwa na zaidi ya timu mbili msimu mmoja. Hili linakatazwa kikanuni.

Kiungo mkongwe wa Simba Amri Kiemba amejiunga na Azam FC kwa mkopo huku klabu hiyo ya Msimbazi ikiwabana wanalambalamba wasimtumie katika mechi zinazozikutanisha timu hizo mbili msimu huu.
TFF kupitia kwa Mkurugenzi wake wa Mshindano, Boniface Wambura imepinga vikali uamuzi huo wa Simba kwa kuwa kanuni zinamruhusu mchezaji huyo kukipiga dhidi ya timu iliyomtoa kwa mkopo kwenda timu nyingine, hata hivyo.
Mchezaji wa Ndanda FC aliyecheza dhidi ya Azam FC msimu huu, akisajiliwa Simba atacheza dhidi ya Azam mara tatu katika mechi za msimu mmoja wa ligi kuu, ikiwa ni mfano wa kilichokosewa na TFF kuruhusu dirisha dogo la usajili msimu huu lifunguliwe ilhali mechi za mzunguko wa kwanza bado hazijakamilika.

CECAFA YASEMA BADO WANAHANGAIKIA MICHUANO YA CHALLENGE CUP KUFANYIKA

BARAZA la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), limesema bado linahangaikia kufanyika kwa michuano ya Kombe la Challenge mwaka huu.

Meneja wa Vyombo vya Habari wa CECAFA, Rogers Mulindwa amesema leo kwamba,  michuano ya Challenge ambayo awali ilikuwa ifanyike Ethiopia, lakini ikajivua uenyeji, bado ipo kwenye uwezekano wa kufanyika.Kamati Kuu ya CECAFA chini ya Mwenyekiti, Mhandisi Leodgar Tenga na Katibu Mkuu, Nicholas Musonye bado inafanyia kazi uwezekano wa kuhakikisha michuano hiyo inafanyika mwaka huu,” amesema Mulindwa.
Mganda huyo amesema kwamba  CECAFA baadaye itatoa taarifa rasmi juu ya mustakabali wa mashindano ambayo hufanyika mwishoni mwa Novemba hadi mwanzoni mwa Desemba.
Nchi wanachama wa CECAFA ni Sudan, Ethiopia, Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda, Burundi, Somalia, Eritrea, Djibouti, Zanzibar na Sudan Kusini.

KLOPP KOCHA WA DORTMUND ASEMA MASHABIKI WA ARSENAL KUWA KIPIGO CHA 2-0 CHA UEFA HAWAWEZI KUPATA KAZI

MENEJA wa klabu ya Brussia Dortmund, Jurgen Klopp ametania kuwa mashabiki wa Arsenal hawatamuhitaji tena baada ya kuona timu yake ikitandikwa mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya juzi.
Klopp amekuwa akihusishwa na tetesi za kuchukua mikoba ya kionoa Arsenal katika wiki kadhaa zilizopita baada ya kuzuka msukumo kwa Arsene Wenger kufuatia kuanza vibaya msimu wa Ligi Kuu. 
Kocha huyo amekiri hivi karibuni kuwa anadhani anaweza kumudu kuhamia katika Ligi Kuu kama akiamua kuondoka Dortmund lakini sasa anadhani nafasi yake ya kutua Arsenal imetoweka. 

Akihojiwa Klopp amesema hafikirii baada ya kiwango cha Dortmund walichokionyesha katika Uwanja wa Emirates kama mashabiki wa Arsenal watamuhitaji. 
Klopp aliteuliwa kuwa kocha wa Dortmund kuanzia mwaka 2008 na kuisaidia timu hiyo kushinda mataji mawili ya Bundesliga, Kombe la Ujerumani, Supercup na kutinga fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. 

ROY KEANE AJIUZULU WADHIFA WAKE ASTON VILLA WA KOCHA MSAIDIZI.


KLABU ya Aston Villa imetangaza kuwa Roy Keane amejiuzulu wadhifa wake wa kocha msaidizi wa timu hiyo. 
Mapema Keane alikaririwa akidai kuwa anapata tabu kuhudumia vibarua viwili alivyokuwa navyo. 
Keane ambaye pia ni kocha msaidizi wa Ireland amesema sio haki kwa pande zote mbili, hivyo anatakiwa kufanya uamuzi wa kuchagua kibarua kimoja. 
Kocha wa Villa Paul Lambert alithibitisha asubuhi ya leo kuwa taarifa hizo na kudai kuwa ana heshimu uamuzi uliochukuliwa.


GALATASARAY BAADA YA KUNTUPIA PRANDELLI SASA YAMCHUKUA HAMZAOGLU KUZIBA NAFASI.

KLABU kongwe jijini Instabul ya Galatasaray wanatarajia kumteua kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Uturuki Hamza Hamzaoglu kuwa meneja mpya wa klabu hiyo baada ya kutimuliwa kwa Muitaliano Cesare Prandelli. 
Klabu hiyo ilimtimua Prandelli baada ya kuitumikia chini ya nusu ya msimu kutokana na matokeo mabovu ambayo wamekuwa wakipata. 
Hamzaoglu amekuwa akiitumikia Uturuki chini ya kocha mkuu Fatih Terim toka mwaka 2013, na uamuzi wake huo umekuja baada ya kufanya mazungumzo na kocha huyo. 
Bodi ya klabu hiyo ilifikia uamuzi wa kumtimua Prandelli baada ya kutandikwa na Anderlecht kwa mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumatano usiku na kufuta matumaini yao ya kufuzu hatua ya mtoano. 
Prandelli alitua katika klabu hiyo Julai mwaka huu akichukua nafasi ya Muitaliano mwenzake Roberto Mancini na kupewa mkataba wa miaka miwili uliokuwa na thamani ya euro milioni 2.3.

DR SHEIN ASEMA KATIKA KUKUZA MPANGO WA UCHUMI NA KUONDOA UMASKINI ZANZIBAR SECTA YA UTALII NDIO SECTA YAKUUNGWA MKONO.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dokta, Ali Mohamed Shein amesema kuwa katika Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini Zanzibar (MKUZA), sekta ya utalii ndio sekta mama na nyegine zimekuwa zikiongeza nguvu hivyo inahitaji kuendelea kuungwa mkono ndani na nje ya nchi.
Dokta, Shein ameyasema hayo wakati alipofanya mazungumzo na Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada Jack Mugendi Zoka,  Ikulu mjini Zanzibar aliyefika kwa ajili ya kuaga kwenda katika kituo chake kipya cha kazi nchini humo  kufuatia uteuzi wa Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete hivi karibuni.
Katika maelezo yake Dokta Shein amemueleza Balozi huyo mpya wa Tanzania nchini Cadana kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imekuwa ikifanyaa juhudi za makusudi katika kuhakikisha sekta ya utalii inaimarika na inaendelea kuwa sekta mama na muhimu hapa nchini.
Akieleza juu ya sekta ya uwekezaji Dokta, Shein amemueleza Balozi Zoka kuwa mbali ya kutilia mkazo uwekezaji katika ujenzi wa mahoteli pia, Serikali imekuwa ikitilia mkazo uwekezaji katika Hospitali za kisasa za binafsi ambazo zinatibu maradhi maalum.

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU IMESEMA ITAENDELEA KUWAPATIA WANANCHI TAKWIMU SAHIHI ZINAZOHUSU SEKTA MBALIMBALI.

SERIKALI kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu imesema kuwa itaendelea kuwapatia wananchi takwimu sahihi zinazohusu sekta mbalimbali ili kuwajengea uwezo wa kushiriki katika ngazi za maamuzi na masuala mbalimbali nchini.
Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es salaam na Waziri wa Fedha wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  Omar Yussuf  Mzee wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yanaoongozwa na kauli mbiu isemayo Takwimu Huria kwa uwajibikaji na ushirikishwaji wa wadau wote.
Amesema upatikanaji wa taarifa na  takwimu sahihi kwa wananchi unaongeza ushiriki wao katika maamuzi na kuwajengea uwezo wa kutathmini utendaji wa Serikali katika masuala mbalimbali yakiwemo mapato na matumizi.
Amesema Ofisi ya Taifa ya Takwimu itaendelea kuhakikisha kuwa takwimu mbalimbali zinapatikana kwa urahisi kupitia mtandao, machapisho na mifumo rahisi ili kuwawezesha wananchi na wadau mbalimbali kuzipata pindi wanapozihitaji.

Thursday, November 27, 2014

FIFA YATOA LISTI YA UBORA DUNIANI TANZANIA YAPOROMOKA NAFASI 2 SAS YA 112.

SHIRIKISHO la soka Duniani FIFA Leo hii imetoa Listi ya Ubora Duniani na Mabingwa wa Dunia Germany wameendelea kushika Namba Moja huku Tanzania ikiporomoka Nafasi 2 na kukamata Nafasi ya 112.
Kulikuwa hamna mabadiliko yeyote ya Timu 7 za juu lakini England, iliyokuwa Nafasi ya 20, imepanda Nafasi 7 na sasa kukamata Nafasi ya 13.
Barani Afrika, Ageria imeendelea kuwa juu kabisa ikiwa Nafasi ya 18 baada kushuka Nafasi 3 ambapo Listi ya Ubora Duniani inayofuata itatolewa Tarehe 18 Desemba 2014.
20 BORA HII HAPA.
1.Germany               
2.Argentina   
3.Colombia    
4.Belgium      
5.Netherlands
6.Brazil
7.Portugal               
8.France
9.Spain          
10.Uruguay                
11.Italy           
12.Switzerland 
13.England                
14.Chile           
15.Romania                
16.Costa Rica  
17.Czech Republic      
18.Algeria       
19.Croatia       
20.Mexico

UONGOZI WA LIPULU FC YATUPIA VIRAGO BENCHI LA UFUNDI


Timu ya Lipuli FC ya Iringa kupitia uongozi wake umeamua kutitupilia virago benchi lake lote la ufundi kutokana na matokeo yasiyoridhisha ya timu yake katika Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
          
Mwenyekiti wa timu hiyo Abuu Changawa amesema wamefikia hatua hiyo baada ya timu yao kuwa na mwendo wa konokono katika ligi hiyo wakiwa nafasi ya tatu katika msimamo wa Kundi A.

Pamoja na kwamba wapo katika nafasi ya tatu kwenye         msimamo wa kundi letu, matokeo ya timu yetu hayaridhishi. Tumekuwa tukishinda 1-0 na kutoka sare ndiyo maana tumeaona tuachane na watendaji wote wa benchi la ufundi,” amesema Majeki.

Lipuli FC, aliyowahi kuifundisha Shadrack Nsajigwa (sasa kocha msaidizi Yanga), imekusanya pointi 21 katika mechi zote 11 za raundi ya kwanza ya FDL, pointi moja nyuma ya Friends Rangers walioko nafasi ya pili na tatu nyuma ya Majimaji FC wanaoshika usukani wa kundi hilo.

Aidha, Majeki amesema kuanzia Alhamisi wataanza msako wa kukamata watu wote wanaojihusisha na biashara haramu ya kutengeneza na kuuza jezi zenye nembo ya klabu yao kwa kuwa hadi sasa hakuna kampuni wala mtu aliyeidhinishwa kutengeneza na kuuza jezi zenye 

EMERSON AANZA TIZI LA KUJIUNGA NA YANGA CHINI YA MAXIMO.

Mbrazil, Emerson Roque ambae anacheza nafasi ya Kiungo leo ameanza kujifua katika kikosi cha Yanga.

Taarifa zilizopo Emerson atafanya majaribio kwa wiki mbili, ambapo leo imekuwa siku ya kwanza.
                 
Katika mazoezi hayo ya Yanga kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam kulikuwa na ulinzi mkali.

Emerson ambaye inaelezwa atachukua nafasi ya mshambuliaji, Jaja alionekana kama vile amezoeana na wachezaji wengine wa Yanga.


Pamoja naye, kiungo Coutinho na Kocha Marcio Maximo, nao walianza mazoezi yao kwa mara ya kwanza baada ya kurejea nchini, jana.

Wednesday, November 26, 2014

BARCA,MADRID,BAYERN YATAWALA ORODHA YA MABEKI FIFPRO WORD XI 2014


KLABU za Barcelona, Real Madrid na Bayern Munich zimetawala orodha ya mabeki wateule katika kikosi cha dunia cha FIFPro World XI 2014 chama cha wachezaji wakulipwa, baada majina 12 ya wachezaji wao kuingia katika orodha kati ya majina 20 yaliyoteuliwa.
Wachezaji wote wanne walioshinda nafasi ya kuwemo katika kikosi hicho mwaka jana wamejumuishwa wakiwemo Dani Alves, Philipp Lahm, Sergio Ramos na Thiago Silva. Leighton Baines, Ashley Cole, Dante na Nemanja Vidic ndio ambayo hayamo katika orodha hiyo ukilinganisha na ya mwaka jana. 
Kwa upande wa Madrid wamo Dani Carvajal, Pepe, Ramos, Raphael Varane na Marcelo wakati Barcelona wamo Jordi Alba, Alves, Javier Marscherano na Gerard Pique huku Bayern wakiwa na David Alaba, Lahm na Jerome Boateng. 
Mabeki wengine wnakamilisha orodha hiyo ni pamoja na David Luiz na Thiago Silva wa Paris Saint-Germain, Pablo Zabaleta na Vincent Kompany wa Manchester City, Branislav Ivanovic na Filipe Luis wa Chelsea, Diego Godin wa Atletico Madrid na Mats Hummels wa Borussia Dortmund. 
Majina manne ya washindi wa beki bora wa dunia yataamuliwa kwa kupiga kura miongoni mwa wachezaji ambapo zaidi ya wachezaji wa kulipwa 20,000 wanatarajiwa kushiriki zoezi hilo.

CAF YAZINDUA MPIRA AINA YA MARHABA KUTOKA ADIDAS KWA AJILI YA AFCON 2015


SHIRIKISHO la Soka la Afrika-CAF na kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas wametoa mpira wa Marhaba kuwa maalumu kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon itakayofanyika huko Guinea ya Ikweta mwakani.
Mpira huo unatarajiwa kutambulishwa rasmi Desemba 3 mwaka huu katika shughuli za upangaji ratiba za michuano hiyo ambazo zitakazofanyika jijini Malabo. 
Mpira huo umebuniwa kwa rangi za aina mbalimbali ambazo zinawakilisha uwanda mpana wa bara la Afrika kuanzia jangwa la sahara, rangi ya ang’avu ya samawati katika anga la bahari ya Hindi na Atlantic. 
Mpira huo wa Marhaba umefanyiwa vipimo vyote stahiki na kuthibitishwa kuwa unaweza kutumika katika hali yeyote katika michuano hiyo.


SERIKALI YATOA SH. BILIONI 5 KIANZIO UJENZI WA JENGO LA MAABARA YA UPASUAJI.

JUMLA  ya shilingi  bilioni tano  zimetolewa  na serikali  kama kianzio cha ujenzi wa jengo la upasuaji  ujenzi wa maabara pamoja na kununua dawa katika hospitali teule ya rufaa  ya Tumbi mkoani Pwani.
Kauli hiyo ya serikali imetolewa na naibu waziri ofisi ya waziri mkuu Aggrey Mwanri mjini Dodoma katika kipindi cha maswali na majibu ambapo amekiri kuwa miundombinu ya hospitali hiyo haiendani na mahitaji yaliyopo.

Amesema kuwa ili kukabiliana na hali hiyo serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufanya upanuzi wa hospitali hiyo, ambapo inakadiriwa shilingi bilioni 30 zilitumika kwa ajili ya shughuli za ujenzi huo kwa mwaka 2010.

ASKARI POLISI WILAYA CHUNYA ATIWA NGUVUNI KWA TUHUMA ZA MAUAJI.

ASKARI polisi wa kitengo cha usalama barabarani Wilayani Chunya Mkoani Mbeya, PC  Zeferin Didas Focas mwenye umri wa miaka (34) amefukuzwa kazi kwa tuhuma za kuhusika na mauji ya raia Abisai Wadi mwenye miaka 22.
Kamanda wa polisi Mkoani Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kufukwa kazi kwa askari huyo baada ya husika na mauji ya raia huyo yaliyotokea  katika Kata ya Igalula barabara ya Itindi Mkwajuni  Wilayani Chunya Mkoani Mbeya.
Amesema,  askari huyo akiwa na mwezie aliisimamisha pikipiki iliyokuwa imempakia abiria nyuma ambapo dereva huyo alikaidi, ndipo askari huyo alichukua jiwe na kuitupia pikipiki hiyo iliyokuwa katika mwendo kasi  na kumpata abiria huyo.
Amesema, jiwe hilo linasemekana lilimkuta abiria aliyepakizwa kwenye poikipiki hiyo lakini haikuwekwa wazi kwamba jiwe hilo lilimpata katika sehemu ipi ya mwili wa marehemu huyo.

Amesema, askari huyo ambaye kwa sasa anatambulika kwa namba ya X6710 anatarajiwa kufikishwa mahakamani  ili kujibu tuhuma za mauji zinazomkabili mbele yake.

Tuesday, November 25, 2014

MWAMBUSI AREJEA MBEYA CITY KUITIA MAKALI KWA LIGI KUU DEC 26

DSC_0051Klabu ya Mbeya City Council Football Club leo 25/11/2014 inatoa ufafanuzi wa mbalimbali ikiwemo suala la utaratibu wa maslahi kwa watumishi wake (benchi la ufundi, wachezaji na watumishi wengine) na uwepo wa fedha za wadhamini katika klabu yetu.
Uamuzi wa kutoa taarifa hii umefikiwa baada ya vikao vya menejimenti na kamati ya fedha na utawala kufuatia taarifa mbalimbali zinazozalishwa kila siku juu ya klabu yetu toka katika vyanzo ambavyo sio vya klabu.
slide3MASLAHI YA WACHEZAJI
Hivi karibuni baadhi ya wadau wa mchezo wa mpira wa miguu wamehusisha matokeo ya uwanjani iliyopata timu na maslahi kwa wafanyakazi wa klabu kama taasisi.
Sehemu kubwa ya wafanyakazi wa klabu ikijumuisha timu ni wafanyakazi chini ya masharti ya mkataba chini ya muajili ambaye ni Halmashauri ya jiji la Mbeya, Hivyo maslahi ya mfanyakazi(kwa kada hii) hujadiliwa na kukubaliana kwa pande zote mbili(Klabu kwa niaba ya muajiri na Mchezaji kama muajiriwa) kulingana na bei ya soko ndipo mkataba husainiwa.
Klabu imeweka utaratibu wa namna ya wafanyakazi wake kujadiliana na mwajili kuhusu mambo mbali mbali yenye lengo la kuboresha utendaji wa kazi na mazao yake pamoja na masuala ya maslahi pindi kukiwa na haja hiyo.
DSC_0058Mishahara ya wachezaji pamoja na kuamuliwa kwa makubaliano baada ya majadiliano ya pande zote mbili bei ya soko huangaliwa na kuzingatiwa. Msimu wa 2014/2015 mishahara ya wachezaji ilipanda kati ya asilimia 100 – 300(%) ikilinganishwa na msimu uliopita 2013/2014.
Posho zote zitolewazo na klabu zilirekebishwa ikilinganishwa na msimu uliopita kwa kuzingatia makubaliano kati ya wachezaji na menejimenti kabla ya kuanza kwa msimu huu.
Klabu inatambua wazi kuwa mpira ni ajira kama zilivyo ajira zingine,maslahi haya yamewekwa kwa makusudi ili kuboresha hali za maisha za wafanyakazi wetu hasa wachezaji kwani hiyo ndiyo ajira yao.
Ukiondoa mshahara unaoendelea kulipwa kila mwezi hakuna mfanyakazi yeyote anayedai chochote kati ya maslahi yake.

FEDHA ZA WADHAMINI:
Pamoja na kuwa na kipengele cha kutotoa siri (Confidentiality)za mikataba yetu na wadhamini wetu, klabu inasikitishwa namna ambavyo umma wa wanamichezo unavyopotoshwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa changamoto ambazo klabu inapitia hivi sasa kama taasisi zinatokana na kuwepo kwa fedha za wadhamini.
???????????????????????????????Klabu inaomba ikumbukwe kuwa katika msimu uliopita 2013/2014 ilitumia zaidi ya shilingi milioni 700 kutoka katika vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmashauri ikiwa kama mmiliki wa klabu. Wadhamini kwa mujibu wa makubaliano hawajatoa wala hawatoi fedha zote mara moja kwa mujibu wa mkataba, fedha hizo hutolewa kila mwezi na kwa awamu.
Matumizi ya kawaida ya klabu kwa mwezi si chini ya shilingi 49,000,000.00(bila kuhusisha mishahara), katika kipindi cha Julai-Sept 2014, Klabu ilikuwa na mdhamini mmoja tu ambaye ni Binslum tyres Co Ltd anayetoa shilingi 15,000,000.00 kwa mwezi sawa na shilingi 180,000,000.00 kwa mwaka kwa mujibu wa mkataba uliopo.
Ukiangalia mahitaji ya klabu kwa mwezi mmoja hapo juu, fedha hizi za mdhamini zilichangia asilimia 30.6(%) ya gharama za klabu kwa mwezi. Hii ikiwa na maana kuwa bado asilimia 69.4(%) ya gharama za uendeshaji wa timu zilitoka Halmashauri.
Kuanzia mwezi oktoba 2014 ambapo kampuni ya coca cola ilisaini mkataba wa udhamini na klabu yetu. Kampuni ya Coca Cola itakuwa inatoa fedha taslimu Tsh 60 milioni ambazo inazitoa kwa mwaka. Fedha hizi hutolewa kila baada ya robo mwaka shilingi milioni 15. Hii ina maana kuwa coca cola inatoa shilingi 5,000,000.00 milioni kila mwezi.
Hivyo kuanzia mwezi oktoba klabu inapata toka kwa wadhamini wake wawili (Binslum Tyre Co Ltd na Coca Cola Kwanza) shilingi 20,000,000.00 kwa mwezi. Fedha hizi zinachangia asilimia 40.8(%) ya gharama za uendeshaji wa timu kwa mwezi na asilimia 59.2(%) ya gharama hizo bado zinabebwa na Halmashauri.
Uwepo wa wadhamini hivi sasa haujaongeza fedha kutoka katika bajeti hiyo bali umepunguza utegemezi wa timu kwa Halmashauri.
Hivyo basi shutuma zinazotolewa na baadhi ya wadau kuwa changamoto ambazo timu inazipitia kwa sasa ni kutokana na kuwepo kwa fedha za wadhamini ni UPOTOSHAJI MKUBWA.

MWALIMU JUMA MWAMBUSI
Mwalimu Juma Mwambusi ni muajiriwa wa Halmashauri ya jiji la Mbeya anayesimamia benchi la ufundi la timu yetu.Menejiment ilikutana na Mwl Juma Mwambusi katika vikao vyake vya kawaida kupitia changamoto kadhaa zilizojitokeza katika michezo saba ya awali mara baada ya kuwasilisha ripoti ya maendeleo ya timu. Mwalimu Mwambusi na menejiment tumeridhiana kwa faida ya mpira wa miguu na jamii inayoizunguka timu yetu anaendelea kuifundisha timu ya Mbeya City Fc.
slide3Nachukua nafasi hii kuujulisha umma kuwa Mwl.Juma Mwambusi ndiye Kocha Mkuu wa timu na hivi sasa anandaa program ya mafunzo kwa mzunguko wa pili wa ligi unaotarajia kuanza disemba 2014.
MWISHO
Klabu kama taasisi inayokuwa inapitia katika changamoto mbalimbali, ni imani ya menejimenti kuwa changamoto hizi zitaiimarisha na kuikomaza klabu ili kuwa klabu bora zaidi kwa vizazi vijavyo.
Tunatoa shukrani za dhati kwa wadau wetu wote wanaoendelea kutuunga mkono katika kipindi hiki.
Imetolewa na
E.E.Kimbe
KATIBU MKUU
MCC FC

STAND UNITED YATUA JANGWANI KUWAFUATA BAHANUZI,SEME.


UONGOZI wa Stand United ya shinynga inmayoshiririki kwa mara ya kwanza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu, umesafiri kutoka usukumani mjini Shinyanga hadi maeneo ya Jangwani jijini Dar es salaam kuzungumza na uongozi wa Yanga SC ili uwasajili Said Bahanunzi, Omega Seme na Hamis Thabit kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Stand United, Muhibu Kanu akizungumza na mkali wa dimba kupitia mtandao huu kwa njia ya simu amesema kuwa wameamua kufika jijini dar kuuona uongozi wa Yanga SC ili aruhusiwe kuwanasa wachezaji hao kuimarisha kikosi chao kilichop[o nfasi ya 10 katika msimamo wa VPL kikiwa na pointi tisa sawa na Mgambo walioko nafasi ya tisa, Polisi Morogoro (8) na Simba (7).

TFF YAWAPA FURSA TFF YAWAPA FURSA WATANZANIA WAIPIGIE KURA JEZI YA STARS

 watanzania wanatakiwa kupigia kura jezi ya timu ya Taifa ya nyumbani na ugenini kupitia mtandao wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wawww.tff.or.tz ambapo jezi hizo zimewekwa.



TFF ilipokea mapendekezo ya mwonekano mpya wa jezi ya timu ya Taifa kutoka kwa Watanzania 86. Jezi 11 za nyumbani, bukta nane za nyumbani, jezi nane za ugenini na bukta tano za ugenini ndizo zimepitishwa kwa ajili ya kupigiwa kura.

Mwisho wa kupiga kura ni Desemba 31 mwaka huu. Mpigaji kura anatakiwa kubonyeza kwenye jezi na bukta ambayo ameichagua. Anatakiwa kufanya hivyo kwa jezi ya nyumbani na jezi ya ugenini.


Tunawashukuru wote waliojitokeza kupendekeza mwonekano mpya wa jezi ya timu ya Taifa.

Sunday, November 23, 2014

WENGER ALAUMU SAFU YAKE YA ULINZI DHIDI YA MAN UNITED.

Kocha wa Arsenal Arsene wenger amesema kuwa safu ya ulinzi ya Arsenal ni hafifu baada ya kushindwa 2-1 na Manchester United katika uwanja wa Emirates.
Arsenal walipatikana wakiwa wazi katika safu ya nyuma walipojaribu kutafuta bao la kukomboa baada ya Kieran Gibs kujifunga.
Wenger amesema kuwa kwa sasa safu hiyo ya ulinzi haina uzoefu wa kutosha kuweza kusoma mechi.
Katika mechi hiyo Arsenal walifanya mashambulizi 23 katika lango la Manchester United.
Wenger amesema Mwisho wa mechi hatukuwa imara katika safu ya Ulinzi na tulifanya makosa ambayo walichukua fursa na kutuadhibu.

NFA YA ZAMBIA YAMNYEMEREA PHIRI KUIONOA TIMU YA TAIFA


Shirikisho la Soka la Namibia (NFA), limeendelea kuonyesha nia ya kumpata Kocha Patrick Phiri kukinoa kikosi chake cha timu ya taifa.
Mmoja wa mtandao wa michezo wa Namibia umeandika kuwa NFA imefanya mazungumzo na Phiri kumshawishi ajiunge na kuchukua nafasi ya kocha wa sasa.
Kwa sasa, Namibia inanolewa na nyota wake wa zamani, Ricarco Manetti ambaye aliwahi kung’ara na Santos ya Afrika Kusini.
Akizungumzia hilo Phili kutoka Lusaka Zambia amekiri kwa mara nyingi kuwa aliwahi kuzungumza na uongozi wa NFA lakini si hivi karibuni.
Phiri yuko mapumzikoni kwao nchini Zambia, anatarajiwa kurejea nchini siku chache zijazo kiuendelea na kazi.

RONALDO NAE YU MBIONI KUVUNJA REKODI LA LIGA"MESSI SAFI

WAKATI Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi Jana akivunja Rekodi na kuwa Mfungaji Bora katika Historia ya La Liga, Cristiano Ronaldo yuko mbioni kuivunja Rekodi ya kufunga Bao nyingi katika Msimu mmoja wa Ligi hiyo ambayo inashikiliwa na Messi.
Messi aliweka Rekodi ya Bao nyingi katika Msimu mmoja kwenye Msimu wa 2011/12 alipofunga Bao 50.
Lakini Jana Ronaldo alifunga Bao 2 wakati Timu yake Real Madrid inaichapa Eibar Bao 4-0 na sasa amefikisha Bao 20 katika Mechi 11 za La Liga Msimu huu kwa jinsi mwendo wake wa kufunga Mabao ulivyo Msimu huu Wachambuzi wanahisi Ronaldo, ambae ni Mchezaji Bora Duniani, anao uwezo wa kufunga zaidi ya Mabao 60 kwa Msimu huu.
Tayari Ronaldo, mwenye Miaka 29, ameweka Rekodi ya kuwa Mchezaji wa kwanza katika Historia ya La Liga kufikisha Bao 20 katika Raundi 12 za mwanzo za Ligi za Msimu huu.
Tangu ajiunge na Real kutoka Manchester United Mwaka 2009, Ronaldo amefunga Mabao 197 kwa Mechi 176 za La Liga na Messi Mabao 253 katika Mechi 289 kuanzia 2004 ambayo ndio hiyo Rekodi ya kuwa Mfungaji Bora katika Historia ya La Liga.
Lakini pia vita hii ya Rekodi za Magoli kati ya Ronaldo na Messi zitaendelea tena kati Wiki wakati Real na Barcelona zitakapojikita kwenye Mechi za 5 za Makundi yao ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL.
Kwenye UCL, Messi amefunga Bao 71 sawa na Mchezaji wa zamani wa Real, Raul, na wao ndio wanaongoza Kihistoria katika Ufungaji Bora kwa Ulaya lakini Ronaldo akiwa na Bao 70 yuko nyuma kwa Bao 1.
Jumanne Barcelona wako Ugenini huko Cyprus kucheza na Apoel Nicosia na Jumatano Real nao wako Ugenini kucheza huko Uswisi na FC Basel.

LIVERPOOL HOI VIPIGO MFULULIZO WAKAA 3-1 KWA C"PALACE

Majogoo wa Jiji la Landon Liverpool wakiwa katika dimba la Ugenini huko Selhurst Park Jijini London waliongoza baada ya Sekunde 90 tu Bao la Rickie Lambert lakini walijikuta wakiambulia kipigo cha Bao 3-1 na Crystal Palace katika Mechi ya Ligi Kuu England.
Palace walisawazisha Bao katika Dakika ya 17 kwa Bao la Dwight Gayle alienasa Shuti la Yannick Bolasie lililopiga Posti na kumrudia.
Kipindi cha Pili Dakika ya 78 Joe Ledley aliwapeleka Palace mbele 2-1 na kisha Dakika 3 baadae Frikiki ya Mita 25 ya Mile Jedinak ilitinga na kuwapa Palace Bao lao la 3.
Mechi hii imewaacha Wadau wa Liverpool wakihoji uchezaji wa Nahodha wao Steven Gerrard na Raheem Sterling ambao wameonyesha kufifia mno.
Kipigo hiki cha Leo kinawafanya Liverpool wawe wamechapwa Mechi 3 mfulilizo za Ligi na kushinda Mechi 1 tu kati ya 5 zilizopita na kuwaacha wakiwa Nafasi ya 12 wakiwa Pointi 18 nyuma ya Vinara Chelsea.
Katika Mechi zao 2 zilizopita, Liverpool wametandikwa 2-1 na Chelsea na 1-0 na Newcastle.
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA/MATOKEO:
Jumapili Novemba 23
Crystal Palace 3 Liverpool 1        
1900 Hull City v Tottenham  
Jumatatu Novemba 24
2300 Aston Villa v Southampton 
Jumamosi Novemba 29
1545 West Brom v Arsenal
1800 Burnley v Aston Villa          
1800 Liverpool v Stoke              
1800 Man Utd v Hull                 
1800 QPR v Leicester                
1800 Swansea v Crystal Palace            
1800 West Ham v Newcastle                
2030 Sunderland v Chelsea                     
MSIMAMO:
BPL-TEBO-23NOV-A